EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Viongozi wa CUF wakiwasili Ikulu leo
UJUMBE watu saba wa Chama cha Wananchi CUF ukiongozwa na Makamu mwenyekiti wa chama hicho, Machano Khamis Ali, leo unakutana na Rais Jakaya Kikwete, ili kujadili Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Mwaka 2011.
Wengine wanaoshiriki katika mazungumzo hayo ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF- Bara, Julius Mtatiro, Ismail Jussa (Naibu Katibu Mkuu Zanzibar), Abdul Kambaya (Mjumbe Baraza Kuu la Uongozi Taifa), Habib Mnyaa (Kiongozi wa Wabunge wa CUF), Mkiwa Kimwanga (Mbunge Viti Maalum CUF), Twaha Taslima (Mwanasheria na Wakili wa CUF).
Taarifa ya CUF kwa vyombo vya habari jana ilisema kikao cha ujumbe wa CUF na Rais kitaanza saa 4:00 na kwamba ajenda zitatolewa baada ya kikao hicho. Juzi taarifa iliyokuwa imetolewa na Ikulu kwa vyombo vya habari ilisema baada ya kupata ombi la CUF Rais alikubali kukutana nao.
Mwananchi.
UJUMBE watu saba wa Chama cha Wananchi CUF ukiongozwa na Makamu mwenyekiti wa chama hicho, Machano Khamis Ali, leo unakutana na Rais Jakaya Kikwete, ili kujadili Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Mwaka 2011.
Wengine wanaoshiriki katika mazungumzo hayo ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF- Bara, Julius Mtatiro, Ismail Jussa (Naibu Katibu Mkuu Zanzibar), Abdul Kambaya (Mjumbe Baraza Kuu la Uongozi Taifa), Habib Mnyaa (Kiongozi wa Wabunge wa CUF), Mkiwa Kimwanga (Mbunge Viti Maalum CUF), Twaha Taslima (Mwanasheria na Wakili wa CUF).
Taarifa ya CUF kwa vyombo vya habari jana ilisema kikao cha ujumbe wa CUF na Rais kitaanza saa 4:00 na kwamba ajenda zitatolewa baada ya kikao hicho. Juzi taarifa iliyokuwa imetolewa na Ikulu kwa vyombo vya habari ilisema baada ya kupata ombi la CUF Rais alikubali kukutana nao.
Mwananchi.