Pawepo na Kampuni ya Vijana Ujenzi Taifa: Vijana wataajiriwa zaidi ya 5,000,000 nchi zima

Pawepo na Kampuni ya Vijana Ujenzi Taifa: Vijana wataajiriwa zaidi ya 5,000,000 nchi zima

Masalu Jacob

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2017
Posts
1,339
Reaction score
1,493
Habari Tanzania !

Napenda kuleta wazo hasa kwa Serikali Tanzania na Vijana wa Tanzania endapo ikiwapendeza.

Tuanzishe taasisi ya Vijana Ujenzi Taifa; waajiriwe vijana wenye nia na kutumika kwenye sekta ya ujenzi Taifa.

Itungwe Sheria ya usimamizi miundombinu na ujenzi majengo Taifa. Pia pawepo na Sera ya Ujenzi Taifa kuhusu Shirika hili la Vijana.

Naomba mapendekezo yafuatayo yatumike kwenye hii taasisi;

1. Ujenzi wowote kuanzia wa miundombinu na ujenzi ngazi ya kijiji/ mtaa, Kata, Wilaya, Mkoa; itasimamiwa na hii taasisi kuanzia ngazi ya upimaji udongo, usanifu wa miundombinu na majengo; ujenzi wa jengo husika na utunzaji wa jengo aidha la mtu binafsi au taasisi hapa nchini.

2. Tenda zote za Taifa hasa miradi ya ujenzi yote hili shirikia lipewe kipaombele na ndio watakuwa wasanifuu wakuu wa miundombinu yote inayohusu ujenzi.

3. Kila mwananchi awe na "UJENZI CARD". Hii kadi itakuwa maalumu kwa kila mwenye uhitaji wa ujenzi. Hata taasisi Binafsi na Umma lazima wawe nayo hii kadi.
Atapaswa kuchangia kiasi kidogo kidogo kutokana na mahitaji yake ya ujenzi na atapewa huduma moja kwa moja juu ya uhitaji wake hata kama hajakamilisha ada yake ya hitaji. Uzuri atapewa ukadiliaji mzuri wa gharama za hitaji lake.
(Ujenzi - Card itaunganishwa moja kwa moja na mifumo mingine kama Banks, NIDA, TRA,POLISI, JWTZ nk).

Angalizo
1. Hii taasisi inauwezo wa kuajiri vijana 5,000,000 kwa mkupuo (moja kwa moja) nchi nzima.

2. Ujenzi ndio sekta pekee yenye utatuzi wa kiuchumi hasa mzunguko wa pesa na ajira kwa jamii.

3. Tutachochea uundwaji wa miundombinu bora na tutazuia ujenzi holela hapa nchini.

4. Serikali ikiwapendeza mnaweza sasa mkawatafutia michongo ya ujenzi nchi za ng'ambo huko vijana wakaleta fedha za kigeni hapa nvhini kukuza Taifa letu.

5. NHC (Shirika la Nyumba Taifa), Suma JKT na TBA (Wakala wa Ujenzi Tanzania) hizi taasisi zisihusike na hiyo taasisis ya Ujenzi Taifa yaani wao waendelee na majukumu yao hivyo hivyo wakae mbali.
 
Habari Tanzania !

Napenda kuleta wazo hasa kwa Serikali Tanzania na Vijana wa Tanzania endapo ikiwapendeza.

Tuanzishe taasisi ya Vijana Ujenzi Taifa; waajiriwe vijana wenye nia na kutumika kwenye sekta ya ujenzi Taifa.

Itungwe Sheria ya usimamizi miundombinu na ujenzi majengo Taifa. Pia pawepo na Sera ya Ujenzi Taifa kuhusu Shirika hili la Vijana.

Naomba mapendekezo yafuatayo yatumike kwenye hii taasisi;

1. Ujenzi wowote kuanzia wa miundombinu na ujenzi ngazi ya kijiji/ mtaa, Kata, Wilaya, Mkoa; itasimamiwa na hii taasisi kuanzia ngazi ya upimaji udongo, usanifu wa miundombinu na majengo; ujenzi wa jengo husika na utunzaji wa jengo aidha la mtu binafsi au taasisi hapa nchini.

2. Tenda zote za Taifa hasa miradi ya ujenzi yote hili shirikia lipewe kipaombele na ndio watakuwa wasanifuu wakuu wa miundombinu yote inayohusu ujenzi.

3. Kila mwananchi awe na "UJENZI CARD". Hii kadi itakuwa maalumu kwa kila mwenye uhitaji wa ujenzi. Hata taasisi Binafsi na Umma lazima wawe nayo hii kadi.
Atapaswa kuchangia kiasi kidogo kidogo kutokana na mahitaji yake ya ujenzi na atapewa huduma moja kwa moja juu ya uhitaji wake hata kama hajakamilisha ada yake ya hitaji. Uzuri atapewa ukadiliaji mzuri wa gharama za hitaji lake.
(Ujenzi - Card itaunganishwa moja kwa moja na mifumo mingine kama Banks, NIDA, TRA,POLISI, JWTZ nk).

Angalizo
1. Hii taasisi inauwezo wa kuajiri vijana 5,000,000 kwa mkupuo (moja kwa moja) nchi nzima.

2. Ujenzi ndio sekta pekee yenye utatuzi wa kiuchumi hasa mzunguko wa pesa na ajira kwa jamii.

3. Tutachochea uundwaji wa miundombinu bora na tutazuia ujenzi holela hapa nchini.

4. Serikali ikiwapendeza mnaweza sasa mkawatafutia michongo ya ujenzi nchi za ng'ambo huko vijana wakaleta fedha za kigeni hapa nvhini kukuza Taifa letu.

5. NHC (Shirika la Nyumba Taifa), Suma JKT na TBA (Wakala wa Ujenzi Tanzania) hizi taasisi zisihusike na hiyo taasisis ya Ujenzi Taifa yaani wao waendelee na majukumu yao hivyo hivyo wakae mbali.
Tekeleza hilo wazo kwenye familia yako
 
Hili linawezekana kama materials zote za ujenzi mnazalisha humu ndani. Lakini kama mnaagiza italeta mkazo kwenye forex, na ukizingatia mabeberu wameondoa shilingi.
 
Hili linawezekana kama materials zote za ujenzi mnazalisha humu ndani. Lakini kama mnaagiza italeta mkazo kwenye forex, na ukizingatia mabeberu wameondoa shilingi.
Tunaweza kiuhalisia kuzalisha hapa hapa nchini.
Hii ndio miongoni mwa minu ya kimkakati ambayo hata Marekani alipoyumba kiuchumi miaka ile ya 2009. Baraka Obama alikuja na project ya Ujenzi Taifa japo haikuwa kwa mtindo huu ila zinafanana atmosphere yake.
 
KWELI ELIMU MHIMU ILA HAMNA SEKTA KUBWA ITAAJIRI VIJANA KAMA KILIMO. UJENZI UNAMAANISHA KILA FAMILIA IWE NA FUNDI MAIKO 🤣
 
Tunaweza kiuhalisia kuzalisha hapa hapa nchini.
Hii ndio miongoni mwa minu ya kimkakati ambayo hata Marekani alipoyumba kiuchumi miaka ile ya 2009. Baraka Obama alikuja na project ya Ujenzi Taifa japo haikuwa kwa mtindo huu ila zinafanana atmosphere yake.
Ni kweli inachochea sana uchumi. Hata China wamefanya hivyo hadi wametengeneza bubble ya real estate. Cha muhimu tujitahidi tu kuzalisha hizo materials. Kama tunaagiza tutafeli.
 
Wengi. Kuna kampuni inaweza uajiri watu milioni tano ikawa na ufanisi? I think watu elf 50 inaweza kuwa manageable
Upo sahihi kwa mtazamo wa sekta binafsi.
Ila hii Taasisi lazima tuifanye kuwa PPP yaani Serikali wanatia hela vijana wanaruka nayo kazi. Pia lazima tuwaze kutawala soko la Ujenzi Afrika Mashariki na kati.

Hapa lazima uwe na manpower ya kutosha.
 
KWELI ELIMU MHIMU ILA HAMNA SEKTA KUBWA ITAAJIRI VIJANA KAMA KILIMO. UJENZI UNAMAANISHA KILA FAMILIA IWE NA FUNDI MAIKO 🤣
Kilimo kinaajiri wengi endapo umekubali kuishi nje na teknolojia rafiki.

Leo hii hiyo sekta inauwezo wa kuleta unafuu kwenye usawazishaji mfumuko wa bei; Kuleta unafuu wa kipato ila kuhusu ajira nyingi sahau rafiki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom