Picha: Bashe na Kubenea Wakizozana Na Nape

Picha: Bashe na Kubenea Wakizozana Na Nape

Nape alipoteuliwa kuwa waziri, nilijua tu wamepeleka shida serikalini, uwezo wake ni mdogo, anapenda kuongeza maadui kuliko marafiki.
 
Hivi ni mojawapo wa vituko vingi vya serikali hii ya awamu ya 5 tutakavyoshuhudia
 
Duu Nape mbona umeamua kumuhalibia Magufuli? Nilisema toka mwanzo mawaziri wa Magufuli alioteuwa tofauti na alivyokuwa akijinadi.. Mmh mama weee bola mjomba Kikwete
 
Walianza vizur sasa naona kabisa mwisho mbaya kwa CCM
 
Kama kaenda bungeni kushughulikia UKAWA; na wewe una muunga mkono, basi una matatizo katikati ya masikio!
Kaenda bungeni akiiwakilisha serikali ya JMT ila ukawa mnajipendekeza kwake. Ataendelea kuwanyorosha
 
Bashe Nadhani Ajiandae Kuitwa Ktk Vikao Vyao, Ambavyo Wanatishiwaga Kunyang'anywa Kadi Za Uanachama!! CHEZEA Mzee Wa Goli La Mkono, Mkuu Wa Zengwe Na Fitina!!! NAKUMBUKA Kipindi Kile Cha Mzee Makamba, Bashe Alipoambiwa Sio MTANZANIA!! HIVYO Ushindi Wake Wa KURA Ya Maamuzi Jimboni Ni BATILI!!! AKAINGIA Kigwangwala!!! SASA Naona Dalili Zileee!!!!! ILA Big Up Kwao!!! HATA Richard Ndassa Mbunge Wa SUMVE Alipinga Mpango Huo!!! WA Kusitisha Matangazo Ya Live!!
 
Ndio tatizo lenu hilo. Sasa biashara ya sifa bungeni hakuna tena mbunge tutakupima kwa maendeleo jimboni
Una point hapa, sasa HAMNA jinsi. Unakuwa mbunge jembe kwa kigezo cha maendeleo jimboni mwako! Sijui Makoka watajengewa barabara maskini??
 
Kama kaenda bungeni kushughulikia UKAWA; na wewe una muunga mkono, basi una matatizo katikati ya masikio!

Hao wabunge wa upinzani nao wako pale kushindana na serikali na ndiyo maana wanataka matangazo ya live ili waonekane,na kibaya kuna watu wanapenda kuona wabunge wao wakifanya fujo mule hata kama kwenye majimbo hakuna wanachofanya.
 
Sie wengine ambao wanasiasa hawajafanikiwa kutugawa katika hayo makundi yao mawili tunachokiona hapa ni kwamba hiyo serikali pamoja na hao wabunge wa upinzani wote wana ajenda zao tofauti na hoja wanazotoleana katika hili suala.

Na huo ndio ukweli.
 
Ni rahisi kumfukuza uliemkuta lakini ni vigumu kumfukura ulimteua mwenyewe ngoja tuone magufuli kama yupo na kama anasikia rais wa kufukuza aliowakuta
 
Back
Top Bottom