Chief Kabikula
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 7,564
- 9,041
Kama tiss ni imara na inafanya kazi kwa maslahi ya nchi ilikuwaje ikaruhusu yafuatayo:1Kati ya wagombea urais 42 ccm kwanini iliruhusu wagombea wenye sifa na weledi wa kutosha wakaachwa wakaletwa hawa? 2.Kwanini iliruhusu mkuu wa nchi Magu kuharibu uchumi wa nchi kwa kupandisha kodi, kusumbua wafanyabiashara mpaka wakafunga biashara zao 3. Kwanini waliruhusu Magu akabadili sheria akapandisha tozo na ushuru mbalimbali bandarini mpaka wafanyabiashara wa nchi za jirani wakaihama bandari yetu hivyo kupoteza mapato. 4.Kwanini wameruhusu Magufuli kubomolea watu maelfu ya nyumba zao, ambapo Magufuli hajapata chochote wala nchi haijapata chochote zaidi ya hasara. 5.Kwanini wameruhusu Magufuli kufukuzana Wafanyakazi vyeti feki wakati wamekaa kwenye utumishi muda mrefu, mfano walimu wamefundisha watu ambao wako ofisini mpaka sasa wakati wao wameondolewa, kwanini amewaacha vyeti feki jeshini , polisi,magerezani, uhamiaji na tiss ? Haya amewafukuza amepata nini sasa? 6.Kwanini tiss wameruhusu Magufuli ateue wakuu wa mikoa na wilaya wasiokuwa na sifa wengine wagonjwa wa afya ya akili.Tiss si wananguvu ya kumlazimisha rais afanyaje kwa maslahi ya nchi, vipi matilioni yamepotea 2.4 sehemu ya fedha hizo voti namba ishirini Ikulu. 7. Kwanini Tiss wameruhusu rais anunue ndege na kufanya matumizi mengine ya pesa za umma bila idhini ya bunge wala kufuata sheria ya manunuzi ya umma, hapa nina respond kwenye posti na 87, yapo mengi tu tiss hebu tusaidieni huu ni mtazamo tu kwa maslahi mapana ya nchi.