PCCB: Tuna manufaa nayo?

PCCB: Tuna manufaa nayo?

Kweli kabisa wangeweza kuwaanika na kusema wazi....kama...
PRELIMINARY INVESTIGATION REPORT

FILE: PCCB/KIL/ENQ/08/2008

SUSPECTS

1) NAME : E.N.LOWASSA[D1]

TITLE : MP MONDULI
,

ADRESS : PRIVATE BAG ,MONDULI

2) NAME : DR I.MSABAHA(BANGUSILO)[D2]

TITLE : MP.....


ADRESS : BOX ...KIBAHA

3) NAME : ROSTAM AZIZ
TITLE : MP,IGUNGA

ADRESS : BOX ...IGUNGA

hapo tungewaelewa kabisa na kusema sasa mambo yameiva..maana hata hao EPA wanazunguka tuu vikao visivyoisha utekelezaji hakuna.....wanashauri wakato wao ni watendaji na wamesapewa amri ya kutekeleza....siasa kila kitu...ndio tatizo jeshi,police wote wanapitia mafunzo ya siasa bado hazijawatoka............

TWasubiriaa Hosea atoke Dec ndio tutaanza kumnyoshea kidole na kusema maozo yake wakati huo nae atakuwa ameshafunga mdomo wake hataongea..i like defensive mechanism ya wanasiasa wa TZ,hakuna kulala......
 
nchi ishageuzwa meli ya muhogo. viongozi wamekuwa walafi, wanashindana kuimegua meli wala hawahofii ikizama hatima itakua nini japo they themselves arent equipped with life jackets.
i think we must turn east ( china,singapore etc )for panacea;kuwa mafisadi waadhibiwe na special tribanals,when found guilty wazawadiwe summary executions by any means be it firing squads,gallowing etc
 
nimesoma gazeti leo kuwa takukuru wameanza kumchunguza ceo wa tanroads, ephraim mrema kwa tuhuma kuwa alipata kazi kwa mlango wa nyuma na kama analipa kodi ya mapato yake inavyopaswa.

Mnaona double standards za serikali yetu na hasa vyombo vya dola na sheria?

Mrema katuhumiwa kuwa haieleweki alivyopata kazi na mshahara wake ni mkubwa, takukuru inaanza kumchunguza bila kimemo.

Lakini kwenye suala la richmond ambalo lowassa na msabaha walihusika na kutuhumiwa pamoja na wengine, takukuru ilisema mapema hakuna kosa na hata baada ya kamati ya bunge ya mwakyembe kubainisha kuwa mchakato mzima wa richmond ulikuwa na walakini mkubwa na kuegemea kuwa na vitendo vya uhalifu na rushwa, takukuru wamekaa kimya.

Njoo suala la karamagi na mkataba wa buzwagi. Mazingira yanaonyesha ama kuna hujuma au rushwa, lakini karamagi anapeta na takukuru wamekaa mguu pande.

Ingiza rada, chenge katuhumiwa, serikali na takukuru wanasema hawafanyi uchunguzi wa ndani, hawana sababu kwa kuwa serikali ya uingereza inaichunguza bae. Sasa kama afisa mwandamizi wa serikali yetu inasadikiwa alipokea rushwa ili nchi iingie mkataba mkenge, kwa nini serikali yetu isimchukulie huyu mtuhumiwa na badala yake kudai fidia kwa muuzaji na si afisa mwandamizi aliyefanya uzembu au uhujumu?

Epa, meremeta, tangold, cis. Sijasikia takukuru kuanza uchunguzi mara moja kwenye hili mpaka slaa alipopiga kelele ingawa tulishaanza kupiga kelele mwaka mmoja kabla ya siri kufichuka. Ni vipi takukuru ilipuuzia suala zima na kujifanya haina uwezo mpaka kulazimishwa na bunge huku uhujumu wa hali ya juu unaendelea bot kwa kisingizio cha usalama wa taifa?

Atcl! Tumeingia mkataba bomu, maafisa wa atcl wamejinunulia magarina kuingia mkataba mmbovu ambao unaigharmu serikali na taifa mamilioni ya fedha. Lakini si takukuru au polisi waliokwenda kwa haraka kuwachunguza kina mattaka kuhusiana na hili.

Ripoti ya cag. Utouh katoa ripoti mwaka jana inayoonyesha uzembe uliokithiri ambao una harufu ya ubadhirifu wa karibu shilingi trilioni 3! Lakini sijasikia takukuru wakichunguza hasa lile suala la mikataba na manunuzi yanayofanyika bila kufuata taratibu.

Cha maana takukuru walichofanya ni kukamata watu kwa tuhuma za rushwa ndogo ndogo na za uzandiki kama suala la kina mollel na laizer wa arusha na kugombea nafasi nec ccm na sasa hili la mrema wa tanroads.

Je kuna faida gani kuendelea kuwa na imani na serikali na vyombo vya dola na sheria ikiwa vinafanya mambo kwa upendeleo?

.......safari ya mrema kwenda kisutu nani anaikawiza?....
 
Imenishangaza kusikia kwamba sasa Rostam badala aende mahakamani alikoshauriwa kwenda kwa lengo la kujisafisha mbele ya jamii ya watanzaia, amekimbilia TAKUKURU.

Lakini ni vema tuangalie kwa nini anakimbilia huko. Je kuna nini huko?

Huko TAKUKURU ndo kule shauri la Richmond lilipopelekwa lilisafishwa kabisa.
Ndo huko huko ambako mkurugenzi wake hashikiki ingawaje amekwishashutumiwa kwa mambo kadhaa.
TAKUKURU ilikuwepo Dr. Slaa alipotaja majina ya mafisadi lakini ilikaa kimya hadi moto ulipozidi ndo wale walaji wa EPA walipopekwa Kisutu.
TAKUKURU isiyo na meno, ambayo RA anaijua vizuri kwamba haina mpango wa kuwabana makada wa CCM na hasa maswahiba wa rais ndo sasa RA anapeleka malalamiko na uthibitisho kwamba Mengi ni mkwepa kodi na madeni ya mabenki.

RA anajua wazi kuwa kufanya hivyo TAKUKURU haitahangaika na ukweli ulioko katika madai kwamba yeye ni fisadi papa na ya kwamba amewahujumu watanzania yeye binafsi.

RA anajua wazi kuwa anaiweka TAKUKURU busy kushughulika na eti madai dhidi ya Mengi na lazima ofisi hiyo yetu tunayoigharamikia kwa kodi nyingi itajifanya blind dhidi ya uozo wa RA na kupoteza muda mwingi kumchunguza Mengi halafu wanaamini kuwa temperature ya madai dhidi ya mafisadi papa itapoa tu yenyewe.

Ninasubiri kuona TAKUKURU itampa tafu gani RA.
 
Imenishangaza kusikia kwamba sasa Rostam badala aende mahakamani alikoshauriwa kwenda kwa lengo la kujisafisha mbele ya jamii ya watanzaia, amekimbilia TAKUKURU.

Watanzania bana mnanichosha sana sijui uvivu wa kufikiri na kung'amua mambo? Huyu papa katumia haki ya msingi na ya kikatiba amepeleka vielelezo vyake vya kumtuhumu Mengi sasa na Mengi nae ana haki ya kutumia haki ya msingi kupeleka ushahidi wake kama anao wa kumtuhumu RA apeleke mahala husika kama alivyo fanya huyu papa.
Mkuu wewe ulitaka apeleke wapi?
 
Huku jamvini hatujuani kwa sura.
Tutajuana tu kwa hoja zetu!!!!!

FI mimi nimeeleza jinsi niijuavyo TAKUKURU na nikaweka hisia zangu kuwa kwa namna ilivyo hiyo TAKUKURU ndo sababu RA kapeleka hoja huko ikapoozwe.

Sasa wewe unaonyesha wazi kuwa hutaki RA ashutumiwe. Basi tukutake radhi!
 
Watanzania bana mnanichosha sana sijui uvivu wa kufikiri na kung'amua mambo? Huyu papa katumia haki ya msingi na ya kikatiba amepeleka vielelezo vyake vya kumtuhumu Mengi sasa na Mengi nae ana haki ya kutumia haki ya msingi kupeleka ushahidi wake kama anao wa kumtuhumu RA apeleke mahala husika kama alivyo fanya huyu papa.
Mkuu wewe ulitaka apeleke wapi?


Our lives begin to end the day we become silent about things that matter.
Martin Luther King Jr.
 
Sasa wewe unaonyesha wazi kuwa hutaki RA ashutumiwe. Basi tukutake radhi!

Mkuu navyo elewa mimi RA ni mwizi,tapeli,n.k na huyu Mengi navyo mwolewa ni mwizi,tapeli,muhujumu n.k hawa watu wamekutana kwa hiyo wanapo gombana wao ndipo siri nyingi tunazijua. Jamaa kapeleka ushahidi wake wa tuhuma dhidi ya Mengi na Mengi naye apeleke mahala husika nae.
 
Watanzania bana mnanichosha sana sijui uvivu wa kufikiri na kung'amua mambo? Huyu papa katumia haki ya msingi na ya kikatiba amepeleka vielelezo vyake vya kumtuhumu Mengi sasa na Mengi nae ana haki ya kutumia haki ya msingi kupeleka ushahidi wake kama anao wa kumtuhumu RA apeleke mahala husika kama alivyo fanya huyu papa.
Mkuu wewe ulitaka apeleke wapi?


You seem to be out of Tanzania tunayoijua Pamoja na TAKUKURU ambayo tukiweka post zako hapa ulizowahi kuilalamikia TAKUKURU na HOSEA utatia aibu !!! na Ndicho kinachowafanya Watanzania wasiopenda UFISADI wahoji kwa nini RA apeleke huko na kwa nini asiende mahakamani kumshitaki Mengi !!! ???? Ili Mengi aje na ushaidi huko mahakamani!!! mahakamani ni openly na wananchi wanaruhusiwa kusikiliza lakini huko alikopeleka wanafanya ni siri na mwisho wa siku wanaibuka na report za kuwashafisha Mafisadi kama walivyofanya kwenye Richmond na sehemu nyingi tu. Hapo ndipo hoja ilipo, elewa kuwa hakuna anayepinga Mengi asipeleke ushaidi, kinachopingwa ni wapi pa kupeleka .
 
Watanzania bana mnanichosha sana sijui uvivu wa kufikiri na kung'amua mambo? Huyu papa katumia haki ya msingi na ya kikatiba amepeleka vielelezo vyake vya kumtuhumu Mengi sasa na Mengi nae ana haki ya kutumia haki ya msingi kupeleka ushahidi wake kama anao wa kumtuhumu RA apeleke mahala husika kama alivyo fanya huyu papa. Mkuu wewe ulitaka apeleke wapi?"

___________________________________________



Fidel80:

Takukuru sasa imekuwa mahakama? -- yaani huyu kapeleka tuhuma za "mtuhumiwa wake" na "mtuhumiwa" maye inabidi apeleke majibu? Tuhuma za Mengi dhidi ya RA na wenzake tayari wanazo Takukuru, tangu siku nyingi. Kwa mfano ile ya Richmond walijaribu hata kuifunika lakini Bunge likaja kuwaumbua akina Hosea.

Takukuru siyo mahakama na ilikuywa hakuna haja kwa RA kufanya event kubwa ukabidhi wake makabrasha ya tuhumna kwa TAKUKURU – anataka ionekane vipi?
 
Imenishangaza kusikia kwamba sasa Rostam badala aende mahakamani alikoshauriwa kwenda kwa lengo la kujisafisha mbele ya jamii ya watanzaia, amekimbilia TAKUKURU.

Lakini ni vema tuangalie kwa nini anakimbilia huko. Je kuna nini huko?

Huko TAKUKURU ndo kule shauri la Richmond lilipopelekwa lilisafishwa kabisa.
Ndo huko huko ambako mkurugenzi wake hashikiki ingawaje amekwishashutumiwa kwa mambo kadhaa.
TAKUKURU ilikuwepo Dr. Slaa alipotaja majina ya mafisadi lakini ilikaa kimya hadi moto ulipozidi ndo wale walaji wa EPA walipopekwa Kisutu.
TAKUKURU isiyo na meno, ambayo RA anaijua vizuri kwamba haina mpango wa kuwabana makada wa CCM na hasa maswahiba wa rais ndo sasa RA anapeleka malalamiko na uthibitisho kwamba Mengi ni mkwepa kodi na madeni ya mabenki.

RA anajua wazi kuwa kufanya hivyo TAKUKURU haitahangaika na ukweli ulioko katika madai kwamba yeye ni fisadi papa na ya kwamba amewahujumu watanzania yeye binafsi.

RA anajua wazi kuwa anaiweka TAKUKURU busy kushughulika na eti madai dhidi ya Mengi na lazima ofisi hiyo yetu tunayoigharamikia kwa kodi nyingi itajifanya blind dhidi ya uozo wa RA na kupoteza muda mwingi kumchunguza Mengi halafu wanaamini kuwa temperature ya madai dhidi ya mafisadi papa itapoa tu yenyewe.

Ninasubiri kuona TAKUKURU itampa tafu gani RA.

Mkuu,

Sasa umeanza kuiita TAKUKURU kimbilio la mafisadi kwa facts zipi?

badala ya kuwashauri watanzania wenye ushahidi kuwasiliana na polisi au TAKUKURU wewe unaanza kutumia jambo la RA kwenda TAKUKURU kuifanya taasisi yote ionekane ya kifisadi?

Inaelekea hapa JF tumechanganyikiwa hata hatujui nini tunataka, hatuna msimamo mmoja unaoeleweka, tunayumba, tunatapatapa kwa kuangalia mhusika ni nani.

RA katumia haki yake kama Mtanzania mwingine, muhimu ni kuwashauri wengine wenye habari kuhusu uhalifu kuweza kuzifikisha kwenye vyombo vyetu vya usalama.

Huwezi kumlazimisha mtu aende sehemu unayotaka wewe, mtu anaweza kwenda polisi, anaweza kwenda vyombo vya habari ili viandike, anaweza kwenda mahakamani, anaweza kwenda TAKUKURU.

Kitu ambacho hutakiwi kufanya ni kuilamu taasisi yote kama TAKUKURU kwamba ni kimbilio la mafisadi. Je wale walioko mahakani baada ya kupelekwa na TAKUKURU sio mafisadi?

Ndio TAKUKURU wana matatizo na wanatakiwa kuongeza ufanisi na kupunguza kuwa tegemezi sana kwa serikali, lakini hiyo sio sababu ya kuwaita TAKUKURU kimbilio la mafisadi.

Sio kila case unaweza kupeleka mahakamani. RA anaweza kwenda mahakamani kumshitaki Mengi kwa kumkashifu lakini hawezi kwenda mahakani kumshitaki Mengi kwa kuiibia NICO au mabank. Hiyo ni kazi ya serikali kama sikosei.

Hawa jamaa watoe ushahidi walio nao ili tuwajue vizuri hawa papa na Nyangumi bila kujali ni Mengi au RA.

Tatizo la watu wengi hapa ni double standards, kama Mengi amekosea sio fisadi, kama RA ni fisadi. Hawa wote mapapa na Nyangumi ni mzigo kwa Tanzania. List haiishii hapo, wako wengi mno. Wakiumbuana ndio faida kwa sisi wananchi.
 
Wanamkimbilia mwokozi wao Hosea na ndio maana wanamlinda kwa gharama yoyote asiondolewe TAKUKURU.
 
Watanzania bana mnanichosha sana sijui uvivu wa kufikiri na kung'amua mambo? Huyu papa katumia haki ya msingi na ya kikatiba amepeleka vielelezo vyake vya kumtuhumu Mengi sasa na Mengi nae ana haki ya kutumia haki ya msingi kupeleka ushahidi wake kama anao wa kumtuhumu RA apeleke mahala husika kama alivyo fanya huyu papa.
Mkuu wewe ulitaka apeleke wapi?

Mahakamani mzee, mahakamani,wengi tulitegemea RA angeelekea huko ili kukata mzizi wa fitna.Kupeleka TAKUKURU ni kuendeleza malumbano tu. Na huko TAKUKURU ndiko walilko kina Sfia Simba , what do you expect.Na TAKUKURU so far hawana track record nzuri, Richmond iliwamaliza the little reputation they had.
Mahakamani, kama zilivyo kesi za Zombe,na Balozi yule wa Italy inafunua mabo mengi hadharani ili wananchi wajionee uozo na kuurekebisha
 
Mkuu,

Sasa umeanza kuiita TAKUKURU kimbilio la mafisadi kwa facts zipi?

badala ya kuwashauri watanzania wenye ushahidi kuwasiliana na polisi au TAKUKURU wewe unaanza kutumia jambo la RA kwenda TAKUKURU kuifanya taasisi yote ionekane ya kifisadi?

Inaelekea hapa JF tumechanganyikiwa hata hatujui nini tunataka, hatuna msimamo mmoja unaoeleweka, tunayumba, tunatapatapa kwa kuangalia mhusika ni nani.

RA katumia haki yake kama Mtanzania mwingine, muhimu ni kuwashauri wengine wenye habari kuhusu uhalifu kuweza kuzifikisha kwenye vyombo vyetu vya usalama.

Huwezi kumlazimisha mtu aende sehemu unayotaka wewe, mtu anaweza kwenda polisi, anaweza kwenda vyombo vya habari ili viandike, anaweza kwenda mahakamani, anaweza kwenda TAKUKURU.

Kitu ambacho hutakiwi kufanya ni kuilamu taasisi yote kama TAKUKURU kwamba ni kimbilio la mafisadi. Je wale walioko mahakani baada ya kupelekwa na TAKUKURU sio mafisadi?

Ndio TAKUKURU wana matatizo na wanatakiwa kuongeza ufanisi na kupunguza kuwa tegemezi sana kwa serikali, lakini hiyo sio sababu ya kuwaita TAKUKURU kimbilio la mafisadi.

Sio kila case unaweza kupeleka mahakamani. RA anaweza kwenda mahakamani kumshitaki Mengi kwa kumkashifu lakini hawezi kwenda mahakani kumshitaki Mengi kwa kuiibia NICO au mabank. Hiyo ni kazi ya serikali kama sikosei.

Hawa jamaa watoe ushahidi walio nao ili tuwajue vizuri hawa papa na Nyangumi bila kujali ni Mengi au RA.

Tatizo la watu wengi hapa ni double standards, kama Mengi amekosea sio fisadi, kama RA ni fisadi. Hawa wote mapapa na Nyangumi ni mzigo kwa Tanzania. List haiishii hapo, wako wengi mno. Wakiumbuana ndio faida kwa sisi wananchi.

Mkuu umesahau tamko la Hosea lililo jaa mbwembwe kwamba RICHMONDI safiiiiiiiiii... ???

Hivi imani itoke wapi?na fact zipi unazitaka zaidi ya uumbukaji wa taasisi ile? baada ya kamati ya bunge kuanika kila kitu?

Kwa taarifa yako, toka wakati ule ile TAKUKURU ilipoteza kabisa credibility machoni petu wananchi, na Kibaya zaidi huyo bosi wao Hosea ndo kabisaaaaa anazidi kuifanya ionekane haifai kabisa,kwanza ni mtuhumia mkubwa, pili utendaji wake unaonekana wazi ni kwa ajili ya kulinda maslahi ya mafisadi period!

lakini pia haijakushanganza, Fisadi papa Rostamu Azizi kwenda Takukuru kupinga tuhuma dhidi yake? yaani huko kweli ndiko alipaswa kwenda tena kwa mbwembwe na picha mnato na muondosheo juu? kama siyo, hivi mtu waweza jisafisha tuhuma kwa kumtuhumu mtu mwingine?
 
Takukuru ni taasisi ya kuzuia Rushwa sio ufisadi, Rostam ni muongo period kukimbilia huko kwa Hosea, kwanza ni aibuu!

FMES!
 
TAKUKURU kimbilio la mafisadi kwa facts zipi?
. Una hisa New Habari Cooperation? Mbona unaelezwa lakini huelewi? Usiwe kama Jackton Manyerere, unaambiwa Takukuru ndiyo iliyosafisha mafisadi wa Richmond na kwamba bila ya jitihada za Kamati ya Bunge ufisadi huu ungepeta, iweje leo Takukuru hiyohiyo iwachunguze tena wahusika walewale iliyokwishawasafisha?
 
. Una hisa New Habari Cooperation? Mbona unaelezwa lakini huelewi? Usiwe kama Jackton Manyerere, unaambiwa Takukuru ndiyo iliyosafisha mafisadi wa Richmond na kwamba bila ya jitihada za Kamati ya Bunge ufisadi huu ungepeta, iweje leo Takukuru hiyohiyo iwachunguze tena wahusika walewale iliyokwishawasafisha?



Offish umemuuliza swali la msingi. Au hafatilii mambo ya siasa za nchini kukumbika uozo wa pcb? Na huyo Manyerere muulizeni kasoma wapi uandishi wa habari? Ni aibu TSJ haijui halafu eo anajifanya mwandishi makini
 
PCCB wapo kwa ajili ya kukamata mahakimu wa mahakama wa mwanzo, trafiki, walimu na watendaji wadogo wa serikali kama wenyeviti wa serikali za mitaa na watendaji wao ambao wanachukua rushwa za sh 2,000/= n.k.
Haina nguvu wala meno ya kushughulika na mapapa na manyangumi wa UFISADI..
 
Na pia tukumbuke RA alimpa masaa 48 aombe radhi la sivyo atamchukulia hatua. Nilitegemea angeenda mahakamani kumshitaki RM kamchafulai jina na amtake mengi alete uthibitisho wa aliyosema. Badala yake kaenda kusema ufisadi wa Mengi. Mengi yeye alikanusha aliyotuhumiwa na akiitwa PCB atapeleka defence yake ila rostam hakukanusha kwa vithibitisho.Hivyo maana yake kwa wenye akili madai ya Mengi kwa rostam kwamba ni fisadi papa yamesimama pale pale
 
Back
Top Bottom