PCCB: Tuna manufaa nayo?

PCCB: Tuna manufaa nayo?

Wambili, wewe unatetea ufisadi tuu ama na wewe ni fisadi?

Hosea lazima ajiuzulu na TAKUKURU lazima ifumuliwe yote kwani ripoti yao ipo miongoni mwa attachments walizopewa wabunge , na inaonyesha jinsi alivyoitetea Ricmond.

Lazima awajibike, haiwezekani PM awajibike na huku Baraza livunjwe naye asiwajibike, .

Kama TAKUKURU wangefanya kazi yao vizuri wakati ule na wakatoa ripoti ya ukweli ni kuwa leo taifa hili lisingekuwa kwenye hali hii ya kuchanganyikiwa kiasi hiki.

Huyu Hosea na TAKUKURU yake ndio imelifikisha hili taifa kwenye ufisadi mkubwa na wa kutisha kiasi hiki, wale mnaofikiri kuwa hapa kuna utani subirini muda utasema .
 
Hosea leo kaifanya TAKUKURU maana yake kuwa ni -Taasisi ya Kubatiza na Kupitisha Rushwa , leo wapo watanzania wanadhubutu hata kumtetea jamani, ama ni yeye binafsi ndio yupo hapa anajiandikia ?

Hosea ,shame on you ;
 
Wambili inaonekana wewe umejiunga JF kuja kumtetea Hosea. kwa faida yako, kwanza kasome kanuni za JF humu hatufanyi finger pointing za kutaja watu majina simply because wametoa hoja ambazo hukubaliani nazo. Infact wewe utakuwa ni muongo umejuaje huyu kwamba ni Awadhi sijui nani? This is JF where we dare talk openly bwana. HOJA HUJIBIWA KWA HOJA. zaidi ya hapo ni uzushi ambao JF hatuuhusudishi....Au unafikiri Hosea alivyokwenda mbele ya Vyombo vya habari na umma wa watanzania kutudanganya..tulikuwa usingizini. Hivi mnajua kwamba mnaishi kwa jasho letu sisi walipa kodi? mbona mnatusaliti hivyo?

Hosea is just another incompetent and hopeless mtendaji in our system. He should be sacked (ingawa nasikia kesha resign)na afilisiwe all his ill gotten wealth!

Bwana WAMBILI hapa tunakesha tunahangaika na maslahi ya taifa na siyo hizi cheap politics za kujikomba komba, ambazo inaonekana unaziendekeza. Anyway kwa vile ni mgeni tunakupa mda..ujirekebishe. Soma kwanza mawazo ya watu humu ujifunze kujenga hoja.

Otherwise karibu Jambo Forum!

Aise..harafu jamaa hiyo ndo post yake ya kwanza!!! duuuuuh!!
 
Jamani tuwe macho na hawa Wanasiasa na wasioitakia mema Takukuru,msitake kupindisha mjadala kwa kuandika masuala yanayomuhusu Dk. Hoseah,ninafahamu kwamba;
Uchunguzi walioufanya Takukuru kama ilivyokuwa kwenye sheria yao ya zamani ulihusu rushwa,na Dk Mwakyembe ktk taarifa yake hakuna sehemu aliyozungumzia kwamba kuna rushwa fulani waliyoiona ambayo Takukuru hawakuifanyia kazi
Na hata ripoti waliyotoa hawakuzuia vyombo vingine kama PPRA visifanyie kazi,nikiikumbuka ile taarifa yao walisema kuwa serikali haikupata hasara hadi wakati ule kwa sababu hakukuwepo pesa iliyolipwa,sasa ulitaka Takukuru wawe wanasiasa kwa kusema wananchi walikuwa gizani hivyo Serikali ilipata hasara na ushahidi huo wapeleke mahakamani?
Tusiwaonee Takukuru na Dk Hoseah,kwa uelewa wangu mdogo wa utumishi wa umma Dk Hoseah siyo ngazi ya uteuzi wa Wakurugenzi,wanateuliwa na Rais,usipotoshe umma kwa kuwadanganya Wananchi kuwa yeye aliteua Wakurugenzi dhaifu,ninachofahamu mimi hao Wakurugenzi wana uzoefu wa muda mrefu kwenye utumishi wa umma,udhaifu wao upo wapi? Kwenye kujibu maswali?
Umedai Dk Hoseah aliikimbia kamati ya Richmond,ulitaka aende nani kama siye Mkurugenzi wa uchunguzi anayesimamia masuala yote ya uchunguzi Takukuru?
Mwacheni Dk Hoseah aitengeneze Takukuru vizuri,kwani hatujui kwamba wakati wa Gen Kamazima wewe Alex Kuhanda na Awadh Mohamed mlikuwa miungu watu? Marupurupu mangapi mlikuwa mkiyapata ambayo watumishi wenzenu walikuwa hawayapati? Ninafahamu kuwa Dk Hoseah kaifanya Takukuru imekuwa ya wote, kawadhibiti kisawasawa,suala la wewe Awadh kushindwa hata kunyoa ndevu,nalo ni la Dk Hoseah? Nani alikutuma uoe wake zaidi ya wawili? nyie endeleeni na juhudi zenu za kupeleka maneno huko na huko ya majungu,hamuwezi kuupotosha umma.Wabunge mliokamatwa na Rushwa tunawajua,tumewaona mnavyochangia kwa kuonyesha chuki zenu,mlitaka msikamatwe? ITENDEENI HAKI TAKUKURU,MTENDEENI HAKI DR HOSEAH.
Big up Wambili,Kuhanda a.k.a Mrundi na Awadh a.k.a Osama mmesikia hotuba ya Waziri Mkuu Mteule Mh. Pinda? "Yaliyopita si ndwele tugange yajayo" Msaidieni Dk Hoseah kupambana na Rushwa,zingatieni masomo yenu badala ya kuzunguka maofisi ya Serikali na kwa watu binafsi kuuza maneno.Kumbe Mh.Mbunge wa Simanjiro TAKUKURU walishaku-tight? Unadhani utaimaliza kesi kwa kuikoromea TAKUKURU? Tumeiona dhamira yako,huko ndio kuwawakilsha wananchi waliokutuma bungeni? TAKUKURU MSIRUDI NYUMA KWA MANENO YA WANASIASA,WASAIDIENI WATANZANIA,IMANI YETU IPO KWENU.
 
Mwacheni Dk Hoseah aitengeneze Takukuru vizuri,kwani hatujui kwamba wakati wa Gen Kamazima wewe Alex Kuhanda na Awadh Mohamed mlikuwa miungu watu? Marupurupu mangapi mlikuwa mkiyapata ambayo watumishi wenzenu walikuwa hawayapati? Ninafahamu kuwa Dk Hoseah kaifanya Takukuru imekuwa ya wote, kawadhibiti kisawasawa,suala la wewe Awadh kushindwa hata kunyoa ndevu,nalo ni la Dk Hoseah? Nani alikutuma uoe wake zaidi ya wawili? nyie endeleeni na juhudi zenu za kupeleka maneno huko na huko ya majungu,hamuwezi kuupotosha umma.Wabunge mliokamatwa na Rushwa tunawajua,tumewaona mnavyochangia kwa kuonyesha chuki zenu,mlitaka msikamatwe? ITENDEENI HAKI TAKUKURU,MTENDEENI HAKI DR HOSEAH.

Heko Wambili

Nimekuwa naudhika sana na hasa hawa vijana wawili hasa huyu Osama - Awadh - mrishog ambaye Dr. Hosea ndiye alimpigia debe akaingia PCB enzi hizo baada ya kushidwa kupata kazi ya maana akitokea uarabuni. Waswahili husema ukimzoe mbwa atakufuata hata msikitini. Tena Osama unatamba kuwa umemmfikisha Hosea Ikulu eti anakunyanyasa halafu wakati huo huo unaweka malicious postings hapa JF huku unajulikana wazi, hivi kweli unazo akili timamu; si unajiaribia kesi yako? Amakweli OSAMA; na huyu shoga yako Kuhanda anayetumia kompyuta za shule Mzumbe kuandika uongo usiothibitika hata hajui kuwa anaacha data trail halafu anajiita mchunguzi, shame on you, unasahau hata Investigation Class 101 "never leave a trail" of your presence when doing covert ops!

My advise to both of you ni kwamba sisi sote ni waajiriwa PCCB, Hosea ana mapungufu yake lakini mnaelewa wazi kuwa kuna njia za kufuatwa na siyo kuvumisha uongo bila dataz na kudhani kuwa hutafahamika hasa baada ya kusema maneno ambayo huwezi kuya substantiate with hard facts. Wewe Awadh unasema kuwa kulikuwa na ripoti mbili je leo ukiambiwa uionyeshe hiyo nyingine utaitoa wapi huku unajua ukweli kuwa ripoti ni moja tu. Someni salama tuacheni tufanye kazi na pindi sheria itakapo rekebishwa na kutupa more latitude then tusulubishwe. Hivi wewe Awadh Osama kila mmoja Takukuru unamponda, mkurugenzi wa upepelezi/uchunguzi unamponda, unasema siyo mwana sheria , na Kihiyo ni bwana misitu, na mkurugenzi wa elimu kwa uma unamponda, wewe kwenda kusoma IFM kwenyewe umeshidwa kumaliza hako kadiploma umeshindwa halafu maneno kibao. Na wewe Kuhanda does "rwukewee" make sense to you kama huelewi pole saana.
 
Mrisho kutokana na uzoefu wangu nakubaliana nawe kwa mengi sana .Hosea ni msabato Fisadi mkubwa na a very opportunist person. Lakini yote hata namwaga lawama kwa JK .Alimpa asante kwa kushiriki siasa za kipuuzi za kumsaidia kummaliza Sumaye .Dhambi ile inaitafuna Serikali ya JK sasa . Mfungo ni msanii kiasi . Kuna issue nilimkalia kooni alionekana sincere lakini si mwelewa hata exposure yake ndogo .Zaidi nadhani anapenda ama alikuwa anafuata habari za bwana mkubwa Hosea .Naomba kwa kuwa Hosea kesha ondoka sasa Mwanasheria Mkuu please leave our office .
 
Mrisho kutokana na uzoefu wangu nakubaliana nawe kwa mengi sana .Hosea ni msabato Fisadi mkubwa na a very opportunist person. Lakini yote hata namwaga lawama kwa JK .Alimpa asante kwa kushiriki siasa za kipuuzi za kumsaidia kummaliza Sumaye .Dhambi ile inaitafuna Serikali ya JK sasa . Mfungo ni msanii kiasi . Kuna issue nilimkalia kooni alionekana sincere lakini si mwelewa hata exposure yake ndogo .Zaidi nadhani anapenda ama alikuwa anafuata habari za bwana mkubwa Hosea .Naomba kwa kuwa Hosea kesha ondoka sasa Mwanasheria Mkuu please leave our office .

Hivi Johnson Mwanyika hajaachia madaraka mpaka sasa?
Nitashangaa kama bado kakalia ofisi.
 
Jamani tuwe macho na hawa Wanasiasa na wasioitakia mema Takukuru,msitake kupindisha mjadala kwa kuandika masuala yanayomuhusu Dk. Hoseah,ninafahamu kwamba;
Uchunguzi walioufanya Takukuru kama ilivyokuwa kwenye sheria yao ya zamani ulihusu rushwa,na Dk Mwakyembe ktk taarifa yake hakuna sehemu aliyozungumzia kwamba kuna rushwa fulani waliyoiona ambayo Takukuru hawakuifanyia kazi
Na hata ripoti waliyotoa hawakuzuia vyombo vingine kama PPRA visifanyie kazi,nikiikumbuka ile taarifa yao walisema kuwa serikali haikupata hasara hadi wakati ule kwa sababu hakukuwepo pesa iliyolipwa,sasa ulitaka Takukuru wawe wanasiasa kwa kusema wananchi walikuwa gizani hivyo Serikali ilipata hasara na ushahidi huo wapeleke mahakamani?
Tusiwaonee Takukuru na Dk Hoseah,kwa uelewa wangu mdogo wa utumishi wa umma Dk Hoseah siyo ngazi ya uteuzi wa Wakurugenzi,wanateuliwa na Rais,usipotoshe umma kwa kuwadanganya Wananchi kuwa yeye aliteua Wakurugenzi dhaifu,ninachofahamu mimi hao Wakurugenzi wana uzoefu wa muda mrefu kwenye utumishi wa umma,udhaifu wao upo wapi? Kwenye kujibu maswali?
Umedai Dk Hoseah aliikimbia kamati ya Richmond,ulitaka aende nani kama siye Mkurugenzi wa uchunguzi anayesimamia masuala yote ya uchunguzi Takukuru?
Mwacheni Dk Hoseah aitengeneze Takukuru vizuri,kwani hatujui kwamba wakati wa Gen Kamazima wewe Alex Kuhanda na Awadh Mohamed mlikuwa miungu watu? Marupurupu mangapi mlikuwa mkiyapata ambayo watumishi wenzenu walikuwa hawayapati? Ninafahamu kuwa Dk Hoseah kaifanya Takukuru imekuwa ya wote, kawadhibiti kisawasawa,suala la wewe Awadh kushindwa hata kunyoa ndevu,nalo ni la Dk Hoseah? Nani alikutuma uoe wake zaidi ya wawili? nyie endeleeni na juhudi zenu za kupeleka maneno huko na huko ya majungu,hamuwezi kuupotosha umma.Wabunge mliokamatwa na Rushwa tunawajua,tumewaona mnavyochangia kwa kuonyesha chuki zenu,mlitaka msikamatwe? ITENDEENI HAKI TAKUKURU,MTENDEENI HAKI DR HOSEAH.

Takukuru imeshindwa kukidhi malengo yaliyoiunda, Period. Kashfa ya Richmond ilichunguzwa kwa miezi sita, report ikaundwa vizuri in favour ya EL et al. Tume imefanya kazi kwa siku 45 na imekuja na analysis iliyomweka chali Duct Hosea na Mwananyika. Sio mpaka wajiuzulu, JK tengua uteuzi mara moja, vinginevyo Tz itakuwa inakwenda hatua mbili mbele then nne nyuma.
 
Nakubaliana na Wambili; Kuhusu Dr. Hosea... kuna haja ya mjadala zaidi kidogo...


1. Ripoti ya TAKURU/PCB ilitoka kipendi cha sheria ya Zamani... ambayo ilikuwa inatambua tu rushwa (bribe) hakuna zaidi ya hapo... na Dr. Mwakyembe pia hakuwahi pata hilo...

Ila pamoja na mapungufu ya TAKURU/PCB enzi hizo at least wangesema basi kulikuwa na mazingira ya GIZA,,, hapa ndio mimi niliwashangaa. Zaidi ya hapo sina shida nao.​

2. Report ya Dr. Mwakyembe, imekuja kipindi cha TAKUKURU/PCCB ambapo wigo wa corruption ni mpana... so... Repoti ya Dr. Mwakyembe haukutenda haki kamili in terms of kuuelezea mambo wazi... lakini bado... taasisi ya kuzuia rushwa bado ina matatizo ya kutosha... kwa hiyo ruhsa kutishwa...

Let us know the two context... before judging!!!
 
Wana JF, PCCB imetuangusha WaTz katika mapambano ya rushwa. Ili tuwe na silaha kali, je tuivunjilie mbali tuunde chombo kipya kitakachokuwa, pengine chini ya wabunge? Au tubadili uongozi wa sasa?
 
Kuvunja PCCB sidhan kama litakuwa jambo la busara..ila Uongozi wa PCCB unahitaji mabadiliko makubwa sana kwa sasa..huenda chini ya Utendaji wa bwana PM.M.K.P.Pinda unaweza kufanya kazi kwa ufanisi na uwazi zaidi.Pili nilipenda mawazo ya mbunge mmoja alipendekeza iundwe tume ambayo itakuwa inashughulikia mikataba mikubwa ambayo inchi inaingia,faida zake na hasara kwa taifa.Nadhan kwa kufanya hivyo kutapunguza matatizo kama yaliyojitokeza kwenye Buzwagi,richmonduli na kwingineko..hata huyu bwana kichaka,George anaekuja kesho huenda akataka kuweka mradi huku kwetu..iwe kwenye mafuta au mbugani huko hii tume iwe na wajibu wa kuichunguza kama nchi itanufaika au ilamba galasa.
 
Kuvunja PCCB sidhan kama litakuwa jambo la busara..ila Uongozi wa PCCB unahitaji mabadiliko makubwa sana kwa sasa..huenda chini ya Utendaji wa bwana PM.M.K.P.Pinda unaweza kufanya kazi kwa ufanisi na uwazi zaidi.Pili nilipenda mawazo ya mbunge mmoja alipendekeza iundwe tume ambayo itakuwa inashughulikia mikataba mikubwa ambayo inchi inaingia,faida zake na hasara kwa taifa.Nadhan kwa kufanya hivyo kutapunguza matatizo kama yaliyojitokeza kwenye Buzwagi,richmonduli na kwingineko..hata huyu bwana kichaka,George anaekuja kesho huenda akataka kuweka mradi huku kwetu..iwe kwenye mafuta au mbugani huko hii tume iwe na wajibu wa kuichunguza kama nchi itanufaika au ilamba galasa.


Nakubaliana nawe Senator kwa asilimia zote .Aletwe mtu msafi mwenye maanadili na uchungu na Nchi then ata restructure PCCB wale wa mikoani kwa faida ya Hosea sasa wawekwe pool na wawe monitored .
 
This is no brainer, Ivunjwe haraka sana; na ikibidi ajiri expatriates unaoweza kuwawajibisha bila kuwaonea soni, kama sisi wenyewe hatuwezi kazi. Drastic measures for drastic situations - this is one amongst the many such situations we face in our country at the moment.
 
Kwanza wakuu huyu HOSEA ameshajiuzulu? Mbona sijasikia lolote toka kwake, any news?
 
Festog, swali zuri hata mimi nadhani nilikuwa najiuliza thesame. Nakumbuka wiki iliyopita nadhani tuliona kwa magazeti kwamba ameandika barua ya kujiuzulu lakini sijaona popote wakisema imekubaliwa.

Back to the point. Sidhani kama tunahitaji "EXPATRIATE" kuja kutuonyesha rushwa jamani.... Ingekuwa in 1961 wakati mwalimu amechukua nchi ningekubaliana na hilo. Pili, nimekuwa nafuatilia issue za anti-corruption hapa nyumbani na kwa kweli tuna nguvu nje ya serikali kuna NGOs zina deal na corruption pekee.

Hatuhitaji kuwa na mtaalamu lakini tunahitaji mtu ambaye ana track record nzuri.... hawa wapo wachache mitaani manake tukumbuke kuna waliofukuzwa humo humo serikalini sababu waligoma kupitisha mambo ya wazee.... Sisemi kwamba ni wasafi saaana ila ninaonelea ule msimamo wao ndio tunaouhitaji kwa sasa esepcially kuzingatia fact kwamba kuna mabomu mengi ambayo inabidi tuyaangalie katika serikali, mikataba kwa sasa.... Kingine ni kwamba kama tunaamua kuvunja uongozi wa PCCB then tusijidanganye kwa kubadili kichwa expecting big changes. Inabidi kama ni mabadiliko basi tuanze top (minimum all directors at HQ), then tuingie mikoani na kubadili the top 3.....

Hapo ni mtihani mkubwa sana kwa JK lakini tukumbuke kuwa hii ziara ya Kichaka may delay things (note the word delay) tungoje tuone moshi na mioto ikiwashwa in March 2008 (my feeling na sio speculation)

Mungu Ibariki Tanzania na watu wake........
 
This is no brainer, Ivunjwe haraka sana; na ikibidi ajiri expatriates unaoweza kuwawajibisha bila kuwaonea soni, kama sisi wenyewe hatuwezi kazi. Drastic measures for drastic situations - this is one amongst the many such situations we face in our country at the moment.

Mkuu Kalamu,

1. inaonekana rushwa imekuwa tatizo kubwa hata kudhoofidha sana uchumi wa Tanzania. Kwa utajiri wa rasilmali tulizonazo, na jinsi zinavyotumika, inawezekana tungekuwa matajiri miongoni mwa nchi za kusini mwa Afrika. Unadhani pengine kwa kutambua uzito wa tatizo, na kwa sababu rushwa mbaya zaidi ni ile kubwa (grand corruption, tuunde chombo cha maafisa wa uwezo wa juu sana kama The Scorpions, wa South Africa?

2. Vinginevyo, tubadilishe muundo wa PCCB kwa kuiweka chini ya wananchi, yaani iwajibike kwa bunge. Hii nayo nadhani ni effective, kwa kuwa hawa watakuwa wanafanya kazi without fear or favour.

Lakini hizi njia zote mbili zinahitaji political willingeness ya serikali, je itakuwa tayari? What do you think?
 
Kama ni Expatriate basi tunahitaji expatriate President yanini kufanya mambo nusu nusu?
 
Kama ni Expatriate basi tunahitaji expatriate President yanini kufanya mambo nusu nusu?

kaka hivi kweli chombo cha kudeal na rushwa una kiona ni sawa na uraisi? ingawa sikubali hili la kueleta hao experts. lakini kama watakuja kwa kufanya uchunguzi wa 'damu' ili kutibu majipu kama alivyosema wangwe, chacha naona itakuwa vizuri! si umesikia mambo mazuri yaliyofantwa na delloite na ernest and young? hawa wote sio makampuni ya ndani! ni wataalum kutoka 'nnje'. na wametuletea matunda mazuri tu. mimi nadhani tunawahitaji kuja kutuonyesha wabaya wetu then watuachie wenyewe tuendelee sasa na kina mwakiembe wetu.
 
Back
Top Bottom