Pengo: Wananipakazia madawa ya kulevya!

Pengo: Wananipakazia madawa ya kulevya!

Kwanini aombe msamaha kama hajadhibitisha, huwa anahakiki akiona tuhuma za kweli ndo anaomba msamaha, bado inteligencial ya papa ni kubwa na kumbuka ni dunia nzima.

Unafanya kazi maeneo yale kanisa katoliki lina monopoly. Unaweza pale mfano unakuta kijijini kanisa ni moja tu waumini wote pale wakatoliki, mjumbe wa nyumba kumi mkatoliki, kiongozi wa kata, tarafa, wilaya, mkoa hadi taifa raisi mkatoliki, mkuu wa polisi mkatoliki, usalama wa taifa mkatoliki hivyo unakuta padri, askofu, kardinali au papa akitaka kupata hata taarifa za yaliyotokea kijiji hata kilichoko mfano Rombo ilikuwa rahisi ni kumpigia simu kardinali wa nchi na yule anampigaia askofu wa jimbo askofu wa jimbo anampigia paroko wa parokia, yule wa parokia anampigia kiongozi wa kigango cha kijijini au wanapata hizo taarifa wanazipeleka juu kwa juu.

Mfumo huo unatumiwa na unafanya kazi hasa kwenye maeneo ya wakatoliki wengi.

Kwenye wakatoliki wengi yes unafanya kazi kusiko na wakatoliki wengi haufanyi kazi. Na pia zamani ulifanikiwa sababu watu walikuwa wasafi kulikuwa hakuna kulindana.

Lakini sasa hivi papa anaweza kuwa hajui kuwa Pengo kwenye list ya watuhumiwa wa madawa ya kulevya! au mheshimiwa unajua kuwa papa anazo hizo taarifa?
 
Waislam hawatetei waovu; only maaskofu ndio huwa hawakosi watetezi ambao hawataki kutumia akili all over the world; watoto wengi scotland na ulaya wameharibiwa wakristo na pope kimya

Wangekaa kimya wewe ungejuaje? Unadai waislamu hawatetei maovu, lini ulishawahi kumsikia muislamu akilaani Al Qaida, Al Shabab, Boko Haram n.k? Au kwako maovu ni nini, anapouliwa mtu anaejiita muislamu hata kama alipouliwa alikuwa anataka kuua binadamu wenzake?
 
Pengo anajua kwa roho yake kuwa huu ni uongo. Kama ni hivyo hatakiwi kuogopa wala kunyamazishwa aendelee na kazi yake ya kukemea maovu bila woga. Lazima tukumbuke hii nchi watu wengi hawako salama kila sehemu kuanzia wa juu mpaka chini ni kutishana tu. Pengo kwa nafasi yake hatakiwi kuogopa hata siku moja.

Kama ni siasa za maji taka aendelee hivyo hivyo. Hila hili jambo lina uzito wake ikichukuliwa kuwa pengo ni kiongozi mkuu wa kiroho katika jamii yetu. Serikali inatakiwa isikae kimya kwa jambo kama hili. Itoe msimamo wake kama either kuna uchunguzi wa jambo hili au ni uongo.
 
kila kitu si siasa,hizi issue za kudhalilisha watoto zinzolikabili kanisa dunoa nzima sasa na wakatoliki wenyewe wanalalamika kwambapapa hachukui hatua anaficha madhambi,JE NI HABARI LEO,CCM AU SIRIKALI INAHUSIKA.yule pdre alomnajisi mtoto chuo kikuu kweye gari ni serekali imetunga au habari leo.anachotakiwa pengo kusema ni kuilazmisha serikali ithibitishe.HE WHO ALLEGE MUST PROVE
Walipobanwa walimtaja yule mnigeria Okoch wa kakanisa fulani pale Biafra.
 
1. Askof Kado wa Same
2.Father Prisna Mkuu wa chuo cha ST JOSEPH MBEZ KIMARA
3.Father Frank wa Youth Katoliki
 
Utaratibu huo umejiwekea na nani? Kanisa katoliki au? Watu wengine bwana au umejiwekea na mkeo?

Mkuu hujawahi kusikia mtu akiambiwa kwamba umetajwa tajwa kuwa ni fisadi hivyo jivue gamba? Kujivua gamba hakuna ushahidi.
 
Hapa umazungumza uongo, mawaziri tunapishana nao madukani kila siku.
nadhan ni suala la muda tu,hata mawaziri wetu Hawajui bei za suti,je hawajiucsh na rushwa?
 
Nadhani hapa hoja ni kua je ni kweli....na je hawezi kujua haki zake Kama kiongozi mkubwa Kama yeye anasingiziwa na je kwanini wasijitokeze nyie mnaokataa kumtetea kuprove kwa umma jamani haya mambo yapo na Chombo cha haki na mahakama kama amechafuliwa na ni clean why tryin to sympathize with the public..... It is an issue that needs to be addresed well na sio kutafuta huruma ya jamii.... It's typical legal matter.....MPOOO?


Ukipenda chongo huita kengeza:lol:
 
1. Askof Kado wa Same
2.Father Prisna Mkuu wa chuo cha ST JOSEPH MBEZ KIMARA
3.Father Frank wa Youth Katoliki

Raisi Kikwete ana akili sana alipohutubia ile hotuba yake mbele ya viongozi wakatoliki akaongea nao kimafumbo kuhusu madawa ya kulevya makanisani waling`aka kwa nini aseme mbele yao? Wakamwona kama ***** vile .Nadhani kuna watuwameanza kubannwa mahali kichinin chini sasa wanalia nyau kutafuta huruma za wananchi na waumini.Waswahili husema lisemwalo lipo na kama halipo linakuja.

Waumini na wananchi waiache serikali ifanye kazi yake. Wasitafute uthibitisho toka serikalini kama Pengo anahusika au hahusiki wao after all sio mahakama.Na pengo aache kukimbilia mahakama ya wananchi au waumini ithibitishe kuwa yeye hahusiki.Mahakama ya wananchi au waumini haipo kwenye katiba wala haipo kwenye sheria yoyote. Kama anaona yuko kwenye tuhuma na anadhani kaonewa akimbilie mahakamani aache kukimbilia mahakama koko isiyokuwepo kisheria ya waumini au wananchi.
 
Kimbunga uko sahihi

Wanasheria wajitokeze kumtetea kwanini achafuliwe na yeye ni clean jamani?

Kama wamekurupuka na yeye ni clean basi akaithibitishie public wangapi wanshinda kesi dhidi ya serikali?
Nadhani na yeye atashinda tuache ushabiki
 
Jamani kwanza mnaojaribu kulihusisha suala la pengo Kama binaadamu na Kanisa Kama institution ni kosa kubwa hebu tuache kulihusisha Kanisa na suala binafsi .... Hizi ni tuhuma Kama waliowahi kuhusishwa wengine sehemu nyingine inakua ngumu kuamini mwanzo lakini ni kitu kinawezekana hapa hoja ni kweli si kweli....


A church it is an institution that existed before himm and will exist after him So tusiwe wapofu kiasi hiki...

Hapa inaweza kugeuka mjadala wa kidini hapa
 
busara za kadinali Pengo zinashangaza....sana....

kazi ya polisi ni kutodharau taarifa yeyote wanayopewa

sasa kama polisi wamepewa jina lake wafanyaje?
si lazima waliweke kwenye uchunguzi mpaka watakapothibitisha vinginevyo??

yeye ana wasiwasi gani ?

kwani wamemtaja hadharani au kwenda kum arrest?????

Hata mimi namshangaa sana sijui anaaogopa nini? Hajui polisi wetu wapo vizuri ku-deal na maandamano zaidi kuliko vitu vingine? Mbona Mwakyembe na Regnand Mengi wamewataja watu na wakiwa na ushahidi lakini mpaka sasa kimya? Hilo jina lake linaweza lisifanyiwe kazi.
 
Hizi siasa za kupima upepo, haya! wanasiasa wajue Pengo yuko vizuri hata kwenye hiyo elimu dunia.
 
Watanzania tunatakiwa kuwa na hofu ya Mungu na tukiwa na hofu hiyo tutawaheshimu pia watumishi wa Mungu bila kujali ni wakristo au Waislamu. Hivyo anayeyazusha haya ni kweli awe na uhakika wa anachokisema la sivyo huku ni kukosa hofu ya Mungu.
 
Hii habari inasikitisha sana. Ningependa Baba Askofu mkuu Pengo aweke hii habari vizuri. Mtumishi wa Mungu akituhumiwa inatisha sana tena tuhuhuma zenyewe zikiwa ni mbaya kama hizi za biashara za madawa ya kulevya.

Akiwa na kazi ya kueneze neno la Mungu, kusema ukweli, na kutetea ukweli hata ikimpasa kufa kama Yesu Kristu, Pengo alipaswa kusema kusema ni nani wanaotumhumu, walimtuhumu wapi, na kwa nini wamtuhumu. Kwanini atajwe yeye, ni mazingira gani yanafanya mpaka atajwe. Je ni kweli wanataka kumyamazisha na kwa nini wamnyamazishe?? Tuhuma za madawa ya kulevya ni nzito anatakiwa kutoa ufafanunuzi.
Tuhuma hizi zinachanganya sana wanakondoo wa Kanisa katoliki.

Baba Askofu weka mambo wazi ili waumini wajue ukweli, ili upande unaotoa tuhuma nao uje kuthibitisha au kukanusha.
Mpaka 2015 Tanzania hakuna kanisa wala msikiti itakuwa uwanja wa vita kati ya wanasiasa wanaotaka madaraka na yeyote anawazuia. Ila makanisa yanatisha yanashiriki na wahuni, wezi, watuhumiwa, majambazi, wahujumu na wala Rushwa. Makanisa na misikiti yanatumia makundi ya watuhumiwa kuchangisha fedha za kazi za Mungu. Kwenye watuhumiwa hawa kwa sababu wana fedha wapo wala rushwa, wauza unga, matapeli nk. Ukishiriki na mwizi na wewe ni mwizi, ukishiriki na mla rushwa na wewe ni mla rushwa, ukishiriki na mbakaji na wewe umebaka.
 
Hizi siasa za kupima upepo, haya! wanasiasa wajue Pengo yuko vizuri hata kwenye hiyo elimu dunia.

Elimu dunia sio kitu kikubwa siku hizi na si kitu cha kutishia mtu, hata mitandaoni wanafundisha, tena bure kabisa.
 
Jina lake kutajwa kuna tatizo gani? Nadhani amekosea. Mbona Obama ametajwa kuwa ndio magaidi na 1 duniani na bado wanaendelea na kazi Kuna tatizo gani? Issue ikiwa kama wamemkamata (sio kumhoji) ndio aseme vinginevyo mimi sikuona sababu ya yeye kusema kuwa ametajwa. Mimi ninachojua kuna Askofu wa kanisa katoliki alikuwa anafanya biashara (sina hakika kama ni ya kulevya, ila sifa yake alikuwa anatoweka jimboni hata miezi 3 hawajui alipo) na alishafukuzwa na kanisa. Huenda yeye kaenda kusema ili kuchafua wengine asitengeneze maswali mengi kuliko majibu
 
Back
Top Bottom