Pilipili ya Akabanga yatinga US & Europe

Pilipili ya Akabanga yatinga US & Europe

Sio jukumu la waziri tu mkuu hata mimi na wewe tunaweza kutengeneza bidhaa yetu.


Walaumu kwa sera maana ndiyo wazitungao.
Jeiwii watauza korosho malekani na uropa
 
Mr Slim anazijua fitna za biashara..wewe mwenyewe si unaona kwenye ligi kuu ya uingereza kuna timu zinavaa jezi zimeandikwa visit Rwanda..nyie endeleeni kungaa sharubu..
 
Hizo bidhaa kapelekewa Na serikali , halmashauri au Maofisa biashara huko Ulaya? Tanzania wako mabilionea akina bakhresa ambao hata Rwanda hawapatikani Na wauza biashara nje je wametajirishwa Na serikali , halmashauri au Maofisa biashara?Wewe mleta mada kaa ukisubiribiri serikali,halmashauri ,mawaziri au Maofisa biashara utakufa maskini ukinya umaskini jiongeze pambana Na hali yako.Utaunadije faida biashara,waziri au maafisa halmashauri ambao maisha yao yote hawajawahi hata kuuza Karanga watusaidie biashara yako!!!! Huyo mnyarwanda hongera zake kapambana Na bidhaa yake hadi imeingia ulaya.
 
Tunakwama wapi?
Rwanda inejikita sana kwenye exports . Rwanda imejipanga kuwa hub ya Wataalamu wabobezi wa fani nyeti kama uinjinia wa fani mbalimbali za aina zote ,udaktari ,nk . Rwanda ina export wasomi wengi mno na serikali inasomesha sana Wataalamu wa fani . Wanyarwanda wasomi Kagame wote anataka wawe internationally certified akiwa ni daktari Rwanda wabataka asome afanye mitihani ya kimataifa ya kuwa certified kwa gharama za serikali.Nenda taaisisi zozote zinazotoa international certification course za fani utakutana Na Wanyarwanda wamekuwa sponsored na serikali kusoma wanasoma hasa..Rwanda kuna international certified wengi kuliko nchi yeyote ya Afrika mashariki Na kati . Anafanya hivyo kujenga soko la ajira la kimataifa linaloingiza pesa za kigeni.Sababu hao watu wengi wanapata ajira nje ya nchi na makampuni ya kimataifa Na taaisisi za kimataifa ambazo hulipa pesa za kigeni hivyo kufanya Wanyarwanda kuwa na pesa nyingi za kigeni kuliko za Rwanda.Pili Rwanda imejikita kwenye exports drive ambapo hata mkulima mdogo aweza uza mazao au bidhaa online popote duniani . Mradi ajisajili . Kwa hiyo wana export sana vitu hata vidogo kama vikapu nk Tanzania tuna doctors,engineers, walimu wa sayansi wengi wako idle kazi hawana tinawaacha tu hao ni exportable product tukiiandaa vizuri . Wakati wa kuwaza tu kahawa,korosho Na pamba kuwa ndio exportable products umepitwa Na wakati .Vichwa vyenye akili ni moja ya exports Dunia ya leo.Ndio maana Marekani hata mtoto wa bilionea Billy Gates akiwa na akili sana serikali inaamua kumsomesha yenyewe.Sababu ni hazina ya nchi .Hapa mtoto hata awe top ten Na aenda kusoma udakitari,uinjinia au masomo ya sayansi atajijua Na hata mkopo kupata aweza kosa.Kama nchi tumekalia tu kuangalia traditional exports tulizoachiwa Na mkoloni.Alituachia chai,kahawa,nk tumekomalia kukodolea macho hapo tu!!!! Rwanda wameenda beyond.
 
Hivi ilikuwaje tuliweza kunywa chai ya maziwa na mikate kila siku na nyama kila siku na ubwabwa? Wakati huo kahawa ilikuwa na soko, katani, pamba tuna viwanda lukuki. Sasa sijui kilichobadilika nini?
Pengine zama za kubana bana matumiz zimeathiri pakubwa sekta hiyo. Ndo maana tunazalisha mabomu jitu lina Masters ya Mzumbe au UDOM halijui hata kuandika proposal
 
Pengine zama za kubana bana matumiz zimeathiri pakubwa sekta hiyo. Ndo maana tunazalisha mabomu jitu lina Masters ya Mzumbe au UDOM halijui hata kuandika proposal
Nyerere alijua jinsi ya kula na vipofu. Alisema misaada na mikopo inahatarisha uhuru wetu lakini aliendelea kwenda kuomba walimu toka nje ambao walitufunza vizuri. He wanted to invest in Education and Industries ambazo alijenga nyingi tu sasa ni Magofu. Je ng'ombe tulionao sasa, tungekuwa nao wakati wa Tanzania Parkers tungekuwa wapi? Nasikia kulikuwa na kiwanda kingine kilianzishwa kanda ya ziwa au kati ta nyama. Vyote vililiwa. Tulipewa unga toka USA, vitabu toka Scandnavian countries and UK. Hao hao ndo tunawatukana tunakimbilia kwa wachina ambao sana sana walijenga reli ya Tazara na pipe ya mafuta kwenda Zambia. Tuliishia kuogea sabuni za Fung fung. Kila kitu kilikuwa cha kichina. Ilibidi tununue kwao kulipa deni.
Lakini Mwalimu alikuwa anapeleka wakusoma Western Countries, hata wengine sie ni wanufaika tena watoto wa wakulima maskini.

Tulikuwa tunauza nyama Middle East kwa raha zetu. Sasa je? Koroshowwww.
 
Rwanda inejikita sana kwenye exports . Rwanda imejipanga kuwa hub ya Wataalamu wabobezi wa fani nyeti kama uinjinia wa fani mbalimbali za aina zote ,udaktari ,nk . Rwanda ina export wasomi wengi mno na serikali inasomesha sana Wataalamu wa fani . Wanyarwanda wasomi Kagame wote anataka wawe internationally certified akiwa ni daktari Rwanda wabataka asome afanye mitihani ya kimataifa ya kuwa certified kwa gharama za serikali.Nenda taaisisi zozote zinazotoa international certification course za fani utakutana Na Wanyarwanda wamekuwa sponsored na serikali kusoma wanasoma hasa..Rwanda kuna international certified wengi kuliko nchi yeyote ya Afrika mashariki Na kati . Anafanya hivyo kujenga soko la ajira la kimataifa linaloingiza pesa za kigeni.Sababu hao watu wengi wanapata ajira nje ya nchi na makampuni ya kimataifa Na taaisisi za kimataifa ambazo hulipa pesa za kigeni hivyo kufanya Wanyarwanda kuwa na pesa nyingi za kigeni kuliko za Rwanda.Pili Rwanda imejikita kwenye exports drive ambapo hata mkulima mdogo aweza uza mazao au bidhaa online popote duniani . Mradi ajisajili . Kwa hiyo wana export sana vitu hata vidogo kama vikapu nk Tanzania tuna doctors,engineers, walimu wa sayansi wengi wako idle kazi hawana tinawaacha tu hao ni exportable product tukiiandaa vizuri . Wakati wa kuwaza tu kahawa,korosho Na pamba kuwa ndio exportable products umepitwa Na wakati .Vichwa vyenye akili ni moja ya exports Dunia ya leo.Ndio maana Marekani hata mtoto wa bilionea Billy Gates akiwa na akili sana serikali inaamua kumsomesha yenyewe.Sababu ni hazina ya nchi .Hapa mtoto hata awe top ten Na aenda kusoma udakitari,uinjinia au masoko ya sayansi atajijua Na hata mkopo kupata aweza kosa.Kama nchi tumekalia tu kuangalia traditional exports tulizoachiwa Na mkoloni.Alituachia chai,kahawa,nk tumekomalia kukodolea macho hapo tu!!!! Rwanda wameenda beyond.
Hizi lawama zinaangukia serikali ya chama cha mapinduzi au Chadema ?
 
Huyo jamaa juhudi zake zinachangia asilimia kubwa, sasa wewe Mtanzania upo kwa mtogole unapiga ulabu halafu unawalalamikia SIDO eti hawajakuwezesha.
Mbona kuna watanzania wanauza bidhaa mbalimbali nje ya nchi kama vinyago,maua na bidhaa za kiutamaduni huko ughaibuni.
Watanzania mnapenda kubustiwa muda wote kama kuku wa kizungu.
PAMBANA NA HALI.
 
Sio jukumu la waziri tu mkuu hata mimi na wewe tunaweza kutengeneza bidhaa yetu.


Walaumu kwa sera maana ndiyo wazitungao.
mpaka umeifikisha ulaya ushapigwa makodi kibao
 
Hiyo itakuwa imelimwa juu ya mwamba ama sehemu za mawe mawe na imevunwa wakati wa kiangazi
Rwanda ni tifu tifu na mvua za kule ni almost mwaka mzima. Hiyo pilipili inaitwa huku kwetu pilipi kichaa. Vifupi lakini wee halafu wanaextract mafuta yake siyo pilipili as you know it. Imagine mafuta toka hiyo pili pili. Vichupa vyake kama dawa ya macho. Vidogo.
 
Imagine mafuta toka hiyo pili pili. Vichupa vyake kama dawa ya macho.
Nimelazimika kucheka...! Hiyo lazima iwe hatari...mafuta ya pilipili....leo ndiyo nimejua pilipili inamafuta. Halafu utasia waafrika hatuwezi kugundua kitu. Hongera mgunduzi wa mafuta ya pilipili ya Akabanga.
===
Nikirudi kwenye post yako: Kama jina linaakisi sehemu inapolimwa...yaani Akabanga (neno la kibantu mlimani) utagundua mlimani maji hayatuami..utililika; kiasi fulani muda mwingi panaweza pakawa pamekauka...hivyo dhana ya kusema pilipili hiyo inalimwa sehemu yenye mawe mawe /pakame inaweza kuwa na mashiko.
 
C
"Mmachinga" toka Rwanda anaetengeneza pilipili maarufu "Akabanga" amefanikiwa kuipenyeza bidhaa yake kwenye masoko huko Marekani & Ulaya. Hapa Bongo tuna SIDO, VETA, TIRDO, Halmashauri kila kona na maafisa biashara na ushirika walionenepeana tu.
#Don't Hate, Be Inspired#
akabanga – From a Little secret to Great flavor

Chonde chonde mkuu! hapa kwetu tuna Bongo ukwaju na Bongo pilipili! please
 
Back
Top Bottom