A stupid thinking capacity.
Nani wa kuchukuwa pendekezo lako dhaifu.
mkuu yule demu alitoa tamko kumpinga Heche alikuwa ametumwa na wale wahanga wa BAVICHA ambao huwa wanashinda fcbk kupiga majungu na soga alafu eti nao ni makamanda, lakini bado haibadilishi uwezo wa Heche kuwa jamaa ni jembe na anakubalika sana na anafaa zaidi japokuwa baadhi ya vijana uchwara wa CDM hawapendi kusikia hilo but still Heche ni dhahabu ndani ya CDM na hata kama akigomeba urais wa dunia sisi vijana wenzake tutampa kula.
Big up John Heche
Ni hoja nzuri kwa maslahi mapana ya chama.Naamini viongozi watalichukua pendekezo hili kwa umakini mkubwa.Hongera mkuu kwa lengo lako zuri la kuimarisha chama zaidi.
mkuu huyu demu alitumwa na wenzake kule fcbk so usipate shida kwani pia ukweli utabaki pale pale John Heche ni jembe wala huwezi kumlinganisha na yuel mzee kijana wa UVCCM Martin shigela.
Jamaa mbaya kwenye kusugua santuri a.k.a chapati alitisha enzi hizo.Ulikuwa ukimkuta katupia shati la ujiuji vifungo kafungua pembeni ana kitaulo atawarusha mpaka majogoo.Nasikia jamaa alikuwa anasugua disc pale bills ni kweli?
Zitto a.k.a mdogo wake Shibuda bado tunamhitaji CDM!! Teh teh teh teh teh teh teh teh!!
Kwani hata Komu si alikuwa mtunza fedha wa Keys hoteli ya Ndesamburo unashangaa hayo CDM.Kuna kipindi fulani Dk slaa alipeleka mapendekezo kamati kuu kwamba mchumba yake ambae ni josephine mushumbusi anafaa kuwa mwasibu mkuu wa chadema lakini wajumbe wakamtosa lakini wa fitna na majungu ya slaa akamuondoa samson mwigamba.
Kwani hata Komu si alikuwa mtunza fedha wa Keys hoteli ya Ndesamburo unashangaa hayo CDM.
Zitto a.k.a mdogo wake Shibuda bado tunamhitaji CDM!! Teh teh teh teh teh teh teh teh!!
Nakushukuru sana mkuu kunisaidia kunyoosha maelezo.Wala sijasema Zitto hafai bali amezidiwa na majukumu ya kibunge.Nafasi ya Naibu Katibu mkuu inapaswa kukabidhiwa kwa mtu asiye na majukumu zaidi ya hilo moja tu la kukisambaza chama kila kona ya nchi.
Naamini kabisa kuna watu wanatumiwa humu ndani kwa makusudi mazima ya kuhakikisha Zitto Kabwe anakuwa mchafu daima ndani ya CDM, na haiishii hapa tu hata baadhi ya magazeti yanafanya juhudi hizo pia
Na Zitto hachafuliwa kwa bahati mbaya, HAPANA..... huu ni mpango mkakati baada ya kuonekana Zitto amekuwa tishio kwa ''wenye'' CDM yao.Maana kwa kadiri mambo yanvyozidi kwenda ndivyo ninavyo shindwa kutofautisha sakata la marehemu Wangwe na CDM kwa ujumla na hili analoandamwa nalo Zitto Kabwe
Toka Zitto amechukua na kugombea uenyekiti wa CDM na sakata zima hadi kuja kuzimwa basi amejitengenezea maadui wakubwa ndani ya CDM, na kama una akili timamu basi pasi na shaka utaelewa ni kundi la uongozi wa juu ndilo hasa lenye uhasama na zitto kabwe
Hivi sasa Zitto anatengenezewa picha ya msaliti, mroho wa madaraka nk nk kwasababu tu naamini ndani ya CDM ni wachache sana wanaoweza kusimama na kusimamia hoja zao ndani ya chama na si matakwa ya "wenye chama" wanavyotaka
Na hii ndio kila chaguzi ndani ya chama wele wenye kufuata matakwa ya wenye chama huwa tofauti na wenye fikra huru za kidemorasia ndani ya chama(akina zitto) na kufanya makundi ya Mbowe(wenye chama) na Zitto(fikra huru)
Tuhuma zote anazotuhumiwa Zitto humu kama kula bata na mukulu na kutooneka kwenye M4C nk hazina ukweli wowote, kwa kadri nijuavyo chama kinapanga kila kitu na si watu wanajipeleka kama unakwenda sokoni, safari zote za Zitto zinajulikana CDM na zinakwenda kwa mujibu wa nafasi zake.
Kama madai hayo yanaukweli mbona makao makuu au viongozi hawasemi chochote juu ya hilo
Wale wote mnaotumiwa katika hili mnatakiwa kufahamu kitu kimoja muhimu sana, mnajenga na kuyapa uhai na nguvu madai ya wapinzani wa CDM kuwa wadini na wakanda
Kwamba wale wote wanaoonekana wanakuwa tishio dhidi ya wa watu wa ukanda fulani basi wanapikiwa zengwe kama inavyotoke kwa mh Zitto Zuberi Kabwe
Just my opinion