Picha za Wanataarabu wa 5 Stars waliokufa Morogoro!

Hii inasikitisha mno , inaumiza sana!
Nashindwa kuvumilia kububujikwa na machozi. Hizi picha zimezidisha simanzi maana zinaonyesha mengi sana:
1.Ajali za barabarani zitatumaliza jamani.
2. Umaskini uliokithiri nchini mwetu - yaani tumeshindwa hata kuwasitiri hawa marehemu japo hata kuwafunika vizuri! Hapo wamesitiriwa na vitambaa vya mabango yao wenyewe tu. Halafu wamewekwa chini - thamani ya binadamu hapo hakuna kabisa.Kama mzazi nimeumia sana!

MUNGU WA REHEMA NA NEEMA ZISIZO NA MWISHO, UWAJAALIE PUMZIKO LA MILELE.

DUNIANI TUNAPITA TU......

Mliotangulia, pumzikeni kwa amani, ole wetu siye tuliobakia!

tusiwalaumu sana wahusika sister kwa kuwasitiri na mabango ya burudani zao, hospitali zetu si unajua hata panadol hakuna? sasa sanda/shuka lipo kweli? hata wagonjwa waliolazwa tunaona wakijifunika kanga zao.

masikini nchi yetu. mashangingi kila mtaa, viongozi wetu kila siku safari za nje ya nchi na msururu wa wasidizi, ofisi na makazi ya kifahari, samani za kifahari zinabadilishwa maofisini kila siku! lakini umasikini hausemekani. eti tunaadhimisha miaka 50 ya uhuru mwaka huu na chama tawala kimekuwa kikishinda kwa kishindo kila uchaguzi toka uhuru! uchaguzi wa mwisho kushinda ulikuwa mwaka jana tu!

lol, RIP wapendwa wetu

in God we trust

amen

Glory to God
 
tusiwalaumu sana wahusika sister kwa kuwasitiri na mabango ya burudani zao, hospitali zetu si unajua hata panadol hakuna? sasa sanda/shuka lipo kweli? hata wagonjwa waliolazwa tunaona wakijifunika kanga zao.

masikini nchi yetu. mashangingi kila mtaa, viongozi wetu kila siku safari za nje ya nchi na msururu wa wasidizi, ofisi na makazi ya kifahari, samani za kifahari zinabadilishwa maofisini kila siku! lakini umasikini hausemekani. eti tunaadhimisha miaka 50 ya uhuru mwaka huu na chama tawala kimekuwa kikishinda kwa kishindo kila uchaguzi toka uhuru! uchaguzi wa mwisho kushinda ulikuwa mwaka jana tu!

lol, RIP wapendwa wetu

in God we trust

amen

Glory to God

UUUWIIIIIII!!! KILIO JAMANI KILIOOOOOO!!!
Nchi yetu tajiri sana lakini siye wananchi ni maskini wa kutupwa hadi tunapoingia kaburini!?
 
WOS. Hiki kitu nilishakisema siku nyingi sana. Maisha ya binadamu Tanzania hayana thamani sana akiwa hai hata akiwa amekufa. Nilishaweka post hapa kinsi maiti zinavyobebwa kwenye landrover za polisi utadhani ni nyama zinatoka butcher. Serikali kweli imeshindwa kununua gari maalumu za kubebea maiti na kuzisambaza kila mkoa? Imekuwa ni rahisi mno kwa serikali kununua magari mengi ya kifahari kila mwaka, lakini imeshindwa kununua magari ya kubebea wagonjwa na maiti. Jinsi unavyodhalilisha maiti, inaonyesha ni jinsi gani kiwango cha utu wako ulipofikia.

View attachment 25559

Ndugu yangu...nashindwa hata la kusema kwa kweli kwa jinsi ninavyoumizwa!
Hebu rudisha hiyo mada yako hapa tujadili upyaaaa.Tutamuomba mod na wenzetu watuvumilie maana tutajadili kwenye context ya hii hali iliyowapata hawa wenzetu kwenye ajali.

SERIKALI HEBU MTUONEE HURUMA WANYONGE ANGALAU KWENYE KIFO TUHIFADHIWE KWA STAHA BASI KAMA WAKATI WA UHAI TUKIWA NA AKILI ZETU TUNAWEZA KUJIHIFADHI TUSIAIBIKE.

AIBU YA MAITI ANAPASWA KUIJUA MUOSHA TU NA SIYO DUNIA NZIMA JAMANI!
 
Baba Mwenyezi tunaomba uwafariji ndugu wafiwa waliopoteza wapendwa wao, inasikitisha mno. R.I.P
 
kwa utu,heshima yao na familia na watanzania kwa ujumla hizi picha hazikustahili kuwepo,so pliz!tuwaheshimu jamani washafariki hakuna sababu ya kuwaondolea heshima yao kwa kuonyesha miili yao katika hali hiyo

kwanzan ni nani aliruhusu hizo picha zipigwe??????????
 
Back
Top Bottom