Mkuu kufuta sifuri hakuwezi kuipandisha thamani ya pesa ya nchi fulani dhidi ya dola. Kuna vitu kama vile exports na imports zenu katika nchi zinachangia sana. Ingekuwa hivyo zimbabwe kipindi ya mwisho cha Mugabe wangeweza kufanya hivyo.Wazambia walifuta sifuri kadhaa kutoka kwenye Kwacha yao.
Hilo linakuonesha kwamba, thamani ya pesa haina maana ya uchumi mzuri.
Hata sisi tunaweza kuondoa sifuri tatu kwenye shilingi yetu, dola moja ya kimarekani iwe shilingi mbili na ushee.
Tunaweza kufanya hilo leo.
Lakini, hilo halitamaanisha kuwa uchumi wetu utaimarika mara elfu.