Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,974
- Thread starter
- #221
105...
Tukio hilo lilifananishwa na lile la gari kulipuka kwa bomu nchini Marekani huku akiwa ndani ya gari hilo na rafiki yake. Kwa sababu katika tukio hilo mhusika alijulikana kwamba ni Petrov, hivyo hata katika tukio hilo lililotokea, watu wakajua kwamba kulikuwa na mkono wa Petrov.
“Ila huyu jamaa kwa nini anafanya hivi?” aliuliza jamaa mmoja.
“Hata mimi sijui.”
Jeshi la Polisi la Tanzania halikukaa kimya, kwa kile kilichotokea kilimaanisha kwamba nchi hiyo ilikuwa ikiingia kwenye aibu kubwa kimataifa hivyo amri kutolewa kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima mtu aliyefanya kitu hicho ajulikane na kukamatwa kisha kufikishwa katika vyombo vya habari haraka sana.
Chuoni hakukukalika, kila kona kulikuwa na gumzo kuhusu kile kilichokuwa kimetokea. Kila mmoja alihuzunika, hawakuamini kama kungekuwa na mwanachuo ambaye angefanya kitu kama kile kwani kila walipoangalia na kufuatilia, hawakuona kama msichana Tatiana aliwahi kuishi Dar es Salaam, makazi yake yalikuwa Shinyanga kijijini, je huyo adui alikuwa nani?
“Huyu atakuwa yule Mrusi! Hivi anamtafutia nini huyu demu?’ aliuliza mwanachuo mmoja.
“Warusi wana roho mbaya sana, hawaangalii sababu, wao wanachotaka kuua tu, hakuna kingine,” alisema jamaa mwingine.
Hiyo ndiyo ikawa habari ya mjini, kila kona tukio hilo lilikuwa likizungumziwa tu. Redioni, taarifa hizo zilitangazwa huku magazeti yote ambayo yalitarajiwa kutoka siku inayofuata, yalionekana kuwa na habari hiyo kwa ukubwa zaidi, hivyo watu wakapanga kuyanunua ili wajue ukweli.
“Dokta! Tuambie ukweli!” alisema professa huku akiinuka kitini.
“Ukweli gani?”
“Juu ya Tatiana. Masaa matano yamepita, hatujui lolote lile,” alisema Professa.
“Naomba twendeni ofisini,” alisema dokta.
Hawakutaka kuchelewa, walichokifanya, wote wakaanza kumfuata daktari yule ambaye alipiga hatua za harakaharaka kuelekea ofisini mwake. Kwa muonekano aliokuwa nao tu ulionyesha kwamba kulikuwa na jambo baya lililokuwa limetokea mule chumbani hivyo kila mmoja akashikwa na hofu moyoni mwake.
Tukio hilo lilifananishwa na lile la gari kulipuka kwa bomu nchini Marekani huku akiwa ndani ya gari hilo na rafiki yake. Kwa sababu katika tukio hilo mhusika alijulikana kwamba ni Petrov, hivyo hata katika tukio hilo lililotokea, watu wakajua kwamba kulikuwa na mkono wa Petrov.
“Ila huyu jamaa kwa nini anafanya hivi?” aliuliza jamaa mmoja.
“Hata mimi sijui.”
Jeshi la Polisi la Tanzania halikukaa kimya, kwa kile kilichotokea kilimaanisha kwamba nchi hiyo ilikuwa ikiingia kwenye aibu kubwa kimataifa hivyo amri kutolewa kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima mtu aliyefanya kitu hicho ajulikane na kukamatwa kisha kufikishwa katika vyombo vya habari haraka sana.
Chuoni hakukukalika, kila kona kulikuwa na gumzo kuhusu kile kilichokuwa kimetokea. Kila mmoja alihuzunika, hawakuamini kama kungekuwa na mwanachuo ambaye angefanya kitu kama kile kwani kila walipoangalia na kufuatilia, hawakuona kama msichana Tatiana aliwahi kuishi Dar es Salaam, makazi yake yalikuwa Shinyanga kijijini, je huyo adui alikuwa nani?
“Huyu atakuwa yule Mrusi! Hivi anamtafutia nini huyu demu?’ aliuliza mwanachuo mmoja.
“Warusi wana roho mbaya sana, hawaangalii sababu, wao wanachotaka kuua tu, hakuna kingine,” alisema jamaa mwingine.
Hiyo ndiyo ikawa habari ya mjini, kila kona tukio hilo lilikuwa likizungumziwa tu. Redioni, taarifa hizo zilitangazwa huku magazeti yote ambayo yalitarajiwa kutoka siku inayofuata, yalionekana kuwa na habari hiyo kwa ukubwa zaidi, hivyo watu wakapanga kuyanunua ili wajue ukweli.
“Dokta! Tuambie ukweli!” alisema professa huku akiinuka kitini.
“Ukweli gani?”
“Juu ya Tatiana. Masaa matano yamepita, hatujui lolote lile,” alisema Professa.
“Naomba twendeni ofisini,” alisema dokta.
Hawakutaka kuchelewa, walichokifanya, wote wakaanza kumfuata daktari yule ambaye alipiga hatua za harakaharaka kuelekea ofisini mwake. Kwa muonekano aliokuwa nao tu ulionyesha kwamba kulikuwa na jambo baya lililokuwa limetokea mule chumbani hivyo kila mmoja akashikwa na hofu moyoni mwake.
