Burkinabe
JF-Expert Member
- Feb 12, 2023
- 1,899
- 3,201
Kwa mjibu wa katibu mwenezi wa CCM Taifa, ndugu Paul C. Makonda, Taifa letu lina viongozi wazalendo ambao wakipewa kazi wanafanya kazi kuhakikisha nchi inapiga hatua kimaendeleo.
Lakini kwa bahati mbaya pia kuna WAHUNI ambao wakipewa kazi, wanaliibia Taifa hili na kukalia kupiga majungu! Lakini mbaya zaidi ni kwamba hawa wahuni wanaonekana wako "smart" zaidi kulinganisha na wazalendo kwa sababu, wao mara nyingi wakiona maslahi yao yanaingiliwa basi hufanya kukaa kimya na kuanza kushughulika n wazalendo wanaoingilia maslahi yao na familia zao kichini-chini.
Hili lilishawekwa wazi na Katibu Mwenezi wa CCM Taifa, wa zamani, ndugu Humphrey Polepole ambaye alisema ndani ya Chama na serikali kuna WAHUNI ambao wakiona umenyooka, basi wanakutafutia zengwe, au wanakutafutia namna ya kukuroga, au kukua iwe kwa ajali, sumu n.k. Kwa sehemu nakubaliana naye kwa sababu wakati wa utawala wa JPM pia aliwahi kukiri kupewa sumu. Lakini pia wakati wa ziara yake kule kusini (?Lindi), Kuna kipindi alitumiwa moshi ambao hata haujulikani ulitokea wapi (kwa wabishi Ingia youtube utaona)!
Sasa huu ukimya wa hawa "panya road" waliovishwa makoti ya uongozi kwa sasa umerudi tena kama ilivyokuwa kabla ya Mzalendo (JPM) kulala. Haikosi kuna jambo baya watakuwa wanalipanga juu ya viongozi wazalendo na watetezi wa wanyonge wa Chama na Serikali akiwemo ndugu Paul Christian Makonda.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu wabariki viongozi wetu wazalendo lakini wale wezi wanaolitesa Taifa hili, uwalaani wao na vizazi vyao.
Amin.
Lakini kwa bahati mbaya pia kuna WAHUNI ambao wakipewa kazi, wanaliibia Taifa hili na kukalia kupiga majungu! Lakini mbaya zaidi ni kwamba hawa wahuni wanaonekana wako "smart" zaidi kulinganisha na wazalendo kwa sababu, wao mara nyingi wakiona maslahi yao yanaingiliwa basi hufanya kukaa kimya na kuanza kushughulika n wazalendo wanaoingilia maslahi yao na familia zao kichini-chini.
Hili lilishawekwa wazi na Katibu Mwenezi wa CCM Taifa, wa zamani, ndugu Humphrey Polepole ambaye alisema ndani ya Chama na serikali kuna WAHUNI ambao wakiona umenyooka, basi wanakutafutia zengwe, au wanakutafutia namna ya kukuroga, au kukua iwe kwa ajali, sumu n.k. Kwa sehemu nakubaliana naye kwa sababu wakati wa utawala wa JPM pia aliwahi kukiri kupewa sumu. Lakini pia wakati wa ziara yake kule kusini (?Lindi), Kuna kipindi alitumiwa moshi ambao hata haujulikani ulitokea wapi (kwa wabishi Ingia youtube utaona)!
Sasa huu ukimya wa hawa "panya road" waliovishwa makoti ya uongozi kwa sasa umerudi tena kama ilivyokuwa kabla ya Mzalendo (JPM) kulala. Haikosi kuna jambo baya watakuwa wanalipanga juu ya viongozi wazalendo na watetezi wa wanyonge wa Chama na Serikali akiwemo ndugu Paul Christian Makonda.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu wabariki viongozi wetu wazalendo lakini wale wezi wanaolitesa Taifa hili, uwalaani wao na vizazi vyao.
Amin.