Paul Chizzi amuumbua Mwakyembe

shule zingine bomu kabisa. labda ni english unreachable. kununua nguo zote ndiyo hiyo dola 18000. weye mwenzetu ati wadhani uniform moja dola 18000?

Hapa hatupo kushinda elimu wewe dada na labda kama hujatembelea JF siku kadhaa zilizopita, huwezi kunielewa. Nukuu kidogo kutoka gazeti la tanzania daima la tarehe 8 inaweza kukusaidia pamoja na hiyo elimu ambayo si ya shule za kata kama yangu.

''Waziri huyo aligusia pia hatua ya baadhi ya maafisa kwenda nchini China na kukaa huko takriban siku 45 kwa ajili ya kusimamia sare za wafanyakazi, jambo ambalo alidai ni ufujaji wa fedha za umma kwa kugharamia sare moja dola 49,900.''

Nilimjibu mleta mada nikitumia nukuu hiyo na si vinginevyo.
 
kwani hizo dola 18,000 ni kidogo? wakati shirika halina hata ndege moja? Tusiwaonee haya wahalifu kama hawa ni hatari kwa nchi yetu

Umeona ehe chizzi acha kulalamika,jezi moja ya mfanyakazi ni sh. 3m?? Nayo ni kubwa mno jezi za china haizidi laki mbili kwa moja.
 
Humu JF tumevamiwa na majuha, ni nani asiyejua ubadhirifu unaofanyika katika sekta ya umma? kitu chaweza kuwa dola 200 lakini kikaandikiwa invoice ya dola 2500 bila aibu, kuna sehemu kwa sekta ya umma mwanzoni mwa mwaka 2000 nilikutana na invoice amboya one of the price ya RJ45 iliwekwa dola 250. Sasa kama unashangaa alichosema Mwakiyembe basi fuatilia hata bajeti zetu uone wanatenga mamilioni mangapi kwa chai na entertainment na kila mwaka hela za fenicha, Chizi mwizi na Mwakiyembe nae mwizi tu, maana mwizi afukuzwi kazi tu na ashitakiwe na kufilisiwa, mshatuona WATZ mabwege sanaaa. Mnakera

Usitutoe kwenye mada hatujathibitisha wizi wa chizi au mwakyembe kinachozungumzwa ni kukanushwa kwa kauli ya mwakyembe na chizi. Mwanzo kabisa wa sakata wengine tulisema kuwa ya mwakyembe hayana mantiki matokeo yake chizi amekanusha tusubiri mwendelezo. Ila ni kweli mawaziri wa serikali ya ccm ina maamuzi ya kukurupuka.
 
Kama kweli bwana Chizi anadhani Dr. Harrison amekosea au alidanganywa then sioni sababu yeye akae kubwabwaja kila siku kwenye vyombo vya habari. Uchunguzi utafanyika, nadhani atapata nafasi ya kujieleza then ukweli utajulikana.

Uwe mkweli mwakyembe kakurupuka, chizi anatufahamisha upande mwingine wa shilingi.
 
Aliyekuwa mtendaji mkuu wa Atcl ameibuka na kusema kwamba Dr Mwakiembe alidanganya umma kutokana taarifa alizopewa kuwa ni za uongo na zisizokuwa na ukweli wowote.Kwa mfano uniform ziligharimu dola 18,000 tu na sio dola 50,000 kama alivyosema mwakiembe, Bwana chizi alisema pia tatizo ni kwamba kuna watu hawajui chochote kuhusu sekta ya anga lakini wanajiganya kuwa wanajua mbele ya umma.
Chanzo: The Guardian on Sunday


Chizi anafahamu sana anachokifanya, ameharibu akubali, aondoke akapumzike.Mwakyembe amezungumzia gharama ya uniforms ni $49,900, tena amesama wazi. lakini chizi kwa usanii wake na huyo mwandishi wanazungumzia bei ya uniform ni $18,000. bei na gharama ni vitu viwili tofauti, sasa sitegemei CEO apindishe tafsiri kati ya bei na gharama.
hao precision air walinunua uniform kwa bei kati ya $ 200 na $ 600 kwa kila mmoja. ATCL hata kama wangenunua kwa bai kama ya precision air, gharama ya ATCL kwa uniform zao bado ni juu , kwani wao (ATCL) walituma wafanyakazi wao kwenda kununua na walitumia siku 45 huko, so maisha yao huko yanaingia ktk gharama ya uniform.je precision air nao walituma watu china kwa siku 45?, kama wangefanya hivyo, si precision air ingeshakufa?. chizi ni mtu mzima ameharibu akubali. baadhi ya waandishi wetu nao ni waandishi uchwara, wana ripoti bila kuchunguza na kutafsiri wanacho ripoti
 
Wakuu, nimejaribu kuyasoma maelezo ya Bw. Chizi, japo lugha iliyotumika inanipa shida sana kuna kitu nimeshindwa kuelewa. Hususan anaposema "the matter is that the amount of money used to purchase the uniforms in China late last year was $18,000 only out of the stated amount, as the remaining amount was spent on the purchase of other materials,” stated Chizi.

Tatizo langu lipo katika hiyo rangi nyekundu, what on earth are these other materials which are not related to the uniforms? and why can't he mention them to justify his cleansing?
Naishia hapo misamiati imeniishia.
 
Sijasoma yote nitasoma baadaye lakini huu ni wizi na uhuni. Amekansha nini sasa hapo kihusu uniform? Anasema hela zingine zilitumika kununua other materials; yapi? Uhuni tu. Hivi angekuwa mbunifu si angewapa wanamitimdo wetu washone nguo zinazofanana fanana na Tanzania badala ya kukimbilia China. Ati CEO hivyo ana mandate; mandate y wizi?
 
Ana ushahidi kweli kwamba kwa kuagiza Uchina ameokoa milioni 40 za Kitanzania? Mbona hiyo difference ni kubwa mno. Uwizi tu kila mahala
 
Wakuu, nimejaribu kuyasoma maelezo ya Bw. Chizi, japo lugha iliyotumika inanipa shida sana kuna kitu nimeshindwa kuelewa. Hususan anaposema "the matter is that the amount of money used to purchase the uniforms in China late last year was $18,000 only out of the stated amount, as the remaining amount was spent on the purchase of other materials,” stated Chizi.

Tatizo langu lipo katika hiyo rangi nyekundu, what on earth are these other materials which are not related to the uniforms? and why can't he mention them to justify his cleansing?
Naishia hapo misamiati imeniishia.


Other materials ndio wizi wenyewe huo. Labda nguo za ndani!
 
kwani hizo dola 18,000 ni kidogo? wakati shirika halina hata ndege moja? Tusiwaonee haya wahalifu kama hawa ni hatari kwa nchi yetu

upo sahihi mkuu. Dola 18000 kwa peace 15 za uniform si sawa. Tena huy u kajikaanga mwenyewe achukuliwe hatua mara moja.
 
Kama kweli bwana Chizi anadhani Dr. Harrison amekosea au alidanganywa then sioni sababu yeye akae kubwabwaja kila siku kwenye vyombo vya habari. Uchunguzi utafanyika, nadhani atapata nafasi ya kujieleza then ukweli utajulikana.

Sidhani kama kuna tatizo, kinachonishangaza ni kwamba huyu bwana yuko busy kutafuta sympathy ya wananchi, kazi si ilikuwa yake? Anataka tumuone innocent mpaka tusiwe na imani na tume? Amekuwa Maige mwingine sasa.

Lowasa alipojiuzulu hakuhangaika kujieleza kwa watu, ila alipobidi akajieleza kwenye mkutano mbele ya JK, naye asubiri muda wake tumemchoka, kama pesa alihonga na kulewa ma-whisky shauri yake, too late.

Lini tena aliongea zaidi ya hiyo jana na ndio leo tunaujua ukweli wa upande wapili, naona harufu ya Fidia kwa wale directors wengine 4.
 
Haijalishi maelezo mengi yanayoweza kutolewa ili kutafuta huruma ya Watanzania. Ukweli ni kuwa sio yeye tu inapaswa shirika zima hao wafanyakazi waondoke wote (imekuwa kama cancer) kwa miaka yote tunachosikia ni kuanguka kwa ndege na kukodisha kusiko mafanikio. Nasema haijalishi ikiwa waziri amekurupuka, wakati fulani tunahitaji watu wakusafisha na kisha mambo mengine baadae. Hivi sasa ATCL inatia aibu kuwa ndio mbeba bendera yetu.

$18,000 tu ndio zimetumika ????, je hizo za watu kukaa siku 45. Ikiwa unaweza nunua kila kitu kwa mtandao kwanini wakakae huko, je wao walikuwa wanazishona. Hii ni kansa, mtiririko wa wezi kupeana dili. Nashauri wafanyakazi wote hadi wafagizi, Waondolewe. Kisha tuanze moja.

Tumechoka kuibiwa kodi zetu!!!...
 
Si ajabu anaitwa chizi....utatumiaje dola 18,000 kushona nguo ambazo zaweza shonwa kwa batiki za hapa hapa na hata Millioni 2 isifike.....

nakuunga mkono ndugu yangu. Tatizo watz hatutaki kukubali kama twaweza kupendeza kwa kuvaa hata hizo batiki ambazo wahudumu wangependeza na kuonyesha utaifa wetu. Kuna wabunifu wengi tu wa kibongo kama kina Manju, naamini wasingeshindwa kubuni vazi la wahudumu wa ndege, naamini wangependeza sana na shirika kutumia gharama nafuu.
 
Hata kama hivyo ndivyo alivyosema, bado kuna tatizo kubwa sana hapo.

USD 18,000 X 1500=Tsh. 27,000,000 kwa unifomu moja! Milioni 27 kweli kwa nguo moja?

Hajaweza bado kuniweka kwenye kundi la watu wa kumuamini na sana sana ananiongezea machungu tu ya PAYE niliyokatwa mwezi uiopita.
Nawewe kama kidhungu hujui si uulize? hizo 18000 ni kwa ajili ya nguo za wahudumu wa ndani ya ndege, mapokezi na marubani. Seti moja yaani viatu, soksi, sketi, chapi(not sure), blause, skafu, nk ni kati ya dola 200 mpaka 600. Na sio pea moja. Sasa rudi uchangie uzi.
 
Chizzi naona anamatatizo ya kisaikolojia kwa sasa hivi kweli anaona kama watanzania hatuna elimu ya kujua huu ni uhuni na huu si uhuni haingii akilini kusema shirt moja ilinunuliwa kwa usd 18000 kweli hata aibu hauna unaongea mbele ya medium bila kuongopa sikutegemea kama ukochizi kama jina lako lilivyo. tuondolee ujinga wako kama unaona nchi haina watu wenye elimu kakae hata na mkeo unaweza pata raha nje yakutuongezea hasira na machungu ya mali zetu mnazofaidi kikundi kidogo kama wewe.
 
Sacked ATCL bossfaces Mwakyembe
By Florian Kaijage
10th June 2012
. Reveals what transpired before he wasfired

The sacked Air Tanzania Company Limited’s acting chief executiveofficer Paul Chizi yesterday emerged, saying all allegations raised by Ministerfor Transport Dr. Harrison Mwakyembe are false and based on hearsay andulterior motives. Chizi, who spoke for the first time since he was dismissed last week, termed the minister’s accusations against him as malice-driven and unfounded, adding that he saved Sh40 million for his decision to procure uniforms for air hostesses and captains from China. He also clarified the $3 million (Sh4.8 billion) insurance payments from Alexander Forbes, saying the government’s instructions reachedhim on May 22, nearly two weeks after the transaction had been effected throughan ATCL account.

Citing the leasing of a Boeing 737-500 plane which ATCL leasedfrom a Dubai-based firm, Aero Vista, Chizi defended the deal, saying he acted within his mandate as the company’s CEO in sealing what he termed as the ‘bestand fairest’ deal within the aviation industry. “For instance, the issue of uniforms which the minister sayseach cost $50,000 (around Sh80 million). If this statement remains uncorrectedpeople will tend to believe it, but the fact of the matter is that the amount of money used to purchase the uniforms in China late last year was $18,000 onlyout of the stated amount, as the remaining amount was spent on the purchase ofother materials,” stated Chizi.

With regard to claims that the prices of air hostesses’ and captains’ outfits were inflated, the sacked CEO said, “The uniforms cost ATCL only $18,000 and not $49,000 as claimed by the minister.” “The process started by inviting local suppliers to submit theirquotations…we did our calculations and established that local suppliers were more expensive,” he added.

“We finally decided to buy directly from the suppliers in China,and in so doing I saved Sh40 million which would have otherwise been spent if the company procured the uniforms locally,” Chizi elaborated. He addd: “The consignment was of high quality material and we decided to make the purchase in China after drawing conclusions that it was more expensive to buy the required material in Tanzania according to the submitted quotations submitted. In fact, by opting for the Chinese material ATCLsaved about Sh40 million” Chizi, a professional aircraft engineer, said he wondered whythe matter had to be raised after his appointment was nullified while, to his knowledge, the uniforms were purchased towards the end of last year.

“The ministry at that time formed a team to investigate the matter following a letter from an anonymous author. The team was led by one Ekingo Magesa from the Civil Service secretariat and its secretary was the ministry’s deputy director of administration and personnel, Hashim Butara,” hesaid, adding:
“The panel also included the ministry’s chief accountant and former director general of the Tanzania Airports Authority (TAA), ProsperTesha. According to the probe team’s report, everything was properly done. Nowwhere do these new accusations arise from?”

He challenged the ministry of Transport to issue the probe team’s findings and state if they were contrary to what he was saying now,adding that even the Public Procurement Regulatory Authority (PPRA) noted thatthe uniforms’ procurement met the legal requirements and that there was valuefor money.
The material included uniforms for the cabin crew, pilots andfront office staff. A quick survey conducted by The Guardian on Sunday hasestablished that a single full pair of an airhostess’s uniform costs between$200 and $600. PrecisionAir last year imported its airhostess’ uniforms from Hong Kong at a similar price, according to details gathered by this paper.

A reliable source told The Guardian on Sunday yesterday that the airline imported several sets of uniforms for its airhostesses last year from Hong Kong at the cost of between $200 and $600 per set. He said the cost of a set depended on the category of the set,adding that the most expensive category could cost as high as $600 while the lowest cost $200. Referring to the transfer of $3 million paid by insurer Alexander Forbes as part of insurance payment for an aircraft, a BombadierDash-8 which crashed when taking off at Kigoma airport last April, Chizi said the minister misrepresented the matter by stating that the ministry had issued directives to have the money deposited in a different bank account to avoid the money being affected by a court order.

“The truth of the matter is that the ministry directed ATCL to contact Consolidated Holding Corporation (CHC) so as to be provided with bank details about where the money from the insurer was to be deposited, but by the time the directive reached us on May 22 the money had already been deposited by the insurer and there is no way the payment could have been deposited in a different account from that of the aircraft owners – ATCL,” Chizi stated.
He added: “The public should also understand that the said courtorder which would have affected the payment had it been deposited in ATCL’s bank account with Stabic Bank is still controversial because there is a valid court injunction owing to there being other matters to be sorted out betweenATCL and the creditor who sought the court order. However, the money is still intact.”

With regard to sour relations between him and senior ministry officials after the minister accused him of acting without the ministry’s knowledge, he said all the matters the minister pointed out were merely executive. “Administrative matters are quite different from those of a technical or executive nature. There is no way a chief executive could seek approval from the parent ministry about every single matter. “The leasing of an aircraft is a technical matter. What isimportant is to inform them (minister), for if you act the way the ministry wants you to you might end up doing entirely nothing because they do not respond to letters in time on the pretext of attending a series of endless meetings,” he said..

He explained that all decision on technical matters are concludedby the ATCL management, except those which need approval from higher authorities, such as government guarantees. He said in the case of leasing theBoeing 737-500 airliner no guarantee or deposit was needed, adding that it was the best leasing deal the country had ever entered into. “The problem is that there are people who know very little about this industry but they tend to project the image that they know much,” he said..

Chizi’s sacking was announced by the ministry of Transport on June 4 through a statement signed by Permanent Secretary Omar Chambo.
It said he would be replaced by Captain Lazaro Lusajo with immediate effect. According to the PS, Chizi and four other top officials had violated the public procurement Act, apart from the fact that his employment did not follow laid down procedures. The statement read: “Through Act No 8 of 2002 and Public Service Principle No 17(4) of 2003, the minister for Transport has revoked the appointment of the acting ATCL director-general with effect from 5 June.”

The other four directors were suspended on the grounds that their services had threatened the survival of a public entity. They are heads of legal, business,finance and technical departments

Kaijage amehongwa senene kuhalalisha wizi umetukosa shule wote tumekwenda ila wewe ni msema chochote hata kama ni uwongo la kuvunda halina ubani kazi kutetea majizi tu shame on you
 
With regard to claims that the prices of air hostesses' and captains' outfits were inflated, the sacked CEO said, "The uniforms cost ATCL only $18,000 and not $49,000 as claimed by the minister." "The process started by inviting local suppliers to submit theirquotations…we did our calculations and established that local suppliers were more expensive," he added.

"We finally decided to buy directly from the suppliers in China,and in so doing I saved Sh40 million which would have otherwise been spent if the company procured the uniforms locally,
Huyu Chizi sasa naona kweli ameingiwa Uchizi.. Yaani ukimsoma tu unaelewa ana matatizo makubwa sana. Kifupi kama kweli wamenunua suti hizo kwa gharama ya Usd 18,000 na kuliepusha shirika gharama ya Usd 40,000 ina maana local supplier walitaka Usd 49,000 kwa suti 15?.. yaani kila suti moja karibu Usd 3,000!.

Hii inaingia akilini kweli jamani mimi naomba hizo tender walizoleta hao jamaa wanaotaka zaidi ya Usd 3,000 kwa suti, halafu kama kweli wamenunua direct China ndio anajifunga kabisaa maana China suti ya wahudumu na hata Ma pilot unaweza kupata kwa Usd 100 hadi 300 inategemea na grade..Hapo China ndio rahisi sana kupiga bao na kwa sababu najua hili nina hakika anayekwenda kununua China ana room ya kucheza na hesabu kwa sababu bei zao huwezi kuzipata sehemu yoyote duniani by far..
 
Angesema nini jana pale cdm square! Anajaribu kukisafisha chama ambacho kilisha oza kabisa cha kutupa.

Anajidahi kuwasafisha alaf wana mpoison.
 
Back
Top Bottom