Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 416
- 1,051
Wakuu mpo salama? Twende moja kwa moja kwenye mada.
Wakuu, haya mabango mawili ni shughuli mbili tofauti ambapo serikali ilialikwa na wadau kushiriki kwenye shughulii hizi.
Hii ya kwanza ilikuwa ni Siku ya Uhuru wa Vyombo wa Habari Duniani na ya pili ilikuwa ni kuadhmisha Siku ya Kimataifa ya Human Resorces.
Katika warsha zote hizi mbili serikali ni waalikwa tu, yaani tukio ni la wadau 100% lakini ukiangalia mabango haya yanatoa ujumbe tofauti. Ni kama inapiga kelele tukio hilo ni la serikali, lakini pia hata ukifuatilia matukio haya utaona serikali kwa mkono mkubwa ndio imeshikilia tukio hilo.
Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lakini bango limejaa picha ya Majaliwa, kwanini? Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari kwanini anaalikwa Majaliwa kama mgeni Rasmi? Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Kamati ya Kumsifia mama wakiwa wamependeza na Tisheti zao za kumuunga mkono Mama wanahusika vipi na tukio hilo?
Maadhimisho ya Siku ya Rasilimali watu lakini picha ya Nchimbi imejaa kwenye bango lote utafikiri ni maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Nchimbi kwanini? Ukiangalia tu bango paap unakaribishwa na sura ya Nchibi badala ya tukio kwanini? Sura ya Nchimbi ingekuwa ndogo au kutokuwepo kabisa tukio lisingefanyika? Au serikali ingetia figisu tukio lisifanyike?
Je, ni takwa Kisheria mgeni rasmi akiwa kiongozi wa serikali basi lazima sura yake ijae kwenye bango hilo? Je, bila sura ya kiongozi kujaa kwenye bango hilo maoni ya wadau hayatiliwi maanani? Je, kuna uhuru wa kutoa maoni kwenye makongamano hayo?
Au ni kwamba wadau wanajipendekeza kwamba wakiweka sura ya kiongozi ikajaa kwenye bando basi hata jambo lao linalofanyika ndio litafanyiwa kazi haraka?
Narudisha mpira kwenu wadau.
Wakuu, haya mabango mawili ni shughuli mbili tofauti ambapo serikali ilialikwa na wadau kushiriki kwenye shughulii hizi.
Hii ya kwanza ilikuwa ni Siku ya Uhuru wa Vyombo wa Habari Duniani na ya pili ilikuwa ni kuadhmisha Siku ya Kimataifa ya Human Resorces.
Katika warsha zote hizi mbili serikali ni waalikwa tu, yaani tukio ni la wadau 100% lakini ukiangalia mabango haya yanatoa ujumbe tofauti. Ni kama inapiga kelele tukio hilo ni la serikali, lakini pia hata ukifuatilia matukio haya utaona serikali kwa mkono mkubwa ndio imeshikilia tukio hilo.
Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lakini bango limejaa picha ya Majaliwa, kwanini? Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari kwanini anaalikwa Majaliwa kama mgeni Rasmi? Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Kamati ya Kumsifia mama wakiwa wamependeza na Tisheti zao za kumuunga mkono Mama wanahusika vipi na tukio hilo?
Maadhimisho ya Siku ya Rasilimali watu lakini picha ya Nchimbi imejaa kwenye bango lote utafikiri ni maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Nchimbi kwanini? Ukiangalia tu bango paap unakaribishwa na sura ya Nchibi badala ya tukio kwanini? Sura ya Nchimbi ingekuwa ndogo au kutokuwepo kabisa tukio lisingefanyika? Au serikali ingetia figisu tukio lisifanyike?
Je, ni takwa Kisheria mgeni rasmi akiwa kiongozi wa serikali basi lazima sura yake ijae kwenye bango hilo? Je, bila sura ya kiongozi kujaa kwenye bango hilo maoni ya wadau hayatiliwi maanani? Je, kuna uhuru wa kutoa maoni kwenye makongamano hayo?
Au ni kwamba wadau wanajipendekeza kwamba wakiweka sura ya kiongozi ikajaa kwenye bando basi hata jambo lao linalofanyika ndio litafanyiwa kazi haraka?
Narudisha mpira kwenu wadau.