Paul Makonda amefanikiwa kuiweka CCM katika mioyo na midomo ya Watanzania

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,262
9,714
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa hakika uteuzi uliofanywa na chama cha Mapinduzi chini ya uongozi shupavu, imara na madhubuti wa Rais na mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan , kumteua Mheshimiwa Paul Christian Makonda kuwa katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa CCM Taifa umekuwa ni uteuzi wa kihistoria na karata ya ushindi iliyochezwa na Rais Samia. imeonyesha uhodari wa Rais Samia kuusoma mchezo wa kisiasa na kujuwa nani aingie wakati gani kuipatia timu na chama ushindi na kuwapa matumaini watanzania kwa chama.

Kiukweli Mheshimiwa Paul Makonda amekirejesha na kukiamsha chama mitaani ,ameleta hamasa iliyokuwa imelala,imeinua matumaini ya watanzania kwa CCM,amefanya chama kuwa kimbilio la wanyonge,kwa kuwa Watanzania siku zote walikuwa wanahitaji kuona CCM yenye kuwajali,kuwasikiliza,kuwafuata waliko ili kujuwa maisha wanayoishi na changamoto zinazowakabili na wanazopitia na kuzipatia majibu stahiki.

Watanzania walihitaji sauti ya chama cha mapinduzi katika kuwasemea, kuwatetea,kuwa nyuma yao,kuwapigania dhidi ya dhuluma, unyonyaji, unyanyasaji,uporwaji wa haki,ukandamizwaji,uonevu pamoja na kuwafuta machozi,kuwapa matumaini,faraja na kuwashika mkono pale wanapokuwa wameishiwa nguvu.

Haya yote kwa sasa yanatekelezwa na CCM kwa mkono na kinywa cha Mheshimiwa Makonda ambaye amejitoa na kujitolea kukibeba chama mabegani mwake kukipeleka kwa wananchi ambao ndio wamekuwa dhamana kuu ya CCM kuwepo na kusalia madarakani kwa karibu nusu karne sasa. Mheshimiwa Makonda anazungumza lugha za watu,kero za watu,.anamsikiliza kila mtu kwa unyenyekevu.anakisemea chama na serikali kwa nguvu zake zote.ameiacha na kuwa mbali na familia yake ili kwenda kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zao.

Ameiacha familia yake mke na watoto wake kwa ziara ndefu ili kwenda kuwafuta machozi Watanzania walioelemewa na mizigo ya kero na tabu katika mioyo na vifua vyao.ndio maana kwa sasa mitaani habari iliyoteka na kutawala katika vinywa vya watu ni kuhusu Mheshimiwa Makonda ,CCM na Rais Samia. hiyo ndio habari kuu iliyoteka hisia za watu wote. Ndio habari inayofuatiliwa kwa karibu hata na wapinzani wa nchi hii kama CHADEMA.ndio maana unaona walivyo karibu katika kufuatilia kila kinachoendelea katika ziara zake.

Sasa kupitia maelekezo ya Mheshimiwa Makonda akitoa maelekezo ya chama kwenda kwa wakuu wote wa mikoa na wilaya nimeshuhudia wakuu wa mikoa wakitekeleza agizo la wao kwenda kwa wananchi kuwasikiliza kero zao na kuwapa majibu.hivi hapa nilipo ilikuwa ni jana ambapo viongozi wote wa mkoa walikuwepo mtaani kwangu kuja kusikiliza kero za wananchi na kutoa majibu,jambo ambalo liliwapa matumaini makubwa sana wananchi, ambao walihudhuria na kutoa kero zao.

Unaweza kuona namna Mheshimiwa Makonda alivyoleta mapinduzi mapya ya kiutendaji kwa viongozi.kwa sasa wananchi wanaona kuwa ukinyimwa au kudhulumiwa haki yako basi ni CCM Pekee unapoweza kupata ufumbuzi na tumaini la shida yako.kwa kuwa ni CCM Pekee inayoweza kutoa msukumo na kuweka nguvu ya wewe kupata haki yako.ndio maana tunaona na kushuhudia mikutano ya Mheshimiwa Makonda ikifurika na kumiminika watu kusikiliza na wengine wakipigana vikumbo kwa jasho na machozi kutafuta kupata nafasi ya kuwasilisha kero zao kwa Mheshimiwa Makonda.

Hii ndio maana ya kuwa chama cha siasa kinachotawala na kuongoza serikali kuhakikisha kuwa kinakuwa karibu ya watu na kuwa kimbilio namba moja la watu, ndio maana sasa watu wanaona ni bora uende kwa Mh Makonda utapata haki yako haraka kuliko kwenda huko kwingine ukaishia kuzungushwa tu kama mpira.

Rai yangu ni kwa wakuu wa mikoa,wilaya,wakurugenzi na viongozi mbalimbali huko mikoani kuendeleza utamaduni huu ambao Mheshimiwa Makonda ameupandikiza na kuja nao kwa kuhakikisha kuwa mnatoka maofisini katika baadhi ya siku na kwenda kwa wananchi kuwasikiliza wananchi.kwa kuwa ninyi ndio mpo na wananchi kila siku na mkilipwa mishahara kwa kazi hiyo ya kuhudumia watu.hakikisheni mnakuwa karibu ya mwananchi,hakikisheni mkiletewa jambo mhakikishe kuwa linapatiwa ufumbuzi na mwenye haki anapatiwa haki yake.

Maana katika ziara za Mheshimiwa Makonda nimesikia wengine wakisema kuwa jambo hili nimefikisha hadi kwa mkuu wa wilaya,mkoa n.k.hii maana yake ni kuwa wengine huwa hamfuatilii kuhakikisha kuwa maelekezo yenu na maagizo yanafanyiwa kazi na watu wanapata haki zao.ndio maana inapotokea ziara za viongozi wakuu wananchi wanajitokeza na mabango wakilia na kububujikwa machozi kwa kuwa ninyi mnakuwa mlishindwa kuwapatia majibu na kuwasaidia kupata haki zao.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
IMG-20240202-WA0004.jpg
 
Ni Kweli kabisa,

Mwenezi hivi sasa ni Maarufu kuliko Mwenyekiti wake SSH!!
Mwenyekiti wa CCM Ni maarufu kuliko mwingine yeyote yule kutokana na kugusa maisha ya watu na kuleta Tabasamu na furaha katika mioyo yao.ndio maana aliamua kuleta mtu ndani ya chama atakayeendana na kasi yake na mahitaji yake ya kuwahudumia watanzania kwa unyenyekevu na utayari wa hali ya juu.ndio maana akatuletea Watanzania Mheshimiwa Makonda mwenye moyo wa unyenyekevu,upendo na ukarimu wa hali ya juu sana.ndio maana tunaona namna alivyo kimbilio la wanyonge kwote apitako huko katika ziara yake ya mikoa ishirini bila kupumzika.
 
Umeme wa uhakika, maisha bora na uongozi imara ndiyo utaweka serikali mioyoni mwa watu, siyo upuuzi mwingine.
Umeme upo sema labda changamoto ndogondogo ambazo nazo zinakwenda kufika kikomo muda siyo mrefu.kwa sababu Vwawa la mwalimu Nyerere linakwenda kuwasha mtambo wa kwanza ambao utatupatia megawati 205 zitakazounganishwa katika grid ya Taifa
 
Mwenyekiti wa CCM Ni maarufu kuliko mwingine yeyote yule kutokana na kugusa maisha ya watu na kuleta Tabasamu na furaha katika mioyo yao.ndio maana aliamua kuleta mtu ndani ya chama atakayeendana na kasi yake na mahitaji yake ya kuwahudumia watanzania kwa unyenyekevu na utayari wa hali ya juu.ndio maana akatuletea Watanzania Mheshimiwa Makonda mwenye moyo wa unyenyekevu,upendo na ukarimu wa hali ya juu sana.ndio maana tunaona namna alivyo kimbilio la wanyonge kwote apitako huko katika ziara yake ya mikoa ishirini bila kupumzika.
Ni Kweli kabisa,

Mwenyekiti amemleta Mwenezi Ili awe maarufu kuliko CCCM yenyewe, pia amewekwa awe maarufu kuliko Mwenyekiti.

Muda utaongea.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa hakika uteuzi uliofanywa na chama cha Mapinduzi chini ya uongozi shupavu, imara na madhubuti wa Rais na mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan , kumteua Mheshimiwa Paul Christian Makonda kuwa katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa CCM Taifa umekuwa ni uteuzi wa kihistoria na karata ya ushindi iliyochezwa na Rais Samia. imeonyesha uhodari wa Rais Samia kuusoma mchezo wa kisiasa na kujuwa nani aingie wakati gani kuipatia timu na chama ushindi na kuwapa matumaini watanzania kwa chama.

Kiukweli Mheshimiwa Paul Makonda amekirejesha na kukiamsha chama mitaani ,ameleta hamasa iliyokuwa imelala,imeinua matumaini ya watanzania kwa CCM,amefanya chama kuwa kimbilio la wanyonge,kwa kuwa Watanzania siku zote walikuwa wanahitaji kuona CCM yenye kuwajali,kuwasikiliza,kuwafuata waliko ili kujuwa maisha wanayoishi na changamoto zinazowakabili na wanazopitia na kuzipatia majibu stahiki.

Watanzania walihitaji sauti ya chama cha mapinduzi katika kuwasemea, kuwatetea,kuwa nyuma yao,kuwapigania dhidi ya dhuluma, unyonyaji, unyanyasaji,uporwaji wa haki,ukandamizwaji,uonevu pamoja na kuwafuta machozi,kuwapa matumaini,faraja na kuwashika mkono pale wanapokuwa wameishiwa nguvu.

Haya yote kwa sasa yanatekelezwa na CCM kwa mkono na kinywa cha Mheshimiwa Makonda ambaye amejitoa na kujitolea kukibeba chama mabegani mwake kukipeleka kwa wananchi ambao ndio wamekuwa dhamana kuu ya CCM kuwepo na kusalia madarakani kwa karibu nusu karne sasa. Mheshimiwa Makonda anazungumza lugha za watu,kero za watu,.anamsikiliza kila mtu kwa unyenyekevu.anakisema chama na serikali kwa nguvu zake zote.ameiacha na kuwa mbali na familia yake ili kwenda kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zao.

Ameiacha familia yake mke na watoto wake kwa ziara ndefu ili kwenda kuwafuta machozi Watanzania walioelemewa na mizigo ya kero na tabu katika mioyo na vifua vyao.ndio maana kwa sasa mitaani habari iliyoteka na kutawala ni kuhusu Mheshimiwa Makonda ,CCM na Rais Samia. hiyo ndio habari kuu iliyoteka hisia za watu wote. Ndio habari inayofuatiliwa kwa karibu haya na wapinzani wa nchi hii kama CHADEMA.ndio maana unaona walivyo karibu katika kufuatilia kila kinachoendelea katika ziara zake.

Sasa kupitia maelekezo ya Mheshimiwa Makonda akitoa maelekezo ya chama kwenda kwa wakuu wote wa mikoa na wilaya nimeshuhudia wakuu wa mikoa wakitekeleza agizo la wao kwenda kwa wananchi kuwasikiliza kero zao na kuwapa majibu.hivi hapa nilipo ilikuwa ni jana ambapo viongozi wote wa mkoa walikuwepo mtaani kwangu kuja kusikiliza kero za wananchi na kutoa majibu,jambo ambalo liliwapa matumaini makubwa sana wananchi, ambao walihudhuria na kutoa kero zao.

Unaweza kuona namna Mheshimiwa Makonda alivyoleta mapinduzi mapya ya kiutendaji kwa viongozi.kwa sasa wananchi wanaona kuwa ukinyimwa au kudhulumiwa haki yako basi ni CCM Pekee unapoweza kupata tumaini la shida yako.kwa kuwa ni CCM Pekee inayoweza kutoa msukumo na kuweka nguvu ya wewe kupata haki yako.ndio maana tunaona na kushuhudia mikutano ya Mheshimiwa Makonda ikifurika na kumiminika watu kusikiliza na wengine wakipigana vikumbo kwa jasho na machozi kutafuta kupata nafasi ya kuwasilisha kero zao kwa Mheshimiwa Makonda.

Hii ndio maana ya kuwa chama cha siasa kinachotawala na kuongoza serikali kuhakikisha kuwa kinakuwa karibu ya watu na kuwa kimbilio namba moja la watu ndio maana sasa watu wanaona ni bora uende kwa Mh Makonda utapata haki yako haraka kuliko kwenda huko kwingine ukaishia kuzungushwa tu kama mpira.

Rai yangu ni kwa wakuu wa mikoa,wilaya,wakurugenzi na viongozi mbalimbali huko mikoani kuendeleza utamaduni huu ambao Mheshimiwa Makonda ameupandikiza na kuja nao kwa kuhakikisha kuwa mnatoka maofisini katika baadhi ya siku na kwenda kwa wananchi kuwasikiliza wananchi.kwa kuwa ninyi ndio mpo na wananchi kila siku na mkilipwa mishahara kwa kasi hiyo ya kuhudumia watu.hakikisheni mnakuwa karibu ya mwananchi,hakikisheni mkiletewa jambo mhakikishe kiwa linapatiwa ufumbuzi na mwenye haki anapatiwa haki yake.

Maana katika ziara za Mheshimiwa Makonda nimesikia wengine wakisema kuwa jambo hili nimefikisha hadi kwa mkuu wa wilaya,mkoa n.k.hii maana yake ni kuwa wengine huwa hamfuatilii kuhakikisha kuwa maelekezo yenu na maagizo yanafanyiwa kazi na watu wanapata haki zao.ndio maana inapotokea ziara za viongozi wakuu wananchi wanajitokeza na mabango wakilia na kububujikwa machozi kwa kuwa ninyi mnakuwa mlishindwa kuwapatia majibu na kuwasaidia kupata haki zao.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.View attachment 2892767
Chawa mazagazaga ktk ubora wake. Kila anakopita Makonda ni vilio vya wananchi kuhusu watendaji na huduma mbovu zinazotolewa na Serikali ya Samia chini ya chama cha mapinduzi. Kwa uchawa wako unasema Makonda kaiweka CCM mioyoni mwa watu. Ziara ya Makonda inaiumbuwa Serkali tumia akili.
 
Ni Kweli kabisa,

Mwenyekiti amemleta Mwenezi Ili awe maarufu kuliko CCCM yenyewe, pia amewekwa awe maarufu kuliko Mwenyekiti.

Muda utaongea.
Mheshimiwa Makonda alikuwa maarufu hata kabla ya kuteuliwa uenezi.kwani wewe kabla ya kuteuliwa kwake ulikuwa humfahamu? Mtanzania yupi ambaye alikuwa hamfahau? Nani alikuwa hajaona kazi kubwa aliyokuwa ameifanya akiwa mjumbe wa bunge la katiba,mkuu wa wilaya na hatimaye mkuu wa mkoa wa Dar es salaam? Nani alikuwa hamfahamu mh Makonda aliyekuwa akifanya kazi ya kuwasaidia wakazi wa Dar wenye shida kuanzia akina mama wajane,wazee, yatima n.k.? Kuna Makonda ni kubwa sana katikaTaifa letu.
 
Chawa mazagazaga ktk ubora wake. Kila anakopita Makonda ni vilio vya wananchi kuhusu watendaji na huduma mbovu zinazotolewa na Serikali ya Samia chini ya chama cha mapinduzi. Kwa uchawa wako unasema Makonda kaiweka CCM mioyoni mwa watu. Ziara ya Makonda inaiumbuwa Serkali tumia akili.
Nani kasema anaiumbua serikali? Kwa hiyo furaha yako unataka watu wafe na shida zao majumbani mwao? Unataka watu waendelee kuteseka na shida zao? Unataka waliopokwa haki zao na watu huko mitaani wasitafute msaada kwa chama? Ziara za Mheshimiwa Makonda zinasaidia sana wananchi na kuonyesha nini kifanyike huko mikoani.ndio maana kwa sasa viongozi kama ma RC na Ma DC wameanza kwenda kwa wananchi kuwasikiliza kero zao na kuwapatia majibu ya kero zao
 
Mheshimiwa Makonda alikuwa maarufu hata kabla ya kuteuliwa uenezi.kwani wewe kabla ya kuteuliwa kwake ulikuwa humfahamu? Mtanzania yupi ambaye alikuwa hamfahau? Nani alikuwa hajaona kazi kubwa aliyokuwa ameifanya akiwa mjumbe wa bunge la katiba,mkuu wa wilaya na hatimaye mkuu wa mkoa wa Dar es salaam? Nani alikuwa hamfahamu mh Makonda aliyekuwa akifanya kazi ya kuwasaidia wakazi wa Dar wenye shida kuanzia akina mama wajane,wazee, yatima n.k.? Kuna Makonda ni kubwa sana katikaTaifa letu.
Hivi sasa umaarufu wake ni mkubwa kuliko mtu yeyote ndani ya chama.

Pia umewahi kukiri jambo Hilo ukitaka awekewe ulinzi na kutunukiwa nafasi ya juu kabisa.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa hakika uteuzi uliofanywa na chama cha Mapinduzi chini ya uongozi shupavu, imara na madhubuti wa Rais na mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan , kumteua Mheshimiwa Paul Christian Makonda kuwa katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa CCM Taifa umekuwa ni uteuzi wa kihistoria na karata ya ushindi iliyochezwa na Rais Samia. imeonyesha uhodari wa Rais Samia kuusoma mchezo wa kisiasa na kujuwa nani aingie wakati gani kuipatia timu na chama ushindi na kuwapa matumaini watanzania kwa chama.

Kiukweli Mheshimiwa Paul Makonda amekirejesha na kukiamsha chama mitaani ,ameleta hamasa iliyokuwa imelala,imeinua matumaini ya watanzania kwa CCM,amefanya chama kuwa kimbilio la wanyonge,kwa kuwa Watanzania siku zote walikuwa wanahitaji kuona CCM yenye kuwajali,kuwasikiliza,kuwafuata waliko ili kujuwa maisha wanayoishi na changamoto zinazowakabili na wanazopitia na kuzipatia majibu stahiki.

Watanzania walihitaji sauti ya chama cha mapinduzi katika kuwasemea, kuwatetea,kuwa nyuma yao,kuwapigania dhidi ya dhuluma, unyonyaji, unyanyasaji,uporwaji wa haki,ukandamizwaji,uonevu pamoja na kuwafuta machozi,kuwapa matumaini,faraja na kuwashika mkono pale wanapokuwa wameishiwa nguvu.

Haya yote kwa sasa yanatekelezwa na CCM kwa mkono na kinywa cha Mheshimiwa Makonda ambaye amejitoa na kujitolea kukibeba chama mabegani mwake kukipeleka kwa wananchi ambao ndio wamekuwa dhamana kuu ya CCM kuwepo na kusalia madarakani kwa karibu nusu karne sasa. Mheshimiwa Makonda anazungumza lugha za watu,kero za watu,.anamsikiliza kila mtu kwa unyenyekevu.anakisema chama na serikali kwa nguvu zake zote.ameiacha na kuwa mbali na familia yake ili kwenda kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zao.

Ameiacha familia yake mke na watoto wake kwa ziara ndefu ili kwenda kuwafuta machozi Watanzania walioelemewa na mizigo ya kero na tabu katika mioyo na vifua vyao.ndio maana kwa sasa mitaani habari iliyoteka na kutawala ni kuhusu Mheshimiwa Makonda ,CCM na Rais Samia. hiyo ndio habari kuu iliyoteka hisia za watu wote. Ndio habari inayofuatiliwa kwa karibu haya na wapinzani wa nchi hii kama CHADEMA.ndio maana unaona walivyo karibu katika kufuatilia kila kinachoendelea katika ziara zake.

Sasa kupitia maelekezo ya Mheshimiwa Makonda akitoa maelekezo ya chama kwenda kwa wakuu wote wa mikoa na wilaya nimeshuhudia wakuu wa mikoa wakitekeleza agizo la wao kwenda kwa wananchi kuwasikiliza kero zao na kuwapa majibu.hivi hapa nilipo ilikuwa ni jana ambapo viongozi wote wa mkoa walikuwepo mtaani kwangu kuja kusikiliza kero za wananchi na kutoa majibu,jambo ambalo liliwapa matumaini makubwa sana wananchi, ambao walihudhuria na kutoa kero zao.

Unaweza kuona namna Mheshimiwa Makonda alivyoleta mapinduzi mapya ya kiutendaji kwa viongozi.kwa sasa wananchi wanaona kuwa ukinyimwa au kudhulumiwa haki yako basi ni CCM Pekee unapoweza kupata tumaini la shida yako.kwa kuwa ni CCM Pekee inayoweza kutoa msukumo na kuweka nguvu ya wewe kupata haki yako.ndio maana tunaona na kushuhudia mikutano ya Mheshimiwa Makonda ikifurika na kumiminika watu kusikiliza na wengine wakipigana vikumbo kwa jasho na machozi kutafuta kupata nafasi ya kuwasilisha kero zao kwa Mheshimiwa Makonda.

Hii ndio maana ya kuwa chama cha siasa kinachotawala na kuongoza serikali kuhakikisha kuwa kinakuwa karibu ya watu na kuwa kimbilio namba moja la watu ndio maana sasa watu wanaona ni bora uende kwa Mh Makonda utapata haki yako haraka kuliko kwenda huko kwingine ukaishia kuzungushwa tu kama mpira.

Rai yangu ni kwa wakuu wa mikoa,wilaya,wakurugenzi na viongozi mbalimbali huko mikoani kuendeleza utamaduni huu ambao Mheshimiwa Makonda ameupandikiza na kuja nao kwa kuhakikisha kuwa mnatoka maofisini katika baadhi ya siku na kwenda kwa wananchi kuwasikiliza wananchi.kwa kuwa ninyi ndio mpo na wananchi kila siku na mkilipwa mishahara kwa kasi hiyo ya kuhudumia watu.hakikisheni mnakuwa karibu ya mwananchi,hakikisheni mkiletewa jambo mhakikishe kiwa linapatiwa ufumbuzi na mwenye haki anapatiwa haki yake.

Maana katika ziara za Mheshimiwa Makonda nimesikia wengine wakisema kuwa jambo hili nimefikisha hadi kwa mkuu wa wilaya,mkoa n.k.hii maana yake ni kuwa wengine huwa hamfuatilii kuhakikisha kuwa maelekezo yenu na maagizo yanafanyiwa kazi na watu wanapata haki zao.ndio maana inapotokea ziara za viongozi wakuu wananchi wanajitokeza na mabango wakilia na kububujikwa machozi kwa kuwa ninyi mnakuwa mlishindwa kuwapatia majibu na kuwasaidia kupata haki zao.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.View attachment 2892767
Labda cha maana tuambie afya ya mzee Mwinyi, anaendeleaje?
 
Umeme upo sema labda changamoto ndogondogo ambazo nazo zinakwenda kufika kikomo muda siyo mrefu.kwa sababu Vwawa la mwalimu Nyerere linakwenda kuwasha mtambo wa kwanza ambao utatupatia megawati 205 zitakazounganishwa katika grid ya Taifa
Utakuwa mgeni nchi hii, unadhani hiyo kauli imeanza kutolewa lini? Hizo changamoto ndogondogo za tangu tupate uhuru 1961 ndizo failure zenyewe. Usituletee siasa zako za kipuuzi
 
Mleta mada una ujinga wa kiwango cha juu sana.
Hongera sana kwa kuwa mjinga wa taifa.

Sisi wengine tunaowaona viazi tu.
 
Utakuwa mgeni nchi hii, unadhani hiyo kauli imeanza kutolewa lini? Hizo changamoto ndogondogo za tangu tupate uhuru 1961 ndizo failure zenyewe. Usituletee siasa zako za kipuuzi
Ukisema tangia uhuru unakuwa Unakosea .maana kumbuka miaka inavyokwenda ndivyo hata mahitaji yanavyoongezeka kutoka na ongezeko la idadi ya watu.tulipokuwa tunapata uhuru tulikuwa milioni 12 lakini leo tupo zaidi ya million 61.sasa kama tumeongezeka ni lazima hata mahitaji nayo yaongezeke kwa kula huduma
 
Back
Top Bottom