Pepo baya kwenye mirathi, limepukutisha wengi

Pepo baya kwenye mirathi, limepukutisha wengi

Nakubalia nawe 101%, haki ya mtu ya mirathi mwachiii....Nyumba zingine huwa zinawaka moto na kuua.... KEMEA PEPO men
 
tatizo watu hawapendi kutafuta vyao. wanasubiri watu wafe wao walimiliki mali za marehemu. tena wengine wanadhulumu mpaka watoto wa marehemu
 
ktk mambo hayo probate and administration of estates Act na Rules zinatoa namba mbalimbali za mgawanyo na sheria mf. islamic,Indian,succession Act nk mambo huwa mabaya pale inapokuwa under customary law,
Fafanua kidogo hapo The Don
 
Last edited by a moderator:
tatizo watu hawapendi kutafuta vyao. wanasubiri watu wafe wao walimiliki mali za marehemu. tena wengine wanadhulumu mpaka watoto wa marehemu

Kumbuka pia wapigaji pia wako kila mahali hata hapa jamvini wapo....!!!
 
Haya sasa....... Madame B na mshana jr mnadhani mmeniweza leo........?.......imekula kwenu........nimeshikiliwa saa hizi nisiogope nilale.........
 
Last edited by a moderator:
Hahahahaaaaaaa Preta hii post ni ya asubuhi mbona?

Aaaah wapi nyie.......asubuhi mbona sikuiona........?......uilete usiku huu......Ili nihisi nipo kwenye haunted house......useme ilikuwa asubuhi.........hi hi hi........siogopi ng'oo..........
 
Aaaah wapi nyie.......asubuhi mbona sikuiona........?......uilete usiku huu......Ili nihisi nipo kwenye haunted house......useme ilikuwa asubuhi.........hi hi hi........siogopi ng'oo..........

Hahahahaaaaaaa
cc: Madame B
 
Last edited by a moderator:
ukitaka maisha yako kuweka rehani kirahisi penda kusogelea mirathi,
 
ukitaka maisha yako kuweka rehani kirahisi penda kusogelea mirathi,

Mi nadhani kuna haja ya kuwajengea dhana watoto ya kutotegemea kabisa wala kuiwaza Mali yako mzazi.maana usipokuwa makini wanaweza wakakutanguliza wakiona huondoki.

Hii iwafanye hata siku mmoja unampa shamba,mwingine baiskeli achukulie ni kama ukumbusho tu sio mali kuzidi alizonazo mwenyewe.
 
Madame B



Na hii inathibitisha kuwa roho zinaishi na ziko hapahapa duniani pamoja nasi


Si kweli mkuu! Ingekua hivyo hivi Jk Nyerere angevumilia huu upuuz wa ccm? Mayatima wanavyoonewa hivi yani wazazi wanaona(ktk roho) alafu wanawaacha tu?

Roho hazikai duniani bro, huyo ni shaitwan tu mtu akishakufa rohi hurudi kwa aliyetoa pumzi na mwili ndio unazikwa
 
Last edited by a moderator:
Umaskini ndio shina la hizi mambo, mtu 1 akiwa vzr baasi akifa huyo wananzengo wote wataka kupata kitu
 
Si kweli mkuu! Ingekua hivyo hivi Jk Nyerere angevumilia huu upuuz wa ccm? Mayatima wanavyoonewa hivi yani wazazi wanaona(ktk roho) alafu wanawaacha tu?

Roho hazikai duniani bro, huyo ni shaitwan tu mtu akishakufa rohi hurudi kwa aliyetoa pumzi na mwili ndio unazikwa

Kaka Nyerere hawezi kudili na ccm yote kwa wakati mmoja kwakuwa ni roho moja kwa nyingi ni kitu kigumu mno...!Sanasana laana na maono yake ndio vinafanya kazi kwasasa na ccm ndio hiyo inaenda harijojo

Ishu ya mayatima kuonewa ni sehemu ya mateso mengi ya mwanadamu hii ni mada pana sana kuna sababu nyingi tu kwenye hili na wale wanaowaonea hujitengenezea moto wao wenyewe

Roho zipo hapahapa duniani mpaka siku ya kiama nimeelezea vizuri tu kuhusu hili kwenye ile mada ya roho zinazotangatanga
 
Bora ya mimi zaidi ya sura zikurithi chochote kwa baba yangu
Kuna jamaa 2 baada ya baba yao kufariki wwaliuza nyumba lakini miezi 3 mbali hakukua na mwenye hali nzuri hata 1, mmoja alianza matanuzi umbali wa mita 10 ana kodi tax, yaani kila aina ya starehe alifanya, akaona haitoshi akahamia dar, mwezi mmoja baadae tukambiwa alizikwa na jiji. Kaka yake akanunua nyumba nyingine,pikipiki,mashine za kufanyia kazi zake na kamuwezesha jamaa yake kwa biashara, lakini si yeye wala huyo jamaa yake mwenye hali nzuri.alianza na kuweka bondi nyumba imeenda kwa laki 3 vimashine vyote kauza pikipiki kauza ofisi kauza saivi anakunywa viroba tu! Wengi tu nina ushuhuda nao wamepata madhara na mambo ya mirathi haya.
 
mshana jr uko sahihi.

Bibi kafariki kaacha nyumba kubwa sana.

Kaacha watoto wawili tu, marehemu mama yangu na mjomba wangu ambae yuko hai.

Yaani huwezi amini, upande wa wakwe wa mjomba yaani wazazi wa shangazi mke wa mjomba wanaitaka ile nyumba maana wamekuja kukaa,kwani inakalika, wakilala usiku ni mijeredi kwa kwenda mbele.

Wapangaji hawakai, usiku taa zinajiwasha zenyewe...ukiweka umeme wa 50,000 kesho yake unakuta 0.00.

Ukisahau pesa juu ya meza unakuta imeliwa na panya japo tuna uhakika panya hakuna.

Ni juzi tu wametufuata sie wajukuu eti tuwaambie bibi yetu alipandikiza nini ndani ya nyumba (sisi wajukuu wa mwanae wa kike ndio tulikuwa tunaelewana sana na bibi).

Tukawaambia bibi kasema mtoke...mbona sie tukikaa hatupati mauzauza?

Sasa wametoka na nyumba iko shwari, ila wakiingia tu wakwe wa mjomba....ngoma inogile mpaka lyamba.

Ajabu sasa, watoto wa mjomba wakija wanasema wanamuona bibi kakaa kwenye kiambaza katanua mikono ili wasiingie ndani lakini tukija wajukuu sisi wa upande wa mwanae wa kike, wala hatuoni kitu na tunaweza lala usingizi mzuri tu.

Urithi huu....muusikie kwenye bomba tu.

Hizi extended families za Africa sasa ni too much, how come wakwe za mjomba waje waishi kwny nyumba ya bibi yenu? Aibu kubwa!

Lakini Madame B hivi kweli haya mambo ya mauza uza (magic) yapo kweli au ni story tu?:sly:
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom