BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,013
Tanzania ni nchi ambayo haikosi vituko! Mtu huwezi kukaa tu na kuwa bored! Nasema hiki ni kituko kingine kama cha komedi maana mwenye akili ataona moja kwa moja kuwa hao (vijana?) wametoka upande gani.
Nasema hivi kwa sababu nimesoma mabango ambayo wameyashika, sijaona bango hata moja linalohimiza serikali nayo kutimiza wajibu wake wa kuboresha afya nchini! Hilo bango huyo mama alilolishikilia linaonyesha tu kuwa hoja kubwa ya madaktari ni kutaka nyongeza ya mishahara.
Jambo kubwa, na ambalo linawagusa wote la kuboresha huduma za afya, wao haliwahusu. Ndio maana nasema vioja haviishi Tanzania...ze Komedi wapo wengi!
Mkuu hawa wanatumiwa tu hawana hata moja walijuwalo.