Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

umenikera sana kumuacha peter,kama haitoshi na smith tena yani kufungua tu macho mwanaume anayekutana nae anamtaka,je akitoka nje akutane nawadunia nzima si atachanganyikiwa sasa
Kachanganyikiwa na kuona mama
 
SEHEMU YA 81...
Japokuwa hakutaka kuwa mpenzi wake lakini Dk. Buffet alimheshimu sana Tatiana, alimchukulia kama rafiki yake wa karibu na ndiye alikuwa mtu pekee aliyemfanya kujulikana zaidi duniani na kujikuta akiheshimiwa kila alipokuwa.
Hakutaka kumuacha binti huyo, aliendelea kuwa karibu naye huku kwa kila alichokuwa akikifanya, alikifuatilia kwa karibu mno.

Kitendo cha Smith kumpiga msichana huyo kilimkasirisha mno, alitamani akutane na Smith na kumwambia ni kwa kiasi gani alikichukia kitendo hicho lakini pia akahofia kuingilia mapenzi ya wapendanao, hivyo akaachana naye.
Aliposikia kwamba gari alilopanda msichana Tatiana lililipuliwa kwa bomu, akashikwa na presha, alihisi mwili wake ukitetemeka mno. Hata yeye mwenyewe alijua kwamba aliyefanya kila kitu alikuwa Smith, hivyo akaanza kumchukia mno.
“Huyu si rafiki tena,” alisema Buffet huku akikunja uso wake kwa hasira.
 
SEHEMU YA 82...
Mara baada ya kuona gari likiwa limelipuka, Petrov hakutaka kubaki mahali hapo, moja kwa moja akawasha gari lake na kuondoka mahali hapo. Moyoni alikuwa na furaha mno, hakuamini kama ile kazi aliyokuwa amepewa angeikamilisha kwa haraka na kwa wepesi namna ile, moyoni mwake akawa na furaha tele kwa kuona kwamba rekodi yake ya kukamilisha kazi zake kwa asilimia mia moja ilikuwa ikiendelea kama kawaida.

Hakutaka kukaa sana nchini Marekani kwa kuogopa kukamatwa, alichokifanya, kesho yake akaondoka kurudi nchini Liberia huku moyo wake ukiwa na furaha mno.
“Nimekamilisha kila kitu,” alisema Petrov alipokuwa akizungumza simuni na Nathan mara baada ya kufika Liberia.
“Hapana! Kazi haikukamilika.”
“Haikukamilika, kivipi na wakati gari lililipuka na yeye akiwa ndani?” aliuliza Petrov huku akionekana kushtuka.
“Tatiana hakufa!”
“Hakufa? Kivipi?”
“Upo sehemu yenye televisheni?”
“Ndiyo!”
“Hebu tazama LTV,” alisema Nathan na Petrov kuwasha televisheni yake na kuweka kituo hicho cha habari ambacho kilijiunga na CNN.

Hakuamini macho yake kile alichokuwa akikiona mahali hapo, Tatiana alikuwa akihojiwa huku akiwa hospitalini, alikuwa akizungumzia kile kilichokuwa kimetokea wakati mlipuko mkubwa ulipotokea.
Petrov hakuamini kile alichokuwa amekisikia, hakujua binti yule alinusurikaje na wakati gari lililipuka na kusikia kelele za yeye na rafiki yake wakipiga kelele na yeye kuondoka. Akajikuta akibadilisha muonekano wa sura yake, akayauma meno yake kwa hasira huku akipanga kurudi tena nchini Marekani.
“Ni lazima nirudi kukamilisha kazi,” alisema Petrov, alikuwa akimwambia Nathan.
“Hapana! Unatafutwa huko.”
“Natafutwa?”
“Ndiyo! Kila mtu anajua kwamba wewe ndiye uliyehusika katika mlipuko huo,” alisema Nathan.
“Haiwezekani!”
“Wewe endelea kutazama televisheni utaliona hilo.”

Petrov akatulia na kuendelea kutazama televisheni, baadae akaiona picha yake ikiwekwa hadharani siku ambayo alihusika katika kulitega bomu lle, picha ile ilikuwa imepigwa kwa kamera ndogo za CCTV zilizokuwa zimewekwa nje ya ukumbi ule.
“Siwezi kurudi, ila nitafanya juu chini huyu mpumbavu afe,” alisema Petrov.
 
SEHEMU YA 83...
Tatiana aliyafumbua macho yake, mtu aliyemuona mahali hapo alikuwa Buffet, tabasamu kubwa likautawala uso wake, hakuamini kama mwanaume huyo angekuwa mtu wa kwanza kuingia chumbani mule kuja kumuona.
Alimpenda sana Nathan, alimchukulia kuwa kila kitu katika maisha yake. Mpaka katika kipindi hicho, mwanaume huyo hakuwa amekubaliana naye kitu kilichompa huzuni kubwa moyoni mwake.
Alichokifanya ni kumuita na kisha kuangaliana kwa karibu. Kila alipokuwa akimwangalia Buffet alishindwa kujizuia na kumwambia tena juu ya hisia kali za kimapenzi alizokuwa nazo kitu kilichomfanya Buffet kuelewa zaidi.
“Tatiana....”
“Abeeee...”

“Pona kwanza, mengine tutayazungumza,” alisema Buffet.
“Najua, lakini ninakuhitaji wewe. Tangu kipindi kile niligundua kwamba Smith hakuwa mwanaume wangu sahihi, ukapingana nami, si umeona mwenyewe.”
“Nimeona Tatiana, lakini bado tunatakiwa kukaa chini na kuzungumza.”
“Sawa. Ila nakupenda sana.”
“Asante.”

Buffet hakuwa na jinsi, Tatiana alipotoka hospitalini, wakakutana katika chakula cha usiku kwenye Mgahawa wa McDonald, wakaanzisha uhusiano mpya wa kimapenzi ambao ulivuma sana katika magazeti na majarida mbalimabali.
Huo ulikuwa mwaka wa tatu tangu amuache Peter, na hakuwa amerudi nchini Tanzania.
**** Kama kuumia Peter aliumia sana lakini hakukuwa na kilichobadilika maishani mwake. Mapenzi yalimtesa mno, yalimkondesha kupita kawaida lakini hakuwa na la kufanya, bado mpenzi wake wa siku nyingi, Tatiana hakurudi maishani mwake.

Mpaka mwaka unamalizika na kuingia kidato cha sita, Tatiana hakuwa amerudi nchini Tanzania, maisha yake yalibadilika na hakuwa msichana yule aliyekuwa masikini bali alikuwa msichana tajiri, mwenye jina kubwa na fedha nyingi.
Peter hakujua kama msichana huyo angeweza kumkumbuka maishani mwake, kila alipokuwa akimwangalia kwenye televisheni, alijikuta akibubujikwa na machozi kwani hakujua ni kitu gani angefanya mpaka msichana huyo kurudi na kuwa kama zamani.
Mwaka huo alijitahidi sana katika masomo yake na alipomaliza, akaanza kukaa nyumbani huku akisubiri matokeo ya mtihani wa kidato cha sita.
 
SEHEMU YA 84...
Katika kipindi hicho ndicho alichokutana na msichana Lydia Andrew. Alikuwa msichana mrembo, mwenye heshima kubwa huku akiwa Mkristo mwenye kumaanisha. Peter alikutana na msichana huyu katika Kongamano la CASFETA lililofanyika mkoani Dodoma.
Hilo ni kongamano kubwa la Vijana wa Kikristo ambalo hufanyika kila mwaka katika mkoa ambao hupangwa. Katika kongamano hilo, vijana walikuwa wakiweka kambi sehemu ambapo huko humuimbia Mungu na kufanya maombi mbalimbali. Alipokutana na msichana huyo, akahisi moyo wake ukianza kumpenda na kuona kwamba inawezekana msichana huyo akawa mke wake baadae.
“Bwana Yesu Asifiwe,” alisalimia Peter.
“Amen!” aliitikia Lydia.
“Umependeza mno, na umenibariki sana kwa siku ya leo, una sauti nzuri sana,” alisema Peter.

“Utukufu kwa Mungu mpendwa!”
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa mazungumzo yao, Peter hakutaka kumuonyeshea Lydia kwamba alikuwa akimpenda, alimheshimu kwani alijua kwamba huo haukuwa muda sahihi wa kumwambia kile alichokuwa amekipanga maishani moyoni mwake.
Aliyahisi mapenzi mazito moyoni mwake, kila walipokuwa kanisani wakiimba, macho yake yalikuwa yakimwangalia Lydia aliyekuwa na sauti nzuri kila alipokuwa akiimba. Hakujua ni kwa namna gani angeweza kuzifikisha hisia zake kwani kila siku moyo wake uligalagazwa vibaya.
Kongamano hilo lililofanyika Dodoma lilichukua wiki mbili na ndipo wakatakiwa kurudi nyumbani kwao. Kwa Peter hakutaka kukubali kirahisi, hakutaka huo uwe mwisho wa kuonana na msichana huyo, alichokifanya ni kumfuata na kuanza kuzungumza naye.
“Lydia...” aliita.
“Abee kaka Peter!”
“Hahaha! Kumbe unanijua!”
“Ndiyo! Wewe si mtoto wa mchungaji Lazaro?”

“Yeah! Ndiye mimi! Wewe ni mtoto wa mchungaji pia?”
“Ndiyo!”
“Mmmh! Mchungaji gani?”
“Marcus wa Morogoro!”
“Waooo! Kumbe! Nimefurahi kukufahamu kwa undani.”
“Asante sana. Nakutakia mchana mwema,” alisema Lydia na kuanza kuondoka, Peter akamuwahi mkono.
“Subiri kwanza...”
“Kuna nini?”
“Kwani huu ndiyo mwisho wetu?”
“Mwisho wa nini?”
“Kuonana na kuzungumza pamoja?”
“Mmmh! Sijui.”
“Ningependa niwasiliane nawe Lydia, nimefurahia huduma yako, hakika Mungu amekubariki,” alisema Peter.
 
SEHEMU YA 85...
Lydia alionekana msichana mpole, msikivu na aliyekuwa makini kwa kila kitu. Alipoambiwa hivyo, akabaki akimwangalia Peter usoni, alimkazia macho, alitaka kuona kama mwanaume huyo alimaanisha kile alichokuwa akikizungumza au la.
Tabasamu pana likaonekana usoni mwa Lydia na kisha kutoa simu yake na kumpa namba ya simu Peter ambaye alionekana kuwa na furaha tele.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa ukaribu wao. Kila siku usiku ilikuwa ni lazima Peter kuwasiliana na msichana Lydia huku akificha kile kilichomfanya mpaka kusisitiza kuchukua namba yake. Baada ya miezi kadhaa, matokeo ya kidato cha sita yakatoka na hatimaye Peter kuchaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
“Hongera sana,” alisema Lydia walipokuwa wakizungumza simuni.
“Nashukuru. Ila kuna kitu.”
“Kitu gani?”

“Lydia, unajua kwa nini niliamua kuwa na mawasiliano nawe?”
“Hapana.”
“Nilitokea kukupenda sana, nilipokuona kwa mara ya kwanza, moyo wangu ulikufa juu ya penzi lako, nikaona si vib....” Peter alisema kwa hisia kali za mapenzi, hata kabla hajamalizia sentensi yake, Lydia akakata simu.
“Hallow...hallow...” aliita Peter.
Peter hakutaka kukubali, alikataliana na ukweli uliokuwepo kwamba msichana huyo alikata simu bali alijifariji kwamba kulikuwa na tatizo la network na hivyo kuanza kumpigia tena. Simu ikaanza kuita, iliita na kuita lakini haikupokelewa kabisa.
Peter hakukata tamaa, hakutaka kuona akimpoteza Lydia kirahisi namna hiyo, alichokifanya ni kuendelea kumpigia lakini matokeo yalikuwa yaleyale kwamba simu haikupokelewa, na alipoendelea zaidi, ikawa haipatikani.

Moyo wake uliumia, hakukuwa na kitu alichomuomba Mungu kila siku kama kutokumpoteza msichana Lydia, moyo wake uliumia sana, aliyakumbuka maumivu makali aliyokutaka nayo kwa Tatiana ambaye kwa wakati huo alikuwa mwanamuziki mkubwa duniani, hakutaka kujiona akiumia tena kwa msichana ambaye aliamini kwamba angekuwa mke wake hapo baadae.
 
SEHEMU YA 86...
Hakukata tamaa, aliendelea kumtafuta msichana huyo lakini hakuwa akipatikana kabisa, na kama alipatikana, hakupokea simu. Peter hakutaka kukubali, alijiona kuwa radhi kupoteza kitu chochote lakini si msichana huyo mrembo, alichokifanya ni kuwaambia wazazi wake kwamba anakwenda Morogoro kutembea.
“Una uhakika ni Morogoro?” aliuliza mchungaji Lazaro.
“Ndiyo baba. Nakwenda Morogoro,” alisema Peter.
Kwa kuwa alikuwa kijana mkubwa aliyejitambua, wazazi wake hawakutaka kumzuia, wakampa ruhusa na hatimaye kuelekea mjini Morogoro huku lengo lake kubwa likiwa ni kuonana na msichana huyo mrembo.

Ndani ya basi Peter alikuwa na mawazo tele juu ya Lydia tu, alikuwa akimpenda mno na kwa kipindi chote ambacho alikuwa hajawasiliana naye, aliona pengo kubwa sana moyono mwake.
Basi lilichukua masaa mawili mpaka kufika Morogoro ambapo akateremka na kuelekea hotelini kisha kuwapigia simu wazazi wake na kuwaambia kwamba alifika salama. “Kwanza ngoja nimpigie simu Lydia,” alisema na kisha kuchukua simu yake na kumpigia simu msichana huyo.
Majibu yalikuwa yaleyale, hakikubadilika kitu chochote kile, simu iliita na kuita lakini haikupokelewa kitu kilichomuongezea huzuni moyoni mwake. Alichokifanya ni kukata simu kisha kujipanga kulitafuta kanisa lao.
Kwa kuwa Kanisa la Praise And Worship lilikuwa maarufu hapo Morogoro, wala hakupata shida kulipata, alipoulizia mara moja tu, akaelekezwa na kuanza mahali kanisa hilo lilipo katika Mtaa wa Madaraka na kuelekea huko.
Alipofika kanisani hapo, akakutana na washirika watatu waliokuwa wakifanya usafi kanisa. Akawasalimia na kuanza kuzungumza nao.

“Mchungaji anaishi Mtaa wa Kingo,” alisema mshrika mmoja.
“Upo mbali kutoka hapa?”
“Si mbali. Twende nikupeleke,” alisema mshirika mmoja na kuanza kuelekea huko.
 
SEHEMU YA 87...
Njiani, mapigo ya moyo yalikuwa yakimdunda mno, kiu ya kumuona Lydia ilikuwa imemkamata lakini alikuwa akiogopa mno. Hakuwahi kufika nyumbani kwao na hakujua wazazi wa msichana huyo wangefikiria nini, ila alichokuwa akikihitaji ni kuwa na msichana huyo tu.
“Nyumba ile pale, ile yenye maua nje,” alisema mshirika huyo.
Mapigo ya moyo yakazidi kudunda kwa nguvu, kwa mbali akaanza kuhisi kibaridi kikali kilichomfanya kuanza kutetemeka lakini cha ajabu kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka. Wakati mwingine alitamani warudi nyuma ili aweze kujipanga upya lakini akapiga moyo konde, wakafika na kuanza kugonga hodi na mlango kufunguliwa, wakaingia ndani.
“Nimemleta mgeni wenu mama mchungaji,” alisema mshirika yule baada ya salamu.

“Asante. Karibu mgeni.”
“Asante.”
Peter akaanza kujitambulisha alikuwa nani, mama mchungaji akafurahi mno kumuona mtoto wa mchungaji Lazaro ndani ya nyumba yao kwani mara nyingi alimwambia mchungaji huyo aje na familia yake lakini ratiba iligongana sana. Alichokifanya akamuita mume wake na kuanza kuzungumza na Peter.
“Nimekuja kwa lengo moja tu,” alisema Peter.
“Lengo gani?”
“Kuzungumza na binti yenu, Lydia.”
“Lydia?”
“Ndiyo,” alisema Peter.
Mchungaji na mkewe wakashtuka!!
 
SEHEMU YA 88

Mara baada ya kukaa nchini Marekani kwa miaka mitatu mfululizo, Tatiana akaamua kupanga safari ya kuelekea nchini Tanzania kwa ajili ya kuwaona wazazi wake na kuwashukuru Watanzania kwa kila kitu walichokuwa wamekifanya kwa ajili yake.

Alijipanga, alichokifanya ni kuchukua ndege yake binafsi, akapanda na mpenzi wake, Buffet na hatimaye safari ya kuelekea nchini Tanzania kuanza.
Ndani ya Jiji la Dar es Salaam mambo yalikuwa balaa. Mara baada ya taarifa kutangazwa kwamba mwanamuziki Tatiana anafika nchini Tanzania, watu wakajiandaa vilivyo kwa ajili ya kumpokea mwanamuziki huyo aliyeiletea Tanzania sifa kubwa na kuifanya ijulikane kimataifa.

Fulana zaidi ya elfu kumi zikachapishwa kwa ajili ya kumkaribisha mwanamuziki huyo, vikundi mbalimbali vya ngoma vikaandaliwa tayari kwa ajili ya kumpokea, watu wengi wakajiandaa vilivyo kumpokea mwanamuziki huyo.
Siku ambayo ndiyo Tatiana alikuwa akifika nchini Tanzania, watu wengi walisimama nje ya uwanja wa ndege kwa ajili ya kumpokea. Kwa sababu kulikuwa na watu zaidi ya milioni moja waliokuwa na hamu ya kumpokea, wakaambiwa wajipange barabarani kwa ajili ya kumpokea mtu huyo.

Hilo halikuwa tatizo, kila mtu alitaka kumuona Tatiana. Kama mwanamuziki huyo aliyekuwa akifanya kazi kubwa nchini Marekani watu walilipia kiasi kikubwa cha fedha kumwangalia, hilo halikuonekana kuwa tatizo kwao kujipanga pembeni mwa barabara kwa ajili ya kumpokea mwanamuziki huyo.

Kama ilivyokuwa katika msiba wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ndivyo ilivyokuwa siku hiyo. Watu walijipanga katika Barabara ya Nyerere, kote huko barabara ilizungukwa na umati wa watu ambapo baada ya kufika Buguruni, wakaunganisha mpaka katika Barabara ya Mandela na walipofika njia panda kwenye maunganiko na Barabara ya Uhuru, wakajipanga pia, katika kila kona, watu walikuwa barabarani kwa ajili ya kumuona mwanamuziki huyo mkubwa.
 
SEHEMU YA 89...
Saa 8:20 mchana, ndege binafsi ya Tatiana ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, watu waliokuwa nje ya eneo la uwanja ule wakaanza kujipanga vilivyo kwani waliisikia sauti iliyokuwa ikitangaza kwamba ndege hiyo ndiyo iliyokuwa imembeba Tatiana aliyekuwa akifika nchini hapo kutokea nchini Marekani.
Waziri wa Wanawake Jinsia na Watoto, bi Paulina Gilbert ndiye aliyeandaliwa kwa ajili ya kumpokea mgeni huyo aliyezua gumzo kubwa duniani kwa kipindi hicho. Mara baada ya ndege kusimama katibu na kapeti jekundu likaandaliwa.

Tatiana aliyekuwa ndani hakuamini kile alichokuwa akikiona, hakuamini kama msichana yeye aliyekulia kijijini Chibe mkoani Shinyanga leo hii alikuwa akipokelewa kama kiongozi mkubwa duniani, alishindwa kuvumilia, akaanza kububujikwa na machozi tu.
“Usilie mpenzi,” alisema Buffet huku akimbeleza Tatiana.
“Sikutarajia jambo kama hili maishani mwangu, hii ni ndoto mpenzi,” alisema Tatiana huku akiendelea kububujikwa na machozi tu.
Mlango wa ndege ukafunguliwa, mtu wa kwanza kabisa kuteremka katika ndege alikuwa Tatiana. Machozi yaliendelea kumbubujika tu. Akaanza kuwapungia watu mikono huku akipiga hatua kuteremka ngazi.

Watu walioandaliwa kwa ajili ya kupiga ngoma za asili, wakaanza kupiga na kucheza kwa furaha huku wakirukaruka. Alipoteremka chini tu, tayari watoto waliokuwa na maua wakamgawia na kisha kusalimia na waziri huyo.
Alishindwa kujizuia, alimwambia waziri yule jinsi alivyokuwa akijisikia kipindi hicho. Bado aliendelea kusisitiza kwamba hakuamini kwani yale maisha aliyokuwa ameyapitia kipindi cha nyuma yalimuumiza mno.

Tatiana, Buffet na waziri wakaanza kupiga hatua kuelekea katika gari la wazi kisha kuingia na safari ya kuelekea katika Hoteli ya Blue Pearl iliyokuwa Ubungo kuanza. Njiani, Tatiana hakuamini, watu walikuwa wamejiopanga barabarani huku wakimpungia mkono, hakuamini kile alichokuwa akikiona, watu wengi walikuwa wamesimama pembezoni mwa barabara wakimpungia mkono kama alivyokuwa akifanya.

Barabara nzima ya Nyerere mpaka makutano ya Barabara ya Mandela, watu walikuwa wamejipanga barabarani tu huku wakiendelea kumpungia mkono kitu kilichoonekana kuwa kama ndoto machoni mwake.
 
SEHEMU YA 90

Walikwenda kwa mwendo wa taratibu mpaka walipofika Ilala ambapo wakachukua Barabara ya Kawawa na walipofika Magomeni, wakachukua Barabara ya Morogoro na kuanza kuelekea Ubungo hotelini.
Kote huko, Watanzania walikuwa wamejazana barabarani, walikuwa wakimpungia mkono mwanamuziki aliyekuwa na jina kubwa ambaye alilipa sifa kubwa Taifa la Tanzania.
Walichukua dakika arobaini mpaka kufika Ubungo ambapo wakaingia hotelini na kisha kupumzika na siku iliyofuata, wakaelekea Ikulu kwa ajili ya kuonana na rais ambapo wakala chakula cha mchana na kesho yake kuanza safari ya kuelekea mkoani Shinyanga huku akiwa na furaha tele.

**** Peter hakuonyesha uoga wowote kwa kuamini kwamba ukweli ndiyo ungemfanya kuwa huru kuonana na binti huyo ambaye mpaka katika kipindi hicho hakujua kama alikuwepo au hakuwepo.
Mchungaji na mkewe walionekana kuwa katika hali ya sintofahamu, ilikuwaje mtu atoke Dar es Salaam na kwenda Morogoro kwa ajili ya binti yao? Walibaki wakimwangalia, Peter alizungumza kwa kujiamini sana, hiyo kidogo ikamfanya mchungaji na mkewe kuona kwamba mtu huyo alimaanisha alichokuwa akikisema.
Walichokifanya ni kumuita Lydia, msichana huyo alipofika sebuleni na macho yake kutua kwa Peter, akashtuka mno, hakuamini kumuona Peter nyumbani hapo, akajikuta akianza kutetemeka kwa hofu kwani alijua iwe isiwe aliitwa na wazazi wake kwa ajili ya kijana huyo.
Peter akaonyesha tabasamu pana, hakuamini kumuona msichana huyo mahali hapo, moyo wake ulikuwa majonzi kwa kipindi kirefu, ukafarijika, kumuona msichana huyo kukamtia nguvu.

“Abeee...” aliitikia Lydia mara baada ya kufika sebuleni hapo.
“Unamfahamu huyu kijana?” aliuliza baba yake.
“Ndiyo!”
“Unajua kwa nini yupo hapa?”
“Hapana baba!”
“Peter, hebu sema kwa nini upo hapa manake hata huyu uliyemfuata naye hajui kwa nini upo hapa,” alisema mchungaji Marcus.

Peter hakutaka kuficha lolote lile, alisafiri kwa umbali mrefu kwa ajili ya kumuona msichana huyo, hiyo ilikuwa nafasi pekee aliyokuwa nayo ambayo aliamini kwa vyovyote vile endapo angezungumza ukweli basi angeweza kuelewekana hivyo kuwa huru.
 
SEHEMU YA 91

Alichokifanya ni kuanza kuhadithia kila kitu kilichotokea walipokuwa Dodoma, alipoanza kuzoeana na msichana huyo mpaka pale walipoanza kuwasuiliana kwenye simu. Hakutaka kuficha lolote lile, katika kipindi chote alichokuwa akisimulia, Lydia alikuwa akitetemeka tu huku wakati mwingine akitamani kumwambia Peter anyamaze lakini mwanaume huyo hakunyamaza, aliendelea kueleze huku mara kwa mara akimwangalia Lydia.
“Ninampenda Lydia, siwezi kuficha hisia zangu. Lengo langu si kumchezea, ninataka kumuoa, kila ninapomwangalia, naona kabisa yeye ni mwanamke wa maisha yangu. Nadhani Mungu alitukutanisha pale Dodoma kwa dhumuni maalumu la mimi na Lydia kufahamiana na hatimaye baadae kuwa mke na mume,” alisema Peter huku akiwaangalia wazazi hao.

“Ooppss...” mchungaji Marcus alishusha pumzi nzito.
“Mchungaji, huo ndiyo ukweli. Mimi si kijana mhuni, ninajiheshimu lakini nimeamua kuja hapa kwa kuwa sikutaka ukaribu na Lydia ufike mwisho kwa kuwa niliona mambo mengi yakiwa mbele yetu,” alisema Peter.
Kila sentensi aliyokuwa akizungumza mahali hapo ilikuwa kama msumari wa moto moyoni mwa msichana huyo, kila alipokuwa akimwangalia Peter, ujasiri aliokuwa nao, akajikuta akianza kuvutiwa naye kwani alionyesha kwamba yeye ni mwanaume asiyeogopa chochote kile na alijitoa kwa lolote lile.

Mchungaji Marcus na mkewe wakabaki wakiangaliana tu. Kijana aliyekuwa mbele yao hawakumfahamu kwa kumuona japokuwa walimfahamu sana baba yake. Hawakujua ni kitu gani walitakiwa kufanya kama wazazi.
“Subiri nimpigie simu baba yako,” alisema mchungaji Marcus, akachukua simu yake na kuanza kupiga.
Alitaka kuzungumza naye kama mzazi hivyo alichokifanya ni kuelekea chumbani. Mama mchungaji hakutaka kubaki sebuleni hapo, kama mzazi, naye alitaka kusikia kile ambacho wachungaji hao wangezungumza simuni. Sebuleni wakabaki wawili.

“Peter! Ndiyo umefanya nini?” aliuliza Lydia kwa sauti ya chini, alikuwa akilalamika.
“Nimefanya nilichofanya, unafikiri ningefanya nini?”
“Si ungenipigia simu!”
“Mara ngapi? Nimekupigia simu kila siku tena zaidi ya mara tatu, lakini simu zote haukuzipokea, nilikuandikia meseji lakini haukujibu hata moja, ulitaka nifanye nini?”
 
SEHEMU YA 92

“Lakini Peter....”
“Lydia, nina moyo wa nyama, ninaumia kama wengine wanavyoumia, nisingeweza kuvumilia na ndiyo maana nimetoka Dar mpaka hapa kwa ajili yako tu, si mwingine, nimekuja kwa ajili yako, sikutaka kuona nikiendelea kuumia zaidi,” alisema Peter huku kwa mbali machozi yakianza kumlenga.
Maneno hayo aliyozungumza peter yaliuchoma moyo wa Lydia, akabaki akimwangalia tu pale kochini alipokuwa amekaa. Kwa mbali, hata naye machozi yakaanza kumlenga. Hapo ndipo alipogundua kwamba Peter alikuwa na upendo wa dhati kwake, hakuwa kama watu wengine ambao walitamani kuwa na mwanamke ili mradi, kwa Peter, alionekana kuwa tayari kufanya lolote lile lakini mwisho wa siku ampate.

“Naomba unisamehe Peter, nilihisi tofauti na ulivyofanya,” alisema Lydia huku akianza kububujikwa na machozi.
“Ooppss...! Lydia, nimefanya hivi kwa kuwa ninakupenda, sitaki kukutania katika hili. Nimekuwa nikikufikiria sana na nisingekuwa tayari kukuacha ukiondoka, nilihitaji kukuonyeshea mapenzi ya dhati Lydia, hakukuwa na kingine zaidi ya hicho, ninakupenda mno,” alisema Peter huku akisimama na kuanza kumsogelea msichana huyo.

Lydia naye hakubaki pale alipokuwa, akapiga hatua kumsogelea Peter alipomfikia, wote wawili wakakumbatiana na kuanza kulia, upendo wa dhati ukaanza kuchipua moyoni mwa msichana Lydia, machozi yao yakaanza kulowanisha migongo yao. Huku wakiwa kwenye hisia kali za kimapenzi, mara mchungaji Marcus na mkewe wakatokea sebuleni hapo, kile walichokiona, kikawashtua.
 
SEHEMU YA 93...

Kila mmoja alistaajabu juu ya kile kilichokuwa kimetokea chumbani pale, walishindwa kuyaamini macho yao juu ya kile walichokuwa wakikiangalia, kiliwashangaza na hawakuamini kama Peter na Lydia walikuwa wamekumbatiana.
Peter na Lydia walikuwa wakibubujikwa na machozi yaliyolowanisha migongo yao, hisia kali zikawachoma wazazi hao na kugundua kwamba watoto hao walikuwa wakipendana kwa mapenzi ya dhati.
Hawakuongea kitu, walibaki wakiwaangalia tu, kwa kiasi fulani walibaki wakiwa na furaha kwani kumuona mtoto wa mchungaji akiwa amemkumbatia binti yao, kidogo wakafarijika mioyoni mwao.

“Ninakupenda Lydia,” alisema Peter, machozi yaliendelea kumbubujika mashavuni mwake huku akimwangalia Lydia usoni.
“Nakupenda pia Peter, naomba unisamehe kwa kila kitu kilichotokea,” alisema Lydia.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa uhusiano wao wa kimapenzi. Walipendana na kuthaminiana huku kila mmoja akimuahidi mwenzake kwamba angekuwa mwaminifu katika kipindi chote cha maisha yao.
Peter hakutaka kuwa msiri, alichokifanya ni kuwaambia wazazi wake kuhusu Lydia, walifurahi kusikia hivyo na wakatoa baraka kwa kila kitu kitakachotokea huku wakitahadharishwa kutokufanya mapenzi mpaka hapo watakapoona na kuwa mume na mke.

“Hilo si tatizo, hatutoweza kufanya,” alisema Peter.
Mpaka anaanza masomo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Peter alikuwa mwaminifu kwa asilimia mia moja japokuwa kulikuwa na wasichana wengi waliokuwa wakimfuatilia lakini bado uaminifu wake kwa Lydia haukupungua.
“Mchungaji, unamjua Tatiana?” aliuliza mwanachuo mmoja, alikuwa akimuuliza Peter ambaye katika kipindi chote alichokuwa chuoni hapo, alipenda kuishi kama mcha Mungu, kila wakati Biblia mkononi kiasi kwamba wanachuo wengine wakampachika jina la mchungaji.

Aliposikia jina la Tatiana, aliusikia moyo wake ukilipuka na kuanza kudunda kwa nguvu, hakutegemea kulisikia jina hilo katika maisha yake, damu ikaanza kutembea kwa kasi mishipani mwake huku akijikuta furaha yote aliyokuwa nayo ikianza kupotea, kumbukumbu juu ya msichana Tatiana zikaanza kujirudia kichwani mwake kama mkanda wa filamu.
“Umesemaje?”
 
SEHEMU YA 94...

“Tatiana anakuja. Aaah! Kumbe wewe mchungaji, utakuwa hamfahamu huyu,” alisema mwanachuo huyo huku akitoa kicheko cha chini.
Hakuwa akipenda miziki ambayo iliitwa ya kidunia, alipenda kusikiliza kwaya lakini hiyo haikutoshakabisa kutokumkumbuka Tatiana, alikumbuka jinsi alivyomuumiza kwa kutembea na mwanaume mwingine, tena kubusiana ukumbini huku akijua kwamba alikuwa amemuacha nchini Tanzania.

“Ndiye nani huyo?” akajifanya kuuliza.
Mwanamuziki mpya, ni noma sana, Mtanzania huyo!”
“Anaimba nyimbo za kidunia?”
“Hahahaha! Ndiyo!”
“Wala simfahamu!”
“Nilijua tu.”
Peter hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea darasani. Moyo wake ukawa kama umefukunyuliwafukunyuliwa, mawazo juu ya Tatiana yakaanza kumwandama tena.

Japokuwa kilikuwa kimepita kipindi cha miaka mitatu lakini akajikuta yale mapenzi aliyokuwa nayop juu ya msichana yule yakianza kurudi tena moyoni mwake. Aliichukia hali hiyo lakini hakuwa na jinsi kwani kila alivyokuwa akijilazimisha kuitoa, iliendelea kuwepo moyoni mwake.
Pasipo kupenda, naye akajikuta akianza kufuatilia kuhusu Tatiana. Mpaka siku ambayo msichana huyo alikuwa akiingia nchini Tanzania huku watu wakijipanga barabarani, naye alikuwa miongoni mwa watu hao.

Kila alipokuwa akimwangalia msichana huyo garini, moyo wake ulimuuma mno, alijikuta akimchukia sana zaidi ya alivyomchukia shetani. Akatamani apate bunduki na kmuua msichana huyo hapohapo garini.

“Nisamehe Mungu! Ninamchukia mno Tatiana,” alijikuta akisema.
Usiku wa siku hiyo, Peter alitulia chumbani kwake na kuanza kulia, ni kweli alimchukia mno Tatiana lakini akajikuta akimuomba Mungu msamaha kwa kile alichokuwa amekisema. Alichokifanya ni kumpigia simu mpenzi wake, Lydia kwani kila alipojaribu kuomba Mungu, hakujisikia kuwa katika hali ya kawaida.
“Una nini mpenzi? Mbona unalia?”
“Naomba unisaidie kuomba.”
“Kuna nini?”
“Nina chuki kali moyoni.”
“Chuki?”
“Ndiyo! Naomba unisaidie!”
“Unamchukia nani?”
“Tatiana!”
“Tatiana yupi?”
 
SEHEMU YA 95...
Peter hakujibu swali hilo, akaendelea kulia zaidi kwani kila alipomkumbuka msichana huyo, alizidi kuumia moyoni mwake.
Katika kipindi hicho kikaonekana kuwa kibaya kwake, kila alipofungulia televisheni, alikutana na matangazo yaliyomhusu Tatiana, kila aliposikiliza redio bado alisikia mengi kuhusu Tatiana.
Siku iliyofuata, matangazo yakaanza kubandikwa chuoni kwamba yule muimbaji aliyekuwa akiitetemesha dunia kwa kipindi hicho, Tatiana alitarajiwa kufika chuoni hapo. Peter alipoyaona matangazo hayo, moyo wake ukaumia mno. Hakutaka kumuona tena msichana huyo, mbaya zaidi, leo kulikuwa na mabango yaliyobandikwa kwamba msichana huyo angefika chuoni hapo.

Tatiana akawa gumzo chuoni, kila kona alizungumziwa yeye tu jambo lililomuuma mno Peter. Kuna kipindi alitamani kuwa mkuu wa chuo na asitishe ule ujio wa msichana huyo chuoni hapo kwani kwake hakupenda kabisa hilo litokee.
Mishemishe ziliendelea chuoni, maandalizi mazito yalipamba moto kwa ajili ya kumkaribisha mwanamuziki huyo aliyekuwa kipenzi cha watu wengi duniani. Kila mtu aliyesikia kwamba Tatiana alitarajiwa kwenda chuo kikuu, akakapanga kwenda huko kwa kuamini kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima Tatiana aimbe.

Wale waliokuwa Kibaha, Bagamoyo na sehemu nyingine zilizokuwa karibu na Jiji la Dar es Salaam wakafika jijini hapo kwa ajili ya kumuona msanii huyo aliyesifika kwa uzuri na sauti yake.
Siku ya ujio wake, japokuwa kulikuwa na ulinzi mkali uliokuwa umewekwa kwamba hakutakiwa kuingia mtu ambaye hakuwa mwanachuo wa chuo hicho lakini walishindwa kuwazuia watu hao, wakajikuta watu wote wakiingia chuoni hapo, tena hata wale wasiokuwa na vitambulisho.

Uwanja wa mpira chuoni hapo ukaonekana mdogo, watu wengi walikuwa wamejazana, jukwaa kubwa lilikuwa limewekwa na kupambwa vilivyo, kila mmoja alitaka kumshuhudia msichana huyo ambapo taarifa zaidi zilisema kwamba angeweza kutumbuiza.

“Mchungaji! Hata wewe?” alisikika mwanachuo mmoja wa kike, alikuwa akimwambia Peter.
“Hata mimi nini?”
“Upo hapa! Nilidhani upo nyumbani unatuandalia neno la kesho kanisani,” alisema msichana huyo, alikuwa akimtania Peter.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom