Paul Chizzi amuumbua Mwakyembe

Paul Chizzi amuumbua Mwakyembe

Mbona anaye kanusha ana zungumzia TUMBONI...! aite press achambue hizo hayo madai sio mwandishi amfuate amuombe kuelezea!.... BIG UP MWAKYEMBE
Fuatilia vizuri we jamaa, hata kama ni gazeti la Kiingereza na shule za kata hazina walimu wa kutosha lakini ukweli ni kuwa Mwandishi wa habari kwa kuogopa kukurupuka kama magazeti yenu mengine alimfuata Chizi kujua ukweli na Chizi akatoa ukweli. Sasa wewe unaona dili na mahala alipozungumzia na sio fact aliyotoa. Ndio maana akina Mwakyembe ni mashujaa kwa kuwa wanajua jamii inayowazunguka inataka nini, yaani WAPE WATOTO NYAMA WANYAMAZE...
 
Wakuu, nimejaribu kuyasoma maelezo ya Bw. Chizi, japo lugha iliyotumika inanipa shida sana kuna kitu nimeshindwa kuelewa. Hususan anaposema "the matter is that the amount of money used to purchase the uniforms in China late last year was $18,000 only out of the stated amount, as the remaining amount was spent on the purchase of other materials,” stated Chizi.

Tatizo langu lipo katika hiyo rangi nyekundu, what on earth are these other materials which are not related to the uniforms? and why can't he mention them to justify his cleansing?
Naishia hapo misamiati imeniishia.

Other materials ndo iyo keep chenji Yao....yani kwa Lugha nyepesi "for tumbo street use only" a.k.a Vijisenti Kama vya Chenge.
inatisha...yani other materials imezidi hata bei ya kupachezi kilichowapeleka huko kwa kina Jack Chan? Mmh!

Mathematics Exercise:

50,000$ - 18,000$= 32,000$
Mmh! Yani other materials imenunuliwa kwa dola 32,000/=......duh! Huyu kweli Chizi.:confused2:
 
Huyu Chizi sasa naona kweli ameingiwa Uchizi.. Yaani ukimsoma tu unaelewa ana matatizo makubwa sana. Kifupi kama kweli wamenunua suti hizo kwa gharama ya Usd 18,000 na kuliepusha shirika gharama ya Usd 40,000 ina maana local supplier walitaka Usd 49,000 kwa suti 15?.. yaani kila suti moja karibu Usd 3,000!.

Hii inaingia akilini kweli jamani mimi naomba hizo tender walizoleta hao jamaa wanaotaka zaidi ya Usd 3,000 kwa suti, halafu kama kweli wamenunua direct China ndio anajifunga kabisaa maana China suti ya wahudumu na hata Ma pilot unaweza kupata kwa Usd 100 hadi 300 inategemea na grade..Hapo China ndio rahisi sana kupiga bao na kwa sababu najua hili nina hakika anayekwenda kununua China ana room ya kucheza na hesabu kwa sababu bei zao huwezi kuzipata sehemu yoyote duniani by far..
ndio sababu hata contracts za kimagumashi siku hizi wanapendelea kuchukua china...maana kule wanapewa bei poa wakija hapa TZ wanacheza dili na mahesabu....kwa kifupi chochote wanachofanya uchina kina faida kubwa sana kwenye wizi wao ukilinganisha na sehemu nyingine duniani....
 
Chizi anafahamu sana anachokifanya, ameharibu akubali, aondoke akapumzike.Mwakyembe amezungumzia gharama ya uniforms ni $49,900, tena amesama wazi. lakini chizi kwa usanii wake na huyo mwandishi wanazungumzia bei ya uniform ni $18,000. bei na gharama ni vitu viwili tofauti, sasa sitegemei CEO apindishe tafsiri kati ya bei na gharama.
hao precision air walinunua uniform kwa bei kati ya $ 200 na $ 600 kwa kila mmoja. ATCL hata kama wangenunua kwa bai kama ya precision air, gharama ya ATCL kwa uniform zao bado ni juu , kwani wao (ATCL) walituma wafanyakazi wao kwenda kununua na walitumia siku 45 huko, so maisha yao huko yanaingia ktk gharama ya uniform.je precision air nao walituma watu china kwa siku 45?, kama wangefanya hivyo, si precision air ingeshakufa?. chizi ni mtu mzima ameharibu akubali. baadhi ya waandishi wetu nao ni waandishi uchwara, wana ripoti bila kuchunguza na kutafsiri wanacho ripoti

Majina mengine uchuro. Hivi zile uniforma mmeziona zilivyo mavi matupu? Hizo nguo nafikiri angepewa mama Africa Sana kuanzia kudesign, kushona kudeliver hazifikia hata milioni hizo walizotuchapa.

Chizi apeleke uchizi wake nyumbani kwake, ma Pilot wafanye kazi.
 
Mkuu mwalimu wako wa kiingereza ana laana, yaani maelezo yanajitosheleza na hadi gharama ya unit imeelezwa bado hujaelewa na unabisha...

Ninashauri sio lazima kuchangia mada kama hujaelewa, haya mambo ya aviation ni ya kitaalam, nyie mliotokea shule za kata kaeni pembeni wataalam walumbane.
Nenda jukwaa la lugha kajifunze kiingereza au hire a translator

Coment za mafisadi Hizi.......eti "kaeni pemben WATAALAM walumbane" mmmmh!
 
Fuatilia vizuri we jamaa, hata kama ni gazeti la Kiingereza na shule za kata hazina walimu wa kutosha lakini ukweli ni kuwa Mwandishi wa habari kwa kuogopa kukurupuka kama magazeti yenu mengine alimfuata Chizi kujua ukweli na Chizi akatoa ukweli. Sasa wewe unaona dili na mahala alipozungumzia na sio fact aliyotoa. Ndio maana akina Mwakyembe ni mashujaa kwa kuwa wanajua jamii inayowazunguka inataka nini, yaani WAPE WATOTO NYAMA WANYAMAZE...
..... unafurahisha mjomba kama huyo jamaa ni msafi, kwanini assiite vyombo vya habari kutoa ufafanuzi badala yake waandishi wamtafute na wamuombe kuzungumzia madai hayo!
 
Ndugu Chizi maagent wako umu wanaweza tupa tafsiri ya other materials ambazo hutaki ata kuzitaja.Au labda ni nguo za ndani za hao Airhostess.
Alafu unaingia mkataba ata AG hajui kisa wewe umesomea mambo ya Anga,so unajua kila kitu on sheria na Anga?
Una bahati ni Tz nchi zingine usingepata ata mda wa kuhojiwa na magazeti.
Ni busara kukaa kimya bse huwezi rudi kwenye iyo post tena na malumbano hayafai bse taarifa alizosema Mwakyembe nyingi ziko featured kwenye vitabu vyenu ambavyo ungekuwa umeondoka navyo angalau ungekuwa umeficha ukweli
 
yaani nguo za wafanyakazi dola 18000 wakati ndege zenyewe hakuna sa hizo nguo wanazinunua wazitumie wapi?? hii nchi hii...sijawahi sikia uniform ya dola 18000
 
Aliyekuwa mtendaji mkuu wa ATCL ameibuka na kusema kwamba Dr Mwakyembe alidanganya umma kutokana taarifa alizopewa kuwa ni za uongo na zisizokuwa na ukweli wowote.

Kwa mfano uniform ziligharimu dola 18,000 tu na sio dola 50,000 kama alivyosema mwakiembe, Bwana Chizi alisema pia tatizo ni kwamba kuna watu hawajui chochote kuhusu sekta ya anga lakini wanajidanganya kuwa wanajua mbele ya umma.



Chanzo: The Guardian on Sunday



Kwani wazazi Wakimwita Mtoto wao "Chizi" ina maana inahitaji wataalamu wa kigeni Kugundua Mtu ni "Chizi" Kweli? Sasa ATCL WALIKUWA WAPI?
 
jiandaeni kulipa bil zingine na fidia juu kwa hawa madirector.......hivi zile za dowans bil 94 mlishalipa ee!!....
Hamnaaaaa ! Hawa tutawazungusha kama wale wa gongo la mboto !
 
Hata wewe unatetea upuuzi wa Mwakyembe!!! Kweli nchi yetu ina safari ndefu sana kufikia maendeleo maana asilimia kubwa mnahitaji heater za kuchemsha akili. Chizi ameact professionally, Mwakyembe ame act ki layman, halafu mwakyembe ndio shujaa kwenu. Stupid.
Huyu ni "Chizi" mdogo, asiwasumbuwe !
 
Si ajabu anaitwa chizi....utatumiaje dola 18,000 kushona nguo ambazo zaweza shonwa kwa batiki za hapa hapa na hata Millioni 2 isifike.....

Jina lake linaeleza kila kitu sina la kuongeza zaidi mie ningepewa jina hilo nisingekurupuka ovyo kwenye media
 
Mkuu kama una nafasi nakuomba ukanunue gazeti la leo la Guardian ndio utaamini kuwa kumbe hata wale wenye Phd za ukweli wana matatizo.

Ndugu mimi nataka kuchangia hapa tu kwenye PHD, PHD au any certification yoyote hapa Tanzania does really stand for its credibility.

Yani hapa Tanzania ukisikia a doctor ukaja kumsikia akiongea (either kwenye mazungumzo au kujibu maswali) unaweza kuasikia wewe aibu. Kuongea i mean the way anavyotoa alivyo navyo kichwani ndo utajua hku africa kuna PHD za academics tu bt not more than that. (bt not all, most of them)

There is time nilikuwa nataka kujua kwanini waingereza na wamarekani wanatu demand tufanye TOEFL na ILETS knowing kabisa kwamba tunatumia english shuleni from form 1 to form six. NIkagundua maybe kwasbb wanajua shule tunakariri tu na tunabahatisha hence our results are questionable so they have to prove for themselves by having us sit for their tests.

Utamkuta mwanfunzi ana A kwenye somo au stright As, bt sit down with the student uone hw much he/she anajua kuhusu ilo somo au hayo masomo, u will be suprised.

but Marekani wanafunzi wanaopata 'A's kwenye masomo au Perfect scores kwenye SATs of ACTs huwa ni extraordinary kids, huwa ni little geniuses. Huwa wana IQ kubwa sana.
 
Sacked ATCL boss faces Mwakyembe
By Florian Kaijage
10th June 2012

. Reveals what transpired before he wasfired


The sacked Air Tanzania Company Limited’s acting chief executiveofficer Paul Chizi yesterday emerged, saying all allegations raised by Ministerfor Transport Dr. Harrison Mwakyembe are false and based on hearsay andulterior motives. Chizi, who spoke for the first time since he was dismissed last week, termed the minister’s accusations against him as malice-driven and unfounded, adding that he saved Sh40 million for his decision to procure uniforms for air hostesses and captains from China. He also clarified the $3 million (Sh4.8 billion) insurance payments from Alexander Forbes, saying the government’s instructions reachedhim on May 22, nearly two weeks after the transaction had been effected throughan ATCL account.

Citing the leasing of a Boeing 737-500 plane which ATCL leasedfrom a Dubai-based firm, Aero Vista, Chizi defended the deal, saying he acted within his mandate as the company’s CEO in sealing what he termed as the ‘bestand fairest’ deal within the aviation industry. “For instance, the issue of uniforms which the minister sayseach cost $50,000 (around Sh80 million). If this statement remains uncorrectedpeople will tend to believe it, but the fact of the matter is that the amount of money used to purchase the uniforms in China late last year was $18,000 onlyout of the stated amount, as the remaining amount was spent on the purchase ofother materials,” stated Chizi.

With regard to claims that the prices of air hostesses’ and captains’ outfits were inflated, the sacked CEO said, “The uniforms cost ATCL only $18,000 and not $49,000 as claimed by the minister.” “The process started by inviting local suppliers to submit theirquotations…we did our calculations and established that local suppliers were more expensive,” he added.

“We finally decided to buy directly from the suppliers in China,and in so doing I saved Sh40 million which would have otherwise been spent if the company procured the uniforms locally,” Chizi elaborated. He addd: “The consignment was of high quality material and we decided to make the purchase in China after drawing conclusions that it was more expensive to buy the required material in Tanzania according to the submitted quotations submitted. In fact, by opting for the Chinese material ATCLsaved about Sh40 million” Chizi, a professional aircraft engineer, said he wondered whythe matter had to be raised after his appointment was nullified while, to his knowledge, the uniforms were purchased towards the end of last year.

“The ministry at that time formed a team to investigate the matter following a letter from an anonymous author. The team was led by one Ekingo Magesa from the Civil Service secretariat and its secretary was the ministry’s deputy director of administration and personnel, Hashim Butara,” hesaid, adding:
“The panel also included the ministry’s chief accountant and former director general of the Tanzania Airports Authority (TAA), ProsperTesha. According to the probe team’s report, everything was properly done. Nowwhere do these new accusations arise from?”

He challenged the ministry of Transport to issue the probe team’s findings and state if they were contrary to what he was saying now,adding that even the Public Procurement Regulatory Authority (PPRA) noted thatthe uniforms’ procurement met the legal requirements and that there was valuefor money.
The material included uniforms for the cabin crew, pilots andfront office staff. A quick survey conducted by The Guardian on Sunday hasestablished that a single full pair of an airhostess’s uniform costs between$200 and $600. PrecisionAir last year imported its airhostess’ uniforms from Hong Kong at a similar price, according to details gathered by this paper.

A reliable source told The Guardian on Sunday yesterday that the airline imported several sets of uniforms for its airhostesses last year from Hong Kong at the cost of between $200 and $600 per set. He said the cost of a set depended on the category of the set,adding that the most expensive category could cost as high as $600 while the lowest cost $200. Referring to the transfer of $3 million paid by insurer Alexander Forbes as part of insurance payment for an aircraft, a BombadierDash-8 which crashed when taking off at Kigoma airport last April, Chizi said the minister misrepresented the matter by stating that the ministry had issued directives to have the money deposited in a different bank account to avoid the money being affected by a court order.

“The truth of the matter is that the ministry directed ATCL to contact Consolidated Holding Corporation (CHC) so as to be provided with bank details about where the money from the insurer was to be deposited, but by the time the directive reached us on May 22 the money had already been deposited by the insurer and there is no way the payment could have been deposited in a different account from that of the aircraft owners – ATCL,” Chizi stated.
He added: “The public should also understand that the said courtorder which would have affected the payment had it been deposited in ATCL’s bank account with Stabic Bank is still controversial because there is a valid court injunction owing to there being other matters to be sorted out betweenATCL and the creditor who sought the court order. However, the money is still intact.”

With regard to sour relations between him and senior ministry officials after the minister accused him of acting without the ministry’s knowledge, he said all the matters the minister pointed out were merely executive. “Administrative matters are quite different from those of a technical or executive nature. There is no way a chief executive could seek approval from the parent ministry about every single matter. “The leasing of an aircraft is a technical matter. What isimportant is to inform them (minister), for if you act the way the ministry wants you to you might end up doing entirely nothing because they do not respond to letters in time on the pretext of attending a series of endless meetings,” he said..

He explained that all decision on technical matters are concludedby the ATCL management, except those which need approval from higher authorities, such as government guarantees. He said in the case of leasing theBoeing 737-500 airliner no guarantee or deposit was needed, adding that it was the best leasing deal the country had ever entered into. “The problem is that there are people who know very little about this industry but they tend to project the image that they know much,” he said..

Chizi’s sacking was announced by the ministry of Transport on June 4 through a statement signed by Permanent Secretary Omar Chambo.
It said he would be replaced by Captain Lazaro Lusajo with immediate effect. According to the PS, Chizi and four other top officials had violated the public procurement Act, apart from the fact that his employment did not follow laid down procedures. The statement read: “Through Act No 8 of 2002 and Public Service Principle No 17(4) of 2003, the minister for Transport has revoked the appointment of the acting ATCL director-general with effect from 5 June.”

The other four directors were suspended on the grounds that their services had threatened the survival of a public entity. They are heads of legal, business,finance and technical departments

Je ungetegemea bwana Chizi asemeje?.
Basi audhibitishie umma kwamba tulipata wazabuni wazawa (orodha na gharama zao), lakini mali ya kichina ndo ikaonekana ni rahisi.
La sivyo hapa ni mbinu za kujitetea, tukizingatia kuwa wengi wa viongozi wa Tanzania wanaingia madarakani kwa lengo la kujinufaisha tu.
 
Hata kama hivyo ndivyo alivyosema, bado kuna tatizo kubwa sana hapo.

USD 18,000 X 1500=Tsh. 27,000,000 kwa unifomu moja! Milioni 27 kweli kwa nguo moja?

Hajaweza bado kuniweka kwenye kundi la watu wa kumuamini na sana sana ananiongezea machungu tu ya PAYE niliyokatwa mwezi uiopita.

Ni vizuri kusoma na kuelewa thread kabla ya kuanza kuchangia. Fedha hizo ni za uniform za wafanyakazi wote wanaoruka na ndege na sio nguo moja tu!!Sasa ni juu yako kujua kuna Pilots na hostesses wangapi ATCL!!
 
huyu mzee ndo maana walimpa misumu afe ..maana anakurupukaga tu...yaleyale ya richmond hakuna cha maana zaidi ya mbwembwe na mikelele
 
Chizi awasilisha barua kwa Waziri Mkuu kupinga 'tuhuma' za Dkt. Mwakyembe dhidi yake - wavuti
Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), Paul Chizi ambaye hivi karibuni alitenguliwa katika cheo hicho na Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe wiki jana, amefikisha ramsi malalamiko yake kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Uchunguzi wa gazeti la Habari Leo umebaini kuwa Chizi amewasilisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu akipinga tuhuma zilizoelekezwa kwake na Waziri, Mwakyembe akidai si za kweli na kwamba zimelenga kumshushia hadhi kwa jamii.

Pamoja na barua hiyo, Chizi amewasilisha lundo la vielelezo vikifafanua tuhuma mbalimbali zilizotolewa na Dkt. Mwakyembe dhidi yake, ili kuthibitisha kutokubaliana na tuhuma hizo kwake. Kaimu Mkurugenzi huyo wa zamani wa ATCL alipotafutwa jana ili kuzungumzia suala hilo alikiri suala hilo kuwasilishwa ofisi ya Waziri Mkuu, ingawa hakuwa tayari kulizungumzia zaidi kwa madai kuwa liko kwenye mamlaka za juu sasa.

Tuhuma ya sare za milioni 80/-

Maelezo ya Chizi kwa Pinda, yanafafanua kwamba ATCL ilinunua loti 30 za vifaa mbalimbali vya wafanyakazi zikiwamo sare zilizotajwa na Dk Mwakyembe kwa thamani ya dola za Marekani 18, 920 na si dola za Marekani 50,000 kama alivyodai Waziri Mwakyembe, hatua ambayo ilifanya ATCL kuokoa zaidi ya Sh milioni 44 kama ingenunua sare hizo nchini kulingana na bei ya ununuzi iliyowasilishwa ATCL.

Tuhuma ya ukodishaji wa ndege

Anapinga pia kuhusishwa na ukodishaji wa ndege aina ya Airbus ambayo Waziri Mwakyembe alisema haikuwa na sababu ya kukodishwa, akisema ndege hiyo ilikodishwa mwaka 2007 na kufanya kazi hadi mwaka 2008, wakati yeye aliteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Agosti 2011. Dk Mwakyembe akizungumzia mkataba huo tata wa Airbus, alisema umeifanya nchi kudaiwa Sh bilioni 69 na kusisitiza kuwa kutokana na hali hiyo, Serikali haikuwa tayari kufumbia macho mambo mengine ya ovyo yanayoendelea katika shirika hilo.

"Kuhusu ukodishaji wa ndege aina ya Boeing 737 – 500 kutoka Kampuni ya Aerovisto, utaratibu wa kawaida wa ukodishaji wa ndege kwa njia ya wetlease ulifanyika, taratibu zote kama zinavyotakiwa kisheria zilifuatwa.

"Ilikuwa ni suala la kushitua sana kwangu pale nilipopata maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu (Wizara ya Uchukuzi, Omar Chambo) kwamba taratibu hazikufuatwa, na hivyo ndege tuliyoikodi haikutakiwa kuruka kinyume na barua ya Waziri Mwakyembe mwenyewe ya Mei 12, akieleza kuridhishwa na hatua tulizochukua katika ukodishaji ndege na kuturuhusu kuendelea na mchakato," ilisema barua hiyo.

"Suala la kupeleka mkataba wa ACMI kwa AG (Mwanasheria Mkuu wa Serikali) ambao si utaratibu wa kawaida, lilikuja wakati mchakato wa kuleta ndege uko katika hatua za juu kabisa. Hata hivyo, maagizo yalizingatiwa; mkataba ulikwenda kwa AG hata baada ya Waziri kutoa maoni yake kuwa ni mzuri. Waziri alitoa kauli kama hiyo pia kwenye kikao cha Kamati ya Bunge ya Miundombinu kilipokaa Ofisi Ndogo za Bunge hivi karibuni," ilisema barua hiyo.

Tuhuma za fedha na akaunti

Barua hiyo kwa Waziri Mkuu ikifafanua kuhusu suala la sare za ATCL ilisema lilishafanyiwa uchunguzi baada ya Chambo kuunda Tume kuchunguza ubadhirifu huo ikiongozwa na DAP wa Sekretarieti ya Utumishi wa Umma Shekiondo Magesa na Tume kubaini hakukuwa na ubadhirifu wowote na kumpongeza Chizi kwa kuokoa fedha za Kampuni.

"Madai ya Waziri Mwakyembe kuhusu fedha za bima ni kwamba kampuni ya Alexander Forbes ilitoa taarifa, kuwa fedha za bima zingetumwa kwenye akaunti yetu wiki ya nne ya Mei 2012.

Menejimenti ya ATCL ilikaa na kutafakari agizo la Wizara kutaka fedha hizo zipelekwe CHC (Kampuni Hodhi ya Mashirika ya Umma).

"Tulisubiri kupata akaunti ya CHC ili tutoe maagizo hayo. Hata hivyo, akaunti hiyo tulichelewa kuipata, ndipo tulipokwenda benki kutaka kupata njia mbadala ya kuhakikisha usalama wa fedha zetu. Mei 28 dola za Marekani milioni 3 zililipwa kwenye akaunti yetu ya Stanbic na Menejimenti ya ATCL ikaagiza benki ihamishe fedha hizo ili zishikiliwe kama dhamana ya ATCL kupata mtaji wa kujiendesha.

"Maagizo ya kuhamishwa pesa hiyo ili zihifadhiwe na benki yalitolewa kwa benki siku hiyo hiyo Mei 28. Asubuhi ya Mei 29 wakati mchakato wa kuzihifadhi haujakamilika, tulitaarifiwa kuwa dola milioni moja zimezuiwa na amri ya mahakama kutoka Kampuni ya Ultimate Security yenye thamani ya dola 993,000.

"Hapo hapo tulielekeza wanasheria wetu wazuie utekelezaji wa amri hiyo na jambo hilo lilifanyika na pesa hiyo ipo kwenye akaunti salama hadi leo, hakuna aliyelipwa kama alivyosema Waziri Mwakyembe. Shauri hilo litatolewa uamuzi Juni 18," ilisema barua hiyo.

Kulingana na vielelezo vilivyowasilishwa Ofisi ya Waziri Mkuu, gazeti la Habari Leo limebaini kuwa wakati Wizara ya Uchukuzi ikiwasilisha barua ya maagizo ya fedha hizo za bima kuwekwa kwenye akaunti ya CHC, malipo hayo ya bima yalikuwa yamelipwa kupitia akaunti ya Stanbic na kampuni ya Alexander Forbes asubuhi siku hiyo.

Gazeti la Habari Leo lilipowasiliana na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo jana, alithibitisha kupokewa kwa malalamiko hayo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu huyo wa ATCL na kusema ofisi yake ilikuwa bado inayafanyia kazi ili kufahamu mwenendo mzima wa suala hilo kabla ya kulizungumzia.

Soma habari nzima katika tovuti ya gazeti la HabariLeo

Source: Previous Posts - wavuti
 
Kila mtu anapokuwa amebanwa lazima atafute utetezi hata kama ni wa uongo, hapo Chizi anatapatapa tu ukweli unabaki palepale, ATCL kulikuwa na ubadhirifu mkubwa saana, Miaka Ishirini iliyopita kulikuwa na ndege kubwa zaidi ya tano,Leo hii shirika hoi, Loh tumechoka kudanganywaa!!!
 
nafikiri ni kwa sababu wanapem\nda kufanya kazi kisiasa sana kuliko kutumia taaluma
na elimu yao ikiwadia.
 
Back
Top Bottom