Pascal Mayalla hapo lazima wamnase. Kwa sababu hakuna uthibitisho wa kuchambua mtu hisia na mihemko yake

Pascal Mayalla hapo lazima wamnase. Kwa sababu hakuna uthibitisho wa kuchambua mtu hisia na mihemko yake

Kuna maoni binafsi na maadili ya kazi.
Mayalla Pale aliongea kama Mwandishi wa habari, mtangazaji na alikuwa kazini.

Hakuongea kama Mimi na wewe hapa.

Ni sawa Daktari aongee Jambo kinyume na maadili ya kazi yake akiwa na mgonjwa
Mayala ni mwandishi wa habari huru na ana uhuru wa kuchambua taarifa au kutoa maoni bila kuingiliwa na mtu yeyote. Sio lazima ashikiwe akili kama msukule na maCCM. Maadili ya uandishi wa habari yanazuia mwandishi kutoa maoni yake kuhusu jambo fulani ktk jamii? Kama ingekuwa hivyo basi wahariri wote wangefungwa jela kwa kolamu za "maoni" kwenye magazeti yao.

Ufahamu kuwa Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari huru mwenye maoni huru na fani yake ya uandishi wa habari inampa uhuru huo. Huyo tutusa anayemtaka ajieleze kuhusu maoni aliyotoa hajui mipaka ya waandishi inapoishia. Arudi shule akasome ili kuondoa ututusa kichwani mwake.
 
Mayala ni mwandishi wa habari huru na ana uhuru wa kuchambua taarifa au kutoa maoni bila kuingiliwa na mtu yeyote. Sio lazima ashikiwe akili kama msukule na maCCM. Maadili ya uandishi wa habari yanazuia mwandishi kutoa maoni yake kuhusu jambo fulani ktk jamii? Kama ingekuwa hivyo basi wahariri wote wangefungwa jela kwa kolamu za "maoni" kwenye magazeti yao.

Ufahamu kuwa Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari huru mwenye maoni huru na fani yake ya uandishi wa habari inampa uhuru huo. Huyo tutusa anayemtaka ajieleze kuhusu maoni aliyotoa hajui mipaka ya waandishi inapoishia. Arudi shule akasome ili kuondoa ututusa kichwani mwake.

Maoni kwenye taaluma?
Maoni yanayokiuka maadili ya KAZI?

Maoni sio tatizo kama yanazingatia Misingi na maadili ya kazi.
 
Paskali ana haki ya kuzungumza maoni yake, hivyo vitisho vimeandaliwa kimkakati ili watu waogope kuendelea kujadili yaliyotokea na reaction ya Mwigulu(alivyolialia akidai kupendwa na mkewe peke yake kunatosha haitaji kupendwa na wananchi) baada ya tukio la kule kanisani.

Mbona Wakati wa Corona wakina Msukuma na baadhi ya wataalamu walipotoa maoni Yao kuhusu tiba ya Corona kuhusu kujifukuza wenye taaluma yao(madaktari) walipiga kelele?

Maoni sio mabaya kama hayakiuki taaluma na maadili
 
waTanzania wote ni ndugu na marafiki zangu sana,
na kwakweli tunapendana na kuheshimiana mno licha ya kutofautiana maoni au mawazo juu ya mambo kadha wa kadha kijamii, kisiasa na kiuchumi.

katika kukemea au kuonya jambo fulani huwa sipepesi macho wala maskio bali huwa naeleza ukweli kwa uwazi na bila kificho. Huenda lugha ya uwazi ninayotumia kukemea nonsense mbalimbali, kwako hua unaona kama ni kauli ngumu, lakini ndivyo ukweli ulivyo,

Mwalimu Pascal Mayalla ni rafiki, kaka, baba, babu, mjomba na mwalimu wa wadau karibu wote humu JF,
huna haja ya kunilisha maneno gentleman kwamba huyu mungwana ni rafiki yangu pekeyangu, huyu ni wetu sote

kama lilivyopita lile la wakati ule aivyoitwa mjengoni dodoma, ni wazi hili nalo litapita kwa salama na amani

Litapita ndio.
Watu wanajadili kwa nini afungwe breki?
 
Nimeona maoni humu watu wanalalalika hapo UDSM kwenye hostel za wanaosomea shahada ya pili na ya ubobevu hakuna maji wiki ya 3 sasa.

Dar es Salaam kuna nyuzi kama 3 humu hawana maji wiki ya 3 , haya ndio mambo yenye tija kufanyiwa kazi ila huyo waziri mkuu wa mtutu na damu za watanganyika yuko busy kupiga porojo tupu.
Jamani naomba tuelewe na kukubali: CCM haitabadilika na kila siku inazidi kwenda low! Viongozi wakishalewa madaraka, halafu wanajua wazi hakuna wa kuwaondoa, ndivyo wanavyofanya vitu vya kijinga. Itafika siku hata kumwangalia mtawala machoni au kuongea naye bila kupiga magoti iwe ni kosa, tena la kuuawa. Kama kuna mtu anayesubiri sijui washughulike na matatizo ya nchi na wananchi, basi nampa pole.
 
Hamjambo wakulungwa!

1. Robert ninapoandika maandiko na makala zangu. Mwanasaikolojia atakuwa na uwezo wa kuchambua Makala na content niliyoandika lakini hataweza kuchambua hisia, mtazamo na kilichopo moyoni mwangu.

2. Mfano, wasomaji wengi wa Makala zangu huniona kama mwanaume mchukia Wanawake, mwenye mfumo dume, Mkali Sana. Au mwenye maneno yamoja Kwa Moja. Hivyo wanaweza kunichambua hivyo kutokana na maandiko Yangu.

3. Lakini uhalisia ukawa mwingine kabisa. Kwamba maandiko au makala hazithibitishi tabia, na hisia za mwandishi.

4. Kwani Mwandishi anaweza kuandika kwa ukali lakini yeye moyoni asiwe mkali. Anaweza kuandika kwa uchungu. Lakini moyoni wala asiwe na uchungu.

5. Mimi watu wengi hasa wanawake wananiona kama Mchukia wanawake. Lakini wanaonijua, wanaoishi pamoja na mimi watatoa maoni tofauti.

6. Ndivyo ilivyo kwa Watoa hotuba. Mtoa hotuba anapozungumza unaweza kuchambua contents anayozungumza lakini huwezi kuchambua hisia zake za ndani.

7. Kwa mchambuzi na mwanahabari kitaaluma wanajua sio maadili kuweka maoni binafsi ya mwandishi katika kuchambua hisia binafsi za mtu ambazo kimsingi huwezi kuthibitisha.

8? Contents anayohutubia unaweza kuichambua kwa sababu inathibitika. Umeisikia au kuisoma. So unaweza kusema contents hii imeandikwa na mtu anayeonekana alikuwa na hasira.

9. Pascal Mayalla kusema Mwigulu Nchemba alikuwa amechukia ni kosa la kiuchambuzi na kiuandishi. Kwa sababu Hana uwezo WA kuthibitisha jambo hilo.

10. Ila angesema Mwigulu alionekana kuchukia aliposema blah blah blahm hapo Pascal angekuwa sahihi kwa asilimia Mia moja kwani amem-judge Mwigulu kulingana na content na context iliyokuwepo.
Lakini ushahidi hana.

11. Mwigulu anaweza kusema sikuwa nimechukia. pascal hataweza kuthibitisha kwamba Mwigulu alichukia au hakupenda.

12. Kuonekana umechukia na kuchukia ni mambo mawili tofauti.
Kuonekana unapenda na kupenda ni mambo mawili tofauti.

13. Hakuna uthibitisho wa hisia za mtu kisaikolojia ila viashiria vinaweza kutoa maana zaidi ya moja na kulingana na mtu na mtu.

14. MTU anaweza akalia na akawa na furaha. Yaani akalia kwa furaha.
MTU anaweza akacheka lakini akacheka kwa huzuni au kebehi.

15. Wanafasihi wao ndio wanaweza kuchambua Jambo kivyovyote kwani sisi tunatoa maoni yetu katika kazi ya Sanaa.

16. Muandishi wa habari sio Mwanafasihi ila anaweza kutumia vipengele vya Fasihi.
Mwandishi anatakiwa kutoa habari, kuripoti habari kama ilivyo. Ukweli.

17. Maoni ya mwandishi WA habari yajikite kwenye contents kuliko hisia za mtu kwani kujikita kwenye hisia za mtu lazima uzue taharuki, lazima uripoti uongo kwa sababu unaongea Jambo ambalo huna ushahidi nalo.

18. Alionekana anafuraha.

19. Ingawaje kesi kama hizi zinaweza kuendeshwa kisiasa au kwa mrengo wa siasa. Kwani Wapo waandishi huchambua hisia za watu na hapa ni viongozi wengine katikaa namna ya kuwasifia. Na waandishi hao hawajawahi kuambiwa wathibitishe uchambuzi wao kwa viongozi hao.

20. Wachambuzi na watangazaji mara kadhaa tumekuwa tukiwasikia wakichambua hisia za watu ambazo hazithibitishiki.
Mfano utasikia mtangazaji akisema, "Namuona Mhe. Rais akifurahia pale. Mambo anayoyapenda Sana haya"
Kisa amemwona Raia anatabasamu na kucheka.
Wakati ingetakiwa kwa mwandishi aseme" Namuona Mhe Rais akitabasamu na akicheka sana. Anaonekana kufurahia pale. Hakika huenda haya ndio mambo ayapendayo"
Hiyo ni kwa muandishi mweledi.

21. Wanafasihi wao ndio wapo huru kutoa maoni kwenye kazi zao. Wao wanachanganya uandishi wa habari, Sanaa ya lugha na maoni Yao kulingana na interest, ujumbe, dhamira n.k.

22. Kwenye kesi kama hiyo kwa Mwanafasihi anachomoa asubuhi tuu kwa sababu msingi mkuu wa wanafasihi ni maoni ya mtunzi na mwandishi. Sio kile ambacho msomaji atatafsiri.

23. Hiyo inaitwa kufungwa break kidogo. Hatari Sana.

Kufikia hapo sina la ziada.

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
Mimi nipo pamoja na Pascal hadi auwawe, hata ningekuwa Mimi ningekata tamaa ..kuishabikia CCM mda wote ule wanalamba teuzi wakina Magoti? Aseeee... Pascal ameona isiwe nongwa liwalo na liliwe ...ametangaza vita dhidi ya selikali haramu.
 
Nimeona maoni humu watu wanalalalika hapo UDSM kwenye hostel za wanaosomea shahada ya pili na ya ubobevu hakuna maji wiki ya 3 sasa.

Dar es Salaam kuna nyuzi kama 3 humu hawana maji wiki ya 3 , haya ndio mambo yenye tija kufanyiwa kazi ila huyo waziri mkuu wa mtutu na damu za watanganyika yuko busy kupiga porojo tupu.
Na wewe itabidi uende mbele ya bodi ya ithibati ukathibitishe taarifa hizi...nchi imeshajifia hii ni utawala wa Maduro na Ayatollah 🐼
 
Mimi nipo pamoja ma Pascal hata ningekuwa Mimi ningekata tamaa ..kuishabikia CCM mda wote ule wanalamba teuzi wakina Magoti? Aseeee... Pascal ameona isiwe nongwa liwalo na liliwe ...ametangaza vita dhidi ya selikali harumu.


Aaah! Mama Yangu Game over!
Pascal ametoa maoni yake lakini akiwa kazini.
Swali linakuja, je mwandishi anaruhusiwa kutoa maoni yake binafsi kuhusu hisia zaa mtu mwingine?
 
Litapita ndio.
Watu wanajadili kwa nini afungwe breki?
hajafungwa breki na hayuko wa kufungwa breki katika nchi hii huru katika kujieleza.
pamoja na hayo,
ni muhimu sana kufahamu kwamba nchi yetu inaongozwa katika misingi ya kisheria inayoambatana na uwazi lakini pia uwajibikaji.

Na kama binadamu, katika mazingira tofauti tofauti tuanweza kukosea, lakini kuna fursa ya kurekebishana na kusahihishana ili hatimae tunaposonga mbele katika ujenzi wa taifa letu tufanye vizuri zaidi kwa umoja na maelewano katika kuchochea ustawi na maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa maslahi mapana ya waTanzania wote.

Ni matumaini yangu na ya wadau wote wa JF kwamba hili nalo litapita kwa salama na amani
 
Back
Top Bottom