Haya sasa ushahidi umeletwa tena wa picha, ni wapi Mwigulu alipo zomewa?
Mtahaha sana mwaka huu, mpaka ifike 2015 kazi kwisha.
Viva CCM Viva Mwigulu.
nadhani kina mtemla,shönza na mwigulu watakimbia arusha!Hivi hao mamia ya wananchi wako wapi hapo? Si mmejaza magari tu hapo. Aisee nasema....CCM ikishinda kiti chochote Arusha mjini, natembea toka ubungo mataa mpaka posta mpya kwa miguu.
Kumbuka ulipo toka hujavuka mamba na Arusha sio wajinga
Picha za kuweka humu mchague wenyewe, halafu utuulize sie? Halafu ulitaka picha zionyeshe sauti za wazomeaji? Hamna picha hata moja ya kuonyesha umati wa watu!
Naibu katibu Mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba akilakiwa na Bibi mwanachama wa CCM eneo la mkutano kaloleni jijini Arusha
Naibu katibu mkuu wa CCM Mh.mwigulu Nchemba akilakiwa na mgombea UDiwani wa kata ya kaloleni kwa tiketi ya CCM Ndugu Emmanuel Thomas
Naibu katibu mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara kwaajili ya kampeni za uchaguzi wa Udiwani kata ya kaloleni jijini Arusha
CCM inalea na kukuza watoto kwaajili ya taifa lenye Heshima na ustaarabu siku za Usoni.Hawa na Vijana wa CCM wakisoma ngonjera mbele ya naibu katibu mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba
Kushoto ni aliyekuwa diwani wa CHADEMA Ndugu Rehema sasa ni kada mtiifu wa CCM.Kulia ni Mgombea Udiwani kwa tiketi ya CCM ndugu Emmanuel Thomas
Bi.Juliana shonza akisisitiza kwamba hakuna chama kama CCM,CCM ni chama chenye mlengo wa kitaifa kimaendeleo.CCM ni chama tawala na kinamaslahi jamii
Naibu katibu Mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba akimnadi mgombea udiwani kata ya kaloleni kwa tiketi ya CCM Ndugu Emmanuel Thomas