Pascal Mayalla hapo lazima wamnase. Kwa sababu hakuna uthibitisho wa kuchambua mtu hisia na mihemko yake

Pascal Mayalla hapo lazima wamnase. Kwa sababu hakuna uthibitisho wa kuchambua mtu hisia na mihemko yake

Mayala kina mchotaka kumtokea ni ile kanuni ya what goes around comes back around

Alishawahi kumchoma muandishi mwenzie humu Kwa magufuli

I think ni kabendera jamii alipitia tabu sana , na sababu alikuwa ni pascal mayala , Baada ya kuanza kumlalamikia kabendera kuwa ana msema vibaya magu ,

Machawa wakaona hizo thread mwisho wa siku waka deal na kabendera,,

Haya Nature Huwa Haina adabu wala huruma Leo nayeye anataka kuongizwa kwenye kaa la moto kazi anayo

Unafikiri wataichukulia serious?
Hapo ni kengele ya onyo tuu.
 
Hayo ni maoni yake binafsi. Wasimfunge mdomo Pascal Mayalla na kumfundisha jinsi ya kufikirl. Naona sasa maCCM yanataka kutushikia akili na kutufundisha jinsi ya kufikiri.

Kuna maoni binafsi na maadili ya kazi.
Mayalla Pale aliongea kama Mwandishi wa habari, mtangazaji na alikuwa kazini.

Hakuongea kama Mimi na wewe hapa.

Ni sawa Daktari aongee Jambo kinyume na maadili ya kazi yake akiwa na mgonjwa
 
Nimeona maoni humu watu wanalalalika hapo UDSM kwenye hostel za wanaosomea shahada ya pili na ya ubobevu hakuna maji wiki ya 3 sasa.

Dar es Salaam kuna nyuzi kama 3 humu hawana maji wiki ya 3 , haya ndio mambo yenye tija kufanyiwa kazi ila huyo waziri mkuu wa mtutu na damu za watanganyika yuko busy kupiga porojo tupu.

😆😆😆 Mambo ni Mengi Bwashee. Hadi unachanganyikiwa. Mtu anaona eeh acha nisijichoshe. Anajiunga na wapiga porojo
 
Ila huyo waziri mkuu wa mtutu na damu za watanganyika yuko busy kupiga porojo tupu.
Naam mkuu, katiba inasema waziri mkuu atatokana wabunge wa kuchaguliwa.

Tarehe 29 hakukua na huo uchaguzi ilikua ni mitutu na damu za watanganyika zaidi ya 10000 mitaani na hata wengine hadi leo hawajapata maiti.

Hivyo ni lazima tuseme wazi huyu ni waziri mkuu wa mitutu na damu za watanganyika maana hana ridhaa wa uhalali kuwepo hapo.
 
Inakuaje Waziri Mkuu una maindi vitu vidogo vidogo kama hivi

Hapana sio vitu vidogo. Ila vinaweza kuchukuliwa kama vitu vidogo(kupuuzwa).

Pascal Mayalla anaeleza yeye kama mwanasaikolojia akitumia maneno kwa watu wanaojua saikolojia alafu anaeleza anachotaka kueleza akifafanua hisia za mtu mwingine.
Anaposema kwa watu wanaojua saikolojia tayari anaandaa wasikilizaji kumuamini kwa kile ambacho ataeleza. Uhakika wa atakachoeleza.
Kwamba ni mbobevu.

Sasa anaweza kuwa mwanasaikolojia kweli. Na hata anachoongea kinaweza kuwa kweli lakini uthibitisho(ukweli) ndio msingi wa habari
 
Ila Bongo kuna ujinga mwingi sana. Hivi hiki ni kitu cha kumtaka mtu kudhibitisha kweli? Hakuna mambo ya msingi ya kujadili? Watu wanarusha drone za hatari huko, sisi tunapeana 24 hrs kwa vitu vya kitoto

Ndio swali hilohilo utaulizwa. Kwa nini Pascal mayalla asijadili mambo ya msingi kama kurusha drone na the likes. Na anajadilli mambo ya hisia au hotuba za watu?

Hapo ni pipa na mfuniko. Kama tutatenda Haki kuwajaji.

Lakini kama tutataka Fair play basi hakuna haja ya bodi ya ithibati kumfuatilia Pascal
 
Kwa sababu ni Rafiki yako sio😀😀
Mbona wengine unatoa kauli ngumu?
waTanzania wote ni ndugu na marafiki zangu sana,
na kwakweli tunapendana na kuheshimiana mno licha ya kutofautiana maoni au mawazo juu ya mambo kadha wa kadha kijamii, kisiasa na kiuchumi.

katika kukemea au kuonya jambo fulani huwa sipepesi macho wala maskio bali huwa naeleza ukweli kwa uwazi na bila kificho. Huenda lugha ya uwazi ninayotumia kukemea nonsense mbalimbali, kwako hua unaona kama ni kauli ngumu, lakini ndivyo ukweli ulivyo,

Mwalimu Pascal Mayalla ni rafiki, kaka, baba, babu, mjomba na mwalimu wa wadau karibu wote humu JF,
huna haja ya kunilisha maneno gentleman kwamba huyu mungwana ni rafiki yangu pekeyangu, huyu ni wetu sote

kama lilivyopita lile la wakati ule aivyoitwa mjengoni dodoma, ni wazi hili nalo litapita kwa salama na amani
 
Hamjambo wakulungwa!

1. Robert ninapoandika maandiko na makala zangu. Mwanasaikolojia atakuwa na uwezo wa kuchambua Makala na content niliyoandika lakini hataweza kuchambua hisia, mtazamo na kilichopo moyoni mwangu.

2. Mfano, wasomaji wengi wa Makala zangu huniona kama mwanaume mchukia Wanawake, mwenye mfumo dume, Mkali Sana. Au mwenye maneno yamoja Kwa Moja. Hivyo wanaweza kunichambua hivyo kutokana na maandiko Yangu.

3. Lakini uhalisia ukawa mwingine kabisa. Kwamba maandiko au makala hazithibitishi tabia, na hisia za mwandishi.

4. Kwani Mwandishi anaweza kuandika kwa ukali lakini yeye moyoni asiwe mkali. Anaweza kuandika kwa uchungu. Lakini moyoni wala asiwe na uchungu.

5. Mimi watu wengi hasa wanawake wananiona kama Mchukia wanawake. Lakini wanaonijua, wanaoishi pamoja na mimi watatoa maoni tofauti.

6. Ndivyo ilivyo kwa Watoa hotuba. Mtoa hotuba anapozungumza unaweza kuchambua contents anayozungumza lakini huwezi kuchambua hisia zake za ndani.

7. Kwa mchambuzi na mwanahabari kitaaluma wanajua sio maadili kuweka maoni binafsi ya mwandishi katika kuchambua hisia binafsi za mtu ambazo kimsingi huwezi kuthibitisha.

8? Contents anayohutubia unaweza kuichambua kwa sababu inathibitika. Umeisikia au kuisoma. So unaweza kusema contents hii imeandikwa na mtu anayeonekana alikuwa na hasira.

9. Pascal Mayalla kusema Mwigulu Nchemba alikuwa amechukia ni kosa la kiuchambuzi na kiuandishi. Kwa sababu Hana uwezo WA kuthibitisha jambo hilo.

10. Ila angesema Mwigulu alionekana kuchukia aliposema blah blah blahm hapo Pascal angekuwa sahihi kwa asilimia Mia moja kwani amem-judge Mwigulu kulingana na content na context iliyokuwepo.
Lakini ushahidi hana.

11. Mwigulu anaweza kusema sikuwa nimechukia. pascal hataweza kuthibitisha kwamba Mwigulu alichukia au hakupenda.

12. Kuonekana umechukia na kuchukia ni mambo mawili tofauti.
Kuonekana unapenda na kupenda ni mambo mawili tofauti.

13. Hakuna uthibitisho wa hisia za mtu kisaikolojia ila viashiria vinaweza kutoa maana zaidi ya moja na kulingana na mtu na mtu.

14. MTU anaweza akalia na akawa na furaha. Yaani akalia kwa furaha.
MTU anaweza akacheka lakini akacheka kwa huzuni au kebehi.

15. Wanafasihi wao ndio wanaweza kuchambua Jambo kivyovyote kwani sisi tunatoa maoni yetu katika kazi ya Sanaa.

16. Muandishi wa habari sio Mwanafasihi ila anaweza kutumia vipengele vya Fasihi.
Mwandishi anatakiwa kutoa habari, kuripoti habari kama ilivyo. Ukweli.

17. Maoni ya mwandishi WA habari yajikite kwenye contents kuliko hisia za mtu kwani kujikita kwenye hisia za mtu lazima uzue taharuki, lazima uripoti uongo kwa sababu unaongea Jambo ambalo huna ushahidi nalo.

18. Alionekana anafuraha.

19. Ingawaje kesi kama hizi zinaweza kuendeshwa kisiasa au kwa mrengo wa siasa. Kwani Wapo waandishi huchambua hisia za watu na hapa ni viongozi wengine katikaa namna ya kuwasifia. Na waandishi hao hawajawahi kuambiwa wathibitishe uchambuzi wao kwa viongozi hao.

20. Wachambuzi na watangazaji mara kadhaa tumekuwa tukiwasikia wakichambua hisia za watu ambazo hazithibitishiki.
Mfano utasikia mtangazaji akisema, "Namuona Mhe. Rais akifurahia pale. Mambo anayoyapenda Sana haya"
Kisa amemwona Raia anatabasamu na kucheka.
Wakati ingetakiwa kwa mwandishi aseme" Namuona Mhe Rais akitabasamu na akicheka sana. Anaonekana kufurahia pale. Hakika huenda haya ndio mambo ayapendayo"
Hiyo ni kwa muandishi mweledi.

21. Wanafasihi wao ndio wapo huru kutoa maoni kwenye kazi zao. Wao wanachanganya uandishi wa habari, Sanaa ya lugha na maoni Yao kulingana na interest, ujumbe, dhamira n.k.

22. Kwenye kesi kama hiyo kwa Mwanafasihi anachomoa asubuhi tuu kwa sababu msingi mkuu wa wanafasihi ni maoni ya mtunzi na mwandishi. Sio kile ambacho msomaji atatafsiri.

23. Hiyo inaitwa kufungwa break kidogo. Hatari Sana.

Kufikia hapo sina la ziada.

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
Paskali ana haki ya kuzungumza maoni yake, hivyo vitisho vimeandaliwa kimkakati ili watu waogope kuendelea kujadili yaliyotokea na reaction ya Mwigulu(alivyolialia akidai kupendwa na mkewe peke yake kunatosha haitaji kupendwa na wananchi) baada ya tukio la kule kanisani.
 
Back
Top Bottom