Tanzania is delicious kwa wenye meno
Ukisoma katiba kwa makini utakuja kugundua kuwa Tanzania serikali inapaswa kupelekwa The Hague kwa mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu.
Mengi wanayofanya ni kinyume na sheria na katiba.... pia wanatoa majibu mepesi kwa maswali magumu...
Ila pastor kishoka usihofu kwa kuwa sisi twaendelea kukua na yale meno yetu yatakua na kuanza kuwang'ata.
Hivi hosea hajajiuzulu??
Ajiuzulu achekwe? aachie hizo pesa zote za Vikamati?
Hivi hujasikia tetesi kuwa kamati ya EPA inaweza ongezewa muda na kila mjume wa Kamati nasikia anakamata laki moja ya Tanzania kwa siku tangu kamati iundwe!
Unalipwa mshahara, halafu unapopewa kazi maalum bado unapewa posho kutimiza wajibu wako ambao unalipwa kwa kupitia mshahara?
Hii sijawahi isikia popote ila Tanzania!
...halafu goddam ripoti inafungiwa kabatini....
Pinda ashasema kuwa waliokwiba EPA ni wazito mno, je alimaanisha TISS au ndo mambo ya vitisho from takukuru??? nasikia hosea anajua sana kucheza karata zake.
Hivi yule waziri mkuu wa israel somebody Rabin alifanywa nini na yule kijana ambaye alikuja kufungwa miaka miwili?.....
Mchungaji..naomba nitume sehemu ya hoja yako katika makala yangu ya Jumatano... umenipa nyongeza nzuri sana... kama ni msosi wa pilau.. umenipa kachumbari, ingekuwa ngoma umenipa manyanga, na ingekuwa ni wimbo basi wako ni "lele mama"... thanks.. kuna kitu tutakionesha kuhusu TAkukuru na kutoa pendekezo ambalo hadi hivi sasa halijatolewa Tanzania kuhusu hii Taasisi.
Daring to go where no one dared to before..!
good work sir!
Sikuandika kwa kusema ni Sheria, nimeandika kwa kuangalia utendaji wao.
Najiuliza wao TAKUKURu kuwa pro-active kumchunguza Mrema wa TANROADS siku tatu baada ya hoja kuletwa Bungeni, lakini hoja nyingine ambazo zina miaka nenda rudi na hata ushahidi wa kimazingira kuwa kuna Rushwa ya hali ya juu, hujasikia TAKUKURU wakijituma kuchunguza!
Sheria ya TAKUKURU ina walakini, hata hivyo, utendaji kazi wao pia una walakini na unaonyesha wazi kuwa TAKUKURU inachagua ni kipi ikichunguze na kipi kipuuzie.
Ndio maana nimehitimisha kuwa kuna maana gani kuendelea kuwa na Imani na Serikali na vyombo vyake vya Dola na Sheria ambavyo vinafanya kazi kwa Upendeleo na Ubaguzi?
but mind you, what's up is upon all... unless others are inverted creatures...i.e. they stand upside down!!SteveD;
Kuchunguza sio vibaya...ni kwa ajili ya kujua whats up!
Hao maofisa wa PCCB wanaovujisha hizo habari naona wameishiwa ... ningewaona ni wa maana sana kama wangeleta report ambazo zinahusu rushwa ya mabilioni na siyo hizi kesi ambazo impact yake ni ndogo sana!