Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 34,050
- 79,392
- Thread starter
- #21
Ina kayatimba kwa mwgl sahv 😄
Ova
Hapo ni kufungwa breki tuu. Sidhani kama ni ishu serious Sana
Ina kayatimba kwa mwgl sahv 😄
Ova
Mayala kina mchotaka kumtokea ni ile kanuni ya what goes around comes back around
Alishawahi kumchoma muandishi mwenzie humu Kwa magufuli
I think ni kabendera jamii alipitia tabu sana , na sababu alikuwa ni pascal mayala , Baada ya kuanza kumlalamikia kabendera kuwa ana msema vibaya magu ,
Machawa wakaona hizo thread mwisho wa siku waka deal na kabendera,,
Haya Nature Huwa Haina adabu wala huruma Leo nayeye anataka kuongizwa kwenye kaa la moto kazi anayo
Hakuna kitu
Hayo ni maoni yake binafsi. Wasimfunge mdomo Pascal Mayalla na kumfundisha jinsi ya kufikirl. Naona sasa maCCM yanataka kutushikia akili na kutufundisha jinsi ya kufikiri.
Ukishapewa Onyo hata watu waliokuwa wana taka kushirikiana na wewe lazima wakutenge kwakuwa watakuona unaweza kuwaingiza matatizoni na serikali,Unafikiri wataichukulia serious?
Hapo ni kengele ya onyo tuu.
Nimeona maoni humu watu wanalalalika hapo UDSM kwenye hostel za wanaosomea shahada ya pili na ya ubobevu hakuna maji wiki ya 3 sasa.
Dar es Salaam kuna nyuzi kama 3 humu hawana maji wiki ya 3 , haya ndio mambo yenye tija kufanyiwa kazi ila huyo waziri mkuu wa mtutu na damu za watanganyika yuko busy kupiga porojo tupu.
Ukishapewa Onyo hata watu waliokuwa wana taka kushirikiana na wewe lazima wakutenge kwakuwa watakuona unaweza kuwaingiza matatizoni na serikali,
So Kuna mirija lazima itaziba tu
Sema paschal anaweza kupenya vizuri tu, kama aliruka kiunzi cha kamati za bunge hata hii atapita.
Kama alichukia Kuna ubaya gani na kama hakuchukia kuna faida gani?
Ni hatari sana , taifa likiwa linadeal na petty issues wakati mambo ya msingi hayaendi haina afya .😆😆😆 Mambo ni Mengi Bwashee. Hadi unachanganyikiwa. Mtu anaona eeh acha nisijichoshe. Anajiunga na wapiga porojo
Naam mkuu, katiba inasema waziri mkuu atatokana wabunge wa kuchaguliwa.Ila huyo waziri mkuu wa mtutu na damu za watanganyika yuko busy kupiga porojo tupu.
Inakuaje Waziri Mkuu una maindi vitu vidogo vidogo kama hivi
Ni hatari sana , taifa likiwa linadeal na petty issues wakati mambo ya msingi hayaendi haina afya .
ni matumaini yangu hili nalo litapita kwa amani
Ila Bongo kuna ujinga mwingi sana. Hivi hiki ni kitu cha kumtaka mtu kudhibitisha kweli? Hakuna mambo ya msingi ya kujadili? Watu wanarusha drone za hatari huko, sisi tunapeana 24 hrs kwa vitu vya kitoto
Inashangaza sana..Ila Bongo kuna ujinga mwingi sana. Hivi hiki ni kitu cha kumtaka mtu kudhibitisha kweli? Hakuna mambo ya msingi ya kujadili? Watu wanarusha drone za hatari huko, sisi tunapeana 24 hrs kwa vitu vya kitoto
Inashangaza sana..
Uchawa umekuwa mwingi mpaka aibu.
Sawa mjumbe wa bodi ya ithibati..Pascal angechambua hisia za mwigulu kwa namna inayompendeza Mwigulu wala asingeitwa kuthibitisha hisia za mwigulu hata kama hazithibitishiki
waTanzania wote ni ndugu na marafiki zangu sana,Kwa sababu ni Rafiki yako sio😀😀
Mbona wengine unatoa kauli ngumu?
Paskali ana haki ya kuzungumza maoni yake, hivyo vitisho vimeandaliwa kimkakati ili watu waogope kuendelea kujadili yaliyotokea na reaction ya Mwigulu(alivyolialia akidai kupendwa na mkewe peke yake kunatosha haitaji kupendwa na wananchi) baada ya tukio la kule kanisani.Hamjambo wakulungwa!
1. Robert ninapoandika maandiko na makala zangu. Mwanasaikolojia atakuwa na uwezo wa kuchambua Makala na content niliyoandika lakini hataweza kuchambua hisia, mtazamo na kilichopo moyoni mwangu.
2. Mfano, wasomaji wengi wa Makala zangu huniona kama mwanaume mchukia Wanawake, mwenye mfumo dume, Mkali Sana. Au mwenye maneno yamoja Kwa Moja. Hivyo wanaweza kunichambua hivyo kutokana na maandiko Yangu.
3. Lakini uhalisia ukawa mwingine kabisa. Kwamba maandiko au makala hazithibitishi tabia, na hisia za mwandishi.
4. Kwani Mwandishi anaweza kuandika kwa ukali lakini yeye moyoni asiwe mkali. Anaweza kuandika kwa uchungu. Lakini moyoni wala asiwe na uchungu.
5. Mimi watu wengi hasa wanawake wananiona kama Mchukia wanawake. Lakini wanaonijua, wanaoishi pamoja na mimi watatoa maoni tofauti.
6. Ndivyo ilivyo kwa Watoa hotuba. Mtoa hotuba anapozungumza unaweza kuchambua contents anayozungumza lakini huwezi kuchambua hisia zake za ndani.
7. Kwa mchambuzi na mwanahabari kitaaluma wanajua sio maadili kuweka maoni binafsi ya mwandishi katika kuchambua hisia binafsi za mtu ambazo kimsingi huwezi kuthibitisha.
8? Contents anayohutubia unaweza kuichambua kwa sababu inathibitika. Umeisikia au kuisoma. So unaweza kusema contents hii imeandikwa na mtu anayeonekana alikuwa na hasira.
9. Pascal Mayalla kusema Mwigulu Nchemba alikuwa amechukia ni kosa la kiuchambuzi na kiuandishi. Kwa sababu Hana uwezo WA kuthibitisha jambo hilo.
10. Ila angesema Mwigulu alionekana kuchukia aliposema blah blah blahm hapo Pascal angekuwa sahihi kwa asilimia Mia moja kwani amem-judge Mwigulu kulingana na content na context iliyokuwepo.
Lakini ushahidi hana.
11. Mwigulu anaweza kusema sikuwa nimechukia. pascal hataweza kuthibitisha kwamba Mwigulu alichukia au hakupenda.
12. Kuonekana umechukia na kuchukia ni mambo mawili tofauti.
Kuonekana unapenda na kupenda ni mambo mawili tofauti.
13. Hakuna uthibitisho wa hisia za mtu kisaikolojia ila viashiria vinaweza kutoa maana zaidi ya moja na kulingana na mtu na mtu.
14. MTU anaweza akalia na akawa na furaha. Yaani akalia kwa furaha.
MTU anaweza akacheka lakini akacheka kwa huzuni au kebehi.
15. Wanafasihi wao ndio wanaweza kuchambua Jambo kivyovyote kwani sisi tunatoa maoni yetu katika kazi ya Sanaa.
16. Muandishi wa habari sio Mwanafasihi ila anaweza kutumia vipengele vya Fasihi.
Mwandishi anatakiwa kutoa habari, kuripoti habari kama ilivyo. Ukweli.
17. Maoni ya mwandishi WA habari yajikite kwenye contents kuliko hisia za mtu kwani kujikita kwenye hisia za mtu lazima uzue taharuki, lazima uripoti uongo kwa sababu unaongea Jambo ambalo huna ushahidi nalo.
18. Alionekana anafuraha.
19. Ingawaje kesi kama hizi zinaweza kuendeshwa kisiasa au kwa mrengo wa siasa. Kwani Wapo waandishi huchambua hisia za watu na hapa ni viongozi wengine katikaa namna ya kuwasifia. Na waandishi hao hawajawahi kuambiwa wathibitishe uchambuzi wao kwa viongozi hao.
20. Wachambuzi na watangazaji mara kadhaa tumekuwa tukiwasikia wakichambua hisia za watu ambazo hazithibitishiki.
Mfano utasikia mtangazaji akisema, "Namuona Mhe. Rais akifurahia pale. Mambo anayoyapenda Sana haya"
Kisa amemwona Raia anatabasamu na kucheka.
Wakati ingetakiwa kwa mwandishi aseme" Namuona Mhe Rais akitabasamu na akicheka sana. Anaonekana kufurahia pale. Hakika huenda haya ndio mambo ayapendayo"
Hiyo ni kwa muandishi mweledi.
21. Wanafasihi wao ndio wapo huru kutoa maoni kwenye kazi zao. Wao wanachanganya uandishi wa habari, Sanaa ya lugha na maoni Yao kulingana na interest, ujumbe, dhamira n.k.
22. Kwenye kesi kama hiyo kwa Mwanafasihi anachomoa asubuhi tuu kwa sababu msingi mkuu wa wanafasihi ni maoni ya mtunzi na mwandishi. Sio kile ambacho msomaji atatafsiri.
23. Hiyo inaitwa kufungwa break kidogo. Hatari Sana.
Kufikia hapo sina la ziada.
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam