Ipi Bora? mi nitakwambia Honda cg 110 ni bora kuliko boxer150. kwasababu;
Honda CG110, Sifa yake ya kwanza ni engine yake ni cc 110, ni nyepesi. Inatembea spidi mita 120 kwa saa. Honda cg 110 inakimbia kwa mwendo wa wastani. Ina mngurumo wa chini yaani silencer yake ipo chini Ina carrier ya kubebea mizigo isiopungua kilo 120. wadau wengi wamependa Honda cg 110 kwenye ulaji wake wa mafuta ni mdogo kuliko pikipiki zingine. inaweza kutembea km 70 kwa lita. kwahiyo kwa bajeti iko vizuri. kwa matengenezo yake utasahau gharama kwa maana spare zake kuisha inachukua miaka 2 mpaka mitatu ndio ubadilishe spare.
Kwa Boxer 150, ina engine cc 150 kwahiyo ni kubwa na nzito. hata kwenye ulaji wake wa mafuta ni mkubwa inatembea km 40 kwa lita. watu wanachopendea boxer 150 ni kwamba ina spidi na ina mwendo wa hatari kuliko piki piki zingine. na vile vile ina carrier kubwa ya kubebea mizigo mizito. tatizo la boxer ni kwamba gharama za kuitunza. ukinunua boxer mpya baada ya miezi mitatu utaanza kubadilisha gasket, mara spocket mara hiki nk. kwahiyo utajikuta unaingia gharama za kwa mara kwa mara kwenye boxer. lakini pamoja na hayo bado wapo wabongo wengi ambao hawajali hasara kwasababu wanaziona boxer zipo nyingi mtaani basi wanakua hawajui effect zake baadaye. kwahiyo shekhe nimeshakujibu hapo.