Pasco Mayalla ana vielement vya unabii afungue kanisa

We hua unatumia mbinu zipi kujua mambo?
kuna vitu wewe kama sio mmoja wao huwezi kuvijua. sasa nashindwa kuelewa awa mashushushu wanajulikana vipi kirahisi rahisi na ngumbalu ambao hata mgambo tu awajapitia. watanzania ifike wakati tubadilike. sio kila kitu ni cha kukihusisha na intelijensia
Wabongo wanawashobokea sana watu wa mfumo sjui kitengo
Wanawaona watu wa ajabu

Ova
wana uspecial gani bwana
 
Mayalla ni very professional. Hilo liko wazi sema hata career yake ya uandishi wa habari angepata nchi yenye uhuru kama Kenya mfano angekuwa moja kati ya waandishi na wanahabari Bora.
Tatizo misingi ya serikali yetu haikumpa nafasi kudevelop zaidi ya kuwa chawa na green guard.
Simjui,hanijui but this mzee is so smart. Natamani siku moja nimuone kwenye nafasi kubwa akiongoza nchi.
Kama wachekeshaji,maslay queen na wasiojua lolote wameweza mayalla ndo aje ashindwe
Kabisa mkuu kuna watu wamekalia ofisi za umma wanakula kodi zetu kichwani zero,Pascal akili nyingi yuko nje ya mfumo,not fair
 
Hata wewe ukianza kuandika utitiri wa threads hapa JF na kuwa unajikwoti na kujirejelea katika kila posti huku ukifuata upepo unavyokwenda kuna mambo utakuwa unabahatisha tu maana ubashiri wa kawaida mara nyingi ni 50 - 50.

Hakuna cha nabii hapo wala nini.

- P

Isitoshe yule ni CIA ya Bongo so likely pia kuna vihabari habari vingine anakuwa navyo ndiyo maana anaweza kuvigusia gusia kwenye baadhi ya nyuzi zake.
Kwa mujibu wa maandiko yake yanayothibitika mzee wake alikuwa kitengo Enzi za mwalimu,ila kuhusu yeye hakuna mwenye ushahidi kwa hilo
 
Ukizaliwa kwenye familia ya vipepeo weusi basi Kwa namna moja au nyingine utajikuta na wewe unatabia za kipepeo mweusi hata kama wewe sio kipepeo mweusi na marafiki nao watakuwa tu na Tabia za kufanana na vipepeo weusi ukiwa nao karibu lazima utajua maua wanayopenda kurukia utajua sehemu wanazopenda ila akipunguza ujuaji nakuwa mpole angekuwa miongoni mwa walamba asali ujana ulimponza saivi amekuwa kipepeo mwenye madoa doa meusi ila sio kipepeo mweusi
 
Nilianza kumuona miaka ile na kipindi chake cha Kitimoto.

Nikaja kukutane nae UDSM akisoma LLB na mimi nikisoma kozi ngumu kuliko zote pale chuoni, namkumbuka akinesanesa na pikipiki lake viunga ya UDSM au Mabibo Hostel nilipokuwa naishi.

Mwaka 2005 Au 2006 NIlikuwa napata lunch Hill Park, tukajikuta tuko meza moja, ila kwa vile alikuwa star sikumshobokea, Kama ilivyo desturi yangu ya kuwakaushia mastaa so hanijui, simjui.

Kwa bahati mbaya wote tulidisco chuo, nikakimbia nchi tena kwa mara ya pili. Sikuwahi kumuona tena zaidi ya kumsoma JF na mimi siangalii TV sijui yuko TV gani siku hizi.

Kupitia JF Nimekuwa nikifuatilia maandishi yake, nara kadhaa, niseme tu maandishi yake yana unabii ndani yake, orodha ni ndefu sana nikiweka hapa hapatoshi, vitu vingine huchukua miaka hata mitano kutokea, hakuna mwana JF anayemfikia kwa hilo.

Kama hana pepo wa utambuzi basi ana roho mtakatifu. Nafahamu yeye ni mkatoliki Mzuri ila afungue tu kanisa atapata wafuasi. Nafahamu pia anapenda siasa, madhabahuni pia ni sehemu sahihi ya kupiga siasa kama akina Mama Rwakatale, Kakobe, Gwajima, Pengo, Mtikila, Sheikh Ponda, Alhad Musa wote hao wanapiga siasa kwenye mimbari.

Atumie hilo pepo la utambuzi au roho mtakatifu aliyenae kuwafikia wengi.

Ni ushauri tu.
Kutoka kuwa mgombea ccm mpaka kuwa nabii, ndio maana nchi haiendeleai aisee
 
Tujadili Issues!!
Hii ni moja ya issues... Usidhani tunamjadili mzee mayalla,tunachokijadili hapa ni kilichobebwa/ kilichomo ndani ya mayalla. Huyu ana uzoefu wa hali ya juu kwenye diplomasia,habari,usalama wa nchi,kuijua vyema katiba na sheria za nchi na uzoefu katika mambo ya utawala.
Tuseme ukweli mayalla ni kiongozi anayepotea kutokana na nepotism na poor governance ya viongozi wetu.
Jokate ameweza
Sabaya
Makonda
Ally happy
Chalamila
Nape
Kafulila
Mwana FA
Ety mayalla aje ashindwe. Huu ni uchawi kabisa. Sio bure.
 
Hii ni moja ya issues... Usidhani tunamjadili mzee mayalla,tunachokijadili hapa ni kilichobebwa/ kilichomo ndani ya mayalla. Huyu ana uzoefu wa hali ya juu kwenye diplomasia,habari,usalama wa nchi,kuijua vyema katiba na sheria za nchi na uzoefu katika mambo ya utawala.
Tuseme ukweli mayalla ni kiongozi anayepotea kutokana na nepotism na poor governance ya viongozi wetu.
Jokate ameweza
Sabaya
Makonda
Ally happy
Chalamila
Nape
Kafulila
Mwana FA
Ety mayalla aje ashindwe. Huu ni uchawi kabisa. Sio bure.
Kinachouma umri wake unakaribia 60,Taifa limeshindwa kabisa kuvuna maarifa yake kwa faida ya wote,sio haki
 
Back
Top Bottom