Picha: Mwigulu Nchemba awasha moto kata ya Kaloleni Jijini Arusha Kampeni za UDIWANI

Mtela Mwampamba

JF-Expert Member
Dec 19, 2012
537
347
Naibu katibu mkuu wa CCM Tanzania bara akiwasili viwanja vya kata ya kaloleni-stendi jioni ya leo kwa ajili ya mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Udiwani kata ya kaloleni Jijini Arusha


Naibu katibu Mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba akilakiwa na Bibi mwanachama wa CCM eneo la mkutano kaloleni jijini Arusha


Naibu katibu mkuu wa CCM Mh.mwigulu Nchemba akilakiwa na mgombea UDiwani wa kata ya kaloleni kwa tiketi ya CCM Ndugu Emmanuel Thomas


Naibu katibu mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara kwaajili ya kampeni za uchaguzi wa Udiwani kata ya kaloleni jijini Arusha


CCM inalea na kukuza watoto kwaajili ya taifa lenye Heshima na ustaarabu siku za Usoni.Hawa na Vijana wa CCM wakisoma ngonjera mbele ya naibu katibu mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba


Kushoto ni aliyekuwa diwani wa CHADEMA Ndugu Rehema sasa ni kada mtiifu wa CCM.Kulia ni Mgombea Udiwani kwa tiketi ya CCM ndugu Emmanuel Thomas


Aliyekuwa diwani wa CHADEMA Ndugu Rehema akisalimia wananchi na kuwaomba waachane na CHADEMA ili wapate maendeleo kuanzia ngazi ya kata hadi wilaya na Kitaifa.Amesisitiza CHADEMA ni chama cha watu wachache na chenye mlengo wa maslahi binafsi.Amewaomba wanaarusha kuchana na adha ya kuamrishwa kila kitu na Mbunge wao wa maandamano Ndugu Godbless Lema.Amesema yeye ameshakaa chadema na anajua uchafu wote unaofanyika kuanzia kwa Mwenyekiti wa chama,katibu mkuu wa chama na hata ngazi za chini.Hivyo amewaomba wanaarusha kumchagua diwani wa CCM kwa maendeleo ya kata ya kaloleni


Kada wa CCM Bi.Juliana Shonza akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi kata ya Kaloleni.Bi.Juliana shonza amewaomba wakaloleni na Wanaarusha kuacha kutumika,Kuacha kuwa wafusai wa mtu,Kuacha kuliangamiza jiji la arusha kiuchumi kwa kuendelea kuikumbatia CHADEMA.Amesisitiza yeye alikuwa chadema na alikuwa kiongozi wa juu ndani ya chama ameona namna chama kinavyoendeshwa kwa maslahi ya watu wachache.Hivyo chaguo sahihi kwa wanakaloleni na wanaarusha ni kuipa nafasi CCM kwenye uchaguzi huu wa Udiwani


Bi.Juliana shonza akisisitiza kwamba hakuna chama kama CCM,CCM ni chama chenye mlengo wa kitaifa kimaendeleo.CCM ni chama tawala na kinamaslahi jamii
Kada wa CCM na aliyekuwa mgombea Ubunge jimbo la mbozi Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA kabla hajachukua uamuzi wa kujiunga na CCM Ndugu Mtela Allam mwampamba akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya kaloleni jijini Arusha.Mtela Mwampamba amewaomba wanaarusha kumpatia elimu mbunge wao kuhusu mahusiano kati ya maendeleo na serikali iliyopo madarakani.Amesema Mbunge w Arusha mjii Godbless Lema hajui maana ya maendeleo na serikali,anafanyakazi kubwa ya kutenganisha maendeleo ya Arusha na serikali.Amesisitiza Lema si mwanasiasa bali ni binadamu aliyezoea maisha ya kihuni ndio maana siku zote anatafuta wahuni wenzake ilikuivuruga Arusha.Ameomba wanakaloleni kumpigia kura Diwani mtarajiwa wa CCM Ndugu Emmanuel Thomas


Hapa kada wa CCM mtela Mwampamba akiwahoji wanakaloleni kwamba yeye amekuwa chadema tena mgombea ubunge mwaka 2010 na kupata kura 32000 jimboni kwake Mbozi,lakini kwa kuchunguza mwenendo wa CHADEMA na kutambua ni chama cha watu wachache wenye maslahi yao akaamua kujiunga na CCM chama chenye mlengo wa kitaifa.Je wanakaloleni mimi mwampamba ninakura 32000 lakini nimeachana na chama cha maandamano,je wewe kijana unayenyweshwa viroba siku za maandamano na hata huyo Mbowe hakujui unanufaika na nini na CHADEMA?


Mtela Mwamapmba akihutubia mamia ya wananchi na wakazi wa kaloleni jioni ya leo tar.8/06/2013.Amewaomba wanakaloleni kumpa kura mgombea wa CCM kwa sababu chadema wanafukuza madiwani bila sababu na kulitia hasara taifa.Pia CHADEMA hawanachakutekeleza zaidi ya kuandaaa maandamano na vurugu ndani ya jiji la Arusha.


Huyu kijana alikuwa kamanda wa CHADEMA,amesema aliachana na CHADEMA baad aya kugundua kuwa anapoteza muda wake kuhangaikia watu binafsi na sio maslahi jamii.hapa alikuwa anaonesha barua na hati mbalimbali anazofanyia utapeli Mbunge wa Arusha mjini Ndugu GodBless Lema.Ameeleza namna Lema alivyoweka ARUSHA DEVELOPMENT FOUNDATION mali ya familia yake,Mke wa Godbless lema ndiye Mkurugenzi wa mfuko huo.Hivyo amewasihi vijana wenzake kuachana na CHADEMA,Wafanye chaguo sahihi kwa kumpa kura mgombea wa CCM


Mh.Munge Devotha Likokola akihutubia mamia ya wananchi wa kaloleni waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni za Uchaguzi jijini Arusha kata ya kaloleni.Amesema wanakaloleni wasipoteze muda wao kwa kukipa nafasi chama chochote cha upinzani.Amesisitiza atasaidiana na akiana mama wa kata ya kaloleni keendeleza mifuko ya VICOBA ambayo ipo chini ya serikali ya CCM


Mh.Mbunge Devotha Likokola akimnadi mgombea wa udiwani kata ya kaloleni Ndugu Emmanuel Thomas kwa tiketi ya CCM.Amesisitiza hakuna mtanzania asiyependa kufika ama kuishi Arusha,Lakini kwa huu upuuzi wa CHADEMA wa kuvuruga jijini ni ishara tosha kwamba hawafai hatakupewa nchi.Hivyo wanakaloleni wampe kura diwani wa CCM.





Mh.Mwigulu Nchemba,Naibu katibu Mkuu wa CCM amehutubia mamia ya wananchi wakata ya kaloleni jijini Arusha jioni ya leo tar.8/6/2013 kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani.Mh.Mwigulu Nchemba ameanza kw akusema uchaguzi unaofanyika sasa kata ya kaloleni ni matunda ya chama mufilisi cha chadema kutotambua haki ya wananchi wanaopiga kura.Amesema CHADEMA walifukuza diwani hapa,je kunahaja ya kuwapa diwani tena?AU walipowafukuza walikuja kuomba ridhaa ya wananchi wa kaloleni?.Huu ubabe kwenye vyama vya siasa ni wakupinga vikali na njia pekee ni kupiga kura za kutosha kwa mgombea wa CCM.


Naibu katibu Mkuu wa CCM akisisitiza jambo kwa wananchi.Amesisitiza sana kuhusu amani wakati wa uchaguzi na wakati wote wa maisha ya kila siku.Amesema ni ajabu kwa Wana kaloleni na wanaarusha kukipigia kura chama kinachoshabikia maauaji,CHADEMA wanashabikia mauaji,Chadema wanatumia misiba kuhadaa wananchi na kutafuta sifa za kijinga.Pia amewaomba wananchi kulaani vikali tabia ya Mbunge wa Arusha mjini kutumia viroba kama fadhila kwa wananchi waliompigia kura.Amesema thamani ya vijana wa Arusha sio viroba,Thamani ya vijana wa arusha ni maendeleo na kudumisha amani.


Hapa Naibu katibu mkuua alikuwa anauliza,Je CHADEMA wamejenga angalau choo cha jumuia hapa kaloleni?Pia akauliza ni kwanini CHADEMA hawafanyi maandamano wilaya ya Hai na karatu?Akahoji zaidi kwa kusema je kunamzazi anafurahia mtoto wake amwagiwe tindikali.


Naibu katibu Mkuu wa CCM Mh.Mwigulu Nchemba akimnadi mgombea udiwani kata ya kaloleni kwa tiketi ya CCM Ndugu Emmanuel Thomas


Hapa naibu katibu Mkuu wa CCM akimpongeza mgombea udiwani kwa tiketi ya CCM kwa kuamua kujitolea kuwasaidia wanakaloleni na Wanaarusha kwa kupitia CCM chama cha watanzania wote




Mgombea udiwani kata ya kaloleni Ndugu Emmanuel Thomas akiomba kura kwa wannachi na kuwaahidi kuendelea kutekeleza ilani ya CCM na kuwaletea maendeleo wanakata ya kaloleni na jiji la Arusha







 
Kumbuka ulipo toka usitukane mamba kabla hujavuka mto uliza wenzio Arusha sio mabwege tusubiri
 
Haya sasa ushahidi umeletwa tena wa picha, ni wapi Mwigulu alipo zomewa?

Mtahaha sana mwaka huu, mpaka ifike 2015 kazi kwisha.

Viva CCM Viva Mwigulu.
 
mbona picha zimepigwa upande upande? tupieni na picha ya kutoka nyuma kuelekea jukwaani
 
Mbona mamia usemayo hayaonekani sana sana tunawaona hawa Mafisadi wenzako Rehema kafukuzwa kama wewe na Juliana mlivyofukuzwa kwa kupenda maslahi sasa ukiwa unaandika sema sie tuliofukuzwa Chadema na sio mlihamia kwa Mafisadi wenzenu kwa kuona ni kuzuri shidaaaaaaa,njaaaaaa zitawauwa wengi na bado tutaona mengi sana.
 
mbona zile za kutolewa nduki sizioni mkuu? hebu weka na zenyewe ni picha pia
 
Mtela acha kuwadanganya watu. Nilipita kwenye huo mkutano na hapakuwa na watu zaidi ya mia moja na tena wote wamevaa sare za ccm kama vile wako kwenye kikao cha chama.

Na watu hawa wameazimwa kutoka kata za jirani na baada ya mkutano Mwigulu na msafara wake wamepita barabara ya Mianzini na wamezomewa barabara nzima.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Daaaaaaaaaaaa kweli vijana wa Lumumba mnasikitisha, Mwigulu leo kazomewa balaaaa, watu wamemwambia arusha hamna ccm na wanamshangaa yeye kwenda kule.
 
Hiyo kofia ya Mtumba kapewa China

Wenzie walivaa enzi za Mao na Falsafa ya Juche.

Mwigulu kaona ni ujanja anaivaa leo karne ya 21.

He is so 1944 :)
Z



images

DSC07104.JPG
 
Inapendeza nyomi ipo ya kutosha bila shaka wana Arusha wameamua kwa dhati kuachana na ubabaishaji wa chadema na kuendeleza imani yao dhidi ya Ccm chama dume.
 
Kama huku nako ni kuwasha Moto basi CCM wana hali Mbaya. BTW yule jamaa aliyemwagiwa tindikali leo alikuwepo na yeye?
 
Haya sasa ushahidi umeletwa tena wa picha, ni wapi Mwigulu alipo zomewa?

Mtahaha sana mwaka huu, mpaka ifike 2015 kazi kwisha.

Viva CCM Viva Mwigulu.


Hicho ni kitu RAHISI SANA; Kama BOMU LILIPIGWA kanisani ARUSHA na WATU KUFARIKI hadi LEO hakuna aliyeshikwa na UGAIDI HUO... Sembuse Kuzomewa? ni rahisi kugushi hilo na ni kazi ya Mtoto ndani ya UVCCM

Just think; Wote waliochoma MAKANISA na kuua MAPADRI hakuna aliyepelekwa MAHAKAMANI na Unawasiwasi na kuzomewa???
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom