Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

105...
Tukio hilo lilifananishwa na lile la gari kulipuka kwa bomu nchini Marekani huku akiwa ndani ya gari hilo na rafiki yake. Kwa sababu katika tukio hilo mhusika alijulikana kwamba ni Petrov, hivyo hata katika tukio hilo lililotokea, watu wakajua kwamba kulikuwa na mkono wa Petrov.
“Ila huyu jamaa kwa nini anafanya hivi?” aliuliza jamaa mmoja.

“Hata mimi sijui.”
Jeshi la Polisi la Tanzania halikukaa kimya, kwa kile kilichotokea kilimaanisha kwamba nchi hiyo ilikuwa ikiingia kwenye aibu kubwa kimataifa hivyo amri kutolewa kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima mtu aliyefanya kitu hicho ajulikane na kukamatwa kisha kufikishwa katika vyombo vya habari haraka sana.
Chuoni hakukukalika, kila kona kulikuwa na gumzo kuhusu kile kilichokuwa kimetokea. Kila mmoja alihuzunika, hawakuamini kama kungekuwa na mwanachuo ambaye angefanya kitu kama kile kwani kila walipoangalia na kufuatilia, hawakuona kama msichana Tatiana aliwahi kuishi Dar es Salaam, makazi yake yalikuwa Shinyanga kijijini, je huyo adui alikuwa nani?

“Huyu atakuwa yule Mrusi! Hivi anamtafutia nini huyu demu?’ aliuliza mwanachuo mmoja.
“Warusi wana roho mbaya sana, hawaangalii sababu, wao wanachotaka kuua tu, hakuna kingine,” alisema jamaa mwingine.
Hiyo ndiyo ikawa habari ya mjini, kila kona tukio hilo lilikuwa likizungumziwa tu. Redioni, taarifa hizo zilitangazwa huku magazeti yote ambayo yalitarajiwa kutoka siku inayofuata, yalionekana kuwa na habari hiyo kwa ukubwa zaidi, hivyo watu wakapanga kuyanunua ili wajue ukweli.

“Dokta! Tuambie ukweli!” alisema professa huku akiinuka kitini.
“Ukweli gani?”
“Juu ya Tatiana. Masaa matano yamepita, hatujui lolote lile,” alisema Professa.
“Naomba twendeni ofisini,” alisema dokta.

Hawakutaka kuchelewa, walichokifanya, wote wakaanza kumfuata daktari yule ambaye alipiga hatua za harakaharaka kuelekea ofisini mwake. Kwa muonekano aliokuwa nao tu ulionyesha kwamba kulikuwa na jambo baya lililokuwa limetokea mule chumbani hivyo kila mmoja akashikwa na hofu moyoni mwake.
 
106..
Hakukuwa na mtu aliyekuwa tayari kupokea taarifa zozote mbaya, walimpenda Tatiana, hawakutaka kuona mschana huyo akifariki dunia kwani bado alionekana kuwa na kazi kubwa ya kuendelea kuitangaza nchi ya Tanzania.
Baada ya kufika ofisini, daktari yule akakifuata kiti chake na kutulia. Akaanza kuwaangalia watu wale, kwa mbali, machozi yakaanza kumlenga, kila mtu akahofia, hasa Buffet ambaye akashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake.
******

“Hali yake ni mbaya sana, mshipa mkubwa unaopeleka damu na ambao unavidhibiti vidole vyake umechanika,” alisema dokta huyo aliyekuwa na kibati kidogo pembeni ya kifua chake katika koti lake kilichoandikwa Dk. Henry.
“Kwa hiyo atapona?” aliuliza Buffet huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Naweza nikasema hamsini kwa hamsini. Ule ni mshipa muhimu sana, umechanika kiasi kwamba amepoteza kiasi kikubwa mno cha damu,” alisema Dk. Henry na kuendelea:

“Hali imeonekana kuwa mbaya zaidi tumboni, kisu kile kilizama na kuchana nyama zinazoshikilia mbavu kiasi kwamba kimeifanya damu kuvilia ndani ya tumbo lake hali ambayo inayoonyesha ni ya hatari sana, inaweza kumletea matatizo zaidi hata kifo chake,” alisema Dk. Henry huku akimwangalia kila mtu usoni.
Maneno aliyowaambia yaliwashtua mno, yaliongeza huzuni kwa Buffet ambaye bado alikuwa na mapenzi ya dhati kwa msichana wake ambaye aliamini kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima amuoe hapo baadae.

Dk. Henry hakutaka kuishia hapo, aliwapa maelezo ya kutosha kwamba hali ya Tatiana ilikuwa mbaya sana, tangu kipindi alichozimia, mpaka katika kipindi hicho hakuwa amerudiwa na fahamu. Alikuwa kwenye hali mbaya mno, kwa kumwangalia kwa nje tu ungeweza kugundua kwamba Tatiana alikuwa kwenye hali hiyo.

Buffet hakutaka kusikia kitu chochote, alichokuwa akikitaka ni kumuona msichana huyo tu. Aliambiwa kuwa hali ya binti huyo haikuwa nzuri lakini hakukubali, alihitaji kumuona msichana huyo hivyohivyo.
 
107...
Dk. Henry hakuwa na jinsi, kama alivyokuwa ametaka, hakuweza kuzuia, alichokifanya ni kuwachukua kisha kuwapeleka katika chumba alicholazwa Tatiana. Kitendo cha Buffet kumuona mpenzi wake akiwa hoi kitandani, machozi yaliyokuwa yakimbubujika yakaongezeka zaidi.
Tatiana alikuwa kimya kitandani, alipumua kwa kusaidiwa na mashine ya oksijeni, kwa juu yake, kulikuwa na dripu moja ya damu na nyingine ya maji ambazo zote hizo zilikuwa zikiingia mwilini mwake.

Kwa jinsi alivyoonekana kitandani pale, alimsikitisha kila mmoja, mamumivu moyoni mwa Buffet yakaongezeka zaidi, hakuamini kile alichokuwa akikiona mbele yake. Kwa hatua fupifupi huku machozi yakiendelea kumbubujika, akaanza kumsogelea msichana yule, alipomfikia, akainama na kumbusu katika paji lake la uso.

Alijikuta akishikwa na hasira za ghafla, akaanza kuwa na kisasi kikubwa moyoni mwake juu ya mtu aliyesababisha yale yote hali iliyomfanya kuhisi ni Petrov kwani huyo ndiye aliyekuwa akiyaweka maisha ya mchumba wake katika hali ya hatari.
Alijiapiza kumtafuta mtu huyo kwa gharama zozote zile na kumkamata kisha kumuuapopote pale kwa ajili ya kuupoza moyo wake ambao kila siku ulikuwa kwenye majonzi mazito.

Tatiana hakuinuka kitandani pale, alikuwa amepoteza fahamu huku akipumua kwa msaada wa mashine ya oksijeni. Siku zikaendelea kukatika, siku ya pili ikaingia, ya tatu ikajisogeza na mwisho wa siku wiki kukatika lakini bado hali ya msichana huyo ilikuwa mbaya kitandani pale.
Kila siku madaktari walijitahidi kuhakikisha kwamba Tatiana anapona kabisa lakini jambo hilo likawa gumu kwani kidonda alichokuwa amekipata mbavuni kiliendelea kuongezeka hali iliyoyahatarisha zaidi maisha yake.

“Ni lazima tumuhamishie Muhimbili,” alisema Dk. Henry.
“Hapa mmeshindwa?” aliuliza Professa.
“Hali ni mbaya zaidi, hatutakiwi kukaa naye sana, pale kuna wataalamu wengi na vifaa vyenye uwezo, nahisi watamsaidia,” alisema Dk. Henry.

Hawakuwa na cha kufanya zaidi ya kile walichokuwa wameambiwa. Siku iliyofuata, gari la wagonjwa likaandaliwa na hatimaye Tatiana kutolewa hospitalini tayari kuingizwa ndani ya gari huku akiwa juu ya machela ili safari ya kwenda Muhimbili ianze.
 
108...
Watu walijazana kwa wingi hospitalini hapo, wengi walimuona Tatiana akiwa kitandani, walihuzunika huku wengine wakilia kabisa, hawakuamini kile walichokuwa wakikiona kwamba msichana mrembo aliyebarikiwa kuwa tajiri baada ya kutoka kwenye umasikini, leo hii maisha yake yalikuwa juu ya kitanda.
Waandishi waliokuwa mahali hapo, kutoka kwenye vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi wakaanza kumpiga picha huku wakiwahoji baadhi ya watu waliokuwa mahali hapo ambapo wengi wakaanza kuelezea hisia zao juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

“Inaniuma sana, ni lazima huyu mtu apatikane,” alisema mwanamke mmoja miongoni mwa wale wengi waliokuwa wamekusanyika hospitalini hapo.
Kila mmoja alizungumza lake lakini wote walikuwa na maneno yaliyofanana kwamba walitamani kuona mtu aliyefanya tukio lile akikamatwa na polisi na kufikishwa mahakamani kutokana na kile kitendo alichokuwa amekifanya.
Watu wakapigiana simu na kupeana taarifa kwamba Tatiana alikuwa njiani kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili hivyo watu wengi kuanza kukusanyika hospitalini hapo kwa ajili ya kuona kile kilichokuwa kikiendelea.

King’ora kilikuwa kikipigwa kutoka katika gari lile la wagonjwa, watu wakapaki magari yao pembeni na kulipisha gari lile lililokuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi hali iliyowafanya watu kushangaa kwani hata kama lilikuwa gari la wagonjwa lakini haikutakiwa kuendeshwa kwa mwendo wa kasi namna ile kwani lingesababisha ajali endapo taili lingepata pancha ya ghafla.

Ndani ya gari lile, Buffet alibaki akimwangalia Tatiana, kama kulia alilia sana lakini hakukuwa na kitu kilichobadilika, kitendo cha Tatiana kulala kitandani pale kilimuumiza moyo wake hali iliyomfanya kila wakati kujiapiza kwamba ilikuwa ni lazima aliyefanya tukio lile akamatwe na kisha kulipa kisasi kwa kile kilichokuwa kimetokea.
“Nitampata tu,” alijisemea Buffet huku akiwa mwenye hasira kali.

Hawakuchukua muda mrefu wakaanza kuingia katika eneo la hospitali hiyo, gari hilo lilipoonekana kwa mbali tu, watu wakajua ndiyo lile lililombeba Tatiana hivyo kuanza kulisogelea huku watu wengine wakilipiga picha mfululizo.
 
109..
Polisi waliokuwa mahali hapo walijitahidi kuzuia ghasia zilizotaka kufanyika kwani kila mmoja alikuwa aking’ang’ania kumuona msichana huyo aliyekuwa hoi kitandani. Hakukuwa na shughuli zilizoendelea, japokuwa kulikuwa na walinzi getini lakini hawakutosha kuwazuia mamia ya watu walioingia hospitalini hapo wakitaka kumuona msichana huyo mrembo.

“Jaribuni kuwazuia,” alisema daktari huku akijiandaa kuufungua mlango wa gari lile.
“Mkuu! Hiyo si kazi nyepesi kabisa, watu hawa hatutoweza kuwazuia, tupo sita, wao wapo zaidi ya mia tano, tutawezaje sasa?” alihoji mlinzi mmoja.
Hata wale watu waliokuwa katika wodi nyingine kama ile ya watoto na watu waliokuwa wakisumbuliwa na magonjwa ya moyo, wakafika kule ilipokuwa gari ile ya wagonjwa kwani walisikia kwamba Tatiana angefika mahali hapo.

Mlango ukafunguliwa, muda wote watu walikuwa bize wakipiga picha juu ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Buffet akateremka, flashi za kamera zikaongezeka. Machela iliposhushwa, kila mtu akataka kusogea ili aweze kumuona Tatiana kwa karibu kabisa.
Wanawake wakashindwa kuvumilia, kile walichokiona kiliwaumiza mno, hawakuamini kama mwisho wa msichana yule ungekuwa namna ile. Machela ile ikaanza kusukumwa mpaka ndani ya jengo la hospitali hiyo ambapo jopo la madaktari kumi wakakutana kwa ajili ya kuizungumzia hali ya Tatiana, walitakiwa kupambana kufa na kupona lakini mwisho wa siku msichana huyo apone kabisa.
“Ripoti kutoka Marie Stoppes inasemaje?” aliuliza Dk. Kobe.

“Amechanika mshipa mkubwa wa damu pia amechanwa nyama zinazoshikilia mbavu mwilini mwake,” alijibu Dk. Mwaki huku akiwa ameshika karatasi tatu zilizokuwa na ripoti juu ya hali ya Tatiana.
Kila daktari alishikwa na hofu, hali aliyokuwa nayo Tatiana ilimuogopesha kila mmoja na kuona kwamba kama wasingepambana vya kutosha basi msichana huyo angeweza kufariki dunia. Kikao hicho kilichukua nusu saa tu, wakatawanyika na kuanza kazi mara moja huku jukumu kubwa la kuhakikisha Tatiana anarudi katika hali ya kawaida akipewa Dk. Kimario ambaye alikuwa bingwa wa upasuaji katika hospitali hiyo.
 
SEHEMU YA 110...
Hali ya Tatiana haikubadilika, japokuwa alipewa dawa za kuweza kukausha kidonda kikubwa alichokipata ubavuni mara baada ya kuchomwa kisu lakini kidonda kile hakikuacha kuvuja damu hali iliyomfanya kutokupata nafuu hata kidogo.
Kila siku ilikuwa ni lazima madaktari waendelee kumchunguza na kumpatia matibabu makubwa ili kuyaokoa maisha yake lakini hakukuwa na kitu kilichosaidia kwani bado kidonda kile kiliendelea kuhatarisha maisha yake kwa asilimia mia moja.

“Hapa tutashindwa, ni lazima tufanye kitu,” alishauri Dk. Kimario, mpaka kutamka maneno hayo, hakuona kama kungekuwa na jambo jingine la kufanya.
“Kitu gani?”
“Huyu mtu asafirishwe na kupelekwa India katika Hospitali ya Ganga yenye wataalamu wa mgonjwa kama huyu,” alijibu huku akionekana kuwa na uhakika.
“Yaani inamaanisha sisi tumeshindwa kabisa?”

“Hiyo ndiyo maana yangu. Sijawahi kushindwa lakini hali ya mgonjwa hasa kile kidonda kutokupona, imenitia hofu sana,” alisema Dk. Kimario.
Walichokifanya ni kumuita Buffet na kumwambia kile walichokuwa wameambiwa kwamba ili kuokoa maisha ya Tatiana ilikuwa ni lazima wamsafirishe na kumpeleka nchini India ambapo huko angepatiwa matibabu makubwa na kumrudisha katika hali ya kwaida.
“Kwa nini tusimpeleke Marekani?” aliuliza Buffet.

“Hapana! India ndiyo kwenye madaktari mabingwa na wagonjwa wa namna hii wamekuwa wakitibiwa sana huko. Tumejadili na kuona ni lazima apelekwe huko,” alisema Dk. Kimario.

Buffet hakuwa na pingamizi, akakubaliana nao kwamba ilikuwa ni lazima mpenzi wake asafirishwe na kupelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu.
“Mungu! Naomba umuokoe Tatiana kwani akifa, nitakuwa na hasira zaidi na mtuhumiwa,” alisema Buffet huku akiyauma meno yake kwa hasira.
 
SEHEMU YA 111...
Kijiji cha Chibe hakikuwa kijiji tena, mabadiliko makubwa yaliyokuwa yametokea yalimshangaza kila mtu aliyekwenda kukiangalia. Kipindi cha nyuma kilitawaliwa na nyumba za nyasi huku kukiwa na nyumba moja tu ambayo iliezekwa kwa bati.
Kwa wakatihuo Chibe ile iliyokuwa kipindi cha nyuma haikuwa hii ya sasa, majengo makubwa yalijengwa, kukawa na mabomba mengi ya maji yaliyopitishwa chini, umeme wa kutosha ulikuwepo, yote haya yalifanywa na msichana Tatiana katika kipindi alichokuwa nchini Marekani.

Heshima kwa wazazi wake ikaongezeka zaidi. Wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali wakafika kijijini hapo na kuwekeza kwa kufungua maduka makubwa, soko kubwa na vitu vingine vingi ambavyo vyote hivyo vilikifanya eneo la kijiji kile kuongezeka zaidi.
Hakukuwa na matatizo ya afya tena, kulikuwa na hospitali kubwa ambapo madawa yote yalipatikana, kulikuwa na wauguzi waliokuwa na ubora zaidi, kwa kifupi, kwa kila kitu kilichokuwa kikiendelea, Tatiana aliamua kuyabadilisha maisha ya watu wa kijiji hicho.

Katika siku ambayo Tatiana alikaribia kutua nchini Tanzania, tayari taarifa zikasambazwa, wazazi wake na wanakijiji wengine wakawa na shauku kubwa ya kutaka kumuona msichana huyo ambaye alipoondoka nchini nchini Tanzania, tayari miaka mitatu na nusu ilikuwa imepita pasipo kurudi.
“Kumbe anarudi?”
“Ndiyo! Nimesikia anafika kesho.”
“Na atafika na huku?”
“Sasa si ndiyo kwao! Kwa nini tena asifike?”

Walikuwa wanakiji wawili waliokuwa wakizungumza, taarifa za kufika kwa Tatiana nchini Tanzania zilijulikana dunia nzima hivyo Watanzania wakajipanga kwa ajili ya kumpokea ndugu yao. Siku hiyo ilipofika, wanakijiji wakapewa taarifa kwamba tayari msichana huyo alikuwa ameingia nchini Tanzania na ndani ya wiki hiyo, angefika kijijini hapo alipozaliwa.
Kila mmoja akajisikia wa thamani moyoni mwake, kitendo cha kijiji hicho kutangazwa zaidi na zaidi kiliwaongezea umaarufu mkubwa hivyo wakawa na kiu ya kumuona msichana huyo akiingia ndani ya Kijiji cha Chibe.

“Unasemaje?”
“Nimesikia alitaka kuuawa?”
“Alitaka kuuawa? Kivipi tena? Yaani yeye mwenyewe alitaka auawe?”
“Hapana! Kuna mtu amemchoma kisu.”
“Wapi?”
 
SEHEMU YA 112...
“Hukohuko Mjini Dar es Salaam,” alisema mwanakijiji mmoja.
Kila mmoja alishtuka, hawakuamini kile kilichokuwa kimetokea kwamba msichana Tatiana alichomwa kisu akiwa Dar es Salaam akizungumza na wanachuo wa chuo kikuu.
Bi Frida alilia sana, hakuamini kile kilichotokea hivyo kumwambia mume wake kwamba iwe isiwe ni lazima waelekee jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumuona binti yao kipenzi. Hawakutaka kuendelea kukaa Chibe, walichokifanya ni kuondoka na kuelekea Dar.

Njiani ndani ya ndege, muda wote bi Frida alikuwa akilia tu, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, kila alipomkumbuka binti yake kipenzi, alijisikia maumivu makali mno. Mzee Sangiwa akawa na kazi kubwa ya kumbembeleza mke wake ambaye hakunyamaza kabisa.

“Nyamaza mke wangu! Ngoja tufike kwanza,” alisema mzee Sangiwa.
Walichukua masaa mawili mpaka kufika Dar es Salaam ambapo moja kwa moja wakaenda kuchukua chumba hotelini na kisha kuanza kuelekea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo huko wakapelekwa moja kwa moja mpaka kwa Dk. Kimario ambaye akawachukua na kwenda naye ofisini huku akiwa na Buffet ambaye kwao alikuwa mgeni ila walijua fika kwamba alikuwa akitembea na binti yao baada ya kuachana na Smith ambaye ndiye walikuwa wakimfahamu.
“Afadhali mmefika,” alisema Dk. Kimario.
“Asante. Ila nini kinaendelea?”

“Ni kwamba binti yenu alichomwa kisu.”
“Vyote tunajua, tunahitaji kujua nini kinaendelea baada ya yeye kuchomwa kisu?” aliuliza mzee Sangiwa.
“Tumejaribu kumtibia lakini hali imekuwa ngumu zaidi hivyo ni lazima asafirishwe.”
“Kwenda wapi?”
“India.”
“Lini?”
“Kesho!”

Bi Frida akazidi kulia zaidi, hakuamini kama kweli mwanaye alitakiwa kusafirishwa na kupelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu. Hapo ndipo walipojua kwamba kweli tatizo alilokuwa amelipata binti yao lilikuwa kubwa na lingeweza hata kupoteza maisha yake.
Mioyo yao iliumia lakini hawakuwa na jinsi, walitakiwa kukubaliana na ukweli kwamba binti yao alitakiwa kusafirishwa na kuelekea nchini India kwa ajili ya matibabu.
“Na sisi tunakwenda.”
 
SEHEMU YA 113...
“Kama mnataka kwenda sawa ila si kwa kesho. Tayari tushafanya maandalizi, tiketi zishapatikana, kama mnataka kwenda nafikiri inatakiwa kufanyika keshokutwa,” alisema Dk. Kimario.
Huo ndiyo uamuzi uliofikiwa, japokuwa hawakutakiwa kuondoka kesho yake lakini wakaomba ruhusa ya kutaka kumuona binti yao, hilo wala halikuwa tatizo, wakachukuliwa na kupelekwa katika chumba alicholazwa Tatiana.

Walipofika hapo, macho yao yalipotua kwa msichana huyo, mzee Sangiwa ambaye macho yake yalikuwa makavu, akashangaa kuona yakianza kulengwalengwa na machozi na ndani ya sekunde kumi tu, machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake.
Alihisi maumivu makali ya moyo, kwa jinsi binti yake alivyokuwa kimya kitandani pale, alijikuta akikata tanmaa ya kuona akinyanyuka tena kitandani pale. Wakamsogelea, bi Frida alikuwa hoi, tayari machozi yaliyokuwa yamekauka kwa muda yakaanza kububujika tena mashavuni mwake.

Picha ile iliyokuwa ikionekana mbele yake ilimuumiza mno, hakuamini kama binti yake aliyempenda kwa moyo wote, msichana aliyetokea kuwasaidia wao kama wazazi wao na kijiji kizima alikuwa kimya kitandani.
“Tatiana amka mwanangu,” alisema bi Frida huku akiendelea kububujikwa na machozi ya uchungu.

Bandeji kubwa ilifungwa tumboni mwake huku bandeji nyingine kubwa ikifungwa kwa wingi ubavuni mwake ambapo hapo ndipo kulipokuwa na jeraha lile la kuchomwa kwa kisu. Mbali na hiyo, hata mkono wake wa kushoto kulikuwa na bandeji nyingine ambayo kwa mbali ilionekana kuchafuliwa kwa damu zilizokuwa zikiendelea kumtoka japo kwa taratibu sana.

“Dokta, mwananagu ataamka lini?” aliuliza mzee Sangiwa huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Ataamka tu.”
“Lini?”
“Hatujajua, ila India ndioyo watatuambia kila kitu. Tumejitahidi sana kuokoa maisha yake, tunatumaini ataamka tu,” alisema Dk. Kimario.

Japokuwa walikuwa na huzuni sana, kulia sana lakini hiyo haikutosha kumuinua Tatiana kitandani pale. Watu walijazana mno hospitalini, kila mtu aliyefika mahali hapo alitaka kuingia ndani ya chumba kile kwa ajili ya kumuona mwanamuziki huyu aliyekuwa hoi kitandani.
 
SEHEMU YA 114...
Hospitali ya Muhimbili ikatembelewa na masupastaa wengi kutoka sehemu nyingine nyingi hasa katika nchi za jirani, kila aliyefika mahali pale na kumuona Tatiana pale kitandani, alihuzunika na kuona kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wa msichana huyo.
“Dokta! Atapona kweli?” aliuliza Golden, mwanamuziki aliyekuwa na jina kubwa nchini Tanzania kipindi hicho.
“Kupona atapona, ila itabidi apelekwe India, vinginevyo, tutashindwa kuyaokoa maisha yake,” alisema Dk. Kimario.
Mbali na wasanii, pia walifika mpaka viongozi wa nchi, mawaziri mbalimbali akiwemo rais na balozi wa Marekani, wote walifika mahali hapo kwa ajili ya kumjulia hali Tatiana ambaye hakuwa na habari juu ya watu walioingia na kutoka chumbani humo.

Maandalizi yaliendelea kufanyika na siku iliyofuata, tayari safari ilitakiwa kuanza kuelekea nchini India. Ndege ya Shirika la Ndege la Indians Airlines ndiyo iliyowabeba na kuanza safari ya kuelekea nchini humo.
Buffet alitulia kitini, hakuwa mbali na mahali ambapo mpenzi wake alipokuwa, alitamani kukaa karibu naye ili hata kama kungetokea muujiza kwa msichana huyo kufumbua macho, basi yeye awe wa kwanza kuona hilo likitendeka.

Safari aliiona kuwa ndefu mno, alitamani wafike nchini India haraka iwezekanavyo kwani hali ya Tatiana ilizidi kuwa mbaya kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Baada ya masaa ishirini na tatu, ndege ikaanza kuingia ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ghandhi na moja kwa moja akuanza kuelekea katika Hospitali ya Ganga ambayo haikuwa mbali kutoka uwanjani hapo.

Walichukua dakika ishirini mpaka kufika katika hospitali hiyo ambapo machela ikashushwa kisha kuanza kusukumwa kuelekea ndani ya jengo la hospitali hiyo. Wakati madaktari walipoona kwamba mtu waliyemtarajia amefika, jopo zima la madaktari ishirini wakakutana katika chumba chao huku wakiwa na ripoti iliyokuwa imetumwa kutoka nchini Tanzania, walipofika kwenye chumba hicho, kitu cha kwanza kila mtu akapewa ripoti ile na kuanza kuipitia.
 
SEHEMU YA 115...
“Kuna kazi kubwa mbele yetu,” alisema Dk. Muntesh, daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake hospitalini hapo.
“Ila nadhani tutafanikiwa na kuiletea heshima nchi hii, hasa kuitangaza hospitali hii,” alisema daktari mwingine, Dk. Kandesh.
“Hilo ndiyo lengo letu. Cha msingi tuanze kazi,” alisema Dk. Madesh ambaye akakabidhiwa jukumu hilo na kusaidiana na madaktari wengine wawili. Kazi ikaanza mara moja huku Buffet akiwa na uhakika kwamba mpenziwake angeweza kupona.
*****

Moyo wa Peter ukaridhika kutokana na kile alichokuwa amekifanya, kitendo cha kumchoma kisu Tatiana na kulazwa hospitalini huku akiwa na lengo la kummaliza kabisa lilimfurahisha mno. Alijiona kutenda haki kwani kile alichofanyiwa na msichana yule hakikuweza kusahaulika moyoni mwake.
Chuki yake haikupungua, kila alipomfikiria msichana huyo, bado alijiona kuwa na kila sababu kuweza kummaliza kabisa. Aliposikia kwamba msichana yule alipelekwa hospitalini na hali yake ilikuwa mbaya, alifurahi mno.

Japokuwa alikuwa amefanya kitu hicho kibaya lakini moyo wake haukuacha kumuomba Mungu, kila siku alipiga magoti chini na kusali, alikwenda kanisani kila alipohitajikahuku wakati mwingine akihubiri neno la Mungu kanisani humo.
Kile alichokuwa amekifanya, wala hakikuonekana kuwa dhambi, kila aliposimama mbele ya watu na kuhubiri kisha kukumbuka tukio lile la kumchoma Tatiana kisu, aliona kama alistahili kufanya vile kwa kile kilichokuwa kimetokea.

Magazeti na vyombo vingine vya habari viliendelea kutoa taarifa kwamba hali ya msichana yule ilikuwa mbaya mno na hivyo isingewezekana kutibiwa nchini Tanzania, alitakiwa kusafirishwa na kupelekwa nchini India.

Taarifa zote alikuwa akizifuatilia lakini bado alitaka kuona msichana huyo akiendelea kuteseka kitandani kwani hakukuwa na kitu kingine ambacho alitakiwa kukipata zaidi ya kile.
“Afi tu!” alijisemea huku akionekana kuwa na hasira.
 
SEHEMU YA 116...
Nathan alifuatilia kila kitu, mara baada ya kuambiwa juu ya chumba alichokuwa amechukua Tatiana, akajiandaa kwa ajili ya kummaliza msichana huyo. Kitu cha kwanza kabisa alichokifikiria ni kumpa kinywaji kilichokuwa na sumu ili atakapokunywa aweze kufa.
Wazo hilo lilikaa akilini mwake lakini kuna kipindi akajiona mjinga kwani angeweza vipi kumpa kinywaji msichana huyo? Kitu cha pili ambacho kilimjia kichwani mwake ni kumpiga risasi Tatiana, pia ugumu katika hilo ukajitokeza juu ya mahali ambapo angeweza kupata bastola kwa ajili ya kumpiga msichana huyo risasi, napo akakosa jibu.

Kitu cha mwisho kabisa kilichokuja akilini mwake ni kumuua msichana huyo kwa kumchomachoma na kisu. Hilo likawa wazo zuri lililopokelewa kwa mikono miwili kichwani mwake, hakukuwa na kazi kubwa ya kupata kisu kwani humohumo hotelini angeweza kukipata na hivyo kumuua Tatiana.

Usiku hakulala, alikuwa akifikiria namna atakavyomuua msichana huyo na kisha kukimbia, hata kama kukamatwa, akamatwe wakati amekwishamuua na kuuridhisha moyo wake. Akajiandaa vilivyo, asubuhi ilipofika, akamuita kijana yule aliyekuwa amemuhudumia na kumuagiza kumletea kisu.
“Cha nini tena?” aliuliza kijana yule.
“Nina kazi nacho.”

“Hapana bwana, haiwezekani, huwa haturuhusiwi kumpa kisu mteja,” alisema kijana yule.
Japokuwa alimuahidi kwamba angemsaidia kwa kila kitu lakini hilo likawa gumu kufanyika, mhudumu yule hakutaka kumpa kisu Nathan kwani moja ya sheria ya hoteli hiyo haikuruhusu kitu kama hicho kifanyike.

Alibembeleza na kubembeleza lakini msimamo wa mhudumu yule ulikuwa uleule kwamba kisu hakikutoka. Nathan hakutaka kubembeleza sana, alichokifanya ni kutoka nje ya hoteli ile na kwenda kule kulipokuwa kunapaki daladala nyingi, katika Kituo cha Ubungo Terminal.
Alikuwa na uhakika kwamba huko angeweza kupata kisu, alipozungukazunguka huku na kule, akafanikiwa kupata kisu kwa muuza vyombo vya ndani ambapo akampatia kiasi cha shilingi elfu kumi, pasipo kuomba chenji yake akaondoka zake.
 
SEHEMU YA 117...
Kila kitu alichokuwa akikitaka kilikamilika. Kwa wakati huo alikuwa tayari kwa kila kitu, alikuwa radhi kuona akikamatwa na polisi na kufungwa lakini mwisho wa siku alitaka kuhakikisha msichana huyo akifariki dunia.
“I will kill her by using this knife,” (nitamuua kwa kutumia kisu hiki) alijisemea Nathan wakati anakiangalia kisu kile.

Siku hiyo ndiyo alipanga kufanya kile alichotaka kukifanya. Hakutaka kuchelewa, japokuwa Petrov alimwambia kwamba alikuwa njiani kuja nchini Tanzania lakini hakutaka kumsubiria, alitaka kufanya kila kitu kivyakevyake kwa kuamini kwamba kama nafasi alikuwa ameipata nchini Marekani lakini hakuifanyia kazi, hivyo kwake aliuona kuwa uzembe mkubwa mno.

Siku hiyo, kila wakati alikuwa akimuita mhudumu yule ambaye alimzoea na kumuulizia kama Tatiana alikuwa amefika au la. Kila alipomuuliza, alimwambia kwamba hakufika na kama angefika angemwambia ili azungumze naye.
“I will let you know, brother,” (Nitakujulisha, kaka) alisema mhudumu yule.

Muda haukusubiri, uliendelea kusonga mbele huku Nathan akiwa kwenye presha kubwa ya kutaka kuonana na Tatiana ili aweze kumuua na kurudi zake nchini Liberia au hata kama kukamatwa, akamatwe lakini akiwa tayari amemuua msichana huyo.

Ilipofika saa tatu usiku, hakukuwa na dalili za kumuona Tatiana hotelini hapo, akashindwa kuelewa ni kitu gani kilichokuwa kimetokea, alichokifanya ni kumuita mhudumu yule kwa lengo la kutaka kujua ukweli juu ya kilichokuwa kimetokea, kama alifika na kuingia kimyakimya au la!.

“Haujapata taarifa?” aliuliza mhudumu yule.
“Taarifa gani?”
“Tatiana ameuawa!”
“Tatiana ameuawa? Na nani? Wapi? Saa ngapi?” aliuliza Nathan maswali manne mfululizo.
“Alikwenda chuo, kuna mtu alimchoma kisu.”
“Nani?”
“Mpaka sasa hivi haijajulikana. Angalia kwenye televisheni,” alisema mhudumu yule.

Nathan hakutaka kusubiri kule chini, alichokifanya ni kupandisha lifti harakaharaka ili aweze kuingia chumbani kwake na kuangalia kwenye televisheni kile kilichokuwa kimetokea, alipofika tu, kitu cha kwanza kilikuwa ni kufungua CNN na kuangalia, habari zilizofika punde ziliendelea kuionyeshwa juu ya kile kilichokuwa kikiendelea nchini Tanzania.
 
SEHEMU YA 118...

“Nani aliyefanya hivi?” alijiuliza huku akiwa haelewielewi,” alisema Nathan huku akiikodolea macho televisheni ile.
Moyo wake haukufurahia hata kidogo, japokuwa alichokiona ndicho kile alichotaka kukifanya lakini hakufurahia kabisa, alitaka kukifanya kile kwa mikono yake na si kufanyiwa na mtu mwingine.
“Huu ni upumbavu, nitakwenda hata hospitalini, lakini ni lazima nimuue kwa mkono wangu,” alisema Nathan huku akionekana kuwa na hasira, wala hazikupita siku nyingi, akapata taarifa kwamba Tatiana alikuwa amesafirishwa na kuelekea nchini India kwa ajili ya matibabu.

Hakutaka kukubali, alihitaji kumaliza kazi hiyo haraka iwezekanavyo, mara baada ya kujua kwamba msichana huyo alitarajia kupata matibabu katika Hospitali ya Ganga, baada ya wiki moja naye akapanda ndege kuelekea huko, hakukubali kurudi nchini Liberia kabla ya kutimiza kile alichokitaka. Alidhamiria kumuua msichana huyo.
 
SEHEMU YA 119...
Madaktari wa Hospitali ya Ganga walijitahidi usiku na mchana kuhakikisha kwamba Tatiana anapona na kurudi katika hali yake ya kawaida. Hakukuwa na mtu aliyelala, walipishana ndani ya chumba kile kwa zamu huku kila mmoja akijitahidi hata kushauri juu ya kile kilichotakiwa kufanyika.
Kitu cha kwanza kabisa ambacho walikifanya ni kuhakikisha kwamba ile damu iliyokuwa inavuja ubavuni inakatika kwani kama ingeendelea vile ilikuwa ni lazima kumwagikia tumboni na hatimaye kupata matatizo zaidi, hivyo wakaanza kulishughulikia suala hilo.

“Tunahitaji kwanza kuua wadudu, lete dawa ya Cristapen,” alisema Dk. Mandesh ambaye ndiye yule aliyepewa jukumu zito la kuhakikisha kwamba msichana Tatiana anarudi katika hali yake ya kawaida.
Akakabidhiwa dawa ile na kisha kuanza kuipulizia ndani ya tumbo la Tatiana kwa kupitia katika jeraha lile alilolipata kwani kabla ya kufanya chochote kile ilikuwa ni lazima kuhakikisha kwamba wadudu wote ambao wangeweza kupita kupitia jeraha lile wanadhibitiwa haraka iwezekanavyo.
Baada ya kuhakikisha kwamba wamefanikiwa kufanya hivyo, mikasi zaidi iliandaliwa kwani kitu kingine walichotakiwa kufanya ni kuchunguza kidonda kile hasa katika nyama zile zilizokuwa zimechanwa na kisu kile.

“Hili ni tatizo kubwa sana, nahisi kunyunyizia dawa ya Cristapen haitoshi, ngoja tuikate kabisa damu hii,” alisema Dk. Mandesh na kisha kufanya hicho alichokuwa amekisema, shughuli ya kukata damu ile ikaanza mara moja.
 
SEHEMU YA 120...
Nathan akatua nchini India katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Coimbatore iliokuwa katika Jiji la Coimbatore. Alipoteremka, akaanza kupiga hatua kuelekea nje ya uwanja huo ambapo akachukua begi lake na kisha kuanza kupiga hatua nje ya jengo la uwanja huo.
“Where to brother?” (Unakwenda wapi kaka?) aliuliza dereva teksi mmoja aliyekuwa amesimama pembeni ya teksi yake.

“Do you know any seven star hotel?” (Unaijua hoteli yoyote ya nyota saba?) aliuliza Nathan.
“Yaap brother! What about Sea Clif Hotel?” (Ndiyo kaka! Unaonaje Hoteli ya Sea Clif?)
“Where is it located?” (Ipo eneo gani?)
“Almost one kilometre from here?” (Kama kilometa moja kutoka hapa)
“And, do you know Ganga hospital?” (Unaifahamu Hospitali ya Ganga?)
“Yaap!”
“Where is it located?” (Ipo eneo gani?)
“That one....” (Ile pale) alisema dereva yule huku akiinyooshea kidole hospitali hiyo, haikuwa karibu, ila kwa kuwa ilikuwa na ghorofa kubwa lililoonekana mpaka hapo, dereva akaona bora amuonyeshee.
Nathan akaridhika, alichokifanya ni kumwambia dereva waelekee katika hospitali ile ambapo malipo yake yalikuwa ni rupii kumi tu. Wakaingia garini na safari kuanza. Japokuwa drevea alikuwa akileta uchangamfu mkubwa lakini kwa Nathan, aliamua kutulia kwani kichwa chake ilikuwa na mawazo mengi.

Alisumbuka sana mpaka kufika nchini Tanzania, alipokuwa hapo, bado alihitaji kusafiri tena kuelekea nchini India ambapo huko ndipo alipopanga kufanya mauaji yake. Bado chuki kubwa dhidi ya Tatiana ilikuwa moyoni mwake, hakumpenda msichana yule na alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile ili mradi afe tu.

Hawakuchukua muda mrefu sana wakawa wamekwishafika katika hospitali hiyo ambapo Nathan akaanza kuiangalia kwa makini, hakutaka kuteremka kutoka garini, alibaki humo huku akiiangalia tu.
“Ndiyo hapa,” alisema dereva yule.
“Ok! Nashukuru! Kuna hoteli hapa karibu?”
“Ndiyo! Ila si nyota saba.”
 
SEHEMU YA 121...
“Nipeleke hiyohiyo, hata kama nyota tano,” alisema Nathan na kuanza kupelekwa huko. Walipofika, wakateremka na kisha kuelekea mapokezini ambapo akachukua chumba na kufuata lifti kupandisha chumbani kwake.
Huko, muda wote macho yake yalikuwa dirishani, alikuwa akifuatilia kwa karibu kila kilichokuwa kikiendelea nje ya hospitali ile. Kama kawaida, kutokana na umaarufu mkubwa aliokuwa nao Tatiana, Wahindi wengi wakiwemo waandishi wa habari walikuwa wamekusanyika nje ya jengo la hospitali ile kwa lengo la kuingia ndani ili waweze kumuona Tatiana.
“Hapa patafaa sana, ngoja nianze kutafuta njia ya kuingia ndani ya hospitali ile. Nitaingia kama daktari, ngoja nitafute kile kitu kinachohitajika,” alisema Nathan.

Kitu chepesi ambacho aliona kama kingefanyika basi kingempa nafasi kubwa ya kumuua Tatiana ni kuingia ndani ya chumba kile huku akiwa na mavazi ya kidaktari ambayo aliamini kwamba kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angeweza kumgundua kwani hospitali hiyo ilikuwa na madaktari wengi mpaka wengine kutokujuana.

Siku iliyofuata, Nathan akaondoka kuelekea mitaani ambapo huko akaanza kuzungukazunguka kwenye maduka makubwa kwa ajili ya kununua mavazi kama ya kidaktari kwa ajili ya kukamilishia kile alichotaka kukifanya.
Kwa kuwa alikuwa na fedha za kutosha, tena akitokea katika familia ya bilionea mmoja nchini Liberia, kuhusu kununua mavazi hayo kwa gharama kubwa wala hakukuwa na tatizo lolote lile, alipoyanunua mavazi hayo, akanunua na mashine ya kusikilizia mapigo ya moyo iitwayo stetoscope kisha kurudi hotelini.
Usiku mzima alikuwa akijifikiria namna ya kuingia hospitalini mule na kufanya kile alichokikusudia pasipo kugundulika na mtu yeyote yule. Mchana wa siku hiyo, akaelekea katika hospitali ile ambapo bado waliendelea kujazana huku kila mmoja akitaka kumuona Tatiana ambaye uwepo wake ndani ya hospitali ile ulimpa umaarufu mkubwa hata zaidi ya waziri mkuu wa nchi hiyo.

Nathan hakutaka kuingilia mlango wa mbele, alitaka kuingilia mlango wa nyuma kabisa, hiyo yote ilikuwa ni kufanya upelelezi wake kama kulikuwa na ulinzi mkali mahali pale.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom