Welsaid, hata hivyo si serikali tu ya kulaumiwa, wananchi ndio wenye kubeba zaidi lawama pamoja na udhaifu wa serikali. Binafsi ninapohitaji kujenga huwa ninaangalia mengi likiwemo hilo la mafuriko.
Nilitafuta kiwanja cha kujenga Morogoro, nikapata serikalini bila taabu cha low density, kilikuwa kipindi cha kiangazi ambapo maeneo mengi yamepimwa sehemu hiyo. Lakini nilipofanya uchunguzi wa kina niliona kiwanja hicho kina mchanga mwingi sana na katikati kumepita mkondo unaoonyesha dalili kipindi cha masika kuna maji yatokayo mlimani yanapita hapo kwa kasi. Pamoja na kwamba niliridhia kiwanja hicho lakinin nikabadili nia na kukiacha auziwe mwingine sababu ya dalili nyingi za mafuriko ingawa ni ya kupita kwa muda kwa kuwa kiko kwenye muinuko kidogo.
Anayesumbuliwa na mafuriko si serikali bali ni yeye aliyeamua kujenga hapo, hivyo makosa ni pande zote.
Wazee wa Jangwani Meli hiyoooooo..uwanja lazima kabla ya Mwkt Manji kustaaf
Hahahahaha,huu ndio wakati muafaka wa kununua kiwanja dar,mambo ya kuuzia kiwanja wakati wa kiangazi sio
usilaumu chama(CCM),hizi picha inabidi zitengeneze tangazo la kuhamasisha watu kuhama mabondeni.
hivi pale shoppers ni bondeni au tatizo ni infrastructures???
aiseee hii hatari sana naona nyumba kibao ziko majini hapo.
Huu ndio muda sahihi wa kwenda kuangalia maeneo ya kununua viwanja ili usije ukauziwa mbuzi kwenye kiroba.
Acha tuu hii mvua adabu kwangu Maji yalijaa balaa kila kitu kimelowana
Tokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbali mbali ya Dar es Salaam, zimepelekea uharibufu wa barabara na mazingira.
Haya ni maeneo ya jiji la Dar es Salaam yaliyoathirika na mvua inayoendelea kunyesha na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi hasa wanaoishi bondeni au kwenye mkondo wa maji mfano mito.
![]()
![]()
Aprili 12, 2014
Duh hadi MUNGU ina abbreviation? kweli we mvivu kuandika.Poleni sana,mng awasaidie
Kuna wakati aliekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mzee Makamba aliwakemea watu wanojenga kwenye mabonde,namnukuu "hivi nyie watu mnaopenda kujenga kwenye mabonde ya mito mmekuwa vyura?" Tatizo hapa sio CCM, tatizo ni watanzania tumekuwa wabishi, hatuwasikilizi viongozi wetu mpaka maafa yatokee ndo tunaanza kuliaumu serekali! Walishaambiwa siku nyingi hawa lakini wamekuwa viziwi na sasa wanavuna walichokipanda. Ukweli ndo huo na unauma.
Hapana, nyumba hazipo majini, maji ndo yapo nyumbani