Pengo: Wananipakazia madawa ya kulevya!

Pengo: Wananipakazia madawa ya kulevya!

Ya Pengo siyajuwi na ndio kwanza nnayasikia leo.

Lakini kuhusu kanisa la Roman Catholic kuhusika na kashfa za madawa ya kulevya na ngono za kuharibu watoto na ngono za wanaume kwa wanaume (gay-ism) nimeshasoma sana kwenye vyombo vya habari. Jee, unabisha nikubandikie humu hizo habari?

Sawa mama, lakini uje na verification ya taarifa hizo maana mtandao (internet) ni gate without gatekeeper. Kwenye mtandao kila mtu ni mwandishi, mhariri na mchapishaji.
 
Hawatweza hata siku moja kumkamata Kardinali pengo...
 
Baada ya sakata la viongozi wa dini na tuhumu za madawa ya kulevya kusimama kwa muda sasa limerejea tena baada ya Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo kueleza jana masikitiko yake ya kutaka kunyamazishwa kwa kuhusishwa na sakata hilo kama njia ya kumnyamaziaha.

KUJIKANGANYA KWA SERIKALI
1. Wakati wa baraza la Idd, Rais Kikwete alisema kauli yake ilieleweka vibaya, akasema taarifa alizopewa ni za mchungaji mmoja wa Kanisa la Biafra Kinondoni na Shehe mmoja, na hakumaanisha viongozi wote.
2. Waziri Mkuu Pinda wakati akijibu swali la Susan Lyimo (MB.) alisema Rais alieleweka vibaya kwani waliokamatwa, kwa kauli yake ni "wachungaji waswahili wa vikanisa vidogo" na wala si maaskofu kama ilivyochukuliwa na vyombo vya habari.

Wakati propaganda hii ikizidi kushika kasi, mtu yeyote makini lazima azingatie yafuatayo.
Kwanza, kwa mfumo wa Kanisa Katoliki, haliitaji kusubili intelijensia ya wabongo iwaambie kiongozi fulani amekengeuka.Kanisa lina intelijensia yake ambayo hata CIA pamoja na nguvu zote wanalitambua hilo.Kiongozi yeyote hata awe Papa akikengeuka kwa issue nyeti kama hii anathibitiwa mara moja,Kwa wale wanaomjua Askofu Koda wa Same waulize leo hii yuko wapi'
Pili, kwa mfumo wa kanisa Pengo kama kiongozi hata nguo zake hajui bei yake. Matunzo yake yote yanafanya na kanisa hadi anakufa, yeye kama yeye haruhusiwi kumiliki hata hela bali alichonacho chote ni mali ya kanisa na hakuna anachokosa.
Tatu, kanisa aligawi vyeo kwa kujuana wala promotion, ni integrity yake, kwa hiyo hadi Pengo anachaguliwa kuongoza kanisa la Tanzania, integrity yake ni beyond any reasonable doubt. Hata akikengeuka upo mfumo wa kudeal naye hata before intelijensia ya bingo kubaini.
Kwa ufupi, Kanisa Katoliki limekuwepo takriban miaka 2000 na litaendelea kuwepo kwa sababu ya misingi yake kiimani na mfumo wake wa kumdhibiti yeyote. Ni mwendawazimu tu atakayedhani serikali hii ya awamu ya nne itapambana nalo kwa kuzusha tuhuma za kitoto ili kuwanyamazisha viongozi wake. Kwa ushauri tu, serikali zote (na vyama vyao) zilizojidai kupambana na kanisa zimefall apart (revise your history), fanyeni tu wanayowakemea for your political survival.

Nakuunga mkono sana mkuu tena pamoja na miguu, askofu Koda alijaribu kusema wanamuonea wivu kwa maendeleo mwisho wa siku kanisa lilimkamata live bila chenga na sasa yupo mafunzoni kuendelea kuisoma imani zaidi. Waache Jk na wezake siwanafikiri kwa urefu wa viatu vyao kumbe wenzao wanafikri beyond that. Big up man for good analysis.
 
Huwezi kulala kitanda kimoja na ng'e na usidungwe!@@@

.
Mmmmh. Unamaanisha wale top five kitaifa kabla hujamkuta Pinda mtu wa 6 kiwadhifa ni ng'e? Hebu tuweke wazi maana ya kauli hii mkuu, kwani utasaidia sana kuondoa utata wa tafsiri.
.
 
Sawa mama, lakini uje na verification ya taarifa hizo maana mtandao (internet) ni gate without gatekeeper. Kwenye mtandao kila mtu ni mwandishi, mhariri na mchapishaji.

suala la kunajis watoto hata intaneshno media wamelijadil,mfano BBC SWAHILI
 
Usifanye simple comparison/analysis!!! Mawaziri si suti tu wana matamanio mengi ya maisha- watoto wao, wake zao etc- lazima wawaachie urithi duniani wakifa. Pia lazima watafute hela kutetea ubunge wao inapoisha miaka mitano- huwezi kulinganisha na askofu>

wote ni binadam,je yule wa biafra c kiongoz wa kiroho?
 
[TABLE="width: 99%"]
[TR]
[TD]
Imeandikwa na Angela Semaya; Tarehe: 31st December 2011 @ 14:59
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali
Pengo, amesema yeye si mfanyabiashara wa dawa za kulevya ila anatajwa kwa nia ya kunyamazishwa asizungumze ukweli.

Kardinali Pengo akizungumza na vijana katika ufukwe wa Bahari ya Hindi eneo la Kawe jana alisema hajapata kuona wala kujua dawa za kulevya, lakini anajua anatajwa hivyo na wanaotaka anyamaze.

“Mimi mwenyewe nimewekwa katika orodha ya dawa za kulevya, naona kwenye vyombo vya habari, dawa zenyewe wala zisijui, lakini naendelea kuzungumza kwa sababu najua yanafanywa na wanaotaka kuninyamazisha … sitanyamaza ng’o,” alisema Pengo.

Alikuwa akiwaeleza vijana kuhusu utandawazi na kuwataka waache kuyumbishwa na kuamini kila wanachoona kimeandikwa kwenye mtandao.

Alisema mambo mengi ya ajabu yamekuwa yakiandikwa na kusemwa, lengo ikiwa ni kunyamazisha maaskofu na mapadri wasiendelee kufundisha ukweli, ili watu wachache wafaidike.

“Ni uzushi unaofanywa na watu kuharibu na kuchimbachimba Kanisa tusiseme ukweli, wachache waendelee kufaidika, naomba vijana msisombwe na hali hii, kwani watu hawa hawana woga ili mradi lengo lao la kuharibu Kanisa lifanikiwe … vijana mna uhai
ndani yenu na mna uwezo kama maaskari wa kupambana na waovu wa Kanisa,” alisema.

“Silaha ya vijana ni maisha yanayojua mnaamini kitu gani, msikubali kuyumbishwa na watu wanaotoa mambo vichwani mwao. Kama mnasikia natajwa, njooni mniulize, Baba mbona nimesikia habari fulani, badala ya kuyabeba na kushabikia…imani yenu si ya kutetereka, endeleeni kuwa imara watetereke wanaotaka tutetereke,” alisema.

Alisema vijana pia wamekuwa wakitumika kama vyombo katika biashara ya kulevya huku watu wachache wakitajirika na kwamba baadhi yao wanaokemea au kuzungumzia, wanapuuzwa au kuambiwa ndio wafanyabiashara wa dawa hizo, jambo ambalo nyuma yake halina ukweli wowote.

Kardinali Pengo alisema lengo ni kutaka kuwanyamazisha watu wanaosema ukweli ili wachache waendelee kutajirika na biashara hiyo kwa kuwatia hasara vijana.

Naye Mhashamu Askofu Salutaris Libena, ambaye aliongoza Ibada Takatifu, alisema vijana wamekutana ili kumshukuru Mungu na kumwomba neema .

Libena ambaye pia ni Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, aliwataka vijana kuingia mwaka mpya kwa kumjua na kumtukuza Mungu.

Mbali na vijana kushiriki ibada hiyo lakini pia zilikuwapo burudani mbalimbali za kwaya na ngoma, sambamba na vijana kupima kwa hiari damu kwa ajili ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama.

Kila mwisho wa mwaka vijana kutoka makanisa mbalimbali ya Kanisa Katoliki hukutana kwa lengo la kumtukuza Mungu na kumshukuru kwa kumaliza mwaka.

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
kanisa lina maadui wengi sana na maadui hao wameongezeka zaidi wakati huu wa propaganda za udini. Sheria ni msumeno kama kuna ushahidi unaojitosheleza kwamba pengo anauza madawa ya kulevya atiwe nguvuni na sheria ichukue mkondo wake. Viongozi wa dini hawako juu ya sheria.
 
What is wrong with Cardinal Pengo? Is water falling through cracks? Why taking a defensive position in public?
 
Issue nadhani ni umesahau kuwa listi haijatolewa, kama kuna waliotajwa hata mimi nakumbuka alikuwa na Askofu sijui wa kanisa gani.

Pia nakumbuka kuwa JK aligeneralise kwamba hata maaskofu wanafanya biashara hiyo, hilo lenyewe bila kuwa specific, basi inaweza kuwa Askofu yeote wa dhehebu lolote, na ndiyo maana baada ya kelele zile, wakaja na huyo mmoja.

Sizungumzii waliotajwa, na yeye kwa mujibu wa habari kwenye thread hii, hazungumzii waliotajwa.

Kuzungumza kwa mafumbo kwa JK hakukuwa solution kama kweli he was serious, sana sana utagunduwa there are some political games.

Na kuzungumza kwa mafumbo kwa bwana Pengo bila kutaja source ya habari zake je?
 
What is wrong witj Cardinal Pengo? Why does he take a defensive position? Is it a sign of being guilty? Just trying to think outside the box! He is my Cardinal and the red price whom I revere so much
 
Ya Pengo siyajuwi na ndio kwanza nnayasikia leo.

Lakini kuhusu kanisa la Roman Catholic kuhusika na kashfa za madawa ya kulevya na ngono za kuharibu watoto na ngono za wanaume kwa wanaume (gay-ism) nimeshasoma sana kwenye vyombo vya habari. Jee, unabisha nikubandikie humu hizo habari?

bandika mama
 
Kwanza, kwa mfumo wa Kanisa Katoliki, haliitaji kusubili intelijensia ya wabongo iwaambie kiongozi fulani amekengeuka.Kanisa lina intelijensia yake ambayo hata CIA pamoja na nguvu zote wanalitambua hilo.Kiongozi yeyote hata awe Papa akikengeuka kwa issue nyeti kama hii anathibitiwa mara moja,Kwa wale wanaomjua Askofu Koda wa Same waulize leo hii yuko wapi'
.

Si kweli mbona lilishindwa kugundua maaskofu na mapadri walawiti watoto waliozagaa nchi nyingi mapema hadi likaingia aibu kubwa hadi kumfanya papa alie kuomba msamaha?
 
Utaratibu tuliojiwekea ni kwamba mtu ukitajwa tajwa basi unatakiwa kujivua gamba. Kwa hiyo Mhashamu Polycap Kardinali Pengo ametajwa tajwa kwenye madawa ya kulevya basi hana budi kujivua gamba asiendelee kulichafua kanisa la la mungu.
Utaratibu huo umejiwekea na nani? Kanisa katoliki au? Watu wengine bwana au umejiwekea na mkeo?
 
Inasikitisha sana kuona wanasiasa wa hii nchi hasa hasa wanamagamba wako tiyari kufanya chochote ili wabaki madarakani bila kujali athari ambazo zitawapata wananchi.Walaaniwe wana magamba!
 
Si kweli mbona lilishindwa kugundua maaskofu na mapadri walawiti watoto waliozagaa nchi nyingi mapema hadi likaingia aibu kubwa hadi kumfanya papa alie kuomba msamaha?
Kwanini aombe msamaha kama hajadhibitisha, huwa anahakiki akiona tuhuma za kweli ndo anaomba msamaha, bado inteligencial ya papa ni kubwa na kumbuka ni dunia nzima.
 
Back
Top Bottom