WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema taarifa nyingi za mjadala wa akaunti ya Escrow iliyofunguliwa kutokana na mgogoro wa malipo ya gharama za umeme kati ya kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ambao unaendelea bungeni, umeongezwa chumvi na wakati ukifika Watanzania watatolewa taarifa kamili.
Kauli hiyo ya Pinda aliitoa kanisa kuu la Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika wakati wa kumsimika Dk Jackson Chilongani kuwa Askofu wa Sita wa dayosisi hiyo.
Awali, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini, Jacob Chimeledya aliitaka Serikali kutoa taarifa juu ya akaunti ya Escrow ili wananchi wajue kilichotokea ili ijulikane ukweli upi na uvumi upi kwani iko hatari ya kutengeneza taifa lenye kuamini uvumi.
Dk Chimeledya alisema Watanzania sasa wanaishi kwenye hali ya sintofahamu kwani hawajui yupi anasema ukweli na yupi ni `mzushi. Alisema ni lazima Serikali itoe maelezo kwa wananchi juu ya kashfa hiyo ili wajue kilichotokea kwani ipo hatari ya kutengeneza taifa linaloishi kwa kuamini uvumi.
Hatutakiwi kuishi kwenye taifa linaloamini uvumi taifa halitapiga hatua kwa taarifa za kusikia tu bila kujua ukweli uko wapi, nini kimetokea na hatua gani imechukuliwa, alisema.
Pia Askofu Chimeledya alitumia fursa hizo kuuzungumzia mchakato wa Katiba iliyopendekezwa na Bunge, akiitaka Serikali kutoa elimu kwa wananchi kabla ya kupiga kura ya maoni Aprili mwaka kesho.
Alisema wananchi waachiwe waamue baada ya kuisoma katiba hiyo na si kuwafuata wanasiasa ambao wamekuwa na milengo tofauti kutokana na wengine kushawishi wananchi kupiga kura ya ndio huku kundi lingine likitaka Katiba hiyo kupigiwa kura ya hapana.
Alisema kama Serikali haitasimama imara kusimamia mchakato huo, basi utatekwa na watu wenye nia mbaya.
Makundi yote yakae kimya Katiba hii ni ya wananchi, waachiwe waamue na si kuwasemea watu wapige kura ya ndio au hapana.
Askofu huyo aliwataka viongozi wa kanisa hilo kuongoza vizuri kwani ni aibu kwa Mkristo au kiongozi wa kanisa kuharibu kanisa, kinachotakiwa kila mmoja kuchukua nafasi yake kuongoza kanisa vyema.
Akitoa salamu za Serikali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema kuhusiana na kashfa ya Escrow na IPTL alisema taarifa nyingi zimeongezwa chumvi. Hata hivyo hakutaka kuingia kwa undani kuzungumzia suala hilo, huku akisisitiza kuwa, wakati ukifika Serikali itatoa maelezo ya kina na kuwafanya Watanzania wapate ukweli.
Sakata la madai ya kuchotwa kwa fedha katika akaunti ya Escrow ndilo linalotawala kwa sasa nchini, hasa baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Swerikali (CAG) kuwasilishwa bungeni, na sasa ikitarajiwa kujadiliwa bungeni kwa siku mbili kuanzia keshokutwa. Akizungumzia Katiba Inayopendekezwa, alisema Serikali itatoa nakala za kutosha za katiba hiyo ili wananchi wengi wasome na kupata fursa ya kutoa maoni yao.
Aidha, alisema Kanisa la Anglikana nchini limetoa mchango mkubwa katika kuendeleza huduma za jamii kwa kujenga shule, hospitali, vituo vya afya na miradi mingine ya kijamii. Pia aliutaka uongozi wa kanisa hilo kuibua fursa za miradi ya maendeleo ili kusaidia familia masikini kuwa na miradi midogo ikiwemo ya ufugaji kuku.
Kwa upande wake, Dk Chilongani aliahidi kuboresha elimu na huduma za jamii na kusimamia kikamilifu vitenga uchumi vya kanisa hilo.
Sikuota kuwa askofu ni neema ya Mungu, alisema.
Chanzo :Habari leo
Kakimbilia chachi? Kweli simba akizidiwa hunywa hata supu ya kabeji.
Ana sura ya kijambazi kabisa.
Kwanini mafisadi wanapenda kukimbilia kanisani?
.Kwanini mafisadi wanapenda kukimbilia kanisani?
Ebu tujadiri hii hoja kisomi tuache ushabiki wa kisiasa,naoma utuambie ni kwa namna gani Mizengo Pinda anahusika na uwizi huo?manake tukikumbuka kwenye sakata la Richmond ripoti ya Mwakyembe ilidadavua vizuri kwa ushahidi uliojitosheleza namna Bw. Edward Lowassa alivyohusika kukwapua fedha za umma bila huruma zaidi shilingi mil.152 kwa siku iwe umeme umezalishwa au haujazalishwa kwenda kwenye gridi ya Taifa.Ebu piga mahesabu kwa mwaka ingekuwaje na je ingekuwa miaka mitano ingekuwaje pia? Edward Lowassa na mafisadi wenzake wangeweza kukwapua kiasi gani cha fedha kama mkataba usingesitishwa baada ya ripoti ya Mwakyembe kuibua uwizi huo.Hiyo ni moja ya mikataba mibovu ya kinyonyaji aliotuingiza Edward Lowassa muda mfupi baada ya kuteuliwa kuwa waziri mkuu.Huyo ndiyo Edward Lowassa kamwe huwezi kumfananisha na Mizengo Pinda katika uaminifu wao,uadilifu wao na weledi wao katika utekelezaji wa majukumu ya serikali.
Ebu Fisadi mbuyu Edward Lowasa njoo ujibu hili swali,vijana huku wanataka majibu!
Makanisa sasa yanatia kinyaa kusafisha Majizi... hapo ndo amefunguka? Ukanjanja katika uandishi sasa yanafikia kilele cha ujinga...
Nafikiri bila shaka ni Edward Lowasa
Ww kimavi kweli..!!! Hooligan...fckd up
Unatumika kinyume na maumbile....ushapasuka msamba ww...!!! Useless...!!
Mbona ushabiki umekuwa mwingi katika sakata la Escrow?tuache siasa tujadili ukweli wa sakata hili kwa hoja zilizojitosheleza kuliko kuwa makuwadi wa kuwatetea wanasiasa fulani na kuwaponda wanasiasa fulani kwasababu ya masilahi binafsi mmeweka utaifa nyuma ubinafsi mbele.
MAFISI wakubwa! kila jitu likaharibu linaenda kukunja makunyanzi kanisani au msikitini. viongozi wa kanisa wanaowaruhusu hawa WEZI kulinajisi kanisa walaaniwe na kila mwananchi anayeitakia mema nchi hii.