Unakuta serikali huwa inasisitiza watu wasikae mabondeni ila hawasikii.
Dah ndo maana naichukia dar
wanajenga na ofisi zao huko huko!Ndiyo maana wajanja wamekimbilia mbezi juu, makongo, goba, ....
Ccm inaingia vipi kwenye maeneo yanayotawaliwa na chadema?..
LEo ni majanga kila kona. Nilikuwa na kikao na DC bagamoyo. Nimefika mapinga daraja ukingo umekatika. Nimerudi nipite Tamco kibaha nakuta foleni kali Kibamba, naambiwa daraja la Kabila ya Mizani Kibaha nalo limekatika.eeeeheh.hayo yote ukandarasi wa KI CCM.
Inanisikitisha hata suala hili nalo mnaliingiza kwenye siasa, hasa kwa kuilaumu ccm utadhani wao ndio wana leta mvua. Ni mara ngapi watu wameambiwa watoke mabondeni hawataki kusikia? Hata kama chama unacho kitaka wewe kingekuwa madarakani ndio kingeweza kuzuia mafuriko? Jaribuni kufikiri kabla ya kuanza kuilaumu serikali moja kwa moja wakati taadhari iliishatolewa, ukizingatia mamlaka za hali ya hewa ziliisha tangaza kwa kipindi hichi kutakuwa na mvua kubwa mpaka mwezi wa tano, mka wapuuzia na kudhani ni wango kama mlivyo zoea kawaida yenu mpaka muone madhara ndio muamini. Poleni nyote mliokumbwa na mafuriko,tumuombe mungu atuepushe na yote pia tukumbuke mungu yupo tumejisaha sana na ndio maana anatukumbusha kwa staili hii.kinachosikitisha makosa haya yaliyofanyika jangwani yanaendelea kufanyika mbezi, kimara na ubungo wananchi kujenga kwenye mikondo ya mito like there is no city planner
hii mbaya sana
ni madhara ya kuendelea kuweka CCM madarakani
ata uje na greda sitoki bondeni raha sana pia bondeni karibu na mjini