Penzi lenye Maumivu

PENZI LENYE MAUMIVU-07
Juma Hiza
0712988278

“Mume wangu uko wapi mtoto amezidiwa huku,” aliniambia Lillian nilipokuwa nikizungumza naye kwenye simu. Wakati huo nilikuwa na Getrude nyumbani kwake.
“Sasa kama amezidiwa si umpeleke hospitali au unataka mpaka nikuitie Ambulance,” nilimwambia kisha nikakata simu, sikutaka kusikia habari za Brighton katika masikio yangu, niliamini hakuwa ni mwanangu hivyo lolote ambalo lililokuwa likimtokea sikuonekana kujali.
“Kuna nini mbona umekata simu?” aliniuliza Getrude baada ya kuona nimekata simu kwa hasira.
“Hakuna kitu mke wangu,” nilimjibu kisha nikatabasamu kuonyesha kuwa nipo sawa lakini Getrude bado alionekana kuwa na wasiwasi.
“Umekata simu lakini?” aliniuliza.
“Ndiyo kuna mtu amenitibua,” nilimjibu.
“Ni nani?”
“Achana naye tuendelee kuzungumza ya kwetu.”
“Niachane naye wakati bado sijamfahamu halafu mbona kama alikuwa anakupa taarifa za mgonjwa?”
“Yeah ni kweli lakini ni mtu amewrong namba,” nilimjibu kisha akaniamini, ule wasiwasi ambao ulionekana kumuingia ukaondoka.
Nilimpenda Getrude kwasababu tayari alikuwa na ujauzito wangu, mapenzi ambayo nilitakiwa kumpa mke wangu Lillian yote niliyahamishia kwake, alikuwa ni mchepuko wangu lakini niliishi naye maisha kama ya mume na mke.
Ingawa kwa upande wa mke wangu Lillian nilimkataza kufanya biashara wala kujishughulisha na chochote lakini kwa Getrude nilikuwa tofauti na msimamo wangu, yeye nilimpa uhuru, nilihakikisha namfungulia biashara na kumtimizia kila alichokuwa akikihitaji. Maisha ya furaha ndiyo ambayo yalikuwa yametawala.
“Nitarajie nini?” aliniuliza huku akiyarembua macho yake, kitendo hicho kikanifanya nizidi kumuona mrembo kushinda mke wangu.
“Tarajia mazuri tena yatakayokufurahisha na kukusisimua mwili,” nilimjibu kisha nikambusu katika tumbo lake.
“Yapi hayo?” aliniuliza huku akionekana kukasirika.
“Ni surprise,” nilimjibu.
“Nataka uniambie bhanaa,” aniliambia huku akiwa ameuvuta mdomo wake, nikatabasamu.
“Nini?”
“Hivi unajua kuwa u mzuri mno, unavutia kila kitu, hisia zangu zinaniambia kama utanizalia jike basi atakuwa mrembo atakayewatetemesha wengi na katika maisha yake atakuja kuwa mrembo wa dunia,” nilimwambia maneno yaliyomfanya akacheka.
“Na kama dume je?”
“Atakuwa handsome kiufupi naye atasumbua sana,” nilimjibu.
Hicho kilikuwa ni kipindi cha maisha ya furaha kati yangu na Getrude. Licha ya kuwa nilimfungulia biashara ya duka la nguo, nilimnunulia nyumba pamoja na gari la kifahari lakini bado nilimuahidi kumfanyia mambo makubwa katika maisha yake na yote hayo ni kwasababu alinibebea ujauzito, nilichokiamini ni kuwa asingeweza kunizalia mtoto mlemavu au mwenye matatizo yoyote kiafya.
****
Baada ya kupita siku tatu nilirudi nyumbani, ilikuwa ni kama dharura baada ya kusikia Brighton alikuwa ni mgonjwa tena alizidiwa. Nilimkuta mke wangu akiwa hana furaha kabisa, aliponiona machozi yakaanza kumdondoka. Nilionekana kuwa kama sababu ya kumtonesha kidonda kilichompa maumivu upya, hata hivyo sikuonekana kujali hilo.
“Imekuwaje kuhusu mtoto?” nilimuuliza swali ambalo lilionekana kuwa kama lenye kejeli maana siku hiyo ilikuwa siku ya nne baada ya kupewa taarifa za kuzidiwa kwake ambazo nilizipuuzia.
“Leo ndiyo unakumbuka kurudi nyumbani, leo ndiyo unakumbuka kuwa una mtoto, leo ndiyo unakumbuka kuulizia hali yake kweli Kelvin unajiona upo sahihi?” aliniuliza Lillian maswali ambayo kiukweli yaliniumiza moyoni lakini kutokana na sikuwa na mapenzi ya dhati kwake bado niliyapuuzia.
“Hujanijibu swali langu lakini…” nilimwambia.
“Kelvin nakuchukia sana wewe ni mwanaume katili, huna huruma wewe ni muuaji,” alizidi kunilaumu Lillian kiasi kwamba maneno yake nikaona kama dada wa kazi alikuwa akiyasikia, nilichoamua kukifanya niliondoka pale sebuleni nikaingia chumbani, hazikupita dakika chache Lillian naye akaingia, alikuwa amembeba Brighton.
“Mke wangu lakini kwanini unaanza kunilaumu wakati hujui huko nilipotoka nimekutana na nini?”
“Kelvin mume wangu najua unamchukia sana huyu mtoto kwasababu ya huu ulemavu wake lakini tambua hata mimi sikupenda kumzaa akiwa hivi isipokuwa ni mipango ya Mungu, umeshamkana huyu mtoto lakini hata ufanye nini bado atabaki kuwa ni damu yako,” aliniambia Lillian.
Maneno ya Lillian yalinifanya nijione kuwa mkosaji na kile nilichokuwa nikikifanya sikustahili kukifanya. Japokuwa moyoni mwangu sikuwa mwema kwake nikamuomba msamaha, akanisamehe, nikamuamisha kuwa nimebadilika na nisingerudia makosa ambayo tayari nilimkosea katika maisha yake.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa maisha mengine mapya ambayo niliyaanza na Lillian baada ya kumuomba msamaha na kuahidi kumpenda mwanangu Brighton na kumpa matunzo yote.
Hilo lilimfurahisha sana Lillian, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea katika maisha yake, aliamini maombi yake pamoja na kilio chake cha kila siku kilikuwa kimejibiwa.
****
Baada ya kupita miezi minne ujauzito wa Getrude uliharibika hivyo ilitakiwa atolewe kiumbe kilichopo tumboni na pia asafishwe kizazi chake. Hilo kwangu lilikuwa ni zaidi ya pigo, sikutaka kuamini kile kilichotokea. Kipindi hicho kikawa ni cha maumivu, hakukuwa kuna furaha kwani kila tulilolitarijia halikuweza kutokea.
Kutoka na imani ambayo nilikuwa nayo kwa Getrude sikutaka ujauzito huo ndiyo uwe sababu ya kumchukia, nilimuamini na kuahidi kuwa na yeye katika hali zote.
Hilo lililotokea nililichukulia kuwa kama ni changamoto za maisha, sikutaka wakati wa maumivu uchukue hatamu kubwa katika nyuso zetu, nilichokuwa nikikihitaji ni furaha hivyo nilichoamua kukifanya nilianza kumpeleka sehemu mbalimbali Getrude ili kuirudisha akili yake pamoja na mawazo yake yawe sawa kama zamani.
Kipindi hicho nakumbuka nilimuaga mke wangu kuwa nilipata safari za nje ya nchi kibiashara hivyo ningekuwa mbali na yeye kwa kipindi fulani. Kutokana na Lillian tayari aliniamini na kutokuwa na wasiwasi wowote juu yangu akanikubalia na kunipa baraka zote za safari njema bila kujua kuwa kumbe haikuwa ni safari ya kibiashara kama nilivyomuaga isipokuwa nilikuwa nikienda kutembea na Getrude nchi kama Afrika kusini, Marekani, Uingereza na Dubai.
Katika nchi zote tulizoenda makazi yetu yalikuwa ni ya hotelini, tulichukua chumba katika hoteli kubwa ya kifahari kisha tukayafurahia mapenzi yetu.
Baada ya kupita kipindi fulani tuliporudi Tanzania Getrude alipata ujauzito mwingine tena lakini kama ilivyokuwa ujauzito wa kwanza na huu pia uliharibika. Hilo lilizidi kuniumiza sikujua tatizo lilikuwa ni nini hasa.
Nilihisi kulikuwa na tatizo kwa upande wa Getrude ambalo lilisababisha mpaka mimba zote zikawa zinaharibika. Ilibidi nimuulize ni nini kilichokuwa kinasababisha lakini hata yeye alinijibu hafahamu kitu chochote. Hilo likazidi kunishangaza, sikutaka kuamini hilo hata kidogo.
“How come?” nilimuuliza.
“Mimi sifahamu kitu Kelvin.”
“Getrude kuna mchezo utakuwa unanichezea haiwezekani.”
“Mchezo gani huo Kelvin inamaana hata daktari pia humuamini?” aliniuliza Getrude lakini sikutaka kumuelewa, nilishabadilika.
 
PENZI LENYE MAUMIVU-08
Mtunzi:Juma Hiza
Simu:0712988278

Kiukweli kila alichokuwa akinieleza Getrude kwa wakati huo hakikuniingia akilini kabisa, nilishaanza kuhisi kuna kitu alikuwa akinificha. Japokuwa majibu ya daktari yalionyesha kwamba ujauzito uliharibika kweli lakini sababu za kuharibika kwake hazikuniingia. Kichwa changu kilitawaliwa na mawazo lukuki, sikutaka kuamini kama kweli zile raha na starehe zote nilizompa kipindi cha ujauzito wake ndizo zilizofanya mpaka ukaharibika. Iliwezekanaje? Bado niliendelea kujiuliza maswali lakini sikupata jibu.
Nilipokuwa nikimuangalia Getrude niliziona pesa zangu, naweza kusema kati ya wasichana wote niliyotembea nao Getrude ndiye alikuwa msichana ambaye nilitumia naye pesa nyingi mno, ukiachilia tu kula starehe za hapa hapa Tanzania lakini pia nilisafiri naye kwenda nchi mbalimbali kula starehe, hayo yote niliyafanya huku nikiamini siku zijazo alikuwa akienda kunipa mtoto.
Nilichokigundua baada ya kufanya uchunguzi wangu wa haraka ni kwamba Getrude hakuwa akibeba ujauzito kama nilivyodhani, alinidanganya na alichokuwa akikifanya ni kuigiza kuwa amebeba ujauzito na kisha kuzitumia pesa zangu kwa ajili ya kumuhudumia mwanaume mwingine ambaye alikuwa ni mpenzi wake.
Hilo sikutaka kuamini, usaliti ndiyo ambao ulikuwa ukiendelea kwa wakati huo. Niliumia mno moyoni mwangu, katika maisha yangu hakukuwa kuna siku niliyowahi kuumia kama ilivyokuwa siku hiyo.
Ukweli ni kwamba Getrude alikuwa na mpenzi wake, mimi ndiye niliyeyaingilia mapenzi yao lakini nilipogundua alinificha bado niliona kama alinifanyia usaliti.
“Getrude! Sitaki kuamini hiki ninachokishuhudia. Unanisaliti?” nilimuuliza kwa sauti ya ukali, alikuwa akilia kwa wakati huo. Hakuwa na kitu cha kunieleza kingine zaidi ya kupiga magoti na kuanza kuniomba msamaha.
Kiukweli nilishindwa kumsamehe, kadri alivyokuwa akiniomba msamaha niliona kama ananipigia kelele masikioni mwangu, kwa hasira nikaamua kuondoka zangu nikamuacha akiendelea kulia.
Kilichokuwa kikiendelea katika moyo wangu ni maumivu makali, niliumia vibaya mno. Barabarani niliendesha gari kwa mwendo kasi, kichwani mwangu bado nilikuwa nikiendelea kujiuliza maswali juu ya usaliti ambao alinifanyia Getrude.
“No! siamini,” nilijisemea huku nikiupigapiga usukani kwa hasira, nilionekana kuwa kama mtu niliyechanganyikiwa.
Baada ya kupita dakika kadhaa hatimaye nilifika nyumbani kwangu, nilipiga honi kisha mlinzi akanifungulia geti nikaingia na kwenda kupaki gari.
Sikumbuki kama nilisalimiana na mlinzi au la ila ninachokikumbuka niliingia ndani kisha nikapitiliza moja kwa moja mpaka chumbani. Kitendo hicho kilimshangaza sana mke wangu Lillian, aliponiona nimeingia ndani na yeye akanifuata, alipoingia akaniuliza kulikuwa kuna tatizo gani ambalo liliniweka katika hali hiyo niliyokuwa nikionekana.
“Hakuna kitu,” nilimjibu lakini hakuonekana kuridhika na jibu langu hilo, akaniuliza tena huku akionekana kuingiwa na wasiwasi.
“Nimekwambia hakuna kitu sasa unataka nikwambie nini?” nilimwambia kisha nikamuuliza huku nikimfokea, alishikwa na bumbuwazi baada ya kuniona hivyo.
“Mume wangu una nini lakini?” aliniuliza Lillian lakini sikumjibu kitu, nilibaki kimya kwa muda wa dakika kadhaa, nilikuwa nikimkumbuka Getrude.
“No! haiwezekani Getrude,” nilijisemea mara baada ya kukaa kimya kwa muda, Lillian akazidi kunishangaa zaidi na zaidi.
Miongoni kati ya matukio ambayo nayajutia katika maisha yangu ni hili tukio la kusababisha machozi ya mke wangu, nilimliza kila siku, wakati wa furaha ulikuwa ni mfupi kushinda wakati wa maumivu ambao ulionekana kuwa mrefu mno.
Ilikuwa imepita miezi kadhaa tangu nilipomuomba msamaha mke wangu na kumuahidi kutorudia makosa ambayo nilimkosea. Katika kipindi hicho nilichokuwa nikiishi naye maisha mapya yenye furaha bado niliendelea kumsaliti, hilo hakulifahamu kabisa.
Nilimuonyesha mapenzi ya dhati ambayo kiukweli ilikuwa ni vigumu yeye kufahamu kwamba nilimsaliti. Nilimuaga nasafiri kwenda nchi kama Marekanai, Afrika kusini, Uingereza mpaka Dubai lakini ukweli ni kwamba nilikuwa nikimsaliti.
Kwa wakati huo mapenzi tayari yalikuwa yamenipa maumivu, mchepuko ambao nilikuwa nikitembea nao ulinipa maumivu makali ambayo sikuyatarajia.
Nilichokikumbuka ni pesa zangu, vitu vya thamani ambavyo nilimpata Getrude katika maisha yake na kummilikisha kama yeye ndiye mmliki wa vitu vyote hivyo.
Lillian alibaki akinishangaa, hakujua ni nini kilichokuwa kimetokea. Kwa jinsi muonekano wake ulivyo alionekana kuwa na shahuku ya kutaka kufahamu kila kitu. Alizidi kuniuliza huku akionekana kunihurumia kutokana na muonekano niliyokuwa nao.
Licha ya kwamba Lillian aliendelea kuniuliza zaidi na zaidi lakini sikuwa tayari kumueleza ukweli, nilifahamu ni ukweli wenye kuumiza mno moyo endani kama ningethubutu kumueleza. Nilichokifanya nilimuondoa hofu ya moyo na kumwambia kuwa hakukuwa kuna kitu kilichotokea.
“Na Getrude ni nani?”
“Ni mfanyabiashara mwenzangu kuna mzigo amenidhulumu.”
“Pole sana mume wangu.”
“Asante,” nilimwambia.
Pamoja na mambo yote yaliyotokea bado mke wangu Lillian alizidi kunionyesha mapenzi ya dhati, hakutaka kuniona nikiwa katika wakati wa maumivu, alinifariji na kuendelea kunipa matumaini.
Ni kama vile niliyadhihaki mapenzi ya Lillian kwani katika kipindi ambacho alikuwa akinifariji na kunipa matumaini akili yangu ilikuwa ikiwaza kwingine, nilimfikiria Getrude.
Sikujua nilitakiwa kufanya nini kwa ajili yake, maumivu ambayo alikuwa amenipa nilihitaji kuyalipiza, nilichokuwa nikikihitaji zaidi ni kuona na yeye akiumia kama nilivyoumia na hiyo ndiyo ingeweza kuwa furaha yangu.
Wazo ambalo lililonijia kichwani mwangu lilikuwa ni la utekaji, yaani nilitakiwa kumteka kwanza mpenzi wake Getrude halafu ikiwezekana nimuue. Kwa kufanya hivyo ni lazima Getrude angepata pigo la maumivu katika maisha yake na maumivu hayo ambayo angeweza kuyapata kwangu ingekuwa kama nimeshalipa kisasi cha mapenzi.
Wazo hilo nilipolifikiria sikutaka kupingana nalo au kwenda kinyume nalo nilichokiona ni kwamba nilikuwa sahihi na tena nilitakiwa kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo.
“Yeah…lazima uumie na wewe kama ulivyoniumiza,” nilijisemea wakati ambao nilikuwa nikiitazama picha ya Getrude.
****
Sikutaka kuzungumza lolote na Getrude, moyo wangu kwa wakati huo ulikuwa na kisasi. Nilipanga kuanza na mpenzi wake kisha nifuate na yeye.
Kupata taarifa za mpenzi wake na mahali alipokuwa wala haikuwa kazi kubwa, nilichoamua kukifanya nilitafuta ukaribu na rafiki yake Getrude ambaye alijulikana kwa jina la Lydia. Nilianza kumtumia Lydia katika kunipa taarifa za mpenzi wake Getrude ambaye alijulikana kwa jina la Christopher.
“Anaishi wapi kwani?”
“Magomeni Mapipa.”
“Anafanya kazi gani?”
“Hana kazi, Getrude ndiye anayemuweka mjini hata hapo alipopanga anamlipia kodi,” aliniambia Lydia, wakati huo tulikuwa tumekaa kwenye mgahawa mmoja uliyowepo maeneo ya Makumbusho.

Je, nini kitaendelea?
 
PENZI LENYE MAUMIVU-09
Mtunzi:Juma Hiza
Simu:0712988278

Maneno ya Lydia yaliendelea kuniumiza sana moyo wangu, aliponiambia kuwa Christopher alipanga Magomeni Mapipa na Getrude ndiye ambaye aliyekuwa akimuhudumia kila kitu nilihisi kuchanganyikiwa.
Nilichokiamini kwa muda huo ni kwamba pesa zangu ambazo nilikuwa nikimpa Getrude ndizo ambazo zilitumika kumuhudumia Chistopher kwa upande wa pili. Hilo lilizidi kuniumiza mno.
Lydia hakutaka kuwa mzungumzaji sana, alichoamua kukifanya ni kunionyesha picha ya Christopher kwenye simu yake.
“Huyo hapo,” aliniambia baada ya kunionyeshea picha ya Christopher. Nilizidi kushikwa na hasira baada ya kumuona mwanaume ambaye alikuwa akizitumia pesa zangu.
Sikutaka kupoteza muda, nilimwambia Lydia anitumie picha hiyo WhatsApp kisha akafanya kama nilivyomwambia. Baada ya mazungumzo kumalizika nilimpatia pesa kiasi cha shilingi milioni moja kutokana na kazi nzuri aliyokuwa ameifanya, alifurahi mno baada ya kumpatia kiasi hicho cha pesa, akaniahidi kunipa ushirikiano kwa msaada wowote ambao ningeuhitaji kutoka kwake.
“Usijali kuhusu hilo,” nilimwambia.
“Ok shem,”aliniambia.
Uso wangu ulitawaliwa na furaha, nilifahamu fika kazi iliyokuwa imebakia mbele yangu haikuwa na ugumu tena kama ilivyokuwa hapa mwanzoni.
Mpaka kufikia muda huo Lydia hakufahamu ni tukio gani ambalo nilikuwa nikienda kulifanya kwa Christopher na laiti kama angefahamu nadhani asingekubali kunipa taarifa za Christopher.
Roho ya mauaji ilikuwa imeshaniingia, sikuwa na huruma hata kidogo, nilichokuwa nikihitaji kukiona ni mwili wa Christopher ukiwa maiti, hiyo ndiyo ilikuwa furaha yangu, nilitaka afe tena kifo cha kikatili.
Kuhusu hilo wala sikuwa na mashaka yoyote, nilichokifanya nilimtafuta jamaa mmoja aliyejulikana kwa jina la Maxwell, alikuwa akiishi Kinondoni. Aliogopeka mno kwa kinondoni nzima.
Michezo yote michafu aliifahamu na yeye ndiyo aalikuwa akitumika katika matukio mbalimbali hususani ya utekaji. Nilipokutana naye nilimpa dili la mauaji, nilihitaji kuona akimuua Christopher.
Baada ya kumpa picha yake pamoja na kumwambia mahali ambapo alikuwa akiishi alihitaji nimlipe kiasi cha shilingi milioni hamsini. Aliponiambia kuwa alihitaji kiasi hicho cha pesa nilitabasamu, nilikiona ni kiasi kidogo mno ukilinganisha na kiasi cha pesa ambacho nilikuwa nikimiliki katika akaunti yangu benki.
Kutokana na hitaji langu kubwa la kuona Christopher akiuwawa nilimuahidi kumlipa kiasi cha shilingi milioni themanini za kitanzania. Akaonekana kufurahi, hii ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kumuona Maxwell akitabasamu tangu nilipokutana naye, muda wote alikuwa ameikunja sura yake iliyoonekana kuwa ngumu na yenye kutisha.
“Huu ni mwaka wa kumi sasa nimekuwa nikiifanya kazi hii ya kutoa roho za watu hivyo tegemea kazi yako ikifanikiwa kwa asilimia mia moja,” aliniambia Maxwell.
“Nitafurahi sana,” nilimwambia huku nikikenua.
“Usijali mkuu baada ya siku mbili utaikuta maiti yake ufukwe wa coco,” aliniambia Maxwell maneno yaliyozidi kunifurahisha mno.
Hakukuwa kuna mtu aliyefahamu kile kilichokuwa kikiendelea, hata kwa upande wa mke wangu hakufahamu kitu chochote. Baada ya kupita siku mbili bila kupata taarifa zozote kutoka kwa Maxwell kama alivyoniahidi nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilihisi labda mpango wa kumuua Christopher ulishindikana, hilo lilinisononesha, sikutaka kuamini kama hilo liliwezekana kutokea.
Muda wote nilikuwa makini kuitazama simu yangu kuona kama Maxwell angenipigia na kunipa taarifa za kufanikiwa mpango wa kumuua Christopher. Yaani kwa jinsi nilivyokuwa makini kuitazama simu yangu siku hiyo ilikuwa ni kama mtu aliyekuwa akisubiria meseji ya ushindi ambao angeupata mara baada ya kubeti.
Usiku wa siku hiyo majira ya saa saba nilipokea ujumbe mfupi kutoka kwa Maxwell, aliniandikia maneno machache ya kingereza “I’m Done,” yaliyomaanisha kwa Kiswahili (Nimemaliza).
Sikutaka kuamini hilo, nilihitaji kuthibitisha na kama nilivyohitaji Maxwell alinitumia picha za mwili wa Christopher ambaye tayari alikuwa maiti.
“Kazi nzuri sana kwahiyo maiti yake umeende kuitelekeza coco beach?” nilimuuliza.
“Ndiyo asubuhi watakuta mzoga wao,” alinijibu.
“Aisee umenifurahisha mno, sikutegemea kwa kweli.”
“Nilikwambia kazi yako lazima ifanikiwe kwa asilimia mia moja,” aliniambia.
Kadri nilivyozidi kuzungumza na Maxwell ndivyo ambavyo furaha ilizidi kunitawala, hakika kifo cha Christopher kilionekana kuwa sababu ya furaha yangu kwa wakati huo.
Siku iliyofuata wala sikutaka kupoteza muda, kama nilivyomuahidi, nilimlipa pesa zake kupitia akaunti yake benki na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kufanya kazi na Maxwell, nilimuhitaji zaidi na zaidi katika kazi zangu nyingine.
****
Mke wangu Lillian alikuwa ni muumini wa kanisa la Praise and Worship lililokuwepo Mwenge jijini Daresalaam. Aliamua kumkabidhi maisha yake Mungu kwani aliamini yeye ndiye pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kumponya Brighton.
Kilikuwa ni kipindi ambacho alisali na kumuomba Mungu kwa nguvu zote lakini pia hakuacha kuiombea amani na furaha ya ndoa yetu ambayo ilionekana kurejea kwa kipindi hicho.
Nilipokuwa nyumbani hakuacha kunikumbusha uwepo wa Mungu katika maisha yangu, alipomaliza kuniambia hayo aliniomba nifunge macho kisha maombi yakaanza. Hayo yote hayakuonekana kuniingia akilini mwangu, japokuwa kila ambalo alilokuwa akihitaji nifanye nilifanya kwa muda huo lakini siri iliyokuwepo moyoni mwangu niliijua mimi peke yangu pamoja na Mungu.
“Asante Mungu kwa kuirudisha furaha ya ndoa yangu,” alisema Lillian huku akiwa ameyafunga macho yake, wakati huo nilikuwa nikimtazama, moyoni mwangu nikajisemea laiti kama ungejua sikupendi wewe pamoja na huyo mwanao wala usingejisumbua hata kumshukuru huyo unayemuita ni Mungu wako.
****
Taarifa zilizagaa kila kona kuhusu tukio la kukutwa maiti ufukwe wa coco, ilikuwa ni maiti ya Christopher. Vyombo mbalimbali vya habari, magazeti nayo hayakuwa mbali kuripoti habari za mauaji yao yaliyoonekana kuwa ya kikatili.
Mwili wa Christopher ulikutwa ukiwa umejeruhiwa vibaya mno sehemu mbalimbali za mwili wake kisha ukiwa ndani ya kiroba. Kila aliyeishuhudia maiti yake hakutaka kuamini, yalikuwa ni mauaji ya kikatili.
Jeshi la polisi likaingilia kati, hakukuwa kuna mtu aliyemfahamu muuaji aliyehusika na mauaji mpaka kufikia muda huo. Hatimaye msako wa kumtafuta muuaji kila kona ukaanza.
Lydia ndiye mtu wa kwanza ambaye aligundua kuwa mimi ndiye niliyesababisha kifo cha Christopher kwani mazingira ambayo Christopher aliuliwa pamoja na siku ile ambayo nilihitaji taarifa zake yalikuwa ni matukio mawili ambayo aliyafananisha.
Hilo lilianza kunipa wasiwasi, niliamini kwa vyovyote ni lazima Lydia angemweleza ukweli Getrude na hata kwenda polisi kutoa ushahidi kwa kile kilichokuwa kimetokea.
Kitendo cha kumuona Lydia akiendelea kuishi kilinihatarishia maisha yangu, sikutaka kujiuliza mara mbilimbili, nilichopanga kukifanya ni kama nilivyofanya kwa Christopher na yeye nilitaka afe ili siri iendelee kubaki ni yangu.

Je, nini kitaendelea?
K
 
PENZI LENYE MAUMIVU-09
Mtunzi:Juma Hiza
Simu:0712988278

Maneno ya Lydia yaliendelea kuniumiza sana moyo wangu, aliponiambia kuwa Christopher alipanga Magomeni Mapipa na Getrude ndiye ambaye aliyekuwa akimuhudumia kila kitu nilihisi kuchanganyikiwa.
Nilichokiamini kwa muda huo ni kwamba pesa zangu ambazo nilikuwa nikimpa Getrude ndizo ambazo zilitumika kumuhudumia Chistopher kwa upande wa pili. Hilo lilizidi kuniumiza mno.
Lydia hakutaka kuwa mzungumzaji sana, alichoamua kukifanya ni kunionyesha picha ya Christopher kwenye simu yake.
“Huyo hapo,” aliniambia baada ya kunionyeshea picha ya Christopher. Nilizidi kushikwa na hasira baada ya kumuona mwanaume ambaye alikuwa akizitumia pesa zangu.
Sikutaka kupoteza muda, nilimwambia Lydia anitumie picha hiyo WhatsApp kisha akafanya kama nilivyomwambia. Baada ya mazungumzo kumalizika nilimpatia pesa kiasi cha shilingi milioni moja kutokana na kazi nzuri aliyokuwa ameifanya, alifurahi mno baada ya kumpatia kiasi hicho cha pesa, akaniahidi kunipa ushirikiano kwa msaada wowote ambao ningeuhitaji kutoka kwake.
“Usijali kuhusu hilo,” nilimwambia.
“Ok shem,”aliniambia.
Uso wangu ulitawaliwa na furaha, nilifahamu fika kazi iliyokuwa imebakia mbele yangu haikuwa na ugumu tena kama ilivyokuwa hapa mwanzoni.
Mpaka kufikia muda huo Lydia hakufahamu ni tukio gani ambalo nilikuwa nikienda kulifanya kwa Christopher na laiti kama angefahamu nadhani asingekubali kunipa taarifa za Christopher.
Roho ya mauaji ilikuwa imeshaniingia, sikuwa na huruma hata kidogo, nilichokuwa nikihitaji kukiona ni mwili wa Christopher ukiwa maiti, hiyo ndiyo ilikuwa furaha yangu, nilitaka afe tena kifo cha kikatili.
Kuhusu hilo wala sikuwa na mashaka yoyote, nilichokifanya nilimtafuta jamaa mmoja aliyejulikana kwa jina la Maxwell, alikuwa akiishi Kinondoni. Aliogopeka mno kwa kinondoni nzima.
Michezo yote michafu aliifahamu na yeye ndiyo aalikuwa akitumika katika matukio mbalimbali hususani ya utekaji. Nilipokutana naye nilimpa dili la mauaji, nilihitaji kuona akimuua Christopher.
Baada ya kumpa picha yake pamoja na kumwambia mahali ambapo alikuwa akiishi alihitaji nimlipe kiasi cha shilingi milioni hamsini. Aliponiambia kuwa alihitaji kiasi hicho cha pesa nilitabasamu, nilikiona ni kiasi kidogo mno ukilinganisha na kiasi cha pesa ambacho nilikuwa nikimiliki katika akaunti yangu benki.
Kutokana na hitaji langu kubwa la kuona Christopher akiuwawa nilimuahidi kumlipa kiasi cha shilingi milioni themanini za kitanzania. Akaonekana kufurahi, hii ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kumuona Maxwell akitabasamu tangu nilipokutana naye, muda wote alikuwa ameikunja sura yake iliyoonekana kuwa ngumu na yenye kutisha.
“Huu ni mwaka wa kumi sasa nimekuwa nikiifanya kazi hii ya kutoa roho za watu hivyo tegemea kazi yako ikifanikiwa kwa asilimia mia moja,” aliniambia Maxwell.
“Nitafurahi sana,” nilimwambia huku nikikenua.
“Usijali mkuu baada ya siku mbili utaikuta maiti yake ufukwe wa coco,” aliniambia Maxwell maneno yaliyozidi kunifurahisha mno.
Hakukuwa kuna mtu aliyefahamu kile kilichokuwa kikiendelea, hata kwa upande wa mke wangu hakufahamu kitu chochote. Baada ya kupita siku mbili bila kupata taarifa zozote kutoka kwa Maxwell kama alivyoniahidi nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilihisi labda mpango wa kumuua Christopher ulishindikana, hilo lilinisononesha, sikutaka kuamini kama hilo liliwezekana kutokea.
Muda wote nilikuwa makini kuitazama simu yangu kuona kama Maxwell angenipigia na kunipa taarifa za kufanikiwa mpango wa kumuua Christopher. Yaani kwa jinsi nilivyokuwa makini kuitazama simu yangu siku hiyo ilikuwa ni kama mtu aliyekuwa akisubiria meseji ya ushindi ambao angeupata mara baada ya kubeti.
Usiku wa siku hiyo majira ya saa saba nilipokea ujumbe mfupi kutoka kwa Maxwell, aliniandikia maneno machache ya kingereza “I’m Done,” yaliyomaanisha kwa Kiswahili (Nimemaliza).
Sikutaka kuamini hilo, nilihitaji kuthibitisha na kama nilivyohitaji Maxwell alinitumia picha za mwili wa Christopher ambaye tayari alikuwa maiti.
“Kazi nzuri sana kwahiyo maiti yake umeende kuitelekeza coco beach?” nilimuuliza.
“Ndiyo asubuhi watakuta mzoga wao,” alinijibu.
“Aisee umenifurahisha mno, sikutegemea kwa kweli.”
“Nilikwambia kazi yako lazima ifanikiwe kwa asilimia mia moja,” aliniambia.
Kadri nilivyozidi kuzungumza na Maxwell ndivyo ambavyo furaha ilizidi kunitawala, hakika kifo cha Christopher kilionekana kuwa sababu ya furaha yangu kwa wakati huo.
Siku iliyofuata wala sikutaka kupoteza muda, kama nilivyomuahidi, nilimlipa pesa zake kupitia akaunti yake benki na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kufanya kazi na Maxwell, nilimuhitaji zaidi na zaidi katika kazi zangu nyingine.
****
Mke wangu Lillian alikuwa ni muumini wa kanisa la Praise and Worship lililokuwepo Mwenge jijini Daresalaam. Aliamua kumkabidhi maisha yake Mungu kwani aliamini yeye ndiye pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kumponya Brighton.
Kilikuwa ni kipindi ambacho alisali na kumuomba Mungu kwa nguvu zote lakini pia hakuacha kuiombea amani na furaha ya ndoa yetu ambayo ilionekana kurejea kwa kipindi hicho.
Nilipokuwa nyumbani hakuacha kunikumbusha uwepo wa Mungu katika maisha yangu, alipomaliza kuniambia hayo aliniomba nifunge macho kisha maombi yakaanza. Hayo yote hayakuonekana kuniingia akilini mwangu, japokuwa kila ambalo alilokuwa akihitaji nifanye nilifanya kwa muda huo lakini siri iliyokuwepo moyoni mwangu niliijua mimi peke yangu pamoja na Mungu.
“Asante Mungu kwa kuirudisha furaha ya ndoa yangu,” alisema Lillian huku akiwa ameyafunga macho yake, wakati huo nilikuwa nikimtazama, moyoni mwangu nikajisemea laiti kama ungejua sikupendi wewe pamoja na huyo mwanao wala usingejisumbua hata kumshukuru huyo unayemuita ni Mungu wako.
****
Taarifa zilizagaa kila kona kuhusu tukio la kukutwa maiti ufukwe wa coco, ilikuwa ni maiti ya Christopher. Vyombo mbalimbali vya habari, magazeti nayo hayakuwa mbali kuripoti habari za mauaji yao yaliyoonekana kuwa ya kikatili.
Mwili wa Christopher ulikutwa ukiwa umejeruhiwa vibaya mno sehemu mbalimbali za mwili wake kisha ukiwa ndani ya kiroba. Kila aliyeishuhudia maiti yake hakutaka kuamini, yalikuwa ni mauaji ya kikatili.
Jeshi la polisi likaingilia kati, hakukuwa kuna mtu aliyemfahamu muuaji aliyehusika na mauaji mpaka kufikia muda huo. Hatimaye msako wa kumtafuta muuaji kila kona ukaanza.
Lydia ndiye mtu wa kwanza ambaye aligundua kuwa mimi ndiye niliyesababisha kifo cha Christopher kwani mazingira ambayo Christopher aliuliwa pamoja na siku ile ambayo nilihitaji taarifa zake yalikuwa ni matukio mawili ambayo aliyafananisha.
Hilo lilianza kunipa wasiwasi, niliamini kwa vyovyote ni lazima Lydia angemweleza ukweli Getrude na hata kwenda polisi kutoa ushahidi kwa kile kilichokuwa kimetokea.
Kitendo cha kumuona Lydia akiendelea kuishi kilinihatarishia maisha yangu, sikutaka kujiuliza mara mbilimbili, nilichopanga kukifanya ni kama nilivyofanya kwa Christopher na yeye nilitaka afe ili siri iendelee kubaki ni yangu.

Je, nini kitaendelea?
K
Kanogewa mauaji ss
Asante Madame S
 
PENZI LENYE MAUMIVU-10
Mtunzi:Juma Hiza
Simu:0712988278
Sikutaka kupoteza muda tena, nilichokuwa nikitaka kuona ni Lydia akiuwawa kama alivyouwawa Christopher. Niliamini kwa kufanya hivyo siri isingeweza kufichuka.
Kama ilivyokuwa kawaida nikampa dili hilo Maxwell huku nikimuahidi kumlipa kiasi kikubwa cha pesa mara mbili ya aliyokuwa akitaka nimlipe.
“Hii kazi sio ngumu hata kidogo mkuu,” aliniambia Maxwell huku akionekana kujiamini kupita kawaida. Hilo lilizidi kunipa matumaini na kuamini kwa asilimia mia moja kuwa ni lazima Lydia angeuwawa na ushahidi wote kupotea.
Ili kuifanikisha kazi hiyo Maxwell alihitaji taarifa za kina kuhusu msichana huyo, hilo halikuwa tatizo, nilimueleza kila kitu.
Lydia alikuwa akiishi Sinza, maisha yake yalitawaliwa na starehe kwa asilimia kubwa, kila wikiendi alikuwa ni mtu wa kwenda klabu. Huko alijichanganya na kutembea na wanaume tofauti tofauti ambao ndiyo walikuwa wakimpa pesa.
Alikuwa ni msichana mzuri mwenye shepu iliyojaa mvuto alikuwa nayo. Mwili wake ulikuwa mwembamba huku kwa mbali hipsi zake zikiwa zinaonekana. Pamoja na shepu yake lakini aliutumia uzuri wake kama rasilimali kwa kutembea na wanaume ambao walikuwa wakimpa pesa kwa maana nyingine tunasema alikuwa ni danga hapa mjini.
Mpaka kufikia muda huo Maxwell alishafahamu ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya kwa msichana huyo. Akatabasamu kidogo kisha akaniahidi kuifanikisha kazi hiyo kama nilivyotaka.
Nilifanya mambo yote haya huku lengo langu likiwa ni kumpa maumivu Getrude moyoni mwake, kifo cha Christopher ambaye ndiye alikuwa mpenzi wake niliamini kilikwenda kumpa maumivu makali mno. Maumivu hayakuishi kwa mpenzi wake tu, baada ya kupita siku kadhaa mwili wa rafiki yake Lydia nao ulikutwa ukiwa tayari maiti ndani ya chumba cha hoteli moja ya kifahari iliyokuwepo hapa jijini Daresalaam. Mwili wake ulijeruhiwa sehemu kubwa huku macho yakiwa yametolewa.
Mpaka kufikia muda huo niliamini mpango wangu ulifanikiwa kwa asilimia mia moja, Getrude alikuwa katika kipindi kigumu cha kuondokewa na mpenzi wake pamoja na rafiki yake kipenzi. Hilo ndilo nililokuwa nikihitaji kuliona kwa wakati huo.
Baada ya jeshi la polisi kufanya uchunguzi wake wa kina ilibidi wamuhoji Getrude kwani tayari mauaji hayo yalionekana kuwa na utata ndani yake. Watu waliyokuwa wakiuwawa walikuwa ni watu wake wa karibu tu.
Baada ya mahojiano hayo kufanyika mtu ambaye alimtaja kama anayemuhisi kuhusika na mauaji hayo alikuwa ni mimi.
Nakumbuka nilikuwa nyumbani kwangu, siku hiyo nilionekana kuwa mwenye furaha mno kushinda siku zote nilizowahi kuwa na furaha katika maisha yangu mpaka mke wangu akawa ananishangaa, siku hiyo nilizidisha mapenzi mpaka kuna muda nikaonekana kuwa wa tofauti maana sikuzoeleka kuwa katika hali kama hiyo.
Huku mke wangu akiwa hajui hili wala lile mara Polisi wawili waliyovalia mavazi ya kiraia waliingia ndani, wakajitambulisha kuwa wao ni Polisi kwa kuonyesha vitambulisho vyao, walipofahamu kuwa mimi ndiye Kelvin wakaniambia kuwa nilikuwa nikihitajika kituoni.
Mke wangu alishangaa, hakujua ni nini kilichokuwa kimetokea kwa wakati huo, kitendo cha kuwaona Polisi wakiwa ndani ya nyumba yetu huku wakinitaka niongozane nao hadi kituoni kilimshtua mno, kama ilivyokuwa kawaida yake machozi yakaanza kumdondoka mashavuni mwake.
“Jamani amefanya kosa gani mume wangu?” aliwauliza huku machozi yakiendela kumdondoka.
“Usijali ataenda kujulia kituoni, kwasasa tunaomba tufanye kazi yetu iliyotuleta hapa,” alisema Polisi mmoja kwa msisitizo.
Hakukuwa kuna muda wa kupoteza, walichokuwa wakikihitaji Polisi kwa wakati huo ni kuondoka na mimi mpaka kituoni, hilo sikutaka kupinga, kwa kuwa nilijiamini, nilifuata vile walivyotaka, nikaondoka nao mpaka kituoni.
Mke wangu alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, hakujua ni nini ambacho alitakiwa kukifanya.
“Unatuhumiwa kwa kesi ya mauaji ya watu wawili,” aliniambia Polisi mmoja mara baada ya kufika kituoni, nikaingizwa kwenye chumba maalum halafu nikaanza kuhojiwa.
“Mauaji?” nilimuuliza huku nikionekana kushangaa, nilionekana kama mtu ambaye nilikuwa sifahamu lolote lililokuwa limetokea.
“Ndiyo,” alinijibu huku akionyesha msisitizo.
“Hapana afande sihusiki katika hilo,” nilimwambia huku nikimuaminisha.
Kwa muonekano ambao niliuonyesha ilikuwa sio rahisi kuamini kwamba mimi ndiye niliyehusika kumtuma mtu akafanye mauaji hayo, kila swali ambalo niliulizwa nililikanusha, sikuwa tayari kukubali kirahisi kesi hiyo ya mauaji.
Kipindi kesi hiyo ikiendelea mke wangu alikuwa ni mtu wa kusali na kuomba Mungu usiku na mchana, hakutaka kuona nikifungwa.
“Naamini tutashinda kesi hii mume wangu, Mungu anatupitisha katika kipindi hiki cha majaribu ili azipime imani zetu, tumuamini yeye ndiye atakayetusaidia,” aliniambia Lillian.
“Sawa nimekuelewa,” nilimwambia huku nikionyesha sura ya huruma.
Kitu ambacho alikuwa akikifahamu ni kwamba kesi hiyo nilisingiziwa na mtu aliyenisingizia alikuwa na lengo la kunichafua. Hilo aliliamini na ndiyo sababu iliyomfanya akawa ananiombea usiku na mchana huku akimlaani mtu huyo vikali, hakujua upande wa pili kama kweli nilihusika.
Siku ziliendelea kukatika, Polisi nao wakaendelea kufanya uchunguzi wao juu ya kesi hiyo ambayo ilikuwa ikinikabili. Nilitumia pesa kuwahonga Polisi pamoja na wanasheria na mwisho wa siku kesi hiyo iliweza kufutwa hapa ni baada ya kuonekana sina hatia yoyote.
Kilikuwa ni kipindi ambacho Getrude hakutaka kuamini kile kilichotokea, japokuwa aliamini mimi ndiye niliyehusika na mauaji hayo lakini hakukuwa kuna mkono wa sheria tena, kila kitu kilikuwa ndani ya uwezo wangu.
“Haya ndiyo maumivu ambayo nilitamani uyasikie na wewe, nilitaka uyaonje maumivu ambayo ulinipa,” nilimwambia Getrude huku nikiamini hakuwa na sehemu nyingine ya kukimbilia.
“Umenifungulia kesi ya mauaji, nimeshinda, hii yote inaonyesha ni jinsi gani nilivyokuwa nina nguvu na uwezo, kwangu hakuna kitu kinachoshindikana,” nilimwambia huku nikijisifia, nilijiona kuwa mshindi.
Maumivu aliyoyapata Getrude niliyafurahia kwasababu nilitaka na yeye aumie kama alivyoniumiza, kitendo cha kutumia pesa zangu na mwanaume mwingine kiliniudhi na ndiyo sababu iliyosababisha mpaka nikafanya mauaji.
Kweli mapenzi yana nguvu na wala usishangae mimi kufanya haya yote, nilifanya kwasababu ya mapenzi. Usaliti ambao alinifanyia Getrude uliniumiza kiasi kwamba naweza kusema nilisahau kabisa kwamba na mimi nilikuwa nikimsaliti mke wangu kwa kutembea naye.
Naamini nitachukiwa na kila mtu ila ukweli ni kwamba moyo wangu ulikuwa katika maumivu katika kipindi hicho, sijui niseme nini ila baada ya kufanikiwa kumtuma Maxwell kufanya mauaji moyo wangu ulikuwa na furaha, maumivu ambayo ulikuwa umeyaonja yalipungua, hapa ni baada ya kumuona Getrude na yeye akiumia mara mbili yangu.
****
Baada ya kupita sekeseke la kesi hiyo ya mauaji iliyokuwa ikinikabili, maisha yaliendelea huku furaha ikionekana kushika hatamu kwa upande wa familia yangu.
Niliishi maisha ya furaha lakini kila nilipokuwa nikimuona Brighton nilikuwa nikijisikia vibaya moyoni mwangu. Kuna kipindi hata kuwaita matajiri wenzangu waje kumuona niliona aibu maana alionekana kuwa kama kituko.
Kwa jinsi alivyokuwa akionekana Brighton hakufanania kabisa kuwa na baba kama mimi ambaye nilikuwa na muonekano mzuri, sijui hata alirithi sura na ulemavu kutoka kwa nani?
NENO LANGU;
Napenda kuwapa pole wale wote waliowahi kuumizwa mapenzini mwaka huu, waliowahi kunyanyasika kwa kuwa hawakuwa na kitu fulani, wanachuo na wanafunzi ambao walikaa nyumbani kwa kuwa walikosa ada huku masomo yakiendelea, wale ambao waliwaamini wapenzi wao japokuwa walikuwa wakisalitiwa, wale ambao walijua thamani ya mapenzi ingawa wao kamwe hawakuonyeshewa thamani hiyo. Pia nawapa pole wale wote ambao mwaka mzima walikosa furaha na amani, waliotengwa kwa kuwa walikuwa na udhaifu fulani au ulemavu miilini mwao, wale ambao walidiriki kupenda pale ambapo kamwe hawakupendwa. Poleni sana, amini kwamba Mungu Yu pamoja nanyi.
 
PENZI LENYE MAUMIVU-11
Mtunzi:Juma Hiza
Simu:0712988278
Nilikuwa ni mwenye furaha lakini furaha yangu haikudumu, kuna muda ilipotea na hatimaye chuki ikanitawala moyoni mwangu. Hali hiyo haikunitokea mara moja tu bali ilinitokea mara kwa mara na ilimchanganya sana mke wangu.
Muda ambao alihitaji faraja kutoka kwangu ndiyo muda huo ambao sikuhitaji ukaribu naye. Niliondoka nyumbani na kurudi usiku ambapo nilikuwa nimelewa chakari. Sikuhitaji muda wa kuzungumza naye zaidi ya kulala mpaka asubuhi ya siku iliyofuata.
Maisha yaliendelea huku Lillian akionekana kuwa mvumilivu wa yale yote niliyokuwa nikimfanyia katika maisha yake. Hakujali nilipomtukana na kumdharau, nilimpoukosoa uumbaji wa Mungu kwa Brighton, nilipompiga na kumfanya ajutie kuolewa na mimi.
Pesa ndiyo iliyokuwa ikinipa kiburi, niliamini hakukuwa kuna kitu ambacho nilishindwa kukifanya katika maisha yangu, nilishafanya mengi mpaka kufikia wakati huo lakini bado niliona ninanafasi kubwa ya kufanya zaidi na zaidi.
Pepo la ngono bado lilikuwa upande wangu, kila msichana niliyekutana naye nilianzisha mahusiano naye ya kimapenzi wala hilo halikuwa jambo gumu kutokea kwasababu nilikuwa nina pesa.
Baada ya kupita mwaka mmoja nilianzisha mahusiano ya kimapenzi na msichana mwingine aliyejulikana kwa jina la Nancy. Huyu Nancy nilianzisha mahusiano naye baada ya kumsaidia Mama yake ambaye alikuwa akisumbuliwa na uvimbe tumboni.
Aliteseka sana na uvimbe huo na kwakuwa kiasi ambacho kilihitajika hospitalini kwa ajili ya matitabu kilikuwa ni kingi mno hawakuweza kukimudu hivyo walikosa msaada.
Kila siku Nancy alikuwa ni mtu wa kuhangaika huku na kule akifanya kazi mbalimbali kwa ajili ya kupata pesa ya kumtibia Mama yake.
Nilikutana naye kwenye baa moja iliyokuwepo Mwenge, majira ya usiku ambapo nilienda kunywa siku hiyo, nilikuwa ni mwenye hasira sana baada nyumbani kugombana na mke wangu.
Wakati nilipokuwa nikinywa pombe kali huku nikimuagiza mhudumu ambaye alikuwa ni Nancy aniongezee nilishangaa kumuona akiwa katika hali ambayo ilinishangaza. Baada ya kuniletea kinywaji nilichomuagiza na kukifungua nilimuona akiyafuta machozi yake na kuzuga kama hakukuwa kuna kitu kilichotokea, tukio hilo likazidi kunishangaza. Nikabaki namuangalia usoni huku nisijue ni nini ambacho kilikuwa kinaendelea.
“Una tatizo gani wewe?” nilimuuliza kisha akaonekana kunishangaa mno.
“Hakuna kitu kwani umeona nini?” alinijibu kisha akaniuliza swali la mashakamashaka. Hakuonekana akijiamini hata kidogo.
“Unalia..” nilimwambia.
“Hapana.”
“Hapana wakati nayaona machozi mashavuni mwako.”
“Usijali hakuna kitu karibu,” aliniambia kisha akanikaribisha kile kinywaji alichokuwa ameshakifungua.
“Naweza kufahamu kinachokusibu kama hutojali?” nilimuuliza.
“Hapana huu ni muda wa kazi kaka angu naomba tuzungumze wakati mwingine,” alinijibu kisha akaonekana kuwa na haraka ya kuondoka kwani aliniambia baadhi ya wahudumu wenzake walishaanza kumuangalia kwa jicho baya.
“Lini sasa tutazungumza?”
“Siku yoyote lakini isiwe hapa kwenye mazingira ya kazi,” alinijibu kisha hapohapo sikutaka kupoteza muda, nilimpatia business card yangu kwa ajili ya mawasiliano lakini pia sikuacha kumpatia kiasi kidogo cha pesa ambacho niliamini kingeweza kumsaidia kwa shida ndogondogo.
“Usisahau kunitafuta,” nilimwambia.
“Sawa nitafanya hivyo,” aliniambia kisha akaondoka.
Siku hiyo sikunywa sana kama ilivyokuwa siku nyingine ambazo huwa nakunywa mpaka nalewa chakari. Nilipoona nimetosheka kunywa nilirudi zangu nyumbani huku moyoni nikiwa bado ninachuki na mke wangu. Nilipofika nyumbani kama ilivyokuwa kawaida sikuzungumza lolote na mke wangu, niliingia bafuni kuoga, nilipomaliza kuoga nilipanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi ambao haukuchukua dakika nyingi uliweza kunipitia.
Niliamka asubuhi ya siku nyingine ambayo nilikutana na ujumbe mfupi wa namba ngeni ambayo ndiyo ilikuwa imenitumia, nilipousoma ujumbe huo niligundua Nancy ndiye ambaye alikuwa amenitumia.
“HII NDIYO NAMBA YANGU, MIMI NI NANCY.” Nilitabasamu baada ya kuusoma ujumbe huo, kiukweli japo nilipomuona Nancy usiku kule baa lakini alionekana kuwa msichana mrembo, alikuwa na hipsi pana kama za mnyama pundamilia, chuchu kama maembe dodo, kiuno chake kilikuwa kimeingia ndani kama mdudu nyigu. Kiufupi alivutia mno.
Mpaka kufikia muda huo nilitamani kujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikiendelea katika maisha yake. Ni ukweli kwamba alionekana kuwa msichana mwenye mvuto mno lakini pia alionekana kuwa na matatizo makubwa.
Sikutaka kupoteza muda, nilimpigia simu Nancy muda huohuo ambao alinitumia ujumbe mfupi. Simu ikapokelewa.
“Hallo Kelvin,” Sauti ya upande wa pili ya Nancy iliniambia.
“Hallo Nancy nimefurahi kuipata namba yako,” nilimwambia.
“Nimefurahi pia Kelvin,” aliniambia.
“Uko wapi?”
“Nipo nyumbani.”
“Sehemu gani?”
“Kigogo.”
“Naweza kukuona?”
“Ndiyo inawezekana lakini mpaka nimuandae mama maana ni mgonjwa na hana mtu mwingine wa kumuangalia zaidi yangu.”
“Anasumbuliwa na nini?”
“Ni stori ndefu Kelvin,” aliniambia kisha akanyamaza, alishindwa kuendelea kuzungumza. Akaanza kulia kwa sauti ya kwikwi. Nilijaribu kumbeleza anyamaze ili kusudi aweze kuniambia ugonjwa ambao ulikuwa ukimsumbua mama yake lakini ilishindikana. Swali langu lilikuwa kama limemtonesha kidonda kilichompa maumivu makali mno.
Baada ya kuona maongezi ya kwenye simu yameshindikana ilibidi nimwambie kuwa nilitaka kuonana naye, akanikubalia ombi langu. Hatimaye tukaweza kuonana.
“Uliniambia Mama yako anasumbuliwa na nini maana kwenye simu tulishindwa kuelewana,” nilimuuliza huku nikiwa makini kusubiri majibu.
“Mama yangu anasumbuliwa na uvimbe tumboni, nimehangaika kutafuta hela ya kumpeleka hospitali ili akatibiwe lakini imeshindikana, pesa ninazozipata zinakidhi mahitaji ya chakula na kulipa kodi ya chumba tulichopanga,” aliniambia.
Kwa jinsi nilivyokuwa nikimuangalia Nancy usoni, alionekana kuwa na shida zaidi ya hiyo aliyonieleza ya kuuguliwa na Mama yake ambaye alikuwa akisumbuliwa na uvimbe tumboni. Nilichokuwa nikihitaji kwa wakati huo ni kufahamu historia ya maisha yake na kumsaidia kwani hilo lilikuwa ndani ya uwezo wangu.
Alinisimulia kila kitu kilichowahi kutokea katika maisha yake mpaka kufika hatua ya kufanya kazi za uhudumu wa baa kwa lengo la kutafuta pesa kwa ajili ya kumtibia mama yake ambaye alikuwa akiteseka.
“Usijali nitakusaidia, nitahakikisha Mama yako anafanyiwa upasuaji na kupona kabisa,” nilimwambia Nancy maneno ambayo hakuyaamini.
Aliteseka sana, alihangaika usiku na mchana kutafuta pesa kwa ajili ya kumtibia mama yake lakini alikosa. Kitendo cha kukutana na mimi katika maisha yake aliniona kuwa kama mkombozi. Hakutaka kuamini kama kweli ningeweza kumsaidia mama yake akafanyiwa upasuaji na kupona.
Nilikuwa tayari kufanya yote hayo lakini mwisho wa siku nilijua ningetembea naye. Kwa wakati huo familia yangu haikuwa akilini mwangu tena, Nancy ndiye mtu aliyekuwa amenikaa na nilipanga kumsaidia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom