Pepo baya kwenye mirathi, limepukutisha wengi

Pepo baya kwenye mirathi, limepukutisha wengi

Mi nafikiri hizo haunted houses nyingi huwa wenye nyumba wanauwawa ili ndugu wagawane mirathi.
Hii inasababisha nyumba kutokalika kwa dhulma ya kutoa roho ya mtu
 
mshana jr uko sahihi.

Bibi kafariki kaacha nyumba kubwa sana.

Kaacha watoto wawili tu, marehemu mama yangu na mjomba wangu ambae yuko hai.

Yaani huwezi amini, upande wa wakwe wa mjomba yaani wazazi wa shangazi mke wa mjomba wanaitaka ile nyumba maana wamekuja kukaa,kwani inakalika, wakilala usiku ni mijeredi kwa kwenda mbele.

Wapangaji hawakai, usiku taa zinajiwasha zenyewe...ukiweka umeme wa 50,000 kesho yake unakuta 0.00.

Ukisahau pesa juu ya meza unakuta imeliwa na panya japo tuna uhakika panya hakuna.

Ni juzi tu wametufuata sie wajukuu eti tuwaambie bibi yetu alipandikiza nini ndani ya nyumba (sisi wajukuu wa mwanae wa kike ndio tulikuwa tunaelewana sana na bibi).

Tukawaambia bibi kasema mtoke...mbona sie tukikaa hatupati mauzauza?

Sasa wametoka na nyumba iko shwari, ila wakiingia tu wakwe wa mjomba....ngoma inogile mpaka lyamba.

Ajabu sasa, watoto wa mjomba wakija wanasema wanamuona bibi kakaa kwenye kiambaza katanua mikono ili wasiingie ndani lakini tukija wajukuu sisi wa upande wa mwanae wa kike, wala hatuoni kitu na tunaweza lala usingizi mzuri tu.

Urithi huu....muusikie kwenye bomba tu.


Duuuh huo uchawi noma hadi kwenye umeme tena wa Luku,muhongo akisikia sijui ata comment vipi?
 
Baba Mdogo aliuza eneo la urithi la home kabisa alilopewa na Babu yake. Kwa kabila lake kithumu/itongo huwa hakiuzwi. maza akamkataza na kumwambia sio vizuri. siku alopokea hela hakulala kabisa usiku akamuona Babu yake kwenye maruerue anamkimbiza. Siku zote alizokaa na zile hela alikuwa anamuota Babu yake. Mbona alienda kurudisha hela kwa aliyemuuzia
 
Mm nmeitwa na baba mdogo anipe sehemu ya shamba lake japo baba yangu kipindi anaumwa nilmwambia nataka kumtafuta baba mdogo aje ila baba alikataa akaniambia uachane nae hutampata! Baada ya baba kufariki nikaja kukutana nae. Siku hz ananisisitiza niende anipe sehemu ya shamba lake ila mm moyo wangu umekuwa mzito xana wa kwenda. Kila siku namwambia nitakuja. Xx sjuh nifanyeje @mshana jr
 
Mm nmeitwa na baba mdogo anipe sehemu ya shamba lake japo baba yangu kipindi anaumwa nilmwambia nataka kumtafuta baba mdogo aje ila baba alikataa akaniambia uachane nae hutampata! Baada ya baba kufariki nikaja kukutana nae. Siku hz ananisisitiza niende anipe sehemu ya shamba lake ila mm moyo wangu umekuwa mzito xana wa kwenda. Kila siku namwambia nitakuja. Xx sjuh nifanyeje @mshana jr
Listen to your heart.. Hata ukienda nenda Kwa kujiandaa
 
uwiii ...
Nna rafiki yangu bibi yake mzaa mama aliacha nyumba,sasa wakaja babu zake wanataka khidhulumu,akanambia ataenda kwa mganga ile nyumba isiuzwe,yeyote akija akitaka kuinunua aishie kuiangalia tu,nyumba ipo Mwananyamala.
Hizi mambo bwana @mshana jr kweli zinarun down the streets
...huyo mganga hawezi fanya yake na sie watu wa Mkwajuni tusalimike?!!
...wiki moja tu imebaki,wafilisti wanatujia!
 
katika maisha yangu mimi sitaki mambo ya mirathi kabisa,sisi kwetu tumezaliwa saba mzee ananyumba zake hapa dar 2,mwanza 1,singida 1,rukwa 1 na shinyanga 1,nasikia tu ndugu zangu wakizisema,mimi hata kukanyaga huko sijawahi na wala sitaki,sasa hivi nina 32yrs old nimebahatika kujenga nyumba yangu kinyerezi,na nyingine ipo kozi ya kumi,najikusanya niimalizie,ya nini kugombea mali za watu,ukiona watu wanashabikia mambo hayo ujue ni ishara za uvivu,na kupenda vya bure.
Mkiwa na mirathi kwenye familia/ukoo wenu na ikaisha kwa amani na salama ni jambo la kumshukuru Mungu sana.

Niandikapo mada hii leo hii kuna kesi nyingi mahakamani zinazoendelea lakini walioteuliwa kusimamia mirathi hiyo wakikwepa kwenda kwakuwa watangulizi wao wa mirathi hiyo hiyo walikufa kwa namna za ajabu ajabu kabisa.

Mirathi mibaya kabisa inayoteketeza na kutesa wengi ni mirathi ya nyumba, kuna nyumba nyingi tu mpaka leo hazikaliki kisa mirathi, asipokufa mtu basi yeyote atakayelala tu nyumba hiyo ni mauzauza tupu kama si kucharazwa viboko usiku mzima basi utatokewa na vitu vya ajabu ajabu vyenye kutisha mno.

Haya mambo yanahusisha na roho na mapepo mabaya kwa asilimia kubwa sana na roho ya marehemu mhusika ikihusishwa na kuhusika moja kwa moja lakini pia kwa baadhi ya kesi uchawi ukihusika pia.

Kama nilivyosema kuwa nguvu ya giza haitibiki kwa nguvu ya giza wala kwa sheria za binadamu ni vema mambo ya mirathi yakatatuliwa kwa kupewa haki mhusika ambaye kwa mazingira ya kawaida anaonekana ndio kadhulumiwa na mara nyingi huwa ni wanawake wajane watoto wa kambo au ndugu wasio na uwezo lakini kwa utashi wa marehemu akawachagua wao kurithi mali zake.

Kuna kesi moja ya mtu wangu wa karibu kabisa inayohusu mirathi imeshapukutisha watu wanne mpaka sasa akiwemo baba yake mzazi. kisa? Babu yake mzaa baba aliuza nyumba kwa housegirl wake bila maandishi na baada ya kufariki dada wa marehemu akiwa na documents zote muhimu akadai nyumba aliachiwa na kaka yake.

Cha marehemu acheni kibaki cha marehemu hasa nyumba na mkishahisi tatizo tokeni kabisa kwenye taratibu za kisheria za kidunia na mambo ya giza!!mtaishia kumalizana tu.

Kisheria mnaweza kushinda kesi kutokana na nyaraka na wakili na Rushwa lakini baada ya hapo jueni fika kwamba nyumba hiyo haitakalika na pengine haitauzika na ikitokea ikauzika hamtakaa mfaidi hiyo pesa!mabalaa yatawaandameni mwanzo mwisho.

Mkiamua kutumia nguvu za giza ndio shetani atashangilia hasa mtauana mpaka mmalizane.

Cha muhimu na cha lazima kufanya ni kuangalia uhalisia na ukweli ulipo na kumpa anayestahili hata kama ni ghorofa la bei kubwa ili muweze kupona na laana ya mirathi.
 
Akili nyingi za waafrika wengi zimejikita penye mirathi.Yaani unatafuta mali kuna ndg zako wanakuwa anamuheshimu mkeo kinafiki siku umezimika wanamtimua nyumbani yaani hapana nawachukia sana wanaosubiri penalty.
 
Akili nyingi za waafrika wengi zimejikita penye mirathi.Yaani unatafuta mali kuna ndg zako wanakuwa anamuheshimu mkeo kinafiki siku umezimika wanamtimua nyumbani yaani hapana nawachukia sana wanaosubiri penalty.
Ndugu wamefanyiana mambo machafu kwasababu ya mirathi wengine wameuana na hata kuwaua wazazi
 
Ndugu wamefanyiana mambo machafu kwasababu ya mirathi wengine wameuana na hata kuwaua wazazi
Inakera sana unabaki unajiuliza waqt wa marehemu kuna baadhi ya ndugu walikuwa hawatii timu hapo unawaza watu wangapi maisha yao yameharibika baada ya wazazi wao kufariki na walikuwa na uwezo?
Kishorn wanakuja watu ambao hawakushiriki penye kilimo unawakuta penye mavuno!
 
Nna rafiki yangu bibi yake mzaa mama aliacha nyumba,sasa wakaja babu zake wanataka khidhulumu,akanambia ataenda kwa mganga ile nyumba isiuzwe,yeyote akija akitaka kuinunua aishie kuiangalia tu,nyumba ipo Mwananyamala.
Hizi mambo bwana @mshana jr kweli zinarun down the streets
Kuna nyumba ipo block 41 kinondoni,ukipanga umo nasikia usiku utakula bakora na vifinjo na vibao vya hatari!warithi walizulumiana basi mmoja akasema hatoishi mtu humo mpk wa leo.
 
Back
Top Bottom