Part 4: TISS bado safari ngumu

Part 4: TISS bado safari ngumu

Wee jamaaa acha utani kwenye mambo ya msingi...
Jf ni kokoro lililojaa takataka Kwa asilimia 70.
Ni forum uliyojaa watu wasio na uwiano au kuwa kiwango fulani cha taaluma au fani.
Tunaunganishwa na kitu kimoja Tu .....
UWEZO WA KUINGIA MTANDAONI. Mostly Kwa kumiliki smartphone tena wengine za kupewa, kurithi au kuiba... achilia mbali wale wengine wanaingia na vibatani vya 30000.
Ukiwa muelewa huwezi kutegemea kupata elimu humu. Unless uwe na ufahamu mpana WA kuanalyse mambo na sio kujifunza.
Mkuu sio kweli sasa wewe uko kwenye category ipi?........Mimi nakuambia hivi jf ni zaidi ya social media
 
Mleta mada uko sahihi.
Kipindi kile Wameifungia JF kwa miezi miwili tulipata hifadhi ya ukimbizi Kenya Forum
Kule tulitapika nyongo haswa kutokana na kukerwa na tabia za uminywaji wa haki za kutoa maoni.

laiti wasingeturudishia JF yetu tungebaki Kenya Forum.
Yaani Jamaa wana mambo ya ajabu sana, yaani wako tayari data, elimu nzito iliyomo kwenye archives za JF izimike na ipotee ilimradi tu kumlinda Jiwe dhidi ya criticisms tu za kawaida za kisiasa.
Leo hii ukigoogle kitu kuhusu Tanzania, JF inatokea kama sehemu mojawapo ya Kukupa Taarifa, Sasa cha ajabu hawa jamaa walitaka JF ife na hazina hii ya data.
Ajabu sana!
Serekali inabidi imlide Mello kwa maslahi ya nchi
 
Mimi nimeanza kujua maana ya TISS miaka ya hapa baada ya Baba wa taifa kututoka, kabla ya hapo, hawa watu huwajui ila wapo, na cha ajabu siku hizi wanatajwa hadharani na wao pia wajitokeza kwenye "live" mtindo wa kisasa, wakikemea mambo.
Yaani Siku hizi wana dili na............ ...... ....... Sio umasikini au rushwa, ufisadi, na mengine..... Mbaya zaidi sasa wanajulikana kama wafia chama na sio Nchi.

Yaani sifa kubwa sasa hivi ya kuwa TISS ni kumsujudia rais na kumfanyizia yoyote asiyekubaliana na mienendo ya rais. Sasa hivi ni sifa kwa TISS kuwa mwanaccm, mpaka imefikia mahali wakuu wa vyombo vya dola wanaona fahari kujisifia na uccm wao huku TISS ikiona ni sawa na kukalia kimya huo uhuni.
 
Part 3 na Part 2
Asante sana mkuu Kihava ktk comment yako post #87, umenikumbusha mbali sana.
Kabla sijaendelea nainukuu post yako Kama ilivyo kwa faida ya wengine ili wajue nini maana ya usalama wa taifa na una umuhimu gani kwa nchi.


"TISS ndio nchi yenyewe kama hujui. Hata ungekuwa na elimu kiasi gani huwezi kufanya jambo lolote la maana kama TISS hawataki. Nakuhakikishia hata kama una uwezo wa kujenga kiwanda kikubwa kiasi gani, kilichopo eneo halali kabisa kama TISS hawataridhika na wewe huwezi! Wewe ni 'mgeni' kwenye utawala wa nchi. Nchi ina wenyewe, sisi wengine hata tungekuwa na cheo kikubwa kiasi gani kama TISS wakisema NO! Huwezi kwenda tofauti nao 'ukaishi'. Hata huyu mzee wetu vituko anavyofanya vya kuwaumiza wenzake ni kwamba TISS wameridhia. Wakisema hatutaki hiki lifanyike hana ubavu wa kukataa. Maan ukiwakatalia wanachokisema kwa maslahi ya nchi basi wewe utaondoka ili Taifa libaki salama. Kwa hiyo kwa ujumla TISS ndio mhimili wa nchi. Hakuna anayeweza 'kukohoa' mbele ya TISS kama wakisema hili hapana. Kwa hiyo hata Musiba TISS waliamua wamwache afanye atakavyo, lakini wangesema MUSIBA 'stop' misiba yako hatuitaki hangekuwa na jeuri ya kuendelea kufanya chochote. Hivyo ndugu yangu jua ya kwamba hakuna mwenye ubavu kuliko TISS ndani ya nchi yoyote duniani. TISS ikiwa dhaifu nchi itakuwa dhaifu tuuuu! Tunaiombea TISS ya nchi yetu iwe imara kwa Taifa imara."

Mwisho wa kunukuu.

Baada ya mashambulizi ya kigaidi Marekani Sept 11,Rais George Walker Bush alifanya kikao cha siri Whitehouse chini ya handaki akiwa na waziri wake wa mambo ya nje, Condollezza Rice, mkuu wa majeshi ya Marekani Jenerari Tommy Franks, pamoja na mkurugenzi mkuu wa CIA Bob Tenet.

Katika kikao hicho Bush alimwambia Bob Tenet kwamba, hakuna Marekani bila CIA imara, CIA ingelikuwa legelege Marekani ingekuwa magofu hapa Duniani au ingekuwa ombaomba na maskini wa kutupwa.

Naandika makala hii kwa uchungu sana, nashangaa Kuna watu wanaleta siasa ktk jambo gumu wakati mimi nazungumzia mustakabali wa taifa letu Halafu watu wanaleta habari ya vyama vya siasa.

Makala hii haina U Chadema wala U CCM, ni maalumu kwa ajili ya taifa lenu.
Marekani, Uingereza, Ujerumani, Japan ,Sweden, Norway Finland, Australia, Canada, viongozi hawana ujanja chini ya idara za usalama wa taifa linapokuja suala la usalama wa nchi na maslahi ya uchumi,huwa wanafanyiwa zengwe na kutolewa.

Mungu ibariki Jamiiforums, makala hii ingelikuwa kwenye Gazeti la hard copy ingekuwa imeshapata misukosuko mikubwa Kama kufungiwa Gazeti na mwandishi kukamatwa.

Pia Mungu ibariki Kenyan forum, hiyo pia imechangia uwepo wa JF, waliona kabisa kwamba endapo wataifungia JF bado tungehamia jumla Kenyan forum ambako ndo ingekuwa hatari kwa sababu watu wangetapika nyongo bila breki, bora hapa kuna speed governor.

Mungu mbariki Maxence Melo kwa kuanzisha huu mtandao unaotikisa Dunia kwa sasa .

INAENDELEA
 
Tatizo Ninaloliona Ndan Ya Idara Yetu Ni Kugawanyika Kwa Idara Katika Vipande Viwili .

Kuna Wanaoleta Habari Za Kweli Na Mafaili Yamejaa Makao Makuu Ya Idara Na Ikulu Ila Cha Kushangaza Hayafanyiwi Kazi Na Mamlaka Wanachoambulia Ni Kupigwa Bench ( Yaan Wanakuwa Ndan Ya Idara Ila Uamz Hawana)

Kundi La Pili Ni Wafia Chama Wanao leta Habari Za Umbea Kama Walivyowafanyia Wakina Simbachawene Kipind Kile, Anthony Mtaka Na Wengine Kibao.

Ili Kund La Pili Lina Nguvu Kuliko La Kwanza Ndio Maana Unaona yanayoendelea xaxa
NAMCHUKIA SANA MWENYEKITI WA SADC WA SASA
 
Mamlaka ya Rais ni makubwa kuliko mamlaka ya Taasisi yoyote Tanzania kulingana na mfumo uliopo, kwa mfumo uliopo, TISS sichochote kwa Magu kwa sasa anaweza kufanya lolote.

Pamoja na mapungufu aliyokuwa nayo Kipilimba, hajaondolewa kwasababu ya mapungufu hayo bali ameondolewa kwenye nafasi yake sababu hafanyi yanayomfurahisha Magu personally.

Naomba ufanye utafiti, Magu hajawahi hata siku moja kumuondosha mtu kazini anayemsifia, anayefanya matakwa yake ambayo hayana maslahi kwa Taifa, n.k. Hatakama atakuwa anavunja Katiba, Sheria za nchi, mtu huyo atabaki salama hata guswa na mtu yeyote au chombo chochote!.
Jf kuna madini sana
 
Mungu ibariki Jamiiforums, makala hii ingelikuwa kwenye Gazeti la hard copy ingekuwa imeshapata misukosuko mikubwa Kama kufungiwa Gazeti na mwandishi kukamatwa.

Pia Mungu ibariki Kenyan forum, hiyo pia imechangia uwepo wa JF, waliona kabisa kwamba endapo wataifungia JF bado tungehamia jumla Kenyan forum ambako ndo ingekuwa hatari kwa sababu watu wangetapika nyongo bila breki, bora hapa kuna speed governor.

Mungu mbariki Maxence Melo kwa kuanzisha huu mtandao unaotikisa Dunia kwa sasa .

INAENDELEA

Mungu ambariki na kuendelea kumpa moyo wa Uvumilivu!.
Kwa hakika atakuwa amepitia mengi mpaka sasa!
Kubwa ni kwa vipi tumefikia hapa na mbeleni kunajipi ya kujikwamua nalo?
Je TISS isukwe upya? Maana kwa sasa inavyoonekana Siasa imekompromise Hadhi na Misingi ya Taasisi!
 
Ebana anzisha uzi kuna point unazo zenye mantiki.TISS msichukizwe uwepo wa hizi mada zinaweza kuwasaidia ni namna gani jamii inavyowachokulia hivyo nyuzi za humu zinawaongezea point rekekebushi kwenye Taasisi yenu.ACHANENI NA DHANA YA KUNG'OA MENO KWA WATU WENYE KUTOA OPINIONS ZAO HASWA KWENYE KUIKOSOA SERIKALI JIKITENI KWENYE KUTAFUTA SOLUTIONS ZA MATATIZO MBALI MBALI yanayolalamikiwa na watawaliwa la sivyo haya malalamiko yatakuwa kama bomu ndani ya nchi.Acheni kutumika kisiasa tumikeni kimaslai ya nchi zaidi ili hata kama chama cha Upinzani kikiingia madarakani kikutte Taasisi yenu imeimarika na ipo focus kwenye maslahi ya taifa na sio kutumika kama misukule ya CCM.
Nchi yoyote ambayo taasisi nyingine au watu binafsi wana nguvu zaidi ya taasisi za usalama,haiwezi kubaki salama.
Unachosema mkuu pamoja na bwana Kivava ndivyo inavyopaswa kuwa.
Ukiona haiko hivyo,kwamba kuna watu au network ya watu regardless ya nafasi zao kwenye jamii,wana nguvu zaidi ya intelijensia ya nchi,basi ujue shida ni kubwa.
Taasisi yetu kwa maoni yangu,inataka kuharibiwa now,na wanasiasa.Na hii ni kutokana na loopholes kwenye sheria za nchi.
Tuweke sawa sheria yetu iipe nguvu kubwa intelijensia ya nchi kiutendaji na kimuundo,lakini pia kiusalama zaidi ni vema tukawa na kitu kimoja kinachoitwa intelijensia ambacho kimegawanywa kwa taasisi mbalimbali zenye mgawanyo wa majukumu kulingana na mahitaji ya nchi kwenye kila nyanja inayogusa mtanzania.
Mfumo wa intelijensia ni kama binadamu alivyo kimaumbile,kichwa kimoja,kinafanya coordination ya maeneo yote ya mwili kwa kupitia nerves.Shughuli zinafanyika maeneo husika kwenye misuli na kemikali zilizo special kwa kiungo,lakini lazima pawe na mawasiliano from head.Kichwa ni kichwa tu,hakiwezi kusema kinasimama pekee bila viungo vingine,wala hamna kiungo kinachoweza kusimama pekee bila vingine,kila kimoja kina kazi yake,ila vyote viko coordinated na kichwa.
Nchi ni kama mwili,intelijensia ni kama ubongo na nerves za fahamu,kuwe na taasisi kuu inayofanya coordination na taasisi nyingine zinazotekeleza majukumu ya kiintelijensia kulingana na matakwa ya nchi.
Matakwa ya nchi yagawanywe,kile kilichopo na kile kinachohitajika kuwepo.Matakwa ya nchi yajulikane kwa maswali yanayojitokeza kupitia uzoefu wa kiitelijensia kwa taasisi zote in coordination,sio maswali yanayoulizwa na viongozi wa nchi tu.
Unapokuwa na intelijensia ambayo muda wote iko busy kutafuta majibu kwa maswali yanayoulizwa na mtu mmoja au wawili sababu ya powers walizo nazo kimfumo,then you are dead as a nation,yanasubiriwa mazishi tu.
Kwa sababu inafika kipindi hata kichwa huwa kinapewa taarifa ya baadhi ya activity ambazo zimeshafanyika na kiungo bila kusubiri zaidi,maana ni urgent,meaning kwamba components za mfumo zinahitajiana,sio moja kuburuza nyingine.
Kama kweli tunataka kuibadili nchi yetu na kukimbizana na maendeleo ya dunia ya leo,hatuna budi kuanza na intelijensia ya nchi,lazima ifumuliwe,itanuliwe sana na kuanza upya.Lakini tunahitaji watu sahihi kuwaingiza na kuwatumia huko.Kila mahali tunahitaji intelijensia,hospitali,michezoni,muzikini,siasani,jeshini..just everywhere penye shughuli-binadamu,lazima kuwe na intelijensia inayokusanya data,kupeleka kichwani na kuimpose response kulingana na maslahi ya nchi,na malengo yake.Kuna mahali huhitaji siasa,bali sayansi,sasa kama intelijensia imejaa siasa tu,unawezaje kudeal na mambo ya kisayansi?lazima utakosea.Intelijensia ni pana mno,na nchi inavyokuwa,mahitaji yanaongezeka,hamwezi kubaki na akili ile ile,lazima iwe "akili kubwa".
Dunia ya sasa,nchi zote makini,lazima intelijensia yake iwe na vitengo ambavyo ni research based kwenye mambo mazito kama uchumi,sayansi,demographics,mabadiliko ya tabia jamii,sera na mahitaji ya kimataifa etc.Sijui tiss yetu iko level zipi kwenye hili,sijui kwa kweli,wasiwasi wangu ni kuwa huenda taasisi ni ndogo kuliko inavyotakiwa kuwa kwa sasa.
 
Tatizo Ninaloliona Ndan Ya Idara Yetu Ni Kugawanyika Kwa Idara Katika Vipande Viwili .

Kuna Wanaoleta Habari Za Kweli Na Mafaili Yamejaa Makao Makuu Ya Idara Na Ikulu Ila Cha Kushangaza Hayafanyiwi Kazi Na Mamlaka Wanachoambulia Ni Kupigwa Bench ( Yaan Wanakuwa Ndan Ya Idara Ila Uamz Hawana)

Kundi La Pili Ni Wafia Chama Wanao leta Habari Za Umbea Kama Walivyowafanyia Wakina Simbachawene Kipind Kile, Anthony Mtaka Na Wengine Kibao.

Ili Kund La Pili Lina Nguvu Kuliko La Kwanza Ndio Maana Unaona yanayoendelea xaxa
Shida kubwa ni kuingiza watu wa TISS kwenye vyeo vya kisiasa , wamekuwa wanaccm na watetezi wa ccm badala ya nchi
 
Hebu tusipepese macho ni kwamba malalamikommengi yanaibuka kwa sababu TISS yetu imekuwa kama mlezi na mlinda maslahi ya chama Tawala.
 
alitaka JF ife na hazina hii ya data.
Nina posts zaidi elf 13...halafu mtu anazipoteza tu hivi hivi...siyo kabisa. Hata hivyo mtu mwenye kuitakia mema Tanzania na yeye mwenyewe...hawezi kudhubutu kufikiria kuifungia JF kamwe kwa mazingira tuliyomo. Nashauri JF wafanye mpango wa kutuandalia mafaili ya zip yatakayobeba posts zetu zote kiasi tukitaka kuzidownload iwe rahisi. FB wamefanya hivyo ingawa kwa mizengwe.
 
Unganisha makala zako ziwe pamoja.....
Asante sana mkuu Kihava ktk comment yako post #87, umenikumbusha mbali sana.
Kabla sijaendelea nainukuu post yako Kama ilivyo kwa faida ya wengine ili wajue nini maana ya usalama wa taifa na una umuhimu gani kwa nchi.


"TISS ndio nchi yenyewe kama hujui. Hata ungekuwa na elimu kiasi gani huwezi kufanya jambo lolote la maana kama TISS hawataki. Nakuhakikishia hata kama una uwezo wa kujenga kiwanda kikubwa kiasi gani, kilichopo eneo halali kabisa kama TISS hawataridhika na wewe huwezi! Wewe ni 'mgeni' kwenye utawala wa nchi. Nchi ina wenyewe, sisi wengine hata tungekuwa na cheo kikubwa kiasi gani kama TISS wakisema NO! Huwezi kwenda tofauti nao 'ukaishi'. Hata huyu mzee wetu vituko anavyofanya vya kuwaumiza wenzake ni kwamba TISS wameridhia. Wakisema hatutaki hiki lifanyike hana ubavu wa kukataa. Maan ukiwakatalia wanachokisema kwa maslahi ya nchi basi wewe utaondoka ili Taifa libaki salama. Kwa hiyo kwa ujumla TISS ndio mhimili wa nchi. Hakuna anayeweza 'kukohoa' mbele ya TISS kama wakisema hili hapana. Kwa hiyo hata Musiba TISS waliamua wamwache afanye atakavyo, lakini wangesema MUSIBA 'stop' misiba yako hatuitaki hangekuwa na jeuri ya kuendelea kufanya chochote. Hivyo ndugu yangu jua ya kwamba hakuna mwenye ubavu kuliko TISS ndani ya nchi yoyote duniani. TISS ikiwa dhaifu nchi itakuwa dhaifu tuuuu! Tunaiombea TISS ya nchi yetu iwe imara kwa Taifa imara."

Mwisho wa kunukuu.

Baada ya mashambulizi ya kigaidi Marekani Sept 11,Rais George Walker Bush alifanya kikao cha siri Whitehouse chini ya handaki akiwa na waziri wake wa mambo ya nje, Condollezza Rice, mkuu wa majeshi ya Marekani Jenerari Tommy Franks, pamoja na mkurugenzi mkuu wa CIA Bob Tenet.

Katika kikao hicho Bush alimwambia Bob Tenet kwamba, hakuna Marekani bila CIA imara, CIA ingelikuwa legelege Marekani ingekuwa magofu hapa Duniani au ingekuwa ombaomba na maskini wa kutupwa.

Naandika makala hii kwa uchungu sana, nashangaa Kuna watu wanaleta siasa ktk jambo gumu wakati mimi nazungumzia mustakabali wa taifa letu Halafu watu wanaleta habari ya vyama vya siasa.

Makala hii haina U Chadema wala U CCM, ni maalumu kwa ajili ya taifa lenu.
Marekani, Uingereza, Ujerumani, Japan ,Sweden, Norway Finland, Australia, Canada, viongozi hawana ujanja chini ya idara za usalama wa taifa linapokuja suala la usalama wa nchi na maslahi ya uchumi,huwa wanafanyiwa zengwe na kutolewa.

Mungu ibariki Jamiiforums, makala hii ingelikuwa kwenye Gazeti la hard copy ingekuwa imeshapata misukosuko mikubwa Kama kufungiwa Gazeti na mwandishi kukamatwa.

Pia Mungu ibariki Kenyan forum, hiyo pia imechangia uwepo wa JF, waliona kabisa kwamba endapo wataifungia JF bado tungehamia jumla Kenyan forum ambako ndo ingekuwa hatari kwa sababu watu wangetapika nyongo bila breki, bora hapa kuna speed governor.

Mungu mbariki Maxence Melo kwa kuanzisha huu mtandao unaotikisa Dunia kwa sasa .

INAENDELEA
 
Nina posts zaidi elf 13...halafu mtu anazipoteza tu hivi hivi...siyo kabisa. Hata hivyo mtu mwenye kuitakia mema Tanzania na yeye mwenyewe...hawezi kudhubutu kufikiria kuifungia JF kamwe kwa mazingira tuliyomo. Nashauri JF wafanye mpango wa kutuandalia mafaili ya zip yatakayobeba posts zetu zote kiasi tukitaka kuzidownload iwe rahisi. FB wamefanya hivyo ingawa kwa mizengwe.

Naunga mkono hoja

yaani kwa idadi ya comments na Threads nilizozianzizha humu, nikizicompile vizuri naweza kuandika Thesis ya PhD iliyosimama kabisa, halafu eti atokee mtu mon
mmoja asiyejielewa huko TISS kwa sababu ya ulevi tu wa madaraka aagize eti fungia JF
Yaani inamaana hawaoni madini yaliyomo humu JF hata ukiweka siasa pembeni!
 
Mkuu kuna swali niliuliza posti zilizopita, bila shaka katika hizi mada watu wa kitengo wapo wengi tu. Swali langu imekuwaje tiss wakaachia nchi ikapata baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wenye tatizo la afya ya akili. Tiss ipo na inasemwa iko imara na makini kulikoni?
Hili ni swali fikirishi sana. Na pia linatakiwa lipate uwanja mpana wa kulijadili. Kuna mapungufu mengi sana yalifanyika mpaka inaonekana tumejikwaa, kuna tuhuma za uraia wa viongozi na meengi ambayo yalitakiwa yafanyiwe kazi na TISS ili yawekwe sawa.
 
Mkuu kuna swali niliuliza posti zilizopita, bila shaka katika hizi mada watu wa kitengo wapo wengi tu. Swali langu imekuwaje tiss wakaachia nchi ikapata baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wenye tatizo la afya ya akili. Tiss ipo na inasemwa iko imara na makini kulikoni?
Mkuu mimi nataka nikubali kuwa TISS imeingiliwa na chama, na hii ni bahati mbaya.
 
Back
Top Bottom