Picha: Viongozi wa CUF watinga Ikulu leo!

Picha: Viongozi wa CUF watinga Ikulu leo!

Full Mr Bean
23k6ihx.jpg


Interesting....
 
na hapa ndio watanzania tunapokwama. Kuna watu wamesharidhika na kilichopo hapa nchini na wanabakia tu kusikilizia kila kukicha upepo unaelekea wapi ili nao waonekane.
cdm hawakwenda Ikulu kupiga picha na kunywa juisi bali walikuwa na ujumbe na baada ya majadiliano kuna makubaliano walifikia.
Kama kweli hawajaenda ikulu kupiga picha tungojee watueleze walichofuata maana kama ni katiba walishaikubali kwa 100%
Wanaenda kufanya nini wakati wameunga mkono muswada wote 100%?
 
There's something about ikulu watu wakienda wanakenua tu kama "mazuzu" Hizo si smile mkuu Lol!

Halafu tatizo wakitoka huko wanakuwa kama walisahau kilichowapeleka na inawachukuwa muda kukaa sawa na kusema walichoongea na mkulu!

Wakivusha mguu tu ndani ya ikulu wanakuwa kama "misukule" wanacheka cheka tu hovyo!

Sijui ni tactic ya JK kuwachekesha na kuwalamba mipicha?

Ama sijui huwa ana wa hypnotize?

Maana si ndiyo wao walikuwa wakidai ooh sijui anacheka cheka na kwamba hayuko serious?

Sasa hii yao mbona kali sana tu?

Teh teh teh...JF kuna machungu na raha zake!

Next time wawe wanaruka ukuta.
 
CDM wametepeta?wewe kweli chizi,hujui CCM na JK sasa ndio hawalali maana wanajua mziki utakao fata kuucheza ni ngumu sana


Nadhani unaota. Muziki gani utafuata? Wewe huwajui Watanzania. CHADEMA ndiyo hiyo inaelekea kuzimu. Wamefanya blunder ya mwaka. Popularity yao inashuka kwa kasi ya ajabu.
 
Cheki wanavyojichekesha, wanaenda kujadili nini wakati walijadili bungeni na wakaipitisha. Pum£&>fu. Muone Mnyaa anavyonyenyekea, mnafiki.
 
kwa pale CC ya CCM ilipomuagiza JK akutane na vyama vyote vya upinzani mlitarajia nini..?! mlipoona amekubali kuwaita CDM peke yake mkamsifu sanaa!!! HEHEHE Kweli JK ni genius.... CDM walidhani peke yao ndio watakwenda ikulu ..

VIVA JK 😛oa
 
Hawana lolote unawaona ........lengo lao lilikuwa kupiga picha tu na rais
 
Viongozi wa CUF wakiwasili Ikulu leo

inwy03.jpg

x5qr00.jpg

a1o1ua.jpg

t0nckm.jpg

1446yqt.jpg

23k6ihx.jpg

35iyrr8.jpg

rwtn3q.jpg


UJUMBE watu saba wa Chama cha Wananchi CUF ukiongozwa na Makamu mwenyekiti wa chama hicho, Machano Khamis Ali, leo unakutana na Rais Jakaya Kikwete, ili kujadili Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Mwaka 2011.

Wengine wanaoshiriki katika mazungumzo hayo ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF- Bara, Julius Mtatiro, Ismail Jussa (Naibu Katibu Mkuu Zanzibar), Abdul Kambaya (Mjumbe Baraza Kuu la Uongozi Taifa), Habib Mnyaa (Kiongozi wa Wabunge wa CUF), Mkiwa Kimwanga (Mbunge Viti Maalum CUF), Twaha Taslima (Mwanasheria na Wakili wa CUF).

Taarifa ya CUF kwa vyombo vya habari jana ilisema kikao cha ujumbe wa CUF na Rais kitaanza saa 4:00 na kwamba ajenda zitatolewa baada ya kikao hicho. Juzi taarifa iliyokuwa imetolewa na Ikulu kwa vyombo vya habari ilisema baada ya kupata ombi la CUF Rais alikubali kukutana nao.

Mwananchi.

Hawa nao kwakuiga kusikia tu cdm wamekutana na huyo rais wa mambo ya nje na ukimya zaidi oh nao wataka au walifikiri cdm wataivunja ndoa yao na ccm
 
sasa wameenda kufanya nn wakati wapo wote kwenye vikoa vya kupitisha muswada wa katiba haramu

cuf bwana wanachekesha kweli ila wajuie ndo wanajifuta kwenye medali za kisiasa. nawakumbusha kilicho wakuta igunga ...
 
R.I.P cuf you will never exist in politics
 
Wiki ijayo zamu ya TLP kwenda Ikulu..

Baada ya kuwapa na wenyewe Juice Machenza JK anawambia kwa kizulu..

"Ndiyajabula Ukukwanzi" Ha! Ha! Ha! Ha!
"

Mrema anajibu; Ungangisinza na!
 
Back
Top Bottom