Picha: Ndege Yapata Kizaazaa Huko Arusha

Picha: Ndege Yapata Kizaazaa Huko Arusha

Mimi niko gado kabisa..

Tumezoea kusikia pilot error, technical prob sasa hii itakuwa porters error....Mazoea na ile pressure ya Arusha airport mida ya saa sita ndivyo vimevimewakamata.....

Mkuu Marejesho umenena...hao watu Arusha airport wangaliwe kwa jicho la tatu

imagine heading,ndege yapata kizazaa hapo tunawaficha wahuni kwa kuitaja ndege on its own,ingewezw kuwa. ; Uzembe wa wahudumu wahatarisha usalama wa abiria na ndege Arusha...such a heading ina amsha wakubwa na kuanza kuwajibishana,kwa wanaofanya kazi mnaelewa madhara ya neno uzembe kuhusishwa na ofisi yako
 
82% ya mada za PJ zinahusu mambo ya ndege ndege
unafanya kazi gani mkuu?
 
Mkuu PakaJimmy unaniogopesha, hii case naona inafanana na wale viongozi walikufa miaka fulan kwa kosa la kujaza magunia ya mchele upande mmoja ikapaa baadae ikapiga mweleka
Yes ni kule Mbeya!
Jamaa walizuzuka na Mchele wa Kyela wakabeba hadi wa kupeleka nyumba ndogo, matokeo yake ndio hivyo, ikatucost maisha ya waziri!
 
halafu naonda ndege bado njema kabisa
Mkuu, Hicho kitu bado Mma kabisa, na ni luxurious sana ndani!...na inakata mawimbi kwa kasi iliyo sawa na ATR 72 zile za Precision!
 
Huo uwanja hauna Department ya Load Control?
Mkubwa,
Nadhani kwa hapo kiwanjani Load Control ni personal issue ya kila Air operator. Sehemu zingine of course kuna makampuni maalum ya kazi hizo.
 
The worst story of it ni kwamba matengenezo ya ndege hiyo ni ghali sana, hakuna Hangar yoyote Tanzania yenye uwezo wa kutengeneza ndege ya jinsi hiyo, hadi South Africa. Kwa macho mtu anawezadhani ni demage ndogo, lakini ndiyo imekuwa grounded hiyo ikisubiri kupigwa x-rays ili kubaini kama haijapata maumivu makubwa zaidi yasiyoonekana kwa macho!
 
katika upakiaji mizigo kuna chart maalum lazima uifuate kulingana na ndege
Moja ya ndege ninayoipenda ndio hiyo laiti kama nina uwezo basi hiyo ndio ndege ya kuwa nayo PILATUS
 
lazima kufanya weight and balance kwenye ndege tofauti yake ni kukaribisha ajali ya ardhini au angani
baada ya kunihuzunisha nimecheka sana, inamaana tembo na twiga walipangwa na kupimwa uzito kabla ya kupanda kwenye ndege ili kubalance uzito?
 
Ndege haikupata matatizo ya kiufundi?
 
aiseeeee babayangu hii si habari kubwa kivile ni swala la rubani,waudumu na habiria kuamia mbele mbona itakaa sawa 2

au mmesahau mkifika chaline mazani mnaambiwa haya mlio njuma amieni mbeli tumefika mizani
 
Back
Top Bottom