Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,153
- 137,162
Huyo kwenye video ni chatu wa Amerika ya Kusini, ajulikanaye kama anaconda.
Inadaiwa kuwa hapo ni kwenye mji wa Porto Velho, nchini Brazil.
Joka lilikuwa linavuka barabara na watu wakasimamisha magari yao na kuliacha livuke kwa amani na utulivu na bila kulidhuru wala kuliua.
Wengine wakashuka toka kwenye magari yao na kulipiga picha za kawaida na za video kwa kutumia simu zao.
Hatimaye joka likamaliza kuvuka na likatokomea kwenye kichaka.
Hiyo ingetokea hapa Tanzania....hahahaa!
Si ajabu yangesemwa mengi sana.
Kwanza, nadhani lingeuliwa. Kama si kwa kukanyagwa na gari basi kwa kupondwa mawe.
Ingiza sasa na zile imani za kijinga.
Si ajabu kuna watu ambao wasingelala usiku kwa kuamini kuwa limetumwa.
Watu wangehaha kwenda kwa waganga 🤣 ili kujua kulikoni!
Wakati hakuna lolote zaidi ya ecosystem kuwa kazini.
Inadaiwa kuwa hapo ni kwenye mji wa Porto Velho, nchini Brazil.
Joka lilikuwa linavuka barabara na watu wakasimamisha magari yao na kuliacha livuke kwa amani na utulivu na bila kulidhuru wala kuliua.
Wengine wakashuka toka kwenye magari yao na kulipiga picha za kawaida na za video kwa kutumia simu zao.
Hatimaye joka likamaliza kuvuka na likatokomea kwenye kichaka.
Hiyo ingetokea hapa Tanzania....hahahaa!
Si ajabu yangesemwa mengi sana.
Kwanza, nadhani lingeuliwa. Kama si kwa kukanyagwa na gari basi kwa kupondwa mawe.
Ingiza sasa na zile imani za kijinga.
Si ajabu kuna watu ambao wasingelala usiku kwa kuamini kuwa limetumwa.
Watu wangehaha kwenda kwa waganga 🤣 ili kujua kulikoni!
Wakati hakuna lolote zaidi ya ecosystem kuwa kazini.
ili kujua kulikoni!
%