Paschal Mayalla: Mwigulu Nchemba hakufurahia Majaliwa, Warioba na Pinda kushangiliwa kwenye mazishi ya Kardinali Pengo

Paschal Mayalla: Mwigulu Nchemba hakufurahia Majaliwa, Warioba na Pinda kushangiliwa kwenye mazishi ya Kardinali Pengo

"Na nikamsikia jana mheshimiwa Waziri Mkuu akisema mimi sibabaiki mambo ya kupendwa na kushangiliwa, mimi sifanyi vitu ili nishangiliwe...yaani hiyo maana yake kwa sisi wanasaikolojia ina maana aliumia, yaani mtu anashangiliwa, Waziri Mkuu mstaafu halafu mimi nipo sishangiliwi! yaani sasa ili kuonesha kwamba sijaumia yaani ile kwamba mimi sijali", - Mayalla
Yeah, Paskali alinyoosha maelezo kiume sana. Kongole kwake mtaalam wa kuuma na kupuliza.
 
"Na nikamsikia jana mheshimiwa Waziri Mkuu akisema mimi sibabaiki mambo ya kupendwa na kushangiliwa, mimi sifanyi vitu ili nishangiliwe...yaani hiyo maana yake kwa sisi wanasaikolojia ina maana aliumia, yaani mtu anashangiliwa, Waziri Mkuu mstaafu halafu mimi nipo sishangiliwi! yaani sasa ili kuonesha kwamba sijaumia yaani ile kwamba mimi sijali", - Mayalla
Mzee wa 'voices from within' aliona hilo..
 
Naomba kueleweshwa, nani amelalamika? Ni JAB au Mwigulu !

Nimesikiliza alichosema Pascal. Kwanza, siku zote amejitanabahisha kuwa news analyst. Zaidi ya hapo ni raia ana uhuru wa kutoa maoni yake. Alichokifanya ni kutumia maneno ya Mwigulu na hadhira iliyokuwepo ya makofi pamoja na reaction ya Mwigulu kufanya analysis. Kosa la Paschal ni lipi? Kufanya uchambuzi ni kosa? Wapi ametumia hisia nje ya yaliyotokea kanisani na alichosema Mwigulu !

Pascal Mayalla JokaKuu
 
Paschal Mayala ana akili nyingi hii nchi sasahivi ukiwa na akili nyingi either ukae kimya au utofautiane na serikali na huwezi kua CCM kama unaakili labda ujitoe ufaham ndio utawezana nao
 
Back
Top Bottom