PCCB: Tuna manufaa nayo?

Kadhia hii imenichefua kweli. Nadhani JK ana kazi kubwa zaidi ikiwa hili nalo lina mantiki ndani yake. Ninapendekeza iundwe taasisi nyingine inayoitwa LIKUTAKURU ( Lijitu la Kuzuia TAKUKURU Kula Rushwa).
 
Jamani,

Si amesha jieleza? mwenye facts alete ku counter his claim! kama hatuna tukae kimya! naamini US sio taabu kupata nani anamiliki nini, sasa tatizo lipo wapi?

Au mimi nimepitwa kidogo na yanayoendelea?
 
SaharaVoice,

Kwanza kabisa ndugu yangu ngoja nikuukize swali hili "Je utamwamini yule aliyepewa nyeti azitunze asimpe mtu halafu akakumegea na kukwambia kuwe iwe siri kwa vile aliyempa hizo siri alimwambi ni siri na hatakiwi mtu mwigine ajue; ila kwa vile wewe ni mshikaji nakumegea ila iwe siri!" . Haya nimbie mwenzangu kuna siri hapo? Wewe siyo custodian wa siri za SIRIKALI na bado watamani kuzipata ili iwe nini? Siri za serikali ni za serikali sio za kila mtu!
MENOSUGU

Menosuga,

Siri za serikali ni zile siri zenye manufaa kwa taifa, manufaa kwa wananchi walio wengi. Siri zenye faida kwa wachache, mafisadi na rafiki zao, hata siku moja haziwezi kuwa siri za taifa.

Civil servants hata kwenye nchi zilizoendelea huwa wanaleakisha siri za namna hiyo, matokeo yake viongozi wao wanawajibika zaidi, hawajiingizi kwenye vitendo vya ovyo kwa kutegemea civil servants watawatunzia siri.

Kwa faida ya nchi yetu, siri za hawa wezi zimwagwe tu. Kwa faida ya wanetu huko mbele, lazima hizio siri zianikwe nje ili wasikose pa kujificha.

Kwa kusoma ujumbe wako naona uko tayari kulinda hata uovu kwa kisingizio cha siri ya serikali, kwa kufanya hivyo na wewe utakuwa fisadi. Tukikujua tutakuumbua tu bila kuogopa.

Kama anavyosema Mwafrika wa Kike, inabidi tufike mahali tuchukie
ili hawa jamaa wasituone wajinga. Wakati ndugu zetu wanakufa huko wilayani, wengine wanapasuliwa vichwa badala ya miguu, sisi tunasema siri za serikali, ni serikali gani hii isiyowajibika kwa watu wake?

Tuleteeni hizo siri wengine tuzimwage hapa. Kama nilivyoandika mwanzoni, sijali mleta siri ana motives zipi, ninachojali ni ukweli wa hizo siri. Kitu ambacho sitaki ni kuwachafua kwa makusaudi watu ambao wanachapa kazi, kama walivyomfanya yule jamaa wa wizara ya elimu.
 
Jamani,

Si amesha jieleza? mwenye facts alete ku counter his claim! kama hatuna tukae kimya! naamini US sio taabu kupata nani anamiliki nini, sasa tatizo lipo wapi?

Au mimi nimepitwa kidogo na yanayoendelea?

FD,

Ni kweli Hosea kajieleza na ni jambo zuri, lakini kwasababu kaamua kujieleza inabidi aweke mambo wazi zaidi. Kama familia wanapanga hiyo nyumba, si aeleze wanapanga wapi na kwa kiasi gani? Akishatoa hiyo habari basi tuna uwezo wa kufuatilia kama kweli wanapanga huko. Refer suala la mke wa Kitine na hospitali yake fake. Hawa wakuu huwa wanajitamkia mambo wakidhani hatuwezi kuchunguza mpaka kupata ukweli. Hakuna kuamini maneno miaka hii maana hawa vigogo wanatufanya wote wajinga.

Mimi naamini Hosea huenda anasema kweli lakini kuamini peke yake hakutoshi tunahitaji ushahidi. Kwa mfano anasema nyumba yake sio ya multi bilions, si angesema imemgharimu kiasi gani kujenga na pesa alitoa wapi? Maana kwa mfanyakazi wa serikali na asiye na biashara nyingine, kujenga nyumba hata ya milioni kama 500 bado inaweza kuleta maswali mengi.
 
Mtanzania,

Yeah, kama kinara wa PCCB angesema, nyumba yangu wanayosema ni ya kwangu ipo OHIO Marekani mtaa wa Narung'ombe plot KXBII12145 ya ghorofa mbili. Hii nyuma nimeipanga kwa Mheshimiwa FIKIRADUNI, mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM na mgombea wa CC-NEC wa uchaguzi ujao, ninamlipa shs 3,000,000 kwa mwezi. Jamani sio nyumba yangu ile!

Pia nenda Immigration ukaone kama mke wangu na watoto waliondoka hapa isivyo halali....

Hapo kweli tungemuelewa!

Asante
 
Waheshimiwa wabunge swali la nyongeza:

Yeye anasema aliitiwa hiyo kazi, sawa kabisa anaweza kutuelezea hiyo pesa ya kujenga nyumba tena kwenye eneo alilolisema alipata wapi? Je, hiyo pesa ilipatikana ki-halali? Kama ilipatikana kihalali alilipia kodi kiasi gani? Na kwa mtu ambaye alikuwa anasoma aliwezaje kuwa na pesa ya kujenga nyumba haraka hivyo? Kweli kukodi nyumba USA inaweza kuwa gharama ndogo anaweza kutuelezea ni kiasi gani analipia hiyo nyumba? (Isije ikawa inakuwa subsidized na serikali ya huko kwa njia za udanganyifu).
 
Mimi nawalaumu hawa Waandishi , kwa nini wakishapewa jibu wanashindwa kuuliza follow up questions! Kama alivyosema FD hapo juu basi ataje hiyo nyumba hiko mtaa gani na jiji gani , na jee ina worth kiasi gani mpaka watoto wanaofanya kazi za part time wanailipia ....

Jamani , i was a little bit skeptical after the story broke out lakini majibu yake yamenifanya niamini ya kuwa something is not right.
 
Bongo tukiwa na watu angalao 30% machachari kama Kitila Mkumbo hapo tutakuwa mbali sana. Kwanza haitaji kuficha jina lake halisi. Big up man!!
 
Bongo tukiwa na watu angalao 30% machachari kama Kitila Mkumbo hapo tutakuwa mbali sana. Kwanza haitaji kuficha jina lake halisi. Big up man!!

Hiyo 30% hutaipata hata usubiri miaka 100. Ukipata kama 10% jua
Tanzania tutapata nafuu.

Wabongo ninaowajua mimi kupata 10% ambao wako serious na wanachoongea na kuandika vinafanana na matendo yao, basi hata hiyo 10% itakuwa kazi kweli kweli kuipata.

Wako wengi wanaotumia majina yao, Mnyika, Zitto na viongozi wengine wa CHADEMA wanatumia majina yao.
 
Tuleteeni hizo siri wengine tuzimwage hapa. Kama nilivyoandika mwanzoni, sijali mleta siri ana motives zipi, ninachojali ni ukweli wa hizo siri. Kitu ambacho sitaki ni kuwachafua kwa makusaudi watu ambao wanachapa kazi, kama walivyomfanya yule jamaa wa wizara ya elimu.


Ndugu yangu Mtanzania;

Siri ni Siri. Matumizi yake na motives za kulifanya jambo liwe siri ni progative ya wale ambao wanahusika na hiyo siri. Kwa hivyo wewe bora uayapate yale maovu hujali kama anayaleta yeye ndiye mwovu zaidi na bora kayaleta sawa. Huo ni upeo wa fikra zako na mimi nakubali kutokubaliana nawe.

Kwa kusoma ujumbe wako naona uko tayari kulinda hata uovu kwa kisingizio cha siri ya serikali, kwa kufanya hivyo na wewe utakuwa fisadi. Tukikujua tutakuumbua tu bila kuogopa.

Sasa la kunieleza kuwa utaniumbua na mimi bila kuniogopa, nasema ruksa! Mimi sitetei wala kulinda uovu, ninachosema ni kuwa ukiapa kutunza siri it does not matter ni ya aina gani. Kama ni uovu na conscious yako inakuambia ni uovu kuna njia za kufuatwa na ikishindikana resign then utoe siri wakati hufungwi na kiapo chako. Sasa kama mie kusema hivyo natetea uovu basi niumbue ndugu yangu maanake naona ndiyo mambo ya JF.

Sasa mini nakupa data zaidi iwe rahisi kuniumbua kama ukikubali and if you don't mind, nitakutumia private message yenye simu yangu na email, anwani ya kazini, na hata mtaa ninaoshi na unauweza kuisambaza kwa vile ni siri .....

Wengine Meno yetu Sugu we have been chewing a lot for quite some times now.

Have a nice weekend!

MENOSUGU
 
MENOSUGU,

Huna haja ya kufika kote huko.................hapa JF mtu ukijaribu tu kumuumbua member mwenzio, sheria zetu hapa JF zinakuangukia.

Aliyeandika ile barua siye aliyeiweka hapa (asumptions) pengine hata yeye mwenyewe hajui kuwa imo humu (pamoja na kuwa ktk barua yake ametishia kuwa ataipeleka barua ktk vyombo vya habari ikiwemo mitandao kama hii).................inawezekana ujumbe wako kaupata au hajaupata bado

Jambo la msingi kwetu sisi hapa JF........tunapewa samaki mwenye miba tunaichambua miba na kula minofu miba huachwa/hutupwa pembeni.............kama samaki kaoza basi hutupwa (kifo asilia).

Ile barua toka mwanzo watu wameishtukia kuwa...................ina walakini, na inaonyesha wazi kuwa ina chuki binafsi................mbali ya kuwa viongozi wetu kuwa na udhaifu wa hapa na pale.

In my opinion ile barua does not make any sense
 
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la sunday citizen la jana waziri wa utawala bora alinukuliwa akisema kuwa serikali itachunguza madai yanayosambaa kwenye mtandao juu ya mkurugenzi mkuu wa PCB akituhumiwa kula rushwa kubwa kubwa.

Swali la kujiuliza je?atachunguzwa na nani?
Pili je?huu sio wakati muafaka akatoka kazini na kuanza kuchunguzwa sasa?
Inawezekana serikali ikachunguza kweli? kwani hapo patatokea mambo mengi na ya ziada juu ya ufisadi huu.

Tembelea www.citizen.co.tz kwa taarifa zaidi. nenda kwenye sunday citizen then itakuta.
 
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la sunday citizen la jana waziri wa utawala bora alinukuliwa akisema kuwa serikali itachunguza madai yanayosambaa kwenye mtandao juu ya mkurugenzi mkuu wa PCB akituhumiwa kula rushwa kubwa kubwa.

Swali la kujiuliza je?atachunguzwa na nani?
Pili je?huu sio wakati muafaka akatoka kazini na kuanza kuchunguzwa sasa?
Inawezekana serikali ikachunguza kweli? kwani hapo patatokea mambo mengi na ya ziada juu ya ufisadi huu.

Tembelea www.citizen.co.tz kwa taarifa zaidi. nenda kwenye sunday citizen then itakuta.

Mpakakieleweke,

Yaliyosemwa na waziri wa utawala bora ni mambo mazuri kama kweli yakitekelezwa. Lakini mi nafikiri tusijiweke tena katika situation ya kuamini yasemwayo na hawa jamaa, kwa sababu tuna mifano halisi mingi tu ambayo tumei-face katika siku chache zilizopita. Give them 2 weeks halafu uje kuona jinsi watakavyojichanganya baada ya Kingunge kuja kuzungumzia suala hili, then Makamba, then JK. Hawa jamaa bwana wana historia ya kutoa statements zinazopingana. Give them time before you hurt your emotions further.... Hawa jamaa wana history ya kutokua na collective statement.. Na hata wakija itoa hiyo collective judgement, on top of that, pia tatizo lao jingine la kihistoria nalo linakuja ----- kwamba they never implement what they say..
 
Ndio maana naona kuna haja ya kuibua huu mjadala ili kushinikiza jambo hilo na kama alilisema ili asiondolewe kwenye cabinet tuweze kujua kwani kwa sasa kila mmoja wao tension iko juu na yupo tayari kumtosa mwenzake ili mradi aweze kubakia kwenye serikali .

Je?wataweza? na je?kesho itakuwa ajabu ukiwasikia na wao wanasema kuwa wanaona haja ya kufungua kesi juu ya mafisadi?hapa kuna ajenda ya kutishana hapa.
 
Akikanusha madai ya kuwa na nyumba Marekani alidai."Sina nyumba marekani, nyumba hiyo nimepangisha. Baadhi ya watu wasichojua ni kwamba kupangisha nyumba marekani siyo ghali sana."

Hii nyumba ni lazima atakuwa kapangisha maeneo ya bei mbaya ambayo gharama ya kupangisha kutokana na ukubwa wa nyumba na thamani yake inaweza kabisa kuanzia $800 na kuendelea. Itakuwa vizuri akitwambia Watanzania analipia nyumba hiyo kiasi gani kwa mwezi.

Haya ndio maneno aliyoyasema.
"I and my family were living in the US. I was doing my doctorate studies before I was called back in the country to take this position. And renting a house in the US is not as expensive as some people might think," he said.
 
Nafikiri huwaga wanapita pita hapa kujisomea na wamepata nilichowambia kupitia ile topiki kuwa ,ni lazima wachunguzi wa rushwa na wao wachunguzwe bila ya kujijua hiki ni chombo kinachohitaji kuendeshwa kwa mafia style bila ya kuoneana haya.Maana kikiwa ni chombo kinacho chunguza watoa na wapokeaji basi hao wanaotoa wataanza kuwapa wao na wao ndio watakuwa wapokeaji wa mwanzo kabla dili halijatekelezwa,ni kuweka usalama wa dili kubwa kubwa,hivo ni lazima kwa hali yeyote ile kuwepo na usiri wa kuchunguzana Polisi iwe wao kupata ruhusa ya ukamataji kutoka sehemu tata kuwakamata wahusika au wafanyakazi wa kitengo hiki.Yaani hapa ni lazima mbinu zizidiane la si hivyo itakuwa kujaza maji kwenye pakacha.
 
Mpakakieleweke,

Yaliyosemwa na waziri wa utawala bora ni mambo mazuri kama kweli yakitekelezwa. Lakini mi nafikiri tusijiweke tena katika situation ya kuamini yasemwayo na hawa jamaa, kwa sababu tuna mifano halisi mingi tu ambayo tumei-face katika siku chache zilizopita. Give them 2 weeks halafu uje kuona jinsi watakavyojichanganya baada ya Kingunge kuja kuzungumzia suala hili, then Makamba, then JK. Hawa jamaa bwana wana historia ya kutoa statements zinazopingana. Give them time before you hurt your emotions further.... Hawa jamaa wana history ya kutokua na collective statement.. Na hata wakija itoa hiyo collective judgement, on top of that, pia tatizo lao jingine la kihistoria nalo linakuja ----- kwamba they never implement what they say..

Inabidi nikupongeze ndugu yangu kwa vile huyu waziri inaoneka alinogewa na kubwatuka hovyo. Hawa jamaa wakipigiwa simu na waandishi wa habari tena hasa yanoyomilikiwa na wageni basi utawasikia wanaji-contradict. Huyu ndugu mheshimiwa PCCB iko chini yake moja kwa moja halafu anasema hayo nani atamwamini?

Jambo lingine ambalo ningependa mnisaidie kulitafakari ni kuhusu haya magazeti ya - Mwananchi, Citizen, Daily Nation, East African, The Monitor n.k. Haya magezeti yako mbele sana katika kufuatilia mambo ya rushwa na has hapa Tanzania. Kama sijakosea gazeti la Nation lilikuwa mstari wa mbele kulivalia njuga issue ya KACC na kulisambaratisha hadi sasa KACC ni sanamu tu.

Mimi kama mzalendo mzawa hawa jamaa sasa hivi nimewashtukia vibaya sana. Mbona mambo ya Kenya hawayazungumzii ?? Kwa mfano napenda kunukuu haya ambayo yanatokea Kenya kuhusu rushwa lakini hutayaona kwenye magazeti hayo, ya humu nchinai wala Kenya kwenyewe:

Kenya: Corruption Perceptions Index 2007 may stop Kibaki’s re-election
2007-10-18

Less than 100 days to the Presidential election Transparency International’s flagship Corruption Perceptions Index (CPI) for 2007 has been published. Kenya’s score of 2.1 out of 10 (rank 150 out of 180) would be classified by Transparency International as indicating rampant corruption within the Government of Kenya. Not for the first time Kenya is the lowest ranked East African Community country, but what will shock some is that Kenya is for the first time lower ranked than Nigeria and apparently as badly regarded as Zimbabwe.

http://www.marsgroupkenya.org/users/?p=70

Yaani Kenya zaidi ya Nigeria .. Mbona Mhariri wa Citizen hutuambi wasomaji hayo? Kulikoni??


Kenya: Parliament forgives looters of billions prior to 2003
2007-09-13

The final gambit has commenced. The Parliament of Kenya has given corruption perpetrators an amnesty for corruption committed prior to May 2003. In the Statute Law (Miscellaneous Amendments) Bill 2007, approved by Parliament on Thursday 6th September 2007 and moved by the Attorney-General and the Minister for Justice and Constitutional Affairs, was an amnesty provision that hitherto had attracted almost no public comment.

http://www.marsgroupkenya.org/users/?p=69

Hii tamuu -- Bunge linasehe walaji kilaiiiiini ....

Kenya: Report reveals scale of corruption
2007-09-06

The scale of corruption carried out in Kenya by family and associates of its former president, Daniel Arap Moi, has been revealed in a secret report which alleges that more than £1 billion of government money was stolen during his 24-year rule. Mr Moi’s regime, which came to an end in 2002, has long been regarded as one of Africa’s most corrupt, but the extent of the graft has never been exposed in so much detail.

http://news.independent.co.uk/world/africa/article2917392.ece

Kenya: Grand Corruption: Kibaki must account - Civil Society
2007-07-27

Mwai Kibaki has once again demonstrated his complete lack of commitment to fight corruption and, even more, that he is a beneficiary of it. The Anglo Leasing and the corruption scandals of Moi, and Kenyatta before him, will remain unresolved so long as Mwai Kibaki is the President. His continued dalliance with Daniel arap Moi is proof enough of his going back on his word to Kenyans that ‘Corruption will cease to be a way of life in Kenya’.

http://www.marsgroupkenya.org/users/?p=55

The looting of Kenya under President Moi
The missing Kenyan billions. A suppressed report into Presidential corruption
2007-08-31

The intricately detailed report, commissioned by President Kibaki after his 2002 election victory but later suppressed, forensically investigates corrupt transactions and holdings by several powerful members of the Kenyan elite. The figures in the report sum to billions of US Dollars - comparable in magnitude to the looting of infamous kleptocrats such as Mobutu (Zaire), Marcos (Philippines), Abacha (Nigeria), Suharto (Indonesia) and Fujimori (Peru). The leaked material is extremely politically sensitive. Ex-President Moi has become a key player in political life in Kenya, and is now an essential pillar in President Kibaki's campaign for re-election in December 2007.

https://secure.wikileaks.org/wiki/KTM_report.pdf

Pamoja na kuchukia rushwa na kukubali kupambana nayo katika facets zake zote lakini naamini na siku itafika wengi mtaona hili ambalo mimi likekuwa linanikera sana. Nyie fanyeni critical analysis ya articles zinazo andikwa na hayo magazeti hasa kuhusu mambo ya Tanzania hasa kuhusu rushwa. Tusije tukawa tunapumbazwa na kele za mwizi mwizi kumbe mpiga kelele ndiye anataka uanza kumfukuza mwizi feki yaya akuibie kilaini... Jama mie nimeshashituka !!! Hawa jamaa waliimaliza KACC hivi hivi na kuwachambua na kupata watendaji wakuu na matokeo yake ndiyo hayo mengine nimeyanukuu, na ukitaka zaidi nenda hapa:
http://www.pambazuka.org/en/category/corruption/

Hivi wewe fikiria kwa makini.. udini wa mtu unahusika vipi na rushwa.. na editor wa gazeti analibandika frontpage. Jana headlines zilikuwa za simu aliyopigiwa Marmo na chini yake picha tofauti. Isije ikawa hawa jamaa wamo kwenye payroll za watuhumiwa.

Hivi neno ufisadi ni gazeti lipi lilianza kulitumia hapa Tanzania??

ZALENDOHALISI ...
 
Hosea angekuwa kweli ni mkristo tena msabato wa kweli bora angeamua kukaa pembeni ili aruhusu uchunguzi ,ila kama atakuwa msafi.

Kwa nini asikubali kuchunguzwa na hizo tuhuma na hili litamjengea heshima kubwa na pia litakuwa somo kwa viongozi wengine na watumishi wengine wa serikali, kuna haja ya mmoja kuonyesha njia ili wengine wafuate ila kila siku wakiwa wanakaa kimya na kugoma kungatuka nchi hii kamwe hatutaweza kuijenga hata kidogo.
 
Back
Top Bottom