Paul Chizzi amuumbua Mwakyembe

Aliyekuwa mtendaji mkuu wa Atcl ameibuka na kusema kwamba Dr Mwakiembe alidanganya umma kutokana taarifa alizopewa kuwa ni za uongo na zisizokuwa na ukweli wowote.Kwa mfano uniform ziligharimu dola 18,000 tu na sio dola 50,000 kama alivyosema mwakiembe, Bwana chizi alisema pia tatizo ni kwamba kuna watu hawajui chochote kuhusu sekta ya anga lakini wanajiganya kuwa wanajua mbele ya umma.
Chanzo: The Guardian on Sunday

Thanks. Mwaki hapo alichemka. Pia kwa namna alivyokuwa anaongea na staff wa ATCL not proper. Alitumia lugha za kihuni. Hopeful marafiki zake wameshamweleza.
 
Huyu Chizi sasa naona kweli ameingiwa Uchizi.. Yaani ukimsoma tu unaelewa ana matatizo makubwa sana. Kifupi kama kweli wamenunua suti hizo kwa gharama ya Usd 18,000 na kuliepusha shirika gharama ya Usd 40,000 ina maana local supplier walitaka Usd 49,000 kwa suti 15?.. yaani kila suti moja karibu Usd 3,000!.

Hii inaingia akilini kweli jamani mimi naomba hizo tender walizoleta hao jamaa wanaotaka zaidi ya Usd 3,000 kwa suti, halafu kama kweli wamenunua direct China ndio anajifunga kabisaa maana China suti ya wahudumu na hata Ma pilot unaweza kupata kwa Usd 100 hadi 300 inategemea na grade..Hapo China ndio rahisi sana kupiga bao na kwa sababu najua hili nina hakika anayekwenda kununua China ana room ya kucheza na hesabu kwa sababu bei zao huwezi kuzipata sehemu yoyote duniani by far..

Mkuu, si kama namtetea Chizi la hasha najaribu kufikirisha kichwa kidogo....hivi unajua ukitaka kununua uniforms locally utapata wazimu, maana utaletewa quotations za ajabu mno! Wabongo si wakweli hasa kwenye eneo la manunuzi. Mie binafsi nashughulika sana na eneo hilo la manunuzi, kununua uniform China was a good idea, kwani hata kama ni nembo ye TZ au batiki, vitenge whatever unavyotaka ndivyo China watakavyokufanyia ili mradi upeleke design. U$ 200 - 600 per uniform si mbaya kwani what matters ni quality. Uniform per person means nguo, viatu, skarf, tie, bags, badges and related. Pia kuingia kwenye soko la ushindani kwenye airlines si kitu cha mchezo kama wengine wanavyodhani eti washonewe batik etc. Wakitoka na pamba dhaifu nyie hao hao mtaanza kuponda tena mkilinganisha na makampuni mengine ya ndege. Wabongo bana...!

Hoja hapa tunajadili Chizi alivyokanusha tuhuma za Mwakyembe. Tatizo viongozi wa TZ mara zote wanakurupuka mambo yanapoharibika. Jiulizeni nani alimteua Chizi? Matatizo ya ATCL hayakuanza na Chizi, hata yeye ameyakuta, wizi na ubadhirifu uliokithiri, kulindana na kupeana ndio mfumo unaoisumbua nchi yetu kwa sasa. Wanasiasa ni wanafiki sana, wanatafuta pa kupumulia na kuwatoa wengine makafara. Nini kazi ya Usalama wa Taifa? ajira za siku hizi hakuna vetting? Tusilalamike tu, tutafute pia kiini cha tatizo!
 
Namjua Dr Mwakyembe;ni Mbunge wangu!Watz tujiandae kumlipa Chizi mamilion ya pesa akienda mahakamani;Dr Mwakyembe ni mtu wa kupenda sifa zisizo na msingi!Yeye na Magufuli hamna aliyemzidi mwenzake!

Kusitishwa kwa ajira ya mtu kuna utaratibu wake inabidi ufuatwe na sio kuwaita waandishi wa habari na kutangaza fulani nimemfukuza kazi!Kwa ufupi Dr Mwakyembe ni abuser mkubwa wa haki za binadam!

Kyela 2015 tumekwisha mkataa na analijua hilo!

Kwenye list yako ya wapenda mijisifa muongezee Sitta na Membe...hahahahaa!

Kiukweli hata kama Chizi alikuwa na matatizo yake Mwakyembe alikurupuka. Kwani Chizi alijiteua? Mbona KM Omar Chambo muasisi wa madudu yote ktk wizara hiyo haguswi?
 
Kama mtu anaona USD 200 - 600 kwa unifirm ni kubwa hakuna namna waweza mweleza gharama za uendeshaji wa shirika la ndege akakuelewa. Akijua za mafuta Dar-Mwanza ni millioni 15 atashauri waweke maji.
Jamani uniform za wafanyakazi wa ndege sio mabatiki kama ya dancers. Suti tu ya rubani sio kama za MC. Kuna viwango vinavyotakiwa kimataifa, otherwise chini ya kiwango hata abiria hupati kama sio kunyang'anywa leseni ya aviation kabisa. . Ndege sio kama wa daladala jamani. Mi ningemheshimu Mwakyembe (PhD) akija na utafiti kutoka mashirika mengine kama Emirates, 540, Precision, KLM, etc. WAO GHARAMA ZAO ZIKOJE? Data Si zipo? Kwa nini tuongee tetesi? If you think education is expensive try ignorance' likewise, If we think Airline Business is expensive let's try daladala"

Precisely!!!
 
Hata kama hivyo ndivyo alivyosema, bado kuna tatizo kubwa sana hapo.

USD 18,000 X 1500=Tsh. 27,000,000 kwa unifomu moja! Milioni 27 kweli kwa nguo moja?

Hajaweza bado kuniweka kwenye kundi la watu wa kumuamini na sana sana ananiongezea machungu tu ya PAYE niliyokatwa mwezi uiopita.

Your suppose to be great thinker, KASOME TENA HABARI.
 
Huyu chizi sasa anajibu kama chizi sasa hiyo dola 18,000 ni ndogo?? kwani wangeshona hizo uniform nchini isingewagharimu hela yote hiyo. Aache kutapatapa ukweli ndio huo watu kama hawa fukuza kazi peleka mahakamani filisi kila kitu warudi vijijini kulima KILIMO KWANZA kinawafaa sh....waini!
Hawa watu wameshaiba hela nyingi sana,ndio maana hizo dola 18,000 anaziona ni ndogo.
 
Namjua Dr Mwakyembe;ni Mbunge wangu!Watz tujiandae kumlipa Chizi mamilion ya pesa akienda mahakamani;Dr Mwakyembe ni mtu wa kupenda sifa zisizo na msingi!Yeye na Magufuli hamna aliyemzidi mwenzake!

Kusitishwa kwa ajira ya mtu kuna utaratibu wake inabidi ufuatwe na sio kuwaita waandishi wa habari na kutangaza fulani nimemfukuza kazi!Kwa ufupi Dr Mwakyembe ni abuser mkubwa wa haki za binadam!

Kyela 2015 tumekwisha mkataa na analijua hilo!
Wewe C__r__s una hasira mno na mbunge wako. mpe muda anaelekea kujirekebisha.
 
Aliyekuwa mtendaji mkuu wa ATCL ameibuka na kusema kwamba Dr Mwakyembe alidanganya umma kutokana taarifa alizopewa kuwa ni za uongo na zisizokuwa na ukweli wowote.

Kwa mfano uniform ziligharimu dola 18,000 tu na sio dola 50,000 kama alivyosema mwakiembe, Bwana Chizi alisema pia tatizo ni kwamba kuna watu hawajui chochote kuhusu sekta ya anga lakini wanajidanganya kuwa wanajua mbele ya umma.

Chanzo: The Guardian on Sunday

OK, kuna makosa katika gharama za uniform:

(a) Je, vipi ile ndege iliyokodiwa kutoka Liberia? Yaani katika sehemu zote za dunia, eti mtu anaenda kukodi ndege kutoka Liberai, ambako wao wenyewe wanahangaika na usafiri wa anga?
(b) Tanzania tuna wabunifu wengi sana wa kimataifa akina hassanali, na Asya Idaruous; je shirika lilishindwa kuwatumia katika kushona hizo uniform?
(c) Je, siyo kweli kuwa yeye alishastaafu na ajira yake haikufuata taratibu za kisheria?
 
Mimi kusema kweli ningependa kufahamu CV au resume ya Paul Chizi. Jee, ana qualifications gani kwenye mambo ya aviation: kwa maana ya vyuo gani alivyosoma: shahada au stashahada zipi alizofanikiwa kupata; na waajiri gani tokea aanze kufanya kazi baada ya kuhitimu?
 
Aliyekuwa mtendaji mkuu wa ATCL ameibuka na kusema kwamba Dr Mwakyembe alidanganya umma kutokana taarifa alizopewa kuwa ni za uongo na zisizokuwa na ukweli wowote.

Kwa mfano uniform ziligharimu dola 18,000 tu na sio dola 50,000 kama alivyosema mwakiembe, Bwana Chizi alisema pia tatizo ni kwamba kuna watu hawajui chochote kuhusu sekta ya anga lakini wanajidanganya kuwa wanajua mbele ya umma.

Chanzo: The Guardian on Sunday
Dola 18,000/ kwa Batik za wat 15 bado anaona sawa !? Na wale maofisa wawaili waliosimamia zoezii kwa miezi 2, je walitumia Dola ngapi kwa miezim miwili !?
 
OK, kuna makosa katika gharama za uniform:

(a) Je, vipi ile ndege iliyokodiwa kutoka Liberia? Yaani katika sehemu zote za dunia, eti mtu anaenda kukodi ndege kutoka Liberai, ambako wao wenyewe wanahangaika na usafiri wa anga?

Hiyo siyo ishu mkuu! Liberia inatumiwa kama "tax haven" na nchi nyingi kwenye nyanja za usafiri wa baharini na anga kwa nia ya kukwepa kodi, na haimaanishi kwamba vyombo vya usafiri wa baharini au wa anga vilivyosajiliwa Liberia vina ubora hafifu.
 
Hiyo siyo ishu mkuu! Liberia inatumiwa kama "tax haven" na nchi nyingi kwenye nyanja za usafiri wa baharini na anga kwa nia ya kukwepa kodi, na haimaanishi kwamba vyombo vya usafiri wa baharini au wa anga vilivyosajiliwa Liberia vina ubora hafifu.

Kuna taarifa za kutosha kabisa kuwa ndege ile ni bomu; ukitaka zaidi wewe google ATCL+Liberia+Airbus. Ingawa ni kweli kuwa deal lile lilianza zamani wakati wa Makatta, huyu mheshimiwa angekuwa ni mtaalamu na mwenye nia njema na shilika, ni wazi kuwa asingesukumiza dili hilo liendelee, angelilipiga stop. Kuna kila dalili za kutia shaka kuwa huenda kabla ya kustaafu kwake, alikuwa ni mmoja waliokoleza dili hilo, na alipopewa mwanya tu basi akalisukumiza kwa nguvu zote lifanikiwa.
 
Kuna taarifa za kutosha kabisa kuwa ndege ile ni bomu; ukitaka zaidi wewe google ATCL+Liberia+Airbus. Ingawa ni kweli kuwa deal lile lilianza zamani wakati wa Makatta, huyu mheshimiwa angekuwa ni mtaalamu na mwenye nia njema na shilika, ni wazi kuwa asingesukumiza dili hilo liendelee, angelilipiga stop. Kuna kila dalili za kutia shaka kuwa huenda kabla ya kustaafu kwake, alikuwa ni mmoja waliokoleza dili hilo, na alipopewa mwanya tu basi akalisukumiza kwa nguvu zote lifanikiwa.

Sawa. inawezekana kabisa kwa sababu moja au nyingine kwamba "ndege ile ni bomu", lakini hoja yako kuwa kwa vile tu ndege imesajiliwa Liberia, basi automatically itakuwa na walakini, kwa kweli haina maana. Ndege au meli inaweza kuwa imesajiliwa Marekani ya Kaskazini au kwenye nchi ya Ulaya ya Magharibi lakini ikaonekana kuwa ni mbovu vilevile, na pamoja na yote, gharama zake zikawa za juu zaidi ya hiyo iliyosajiliwa Liberia.
 
Sawa. inawezekana kabisa kwa sababu moja au nyingine kwamba "ndege ile ni bomu", lakini hoja yako kuwa kwa vile tu ndege imesajiliwa Liberia, basi automatically itakuwa na walakini, kwa kweli haina maana. Ndege au meli inaweza kuwa imesajiliwa Marekani ya Kaskazini au kwenye nchi ya Ulaya ya Magharibi lakini ikaonekana kuwa ni mbovu vilevile, na pamoja na yote, gharama zake zikawa za juu zaidi ya hiyo iliyosajiliwa Liberia.

Nafikiri kwa mtu yeyote mwenye akili anajua kuwa swala kubwa hapa lilikuwa ni ubora wa ndege. Fortunately kuna uhusiano mkubwa sana wa baina ya ubovu wa bidhaa na kule ilikotoka, ingawa ubora wa bidhaa unaweza usihusiane sana na kule ilikotoka.
 
BA pamoja na kuwa na ndege nyingi wanatumia washonaji wa ndani ya nchi !!, Inakuwa je sisi tunaotumia ndege za kukodi ,matumizi yetu yanakuwa makubwa hivyo?
 
Kama kulikuwa na option ya kushona kwa bei ya chini ambayo ni $ 200 kwa uniform kwa nini hawakuitumia ilhali shirika halina na uwezo mkubwa kwa sasa, mimi haja ni convice hata kidogo $ 18000 still is too much lets be realistic.

Mkuu hawaja nunua uniform 15 kwani huyo idadi ya mapilot ATC inazidi 15 na kila mtu amapata zaidi ya uniform moja ili isiwa kauka ni kuvae
nguo zimenunuliwa nyingi sana
 
Dola 18,000/ kwa Batik za wat 15 bado anaona sawa !? Na wale maofisa wawaili waliosimamia zoezii kwa miezi 2, je walitumia Dola ngapi kwa miezim miwili !?

Mkuu hakuna lolote hapo Mwakiembe kaingia choo cha kike tena baada ya kutulipisha Bilion 94 kwa dowan sasa hivi itakuwa another bilion 9.4 kwa chizi
Chizi yupo entitled na compensasion kutokana na defamation aliyoitoa kwenye magazeti,
 
Huyu bwana asijitetee amefanya hujuma dhidi ya shirika la ndege. kwanini alituma watu kununua sare ulaya badala ya kutangaza tenda?taratibu za manunuzi za umma zinajulikana ,kwanini alizikiuka? hafu zile nguo zina thamani hiyo kweli? hao aliowatuma aliwalipa fedha shs ngapi?shaka yangu ni kwa watu wanao mtetea,kuna nini nyuma ya pazia wakati madudu aliyo ya fanya yako wazi?watanzania bwana!!!!!
 
Mkuu hawaja nunua uniform 15 kwani huyo idadi ya mapilot ATC inazidi 15 na kila mtu amapata zaidi ya uniform moja ili isiwa kauka ni kuvae
nguo zimenunuliwa nyingi sana
taratibu za manunuzi zimekiukwa na zaidi yate maslahi ya shirika hayakuzingatiwa,kwanini mnamtetea? au bado mnaendeleza mapambano ya kule bungeni ya nani kaharibu ulaji wa nanani hapa? tubadilike watanzania bila kutanguliza maslahi ya Nchi yetu tutaiua nchi hii.
 
Back
Top Bottom