Pepo baya kwenye mirathi, limepukutisha wengi

Pepo baya kwenye mirathi, limepukutisha wengi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
373,200
Reaction score
864,574
Mkiwa na mirathi kwenye familia/ukoo wenu na ikaisha kwa amani na salama ni jambo la kumshukuru Mungu sana.

Niandikapo mada hii leo hii kuna kesi nyingi mahakamani zinazoendelea lakini walioteuliwa kusimamia mirathi hiyo wakikwepa kwenda kwakuwa watangulizi wao wa mirathi hiyo hiyo walikufa kwa namna za ajabu ajabu kabisa.

Mirathi mibaya kabisa inayoteketeza na kutesa wengi ni mirathi ya nyumba, kuna nyumba nyingi tu mpaka leo hazikaliki kisa mirathi, asipokufa mtu basi yeyote atakayelala tu nyumba hiyo ni mauzauza tupu kama si kucharazwa viboko usiku mzima basi utatokewa na vitu vya ajabu ajabu vyenye kutisha mno.

Haya mambo yanahusisha na roho na mapepo mabaya kwa asilimia kubwa sana na roho ya marehemu mhusika ikihusishwa na kuhusika moja kwa moja lakini pia kwa baadhi ya kesi uchawi ukihusika pia.

Kama nilivyosema kuwa nguvu ya giza haitibiki kwa nguvu ya giza wala kwa sheria za binadamu ni vema mambo ya mirathi yakatatuliwa kwa kupewa haki mhusika ambaye kwa mazingira ya kawaida anaonekana ndio kadhulumiwa na mara nyingi huwa ni wanawake wajane watoto wa kambo au ndugu wasio na uwezo lakini kwa utashi wa marehemu akawachagua wao kurithi mali zake.

Kuna kesi moja ya mtu wangu wa karibu kabisa inayohusu mirathi imeshapukutisha watu wanne mpaka sasa akiwemo baba yake mzazi. kisa? Babu yake mzaa baba aliuza nyumba kwa housegirl wake bila maandishi na baada ya kufariki dada wa marehemu akiwa na documents zote muhimu akadai nyumba aliachiwa na kaka yake.

Cha marehemu acheni kibaki cha marehemu hasa nyumba na mkishahisi tatizo tokeni kabisa kwenye taratibu za kisheria za kidunia na mambo ya giza!!mtaishia kumalizana tu.

Kisheria mnaweza kushinda kesi kutokana na nyaraka na wakili na Rushwa lakini baada ya hapo jueni fika kwamba nyumba hiyo haitakalika na pengine haitauzika na ikitokea ikauzika hamtakaa mfaidi hiyo pesa!mabalaa yatawaandameni mwanzo mwisho.

Mkiamua kutumia nguvu za giza ndio shetani atashangilia hasa mtauana mpaka mmalizane.

Cha muhimu na cha lazima kufanya ni kuangalia uhalisia na ukweli ulipo na kumpa anayestahili hata kama ni ghorofa la bei kubwa ili muweze kupona na laana ya mirathi.
 
mshana jr uko sahihi.

Bibi kafariki kaacha nyumba kubwa sana.

Kaacha watoto wawili tu, marehemu mama yangu na mjomba wangu ambae yuko hai.

Yaani huwezi amini, upande wa wakwe wa mjomba yaani wazazi wa shangazi mke wa mjomba wanaitaka ile nyumba maana wamekuja kukaa,kwani inakalika, wakilala usiku ni mijeredi kwa kwenda mbele.

Wapangaji hawakai, usiku taa zinajiwasha zenyewe...ukiweka umeme wa 50,000 kesho yake unakuta 0.00.

Ukisahau pesa juu ya meza unakuta imeliwa na panya japo tuna uhakika panya hakuna.

Ni juzi tu wametufuata sie wajukuu eti tuwaambie bibi yetu alipandikiza nini ndani ya nyumba (sisi wajukuu wa mwanae wa kike ndio tulikuwa tunaelewana sana na bibi).

Tukawaambia bibi kasema mtoke...mbona sie tukikaa hatupati mauzauza?

Sasa wametoka na nyumba iko shwari, ila wakiingia tu wakwe wa mjomba....ngoma inogile mpaka lyamba.

Ajabu sasa, watoto wa mjomba wakija wanasema wanamuona bibi kakaa kwenye kiambaza katanua mikono ili wasiingie ndani lakini tukija wajukuu sisi wa upande wa mwanae wa kike, wala hatuoni kitu na tunaweza lala usingizi mzuri tu.

Urithi huu....muusikie kwenye bomba tu.
 
Madame B


Wamewaza vyema kuwafuateni wangejaribu kwenda kwa sangoma wangeisoma au pengine walijaribu wakaambiwa huu ni mziiki mnene
Na hii inathibitisha kuwa roho zinaishi na ziko hapahapa duniani pamoja nasi
 
Last edited by a moderator:
Waafrika hasa wabantu tunasumbuliwa sana na mirathi. Ni namshukuru Mungu ya kwetu iliisha salama japo kwa timbwili kidogo.
Chanzo kikubwa ni utegemezi wa (bread winner mmoja katika familia).
 
Wamewaza vyema kuwafuateni wangejaribu kwenda kwa sangoma wangeisoma au pengine walijaribu wakaambiwa huu ni mziiki mnene
Na hii inathibitisha kuwa roho zinaishi na ziko hapahapa duniani pamoja nasi

Kabisa...
Kwa maana nakumbuka kauli ya mmoja wa mtoto wa mjomba alisema kuwa "bibi akifariki, nyumba nitairithi mie"....naona alipata nguvu kwa kuwa alijiona yeye ni mtoto wa kwanza kwa mjomba ambae ndio pekee aliyebaki baada ya mama yetu kufariki....sasa kunakalika sasa.
Kiranga komooooo!!!!!

Yaani imefikia hatua mpaka kodi za mafremu wakichukua, kama wamechukua laki 6, wakiziweka asubuhi wanakuta imebaki 10,000/=
Ila tukichukua sisi upande wa mwanae wa kike, hakuna shaka.
Hii nyumba kula kwa tindo anaijua, House Wife nae anaijua...na wala situngi hii story
 
Last edited by a moderator:
solution ya yote andikeni urithi mnapokufa inapunguza migogoro,Mali nyingi zilizogawanywa kwa njia hiyo(testate) haina migogoro kama ya (intestate), sheria ituongozayo ktk mambo hayo probate and administration of estates Act na Rules zinatoa namba mbalimbali za mgawanyo na sheria mf. islamic,Indian,succession Act nk mambo huwa mabaya pale inapokuwa under customary law,hii ni kutokana na ukweli kuwa customs nyingi huusisha mila na ibada za jadi zenye matambiko na kafara nyingi ndio maana wale waigombaniayo mirathi ile huumia kwa kutokujua misingi yake.
 
solution ya yote andikeni urithi mnapokufa inapunguza migogoro,Mali nyingi zilizogawanywa kwa njia hiyo(testate) haina migogoro kama ya (intestate), sheria ituongozayo ktk mambo hayo probate and administration of estates Act na Rules zinatoa namba mbalimbali za mgawanyo na sheria mf. islamic,Indian,succession Act nk mambo huwa mabaya pale inapokuwa under customary law,hii ni kutokana na ukweli kuwa customs nyingi huusisha mila na ibada za jadi zenye matambiko na kafara nyingi ndio maana wale waigombaniayo mirathi ile huumia kwa kutokujua misingi yake
The Don nimejifunza kitu kutoka kwako
 
Last edited by a moderator:
Navyojua roho ya marehemu huwa inarudi kutembelea nyumbani kwake mara kwa mara, sasa akikuta mambo ya ajabu ndo kinanukaa...bora mdhulumu mali nyingine lakini sio nyumba.
 
Navyojua roho ya marehemu huwa inarudi kutembelea nyumbani kwake mara kwa mara, sasa akikuta mambo ya ajabu ndo kinanukaa...bora mdhulumu mali nyingine lakini sio nyumba.

Kim nana sio nyumba tu, hata kwa baadhi ya vyombo vya usafiri au wanyama.

Hii njia kama unaelekea Mkwajuni...kuna Toyo imepaki mwaka wa 3 huu...nasikia mwenye nayo alifariki...mrithi akaiuza, weee, imeua watu 3, mpaka leo imepaki tu.
ila cha ajabu, kila ukiikuta ni safi na anayeisafisha hajulikani.
 
Last edited by a moderator:
mshana jr uko sahihi.
Bibi kafariki kaacha nyumba kubwa sana.
Kaacha watoto wawili tu, marehemu mama yangu na mjomba wangu ambae yuko hai.

Yaani huwezi amini, upande wa wakwe wa mjomba yaani wazazi wa shangazi mke wa mjomba wanaitaka ile nyumba maana wamekuja kukaa,kwani inakalika, wakilala usiku ni mijeredi kwa kwenda mbele.
Wapangaji hawakai, usiku taa zinajiwasha zenyewe...ukiweka umeme wa 50,000 kesho yake unakuta 0.00.
Ukisahau pesa juu ya meza unakuta imeliwa na panya japo tuna uhakika panya hakuna.

Ni juzi tu wametufuata sie wajukuu eti tuwaambie bibi yetu alipandikiza nini ndani ya nyumba (sisi wajukuu wa mwanae wa kike ndio tulikuwa tunaelewana sana na bibi)
Tukawaambia bibi kasema mtoke...mbona sie tukikaa hatupati mauzauza?
Sasa wametoka na nyumba iko shwari, ila wakiingia tu wakwe wa mjomba....ngoma inogile mpaka lyamba.
Ajabu sasa, watoto wa mjomba wakija wanasema wanamuona bibi kakaa kwenye kiambaza katanua mikono ili wasiingie ndani lakini tukija wajukuu sisi wa upande wa mwanae wa kike, wala hatuoni kitu na tunaweza lala usingizi mzuri tu.

Urithi huu....muusikie kwenye bomba tu.

Madame B, ile nyumba yetu ya Ntwara?
 
Last edited by a moderator:
Mmmh hii thread itanifanya nisilale bure mie maana imekaa kichawichawi. Haya ndo mambo ya MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
Waafrika hasa wabantu tunasumbuliwa sana na mirathi. Ni namshukuru Mungu ya kwetu iliisha salama japo kwa timbwili kidogo.
Chanzo kikubwa ni utegemezi wa (bread winner mmoja katika familia).

Kama ndugu wote mnaelewana hakuna shaka..ila akijitokeza mtu tu na ambaye nae ana uhalali wa mali akapinga, hapo ndo picha linapoanza
 
Back
Top Bottom