PICHA: Kwa mbinu hii ya Bukoba, JK anatisha

Hahahahahahahahahaaaaaaa wameenda na wasanii kama kawaida yao xo watu wanaenda kumwona diamond,juma nature na wengineo duh!
 
Ukubwa wa pua sio wingi wa makamasi, magari mangapi yamekodiwa kuleta watu, shule ngapi zimefungwa, wanafunzi wamelazimishwa kuhudhuria huo mkutano. Wasanii wangapi walikuwepo kuburudisha na mapipa mangapi ya ubwabwa yamepikwa kuwalisha hao watu. "Usione vyaelea, vimeumbwa"

Acha dharau kwa watz wenzio. Umeona ubwabwa ukigawiwa hapo? Au umewahi kuckia kagera kuna njaa. Huko kwenu kulikojaa wavivu ndiyo kuna njaa. Mjinga wewe.....
 
Eti CCM inaimarika una akili wewe au umetumwa na buku7 za Lumumba,nani asiyejua mwisho wa hiki chama cha mafisadi na wazulumati kimefiikia mwisho
 
Hivi wale wanaokwenda mikutano ya chadema wote huenda kwa miguu
WanaBukoba wamechangishwa Shs 1000 kwa ziara ya Rais. Je unajua kwa maisha ya kijijini Shs 1000 ni kiasi kikubwa sana? Imagine kama ingekuwa wewe, ungefurai kuibiwa pesa zako kukodia magari? I don't really like CDM per se, but nakubaliana na mambo yao mengi
 
Aje hapa arusha na Kawambwa alafu atuambie mafanikio ya wizara hii ya elimu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kila wilaya za mkoa wa KAGERA alikoenda JK, wakurugenzi wa wilaya waliwarazimisha wakuu wa shule kufunga shule na wanafunz wote waende kumpokea rais, shule zote zinafungwa saa nne asubuh. Hivyo wanafunzi ndio wanaohudhuria na baadh ya wafuasi wa ccm
 
Ndo maana katiba mpya inapaswa kudefine vizuri how ministers are to be elected. Huu ni utumiaji mbaya wa mda. Yaani shughuli za kiofisi zisimame kwa sababu kuna kampeni za Chama. Huu ni upumbavu. Utumiaji mbaya wa madaraka na kiusalama si sawa kubeba jopo la mawaziri kwa mpigo kwa kampeni za chama

Haijarishi lakini cha moto mtakipata,hapo kwenye picha hizo umeona msanii anaimba mnajifanya mnamakengeza hamuoni vizuri mtaona tu.



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kila wilaya za mkoa wa KAGERA alikoenda JK, wakurugenzi wa wilaya waliwarazimisha wakuu wa shule kufunga shule na wanafunz wote waende kumpokea rais, shule zote zinafungwa saa nne asubuh. Hivyo wanafunzi ndio wanaohudhuria na baadh ya wafuasi wa ccm
Mkuu mbona hii ni kawaida sana - hata utawala wa Kambarage wakati tuko shule ya msingi mbona tulikuwa tunakwenda kumpokea RAIS akija mkoani Kagera. Hivi JK ni RAIS wa TANZANIA/TAIFA au wa CCM - Jibu unalo mkuu Kalyankerere/mashasha!
 
Nadhani tunahitaji KUONA zaidi kuliko KUSIKILIZA.Maendeleo huwa yanaonekana, haitaji simulizi! Barabara nzuri zitaonekana, walimu watakuwepo shuleni, vitabu vitakuwepo, mashamba yatamwagiliziwa kwa mabomba tutaona(kilimo cha umwagiliaji),mahakama zitatenda haki, timu zetu za taifa zitapiga watu magoli tutaona,kipato cha mwananchi kitakua kizuri tutaonana nk MAENDELEO HAYAHITAJI MANENO MANENO,MAMBO HADHARANI! Ukimuona mtu yupo madarakani na bado ana hadithi nyingi za maendeleo yasionekana kwa macho, mpotezee tu!
 
Ukubwa wa pua sio wingi wa makamasi, magari mangapi yamekodiwa kuleta watu, shule ngapi zimefungwa, wanafunzi wamelazimishwa kuhudhuria huo mkutano. Wasanii wangapi walikuwepo kuburudisha na mapipa mangapi ya ubwabwa yamepikwa kuwalisha hao watu. "Usione vyaelea, vimeumbwa"
Hivi kweli wewe Fitinamwiko kweli NI. Mtanzania Au wewe NI Mjukuu wa Nduli Idd Amin Dada? WanaKagera ndio walioathirika sana Na uvamizi wa nduli Amin, lakini wewe kuwaona wamejitokeza Kwa wingi kuwakumbuka walijitoa muhanga wa maisha yao kuwatetea kutokana Na uvamizi wa babu yako nduli Amini tayari imekuuma. Waombe radhi Wananchi wa Kagera vinginevyo roho yako itakuwa inasononeka Kila utakapokuwa unakutana Na mwenye asili ya Kagera. Mungu ibariki Tanzania.
 
Haijarishi lakini cha moto mtakipata,hapo kwenye picha hizo umeona msanii anaimba mnajifanya mnamakengeza hamuoni vizuri mtaona tu.
Inawezekana kweli mnakubalika.. sasa basi msing'oe watu kucha bila ganzi maana hiyo hufanyika pale tu inapoonekana kuna hatari ya kupoteza uwakilishi wa wananchi
 
Back
Top Bottom