Pendekezo: Kiswahili kitumike kama lugha ya kufundishia ngazi zote za elimu, ili tukomboke kifikra

Ushora Ndago, Nafikiri kwa kuanzia tuwe na shule na vyuo ambavyo vitafundisha masomo yote kwa Kiingereza, na vingine vifundishe masomo yote kwa Kiswahili. Watu wapewe chaguo la wapi watawapeleka watoto wao.

Halafu tutaangalia mtoto wako na wa mawaziri na makatibu wakuu, watapelekwa shule na vyuo vya mudium ipi. Ila sisi wengine, tutapeleka zile za English medium maana sitaki mwanangu apate shida hata siku nikiamua masomo ya degree au mafunzo mengine yoyote afanye nje ya Tanzania. Na sitaki mwanangu nimpunguzie uwigo wa ajira Duniani kwa sababu tu ya kigezo cha lugha.

Wachina, Waturuki, Wamalaysia, Wahindi, wote wamekazana kuwa na vyuo vinavyotoa masomo ya level mbalimbali kwa lugha ya Kiingereza, sisi tunataka tutoke kwenye Kiingereza, twende kwenye Kiswahili.

Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, 'tunajivunia Kiswahi lakini hatuna namna ya kukikwepa Kiingereza maana ndiyo Kiswahili cha Dunia".

Kama tungekuwa na watu wanaojali maendeleo ya Elimu, wangeweka utaratibu wa masomo yote kufundishwa kwa Kiinhereza toka primary mpaka university.
 
na interview iwe kwa kiswahili. mwekezaji akija ajifunze kiswahili kabla ya yote. Mkiweza hili basi Mtajikomboa Watanganyika. sorry WaTZ
 
Yaani kwa kuwa jamaa lugha inamgonga ndiyo unaleta pendekezo hilo sasa, hapana. Mtu ni PhD holder halafu simple english inamtoa kamasi inaahangaza .
 
Mtoa maada kama ulisoma kozi yenye kiswahili chuo unaweza kuona mambo ni rahisi.

Ila nakuapia Kama umesoma Kozi ya Afya au Engineering chuo huwezi kuongea huu ushubwada.

Ningekuona wa maana kama ungepigania kiswahili kiongezewe maneno zaidi na zaidi kabla ya kuanza kufikiria kiswahili kuwa lugha ya kufundishia. MASSHELE,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanangu siwezi wafundisha kiswahili Mimi sijaona faida take! Kalugha ka kuunga unga kako kwa ajili ya kujazana ubishi tu. Hivi taaluma za kuunda meli, ndege, udaktari nk utatumua kiswahili gani kuwaelewesha wanafunzi? Hebu tuache ujinga basi!
Mtoa maada sijui amekula nini leo. Engineering au Health sciencies zilivyo ngumu kwa kiingereza eti uje utumie kiswahili. Acheni ujinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumechelewa sana mkuu tukikurupukia na hili tutakwenda kuwa vichekesho vya dunia
 
Acha Alinacha zako. Kuna Watanzania wengi tu ambao ni wazalendo hawakusoma kwa Kiswahili. Au unataka kutuambia kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa na kasumba ya ukoloni?
Kama hujui English wewe jitahidi tu kujifunza. Hakuna sababu ya kutaka kila mtu akose fursa ili tu mlingane.
Kwani sasa tunapata fursa gani kwa kufundishwa kwa kiingereza? Maana pamoja na kufundishwa kwa kiingereza bado kiingereza hatujui si wasomi wala wasio wasomi.
 
Akilindogosana,
Tatizo sio lugha ya asili bali lugha ambayo unayoifahamu vizuri,sasa hapa Tz inajulikana kabisa kiingereza ni shida na muda mwingi tunatumia kiswahili katika mambo yetu.
 
mb

mbona wewe huna akili kabisa kwani technolojia haiwezi fundishwa kwa kiswahili jinga kweli wachina wanajua kiingereza? mbona wameenda mwezini

hakuna utumwa mbaya kama wa fikra afadhali wa kipato
Sasa wewe na mchina mko sawa? Veta wanafundishwa kiswahili ukitajiwa components za engine ya gari na mwalimu wa VETA hutawahi kukitamani hicho kiswahili unachokisifia.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
wewe ndo mjinga mkubwa usiye elewa maana ya kufundisha kwa kiswahili watanzania wote tunaongea kiswahili alafu lugha yenye kuongelewa na wale waliopata bahati ya kusoma iwe lugha ya kufundisha. Huu ni unyanyasaji watoto wetu wangefaulu na kuelewa masomo vizuri

Na huenda una wadhifa katika serikali hii wewe mzigo mkubwa sana
Tatizo mnataka kila neno kwenye techonology basi ulitafutie neno lake la kiswahili tena mara nyingi linakuwa gumu.

Huwezi kufundishia kiswahili elimu ya juu. Hasa kwa field za health sciences na Engineering.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe una elimu gani kwanza. Tuanzie hapo.
wewe ndo mjinga mkubwa usiye elewa maana ya kufundisha kwa kiswahili watanzania wote tunaongea kiswahili alafu lugha yenye kuongelewa na wale waliopata bahati ya kusoma iwe lugha ya kufundisha. Huu ni unyanyasaji watoto wetu wangefaulu na kuelewa masomo vizuri

Na huenda una wadhifa katika serikali hii wewe mzigo mkubwa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
China hadi leo hii haitaki kuitwa first world (developed) country. Na ina vyuo vingi tu vinavyotoa kozi zao kwa Kiingereza. Unadhani ni kwa nini?
Unadhani ni kwa nini nchi nyingi duniani hadi leo zinatumia terminologies za Kilatini kwenye legal matters?
Can you explain that?
Sasa waswahili wanataka maneno ya kilatini wayaweke kwa lugha ya kisukuma halafu hiyo lugha ndo tufundishie. Aiseee hebu tuwe serious.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom