afrodenzi
Platinum Member
- Nov 1, 2010
- 18,152
- 9,268
Mara ya mwisho kumuona mwanzoni mwa miaka ya 90 nikisoma moshi mjini alikuwa na honda...i mean boonge la honda na aliiwekea exhaust 2 so ilikuwa akivinjari maeneo ya shanty town na soweto mtaa unakuwa bariiidi kidume kinapita.... sasa hivi vya urubani sijui vimeanza lini tena peke yake kwenye ndege!
Urubani ni kitu kirahisa sana kama kweli unataka kuwa rubani.
"I mean you are really passion abou it"..
umri kuanzia miaka 18 , sasa yeyote, mtu yeyote anaweza kurusha ndege.
kitu cha kwanza u pass "medical" mengine ni wewe na kitabu na ndege .. Passing zako za awali ndizo zitakazo kuingiza . .
sio ngumu.
Kwa hiyo sintoshangaa kusikia hapa JF kuna marubaini kibao..
na pia kuna tofauti za urubani.
kuna wale wanaosomea ajili wanataka kufanya kazi kwenye "airline, airforce"
kuna wengine wanapenda kufanya general flying mfano " bush flying"
kuna wengine wanafanya for fun na ajili ya mashindano mfano "aerobatics pilots"
Kuna wengine wanasomea urubani ili wafundishe marubani "Instuctors " na hao nao wamegawanyika kwenye makundi mengine....
halafu kuwa rubani kuna aina mbili za licence ..
PPL (Private Pilot Licence)
Ukiwa na hii unaruka kokote ndani ya nchi hiyo , unaweza kupata type ratings
za ndege nyingine ndogo, unaweza kurusha ndugu jamaa na marafiki lakini
hulipwi sababu ni kinyume cha sheria. Na pia ni ngumu kupata ajira .
wengi ambao hupata hii licence huwa na ndege zao binafsi....
halafu kuna hii sasa
CPL ( commercial pilot licence)
Hii ni kwa ndugu zangu wale ambao wanategea kuajiriwa na shirika fulani la ndege
kufanya kazi . Pia kupata hii licence sio ticket ya kuingia airline .. kuingia air line
unatakiwa kuwa na "multi engine instrument rating" hapo ndio utapata kazi airline ..
NA ukifika airline ukitaka kupanda ngazi kuwa captain unatakiwa kufanya mitiha ya ATPL "airline transport pilot licence"
na ukitaka kupanda ngazi zaidi na kuwa train watu kuwa ma captain unatakiwa kusoma kozi zaidi kama vile "instructing"
Kwa ufupi sijui alikuwa na licence gani.
Na kupata licence ya urubani si kazi ngumu.
Akili yako na fedha na kujituma kupita kiasi ..
Sipendagi tabia ya watu kuona kitu ni kigumu na wakati mtu hajajaribu..
NA wapa moyo kwa kila anaetaka kuwa rubani.
sio ngumu sana bali ni "Risky business "
You only live once......