Penzi la Bar maid

Penzi la Bar maid

nimechafukwa

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2013
Posts
290
Reaction score
237
Wadau niko kwenye Hali ya sintofahamu baada ya kumuacha mpenzi wangu mwenye qualities kama zangu (Degree,Cpa t na masters) nimeangukia Penzi la bar maid,familia, marafik,i ndugu hakuna anaenielewa kabisa nikiwaelezea..

Ushauri please...ni sawa mm kumuoa barmaid??
 
wacha niwahi siti ya mbele..tukiwasubiri waje wacha nijiburudishe kwa kuvuta mtemba.. naomba mtoa mada nipitishie hiyo miwani nipitiepitie hili jarida la how to make a woman reach multiple orgasm kabla wataalamu wawasili..
 
Ni sawa tu kama umempenda kwa dhati. Hakuna jambo zuri kama kuwa na mke au mpenzi ambaye umempenda kwa dhati, na yeye akakupenda. Raha sana. Kumbuka hata barmaid ni mwanamke kama walivyo wengine cha msingi awe na heshima, utulivu katika mahusiano na heshima.
 
Kweli we umechafukwa...

Umetema Big G kwa karanga za kuonjeshwa
 
Na yy pia mwanamke ana haki ya kupendwa
 
Kikubwa mapenzi ya dhati mkuu. Acha kusikiliza watu, wewe ndo utakae ishi na mke si wao.
Unaweza ukaoa wanaemtaka wao lakini usifurahie maisha ya ndoa.
 
Ungewauliza Kwani barmaid ndio sio binadamu?kama umejiakikishia ametulia na msikivu kwako..!oa tuh!
 
Hivi ni kwanini barmaid wanadharaulika sanaaa???
 
kuoa ni kuamua kama unashindwa hata kuamua umuoe nan bas acha tu usioe kabisa
 
kama wenyewe mnapendana hakuna shida kikubwa muwe na amani ya moyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom