Ndugu yangu maoni na ushauri wako uko sahihi ila shida ni namna ya kuyatekeza hayo, ukiangalia vyombo vyote vya kimaamzi kama, Rais, Bunge, labda na mahakama vimejaa wahuni ambao hayo uliyoyashauri yafanyike hawawezi kuyaruhusu yafanyike kwa kuwa wanamaslahi nayo binafsi yasiyo maslahi ya Taifa.Nyie mnaoilalamikia TISS kila kukicha, hebu jaribuni kwanza kufanya utafiti wa kina kuhusiana na hiyo Taasisi yenyewe kwanza.
Fanyeni utafiti TISS ukilinganisha na Taasisi zingine za Ujasusi ktk nchi zingine mbalimbali, kuizingatia suala LA Sheria, na Kanuni za Taasisi husika, Miundo yao ya Utendaji, Recruitment systems zake, n.k.
Narudia tena kusema kuwa, tatizo kubwa linaloikabili TISS linatokana NA kuwepo kwa Sheria mbaya , Kanuni, Miongozo NA Taratibu zilizopo ambazo hazifai zinazosimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za Taasisi yenyewe.
Sheria na Kanuni ni mbaya, zimepitwa na wakati, hazifai NA wala hazina tija ktk Kulinda NA Kuitetea Maslahi mapana ya umma wa wananchi wa Tz.
USHAURI ILI IWEPO TISS NZURI TZ
1.KUREKEBISHA SHERIA
Yafanyike Marekebisho ya Sheria, Kanuni, Miongozo mbalimbali inayotumika ktk kusimamia uendeshaji wa Shughuli za kila siku za Taasisi hii nyeti kabisa, TISS .
Bila kusahau kurekebisha Katiba ya nchi.
Sheria na Kanuni zibadilishwe ili ziendane na mahitaji ya wakati wa sasa wa Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia, Utandawazi, Ushindani wa Kiuchumi kupitia nguvu ya Soko.
TISS ijikite zaidi NA ielekeze nguvu zaidi ktk kufanya UJASUSI wa Kiuchumi, badala ya Ujasusi wa Kisiasa ambao hauna tija yoyote ile kwa maslahi mapana ya umma.
TISS iwe ni Taasisi ya UKOMBOZI WA KIUCHUMI KWA Watz, KWA sababu adui mkubwa zaidi KWA sasa nchini Tz ni Umaskini na Uchumi mbaya kwa nchi na wananchi wake KWA ujumla
2.KUFANYA MAPINDUZI YA FIKRA KUPITIA "ELIMU BORA"
Elimu Bora ni silaha nzito zaidi kuliko zote ili kuleta maendeleo endelevu yaliyo ya kweli mahali popote pale. Bila ya Elimu bora hakuna maendeleo ya kweli, kamwe maendeleo hawawezi kuja KWA miujiza isipokuwa kupitia Elimu bora.
Wananchi wote wahimizwe kuhusu suala la Elimu bora.
TISS nayo ifanye recruitment ya Watu wenye upeo mkubwa, ambao watakuwa na tija ktk Taasisi hiyo NA KWA nchi KWA ujumla. Watu waajiriwe kulingana na UWEZO wao NA taaluma zao walizonazo, wala siyo kutokana na mitazamo yao ya kiitikadi kwenye masuala ya Kisiasa kama ilivyo hivi sasa.
ELIMU (Intelligence) ndio nguzo kuu kabisa ktk kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake yote kwenye Taasisi yoyote ile ya Ujasusi popote pale duniani, ndio maana zinaitwa "INTELLIGENCE SECURITY AGENCY"
3.KUUNDA TAASISI ILIYO COMPETENT KIUTENDAJI
Taasisi hii ni nyeti sana ktk nchi yoyote ile, hivyo basi, inatakiwa itawaliwe na weledi WA hali ya juu kabisa ktk utendaji wao wa kazi, isiingilwe hovyo hovyo kiutendaji na wanasiasa.Ni hatari sana KWA Usalama wa nchi NA wananchi wake.
Endapo kama wanasiasa na watu wengine wasiohusika watakuwa na maamuzi kwenye Taasisi nyeti kabisa kama hii, hatari yake ni kwamba badala ya kuwa Taasisi ya Usalama WA Taifa itageuka NA kuwa Taasisi HATARI ZAIDI kwa Usalama WA nchi NA wananchi wake. Itakuwa ni "Genge LA Mauaji" ktk nchi husika, "Mafia Gangs", na mifano hao ipo mingi sana kwenye hili, e.g. KGB, GESTAPO, etc.
Isipokee maagizo ya hovyo hovyo kutoka WA Wanasiasa NA kuyatekekeza pasipo na kuyafanyia upembuzi yanikifu kwanza, uzalendo na maslahi mapana ya umma yawekwe mbele kwanza KWA kila uamuzi au muafaka unaofikiwa au KWA kila jambo litakaloamriwa NA Taasisi hii.
Mfano mzuri wa maamuzi bora kabisa ya kizalendo KWA maslahi mapana ya umma ni kupitia tukio moja LA kisa cha kweli huko nchini Afrika Kusini. "Mamlaka" ziliwahi kutoa Amri za Kuua (Assassination Orders ) zikipendekeza kuuliwa kwa mwanasiasa kijana wa upinzani, ambaye ni machachari zaidi na mkosoaji mkubwa zaidi wa Serikali Bwana Julius Malema. Baadhi ya Wajumbe wa Security Committees ambao kisheria wana mamlaka ya kuidhinisha assassination orders kabla ya kutekelezwa kwake, walipinga pendekezo hili la kumuua huyo mwanasiasa. Pale Mamlaka zilipoendelea kutoa pendekezo hili kwa kurudia rudia, baadhi ya wajumbe WA Security committee walikerwa na badala yake waliamua kuvujisha taarifa hizi nyeti kabisa kwa umma ili kuzima kabisa hilo jaribio ovu la kumuua huyo mwanasiasa.
Mimi ushauri wangu, TISS wakiamua wanaweza kuwa chachu ya mabadiliko ya kweli kwa kuvujisha taarifa za magenge hayo yanayojinufaisha ili wanachi wapate taarifa zakutosha za maovu ya magenge hayo ili ziwakere wananchi na hatimaye wananchi washinikize utekelezaji wa maoni na ushauri wako.
