kweli bwana katoa kisha katwaa jina lake liidimiwe milele amina kilicho baki kwetu ni sisi kujihoji je muda utakapofika kwenda mbele za haki tutakuwa tumejiandaaje kwa sababu wenzetu kila mmoja atakwenda mbele za haki kwa nafasi yake je sisi tulio hai tunajifunza nini tutakapo kutwa na mauti? Basi ni vyema tukajiandaa
Hii inasikitisha mno , inaumiza sana!
Nashindwa kuvumilia kububujikwa na machozi. Hizi picha zimezidisha simanzi maana zinaonyesha mengi sana:
1.Ajali za barabarani zitatumaliza jamani.
2. Umaskini uliokithiri nchini mwetu - yaani tumeshindwa hata kuwasitiri hawa marehemu japo hata kuwafunika vizuri! Hapo wamesitiriwa na vitambaa vya mabango yao wenyewe tu. Halafu wamewekwa chini - thamani ya binadamu hapo hakuna kabisa.Kama mzazi nimeumia sana!
MUNGU WA REHEMA NA NEEMA ZISIZO NA MWISHO, UWAJAALIE PUMZIKO LA MILELE.
DUNIANI TUNAPITA TU......
Mliotangulia, pumzikeni kwa amani, ole wetu siye tuliobakia!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.