Picha yangu ya leo hii

Picha yangu ya leo hii

Ng%60ombe.jpg

Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi Mkazi wa Wilaya ya Longido ng'ombe watano na mbuzi ambaye ni miongoni mwa kaya 6,128 za wilaya hiyo, Monduli na Ngorongoro mkoani Arusha ambazo mifugo yao yote ilikufa kwa kukosa maji na malisho kutokana na ukame.(PICHA:IKULU)
 
kisarawemwanafunzi.jpg

Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Maruwi Mipera iliyopo katika Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, akiendesha kigari alichokitengeneza kwa kutumia nyaya na vipande vya mbao huku akiwa na panga mkononi kuelekea shuleni. Kwa mujibu wa ratiba ya shule hiyo. Kila Jumatatu ni siku ya shughuli za shamba ambapo wanafunzi hutakiwa kwenda na majembe na mapanga
 
Melisamakidar.jpg

Meli ya uvuvi ya Taiwan, inayomilikiwa na kampuni ya Oman, MV FV Tawariq-1, ikiwa inazama kwenye ufukweni wa Bahari ya Hindi jirani na Bandari ya Dar es Salaam jana. Meli hiyo iliyokamatwa Machi 9, 2009, ikiwa na wavuvi 36 na wakala wao wawili kwa kufanya uvuvi haramu kwenye eneo la maji ya Tanzania, ni moja ya vielelezo muhimu katika kesi inayowakabili watuhumiwa wa uvuvi huo.
 
Songeafujo.jpg

Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Ruvuma wakimshikilia mmoja wa vijana waliodaiwa kuandamana kinyume cha sheria mjini Songea kupinga mauaji ya raia. Inadaiwa kuwa watu wawili waliuawa na wengine kujeruhiwa kwa kupigwa risasi na polisi.
 
Philipinojela.jpg

Raia wawili wa Kichina, Hsui Chintai (63), kushoto, na wakala wake, Zhao Hinqui, wakisindikizwa na askari Magereza kwenye Mahakama Kuu Tanzania jana, baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kuvua samaki ndani ya eneo la maji ya Tanzania kinyume cha sheria.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom