Tomorrow is jus a phenomenon...!tomorrow never existed...!!! Mtia nia
Umefikiri mbali sana,na kwa 99.99% umenigusa
Kimwili hapana kiroho ndio
Si kweli mkuu! Ingekua hivyo hivi Jk Nyerere angevumilia huu upuuz wa ccm? Mayatima wanavyoonewa hivi yani wazazi wanaona(ktk roho) alafu wanawaacha tu?
Roho hazikai duniani bro, huyo ni shaitwan tu mtu akishakufa rohi hurudi kwa aliyetoa pumzi na mwili ndio unazikwa
Mi nashukuru iliisha salama kabisaaa bila figisu,maana marehemu alikua lofa,so hakukua na mgaoWaafrika hasa wabantu tunasumbuliwa sana na mirathi. Ni namshukuru Mungu ya kwetu iliisha salama japo kwa timbwili kidogo.
Chanzo kikubwa ni utegemezi wa (bread winner mmoja katika familia).
Mizimu ya Kiafrika huwa inatenda, sio kama Yesu wa kubumba ambae hana miujiza yoyote.Madame B
Wamewaza vyema kuwafuateni wangejaribu kwenda kwa sangoma wangeisoma au pengine walijaribu wakaambiwa huu ni mziiki mnene
Na hii inathibitisha kuwa roho zinaishi na ziko hapahapa duniani pamoja nasi
Dawa ni kuacha mali zote ziwe za msikiti au kanisa. ...siku inasomwa mirathi wanabaki wanatoa machoSio wote wako hivyo wengine wanasubiri uzimike ili warithi
uwiii ...mshana jr uko sahihi.
Bibi kafariki kaacha nyumba kubwa sana.
Kaacha watoto wawili tu, marehemu mama yangu na mjomba wangu ambae yuko hai.
Yaani huwezi amini, upande wa wakwe wa mjomba yaani wazazi wa shangazi mke wa mjomba wanaitaka ile nyumba maana wamekuja kukaa,kwani inakalika, wakilala usiku ni mijeredi kwa kwenda mbele.
Wapangaji hawakai, usiku taa zinajiwasha zenyewe...ukiweka umeme wa 50,000 kesho yake unakuta 0.00.
Ukisahau pesa juu ya meza unakuta imeliwa na panya japo tuna uhakika panya hakuna.
Ni juzi tu wametufuata sie wajukuu eti tuwaambie bibi yetu alipandikiza nini ndani ya nyumba (sisi wajukuu wa mwanae wa kike ndio tulikuwa tunaelewana sana na bibi).
Tukawaambia bibi kasema mtoke...mbona sie tukikaa hatupati mauzauza?
Sasa wametoka na nyumba iko shwari, ila wakiingia tu wakwe wa mjomba....ngoma inogile mpaka lyamba.
Ajabu sasa, watoto wa mjomba wakija wanasema wanamuona bibi kakaa kwenye kiambaza katanua mikono ili wasiingie ndani lakini tukija wajukuu sisi wa upande wa mwanae wa kike, wala hatuoni kitu na tunaweza lala usingizi mzuri tu.
Urithi huu....muusikie kwenye bomba tu.