Picha: CCM waendelea kujimaliza Muhambwe

Picha: CCM waendelea kujimaliza Muhambwe

Ccm wameishiwa kweli yaani ushauri tuliowapa ACT wa kufanya mikutano sehemu za Stand na madukani ili kupata wasikilizaji wao ndiowanaufanyia kazi...!!! Ukongwe wao uko wapi sasa hawa?

Nilimuona Katibu wao leo tena hawa wameandaa mkutano stendi tena mkutano wenyewe wa Wilaya..!!!! kazi kweli kweli

BACK TANGANYIKA



Kwa sasa wananchi hawawataki hata kuwasikia
 
Barabara ya Kidawe kwenda Nyakanazi ndio inaiadhibu ccm huko siasa ya Kigoma ni ya aina yake tusishangae awam hii hata ACT ikanyakua majimbo huko


Only if UKAWA wataamua vibaya,hasa kuwaachia NCCR majimbo ya Buyungu,Muhambwe,Kasulu Mjini na Manyovu
 
Katibu huyu wa wilaya CCM bwana Kinanda anasema viongozi wa dini kama wamekosa waamini wayageuze mkanisa vyama vya kisiasa na wayasajiri ili waweze kuongea siasa,kwani wao si wasafi pia

mbona namuona mama mmoja akipanga mafungu ya nyanya.
 
mbona namuona mama mmoja akipanga mafungu ya nyanya.


Na hiyo ndo sababu yaa-CCM kuilupeleka mkutano eneo hilo,kwani jioni huwa kuna kuna mama wafanyabiashara wadogowadogo wanauza mbogamboga,so wanajua watasaidia kuongeza watu kwenye mkutano,bt waliendelea kuzomewa tu
 
Huyu kijana mnamfahamu?naona anafanya kampeni yake facebook,huko mtaani mnamfahamu?
10353094_1040645012615555_4534661559093868271_n.jpg

Kaka Viol heshima mbele sana kaka.

Namfahamu huyu jamaa, nilikutana nae London mwaka 2010 kwa mara ya kwanza kwenye shughuli za chama chao CCM, Kipindi hicho ailikuwa ametokea kwao Kibondo kwenye uchaguzi na alikuwa njiani kuelekea Russia alikokuwa masomoni chini ya scholarship ya serikali hivi majuzi tulikutana kwenye hija ya vijana wa katoliki mjini Tabora. Kuna vitu kadhaa naweza kusema kuhusu huyu jamaa..
1. Ni kijana he's about 28 0r 29
2. Ni msomi ana masters ya masuala ya Utawala katika Serikali Kuu na Manispaa
3. Ni mcha mungu wala hali kilevi
4. Anaipenda Kibondo sana na anaijua haswa, amezaliwa na amesoma Kibondo kmuda mwingi huongelea kibondo na maisha yake ya shule akiwa Kibondo
5. Ni mjengaji hoja mzuri sana
6. Anakipaji cha uongozi..

Asante
 
Huyu gamba namfahamu,tunamfahamu,hawezi tusumbua wanaMuhambwe kwa sababu wananchi wanamtaka mbunge na diwani anaetokana na wao wenyewe,na si mtu anaegeuza jimbo na wananchi kama vitalu vya kuwindia ,anaekuja kukagua kitalu kama kuna wananyama then anarudi ughaibuni,yeye aendelee kujidanganya kwamba atachaguliwa kwa sababu tu eti amesomea nje

Mkuu huyu jamaa amesharudi nyumbani kutoka masomoni muda mrefu sana toka mwaka juzi, na ninavyoongea na wewe nimeongea naye yuko Kibondo anamalizia kitabu chake cha maswala ya serikali za mitaa.

BTW Huyu ndiye Mbunge wenu ajaye, sasa jiandae kisaikolojia
 
we unadhani ccm watampitisha agombee?acha upinzania najua ccm hawana lao pale,ila huyu hata ccm watampitisha?

Kaka Viol

1. Kwa uchunguzi niliofanya, "na mimi ni mwana Kibondo" uhakika wa jamaa kupita kwenye kura za maoni ni mkubwa sana.
2. Wote tunajua sababu zilizompa ushindi mgombe wa NCCR 2010, alijikusanyia maelfu ya kura za hasira kutoka CDM na CCM, Hili unalijua sana limetokea Mbeya Mjini, Iringa Mjini etc
 
Siku hizi chama tawala wanatumia hadi fisi ili kustawisha mahudhurio!naona siku hiyo waliwaacha mara nyingi nimeona wanakua na mzee kinana
 
Back
Top Bottom